🔥 0 siku mfululizo
📖 Sura ndefu — imegawanywa sehemu ndogo (182 Aya)
📚 Sura Zote
30%
🎤 Gusa ikoni ya maikrofoni 🎙️ karibu na aya yoyote ili kujirekodi, kisha sikiliza na ulinganishe na qari.
0/182
37:1 🔁 0/5
وَٱلصَّٰٓفَّٰتِ صَفًّا  ۝١
Wassaaaffaati saffaa
Naapa kwa wanao jipanga kwa safu.
🎤 Rekodi yako:
37:2 🔁 0/5
فَٱلزَّٰجِرَٰتِ زَجۡرًا  ۝٢
Fazzaajiraati zajraa
Na kwa wenye kukataza mabaya.
🎤 Rekodi yako:
37:3 🔁 0/5
فَٱلتَّٰلِيَٰتِ ذِكۡرًا  ۝٣
Fattaaliyaati Zikra
Na kwa wenye kusoma Ukumbusho.
🎤 Rekodi yako:
37:4 🔁 0/5
إِنَّ إِلَٰهَكُمۡ لَوَٰحِدٌ  ۝٤
Inna Illaahakum la Waahid
Hakika Mungu wenu bila ya shaka ni Mmoja.
🎤 Rekodi yako:
37:5 🔁 0/5
رَّبُّ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضِ وَمَا بَيۡنَهُمَا وَرَبُّ ٱلۡمَشَٰرِقِ  ۝٥
Rabbus samaawaati wal ardi wa maa bainahumaa wa Rabbul mashaariq
Mola Mlezi wa mbingu na ardhi, na yaliyomo kati yao, na ni Mola Mlezi wa mashariki zote.
🎤 Rekodi yako:
37:6 🔁 0/5
إِنَّا زَيَّنَّا ٱلسَّمَآءَ ٱلدُّنۡيَا بِزِينَةٍ ٱلۡكَوَاكِبِ  ۝٦
Innaa zaiyannas samaaa `ad dunyaa bizeenatinil kawaakib
Hakika Sisi tumeipamba mbingu ya karibu kwa pambo la nyota.
🎤 Rekodi yako:
37:7 🔁 0/5
وَحِفۡظًا مِّن كُلِّ شَيۡطَٰنٍ مَّارِدٍ  ۝٧
Wa hifzam min kulli Shaitaanim maarid
Na kulinda na kila shet'ani a'si.
🎤 Rekodi yako:
37:8 🔁 0/5
لَّا يَسَّمَّعُونَ إِلَى ٱلۡمَلَإِ ٱلۡأَعۡلَىٰ وَيُقۡذَفُونَ مِن كُلِّ جَانِبٍ  ۝٨
Laa yassamma `oona ilal mala il a`alaa wa yuqzafoona min kulli jaanib
Wasiweze kuwasikiliza viumbe watukufu. Na wanafukuzwa huko kila upande.
🎤 Rekodi yako:
37:9 🔁 0/5
دُحُورًاۖ وَلَهُمۡ عَذَابٌ وَاصِبٌ  ۝٩
Duhooranw wa lahum `azaabunw waasib
Wakifurushwa. Na wanayo adhabu ya kudumu.
🎤 Rekodi yako:
37:10 🔁 0/5
إِلَّا مَنۡ خَطِفَ ٱلۡخَطۡفَةَ فَأَتۡبَعَهُۥ شِهَابٌ ثَاقِبٌ  ۝١٠
Illaa man khatifal khatfata fa atba`ahoo shihaabun saaqib
Isipo kuwa anaye nyakua kitu kidogo, na mara humfwatia kimondo kinacho ng'ara.
🎤 Rekodi yako:
37:11 🔁 0/5
فَٱسۡتَفۡتِهِمۡ أَهُمۡ أَشَدُّ خَلۡقًا أَم مَّنۡ خَلَقۡنَآۚ إِنَّا خَلَقۡنَٰهُم مِّن طِينٍ لَّازِبِۭ  ۝١١
Fastaftihim ahum ashaddu khalqan am man khalaqnaa; innaa khalaqnaahum min teenil laazib
Hebu waulize: Je! Wao ni wenye umbo gumu zaidi au hao wengine tulio waumba. Hakika Sisi tuliwaumba wao kwa udongo unao nata.
🎤 Rekodi yako:
37:12 🔁 0/5
بَلۡ عَجِبۡتَ وَيَسۡخَرُونَ  ۝١٢
Bal`ajibta wa yaskharoon
Bali unastaajabu, na wao wanafanya maskhara.
