Surah Al-Muddaththir with Swahili

  1. Surah mp3
  2. More
  3. Swahili
The Holy Quran | Quran translation | Language Swahili | Surah Muddathir | المدثر - Ayat Count 56 - The number of the surah in moshaf: 74 - The meaning of the surah in English: The One Wrapped Up.

يَا أَيُّهَا الْمُدَّثِّرُ(1)

 Ewe uliye jigubika!

قُمْ فَأَنذِرْ(2)

 Simama uonye!

وَرَبَّكَ فَكَبِّرْ(3)

 Na Mola wako Mlezi mtukuze!

وَثِيَابَكَ فَطَهِّرْ(4)

 Na nguo zako, zisafishe.

وَالرُّجْزَ فَاهْجُرْ(5)

 Na yaliyo machafu yahame!

وَلَا تَمْنُن تَسْتَكْثِرُ(6)

 Wala usitoe kwa kutaraji kuzidishiwa.

وَلِرَبِّكَ فَاصْبِرْ(7)

 Na kwa ajili ya Mola wako Mlezi, subiri!

فَإِذَا نُقِرَ فِي النَّاقُورِ(8)

 Basi litapo pulizwa barugumu,

فَذَٰلِكَ يَوْمَئِذٍ يَوْمٌ عَسِيرٌ(9)

 Siku hiyo, basi, itakuwa siku ngumu.

عَلَى الْكَافِرِينَ غَيْرُ يَسِيرٍ(10)

 Kwa makafiri haitakuwa nyepesi.

ذَرْنِي وَمَنْ خَلَقْتُ وَحِيدًا(11)

 Niache peke yangu na niliye muumba;

وَجَعَلْتُ لَهُ مَالًا مَّمْدُودًا(12)

 Na nikamjaalia awe na mali mengi,

وَبَنِينَ شُهُودًا(13)

 Na wana wanao onekana,

وَمَهَّدتُّ لَهُ تَمْهِيدًا(14)

 Na nikamtgenezea mambo vizuri kabisa.

ثُمَّ يَطْمَعُ أَنْ أَزِيدَ(15)

 Kisha anatumai nimzidishie!

كَلَّا ۖ إِنَّهُ كَانَ لِآيَاتِنَا عَنِيدًا(16)

 Hasha! Kwani hakika yeye alikuwa akizifanyia inadi Aya zetu!

سَأُرْهِقُهُ صَعُودًا(17)

 Nitamtesa kwa mateso yasio wezekana.

إِنَّهُ فَكَّرَ وَقَدَّرَ(18)

 Kwani hakika yeye alifikiri na akapima.

فَقُتِلَ كَيْفَ قَدَّرَ(19)

 Basi ameangamia! Vipi alivyo pima!

ثُمَّ قُتِلَ كَيْفَ قَدَّرَ(20)

 Tena ameangamia! Vipi alivyo pima!

ثُمَّ نَظَرَ(21)

 Kisha akatazama,

ثُمَّ عَبَسَ وَبَسَرَ(22)

 Kisha akakunja kipaji, na akanuna.

ثُمَّ أَدْبَرَ وَاسْتَكْبَرَ(23)

 Kisha akaipa kisogo haki, na akatakabari.

فَقَالَ إِنْ هَٰذَا إِلَّا سِحْرٌ يُؤْثَرُ(24)

 Na akasema: Haya si chochote ila ni uchawi ulio nukuliwa.

إِنْ هَٰذَا إِلَّا قَوْلُ الْبَشَرِ(25)

 Haya si chochote ila kauli ya binaadamu.

سَأُصْلِيهِ سَقَرَ(26)

 Nitakuja mtia kwenye Moto wa Saqar.

وَمَا أَدْرَاكَ مَا سَقَرُ(27)

 Na nini kitakujuulisha ni nini huo Moto wa Saqar?

لَا تُبْقِي وَلَا تَذَرُ(28)

 Haubakishi wala hausazi.

لَوَّاحَةٌ لِّلْبَشَرِ(29)

 Unababua ngozi iwe nyeusi.

عَلَيْهَا تِسْعَةَ عَشَرَ(30)

 Juu yake wapo kumi na tisa.

وَمَا جَعَلْنَا أَصْحَابَ النَّارِ إِلَّا مَلَائِكَةً ۙ وَمَا جَعَلْنَا عِدَّتَهُمْ إِلَّا فِتْنَةً لِّلَّذِينَ كَفَرُوا لِيَسْتَيْقِنَ الَّذِينَ أُوتُوا الْكِتَابَ وَيَزْدَادَ الَّذِينَ آمَنُوا إِيمَانًا ۙ وَلَا يَرْتَابَ الَّذِينَ أُوتُوا الْكِتَابَ وَالْمُؤْمِنُونَ ۙ وَلِيَقُولَ الَّذِينَ فِي قُلُوبِهِم مَّرَضٌ وَالْكَافِرُونَ مَاذَا أَرَادَ اللَّهُ بِهَٰذَا مَثَلًا ۚ كَذَٰلِكَ يُضِلُّ اللَّهُ مَن يَشَاءُ وَيَهْدِي مَن يَشَاءُ ۚ وَمَا يَعْلَمُ جُنُودَ رَبِّكَ إِلَّا هُوَ ۚ وَمَا هِيَ إِلَّا ذِكْرَىٰ لِلْبَشَرِ(31)

 Na hatukuwafanya walinzi wa Motoni ila ni Malaika, wala hatukuifanya idadi yao hiyo ila kuwatatanisha walio kufuru, wapate kuwa na yakini walio pewa Kitabu, na wazidi Imani wale walio amini, wala wasiwe na shaka walio pewa Kitabu na Waumini, na wapate kusema wenye maradhi katika nyoyo zao na makafiri: Mwenyezi Mungu amekusudia nini kwa mfano huu? Ndio kama hivyo Mwenyezi Mungu humwacha apotee amtakaye, na humwongoa amtakaye. Na hapana yeyote anaye jua majeshi ya Mola wako Mlezi ila Yeye tu. Na haya si chochote ila ni ukumbusho kwa binaadamu.

كَلَّا وَالْقَمَرِ(32)

 Hasha! Naapa kwa mwezi!

وَاللَّيْلِ إِذْ أَدْبَرَ(33)

 Na kwa usiku unapo kucha!

وَالصُّبْحِ إِذَا أَسْفَرَ(34)

 Na kwa asubuhi inapo pambazuka!

إِنَّهَا لَإِحْدَى الْكُبَرِ(35)

 Hakika huo Moto ni katika mambo yaliyo makubwa kabisa!

نَذِيرًا لِّلْبَشَرِ(36)

 Ni onyo kwa binaadamu,

لِمَن شَاءَ مِنكُمْ أَن يَتَقَدَّمَ أَوْ يَتَأَخَّرَ(37)

 Kwa anaye taka miongoni mwenu kutangulia au kuchelewa.

كُلُّ نَفْسٍ بِمَا كَسَبَتْ رَهِينَةٌ(38)

 Kila nafsi imo rahanini kwa mabaya iliyo yachuma.

إِلَّا أَصْحَابَ الْيَمِينِ(39)

 Isipo kuwa watu wa kuliani.

فِي جَنَّاتٍ يَتَسَاءَلُونَ(40)

 Hao watakuwa katika Mabustani, wawe wanaulizana

عَنِ الْمُجْرِمِينَ(41)

 Khabari za wakosefu:

مَا سَلَكَكُمْ فِي سَقَرَ(42)

 Ni nini kilicho kupelekeni Motoni?

قَالُوا لَمْ نَكُ مِنَ الْمُصَلِّينَ(43)

 Waseme: Hatukuwa miongoni walio kuwa wakisali.

وَلَمْ نَكُ نُطْعِمُ الْمِسْكِينَ(44)

 Wala hatukuwa tukiwalisha masikini.

وَكُنَّا نَخُوضُ مَعَ الْخَائِضِينَ(45)

 Na tulikuwa tukizama pamoja na walio zama katika maovu.

وَكُنَّا نُكَذِّبُ بِيَوْمِ الدِّينِ(46)

 Na tulikuwa tukiikanusha siku ya malipo.

حَتَّىٰ أَتَانَا الْيَقِينُ(47)

 Mpaka yakini ilipo tufikia.

فَمَا تَنفَعُهُمْ شَفَاعَةُ الشَّافِعِينَ(48)

 Basi hautawafaa kitu uombezi wa waombezi.

فَمَا لَهُمْ عَنِ التَّذْكِرَةِ مُعْرِضِينَ(49)

 Basi wana nini hata wanapuuza onyo hili?

كَأَنَّهُمْ حُمُرٌ مُّسْتَنفِرَةٌ(50)

 Kama kwamba wao ni mapunda walio timuliwa,

فَرَّتْ مِن قَسْوَرَةٍ(51)

 Wanao mkimbia simba!

بَلْ يُرِيدُ كُلُّ امْرِئٍ مِّنْهُمْ أَن يُؤْتَىٰ صُحُفًا مُّنَشَّرَةً(52)

 Ati kila mmoja katika wao anataka apewe nyaraka zilizo funuliwa.

كَلَّا ۖ بَل لَّا يَخَافُونَ الْآخِرَةَ(53)

 Hasha! Kwani wao hawaiogopi Akhera?

كَلَّا إِنَّهُ تَذْكِرَةٌ(54)

 Hasha! Kwa hakika huu ni ukumbusho!

فَمَن شَاءَ ذَكَرَهُ(55)

 Basi anaye taka atakumbuka.

وَمَا يَذْكُرُونَ إِلَّا أَن يَشَاءَ اللَّهُ ۚ هُوَ أَهْلُ التَّقْوَىٰ وَأَهْلُ الْمَغْفِرَةِ(56)

 Na hawatakumbuka isipo kuwa Mwenyezi Mungu atake. Uchamngu ni kwake Yeye, na msamaha ni wake Yeye.


More surahs in Swahili:


Al-Baqarah Al-'Imran An-Nisa'
Al-Ma'idah Yusuf Ibrahim
Al-Hijr Al-Kahf Maryam
Al-Hajj Al-Qasas Al-'Ankabut
As-Sajdah Ya Sin Ad-Dukhan
Al-Fath Al-Hujurat Qaf
An-Najm Ar-Rahman Al-Waqi'ah
Al-Hashr Al-Mulk Al-Haqqah
Al-Inshiqaq Al-A'la Al-Ghashiyah

Download surah Al-Muddaththir with the voice of the most famous Quran reciters :

surah Al-Muddaththir mp3 : choose the reciter to listen and download the chapter Al-Muddaththir Complete with high quality
surah Al-Muddaththir Ahmed El Agamy
Ahmed Al Ajmy
surah Al-Muddaththir Bandar Balila
Bandar Balila
surah Al-Muddaththir Khalid Al Jalil
Khalid Al Jalil
surah Al-Muddaththir Saad Al Ghamdi
Saad Al Ghamdi
surah Al-Muddaththir Saud Al Shuraim
Saud Al Shuraim
surah Al-Muddaththir Abdul Basit Abdul Samad
Abdul Basit
surah Al-Muddaththir Abdul Rashid Sufi
Abdul Rashid Sufi
surah Al-Muddaththir Abdullah Basfar
Abdullah Basfar
surah Al-Muddaththir Abdullah Awwad Al Juhani
Abdullah Al Juhani
surah Al-Muddaththir Fares Abbad
Fares Abbad
surah Al-Muddaththir Maher Al Muaiqly
Maher Al Muaiqly
surah Al-Muddaththir Muhammad Siddiq Al Minshawi
Al Minshawi
surah Al-Muddaththir Al Hosary
Al Hosary
surah Al-Muddaththir Al-afasi
Mishari Al-afasi
surah Al-Muddaththir Yasser Al Dosari
Yasser Al Dosari


Monday, May 6, 2024

لا تنسنا من دعوة صالحة بظهر الغيب