🎤 Rekodi yako:
37:13 🔁 0/5
وَإِذَا ذُكِّرُواْ لَا يَذۡكُرُونَ  ۝١٣
Wa izaa zukkiroo laa yazkuroon
Na wanapo kumbushwa hawakumbuki.
🎤 Rekodi yako:
37:14 🔁 0/5
وَإِذَا رَأَوۡاْ ءَايَةً يَسۡتَسۡخِرُونَ  ۝١٤
Wa izaa ra aw Aayatinw yastaskhiroon
Na wanapo ona Ishara, wanafanya maskhara.
🎤 Rekodi yako:
37:15 🔁 0/5
وَقَالُوٓاْ إِنۡ هَٰذَآ إِلَّا سِحۡرٌ مُّبِينٌ  ۝١٥
Wa qaalooo in haazaa illaa sihrum mubeen
Na husema: Haya si chochote ila ni uchawi tu ulio dhaahiri.
🎤 Rekodi yako:
37:16 🔁 0/5
أَءِذَا مِتۡنَا وَكُنَّا تُرَابًا وَعِظَٰمًا أَءِنَّا لَمَبۡعُوثُونَ  ۝١٦
A-izaa mitnaa wa kunnaa turaabanw wa `izaaman `ainnaa lamab`oosoon
Ati tukisha kufa na tukawa udongo na mifupa ndio kweli tutafufuliwa?
🎤 Rekodi yako:
37:17 🔁 0/5
أَوَءَابَآؤُنَا ٱلۡأَوَّلُونَ  ۝١٧
Awa aabaa`unal awwaloon
Hata baba zetu wa zamani?
🎤 Rekodi yako:
37:18 🔁 0/5
قُلۡ نَعَمۡ وَأَنتُمۡ دَٰخِرُونَ  ۝١٨
Qul na`am wa antum daakhiroon
Sema: Naam! Hali nanyi ni madhalili.
🎤 Rekodi yako:
37:19 🔁 0/5
فَإِنَّمَا هِيَ زَجۡرَةٌ وَٰحِدَةٌ فَإِذَا هُمۡ يَنظُرُونَ  ۝١٩
Fa innamaa hiya zajra tunw waahidatun fa izaa hum yanzuroon
Huko utapigwa ukelele mmoja tu! Na hapo ndio wataona!
🎤 Rekodi yako:
37:20 🔁 0/5
وَقَالُواْ يَٰوَيۡلَنَا هَٰذَا يَوۡمُ ٱلدِّينِ  ۝٢٠
Qa qaaloo yaa wailanaa haazaa Yawmud-Deen
Watasema: Ole wetu! Hii ndiyo Siku ya Malipo.
🎤 Rekodi yako:
37:21 🔁 0/5
هَٰذَا يَوۡمُ ٱلۡفَصۡلِ ٱلَّذِي كُنتُم بِهِۦ تُكَذِّبُونَ  ۝٢١
Haazaa Yawmul Faslil lazee kuntum bihee tukaziboon
Hii ndiyo Siku ya Hukumu mliyo kuwa mkiikadhibisha.
🎤 Rekodi yako:
37:22 🔁 0/5
۞ ٱحۡشُرُواْ ٱلَّذِينَ ظَلَمُواْ وَأَزۡوَٰجَهُمۡ وَمَا كَانُواْ يَعۡبُدُونَ  ۝٢٢
Uhshurul lazeena zalamoo wa azwaajahum wa maa kaanoo ya`budoon
Wakusanyeni walio dhulumu, na wake zao, na hao walio kuwa wakiwaabudu -
🎤 Rekodi yako:
37:23 🔁 0/5
مِن دُونِ ٱللَّهِ فَٱهۡدُوهُمۡ إِلَىٰ صِرَٰطِ ٱلۡجَحِيمِ  ۝٢٣
Min doonil laahi fahdoohum ilaa siraatil Jaheem
Badala ya Mwenyezi Mungu. Waongozeni njia ya Jahannamu!
🎤 Rekodi yako:
37:24 🔁 0/5
وَقِفُوهُمۡۖ إِنَّهُم مَّسۡـُٔولُونَ  ۝٢٤
Wa qifoohum innahum mas`ooloon
Na wasimamisheni. Hakika hao watasailiwa:
🎤 Rekodi yako:
37:25 🔁 0/5
مَا لَكُمۡ لَا تَنَاصَرُونَ  ۝٢٥
Maa lakum laa tanaasaroon
Mna nini? Mbona hamsaidiani?
🎤 Rekodi yako:
37:26 🔁 0/5
بَلۡ هُمُ ٱلۡيَوۡمَ مُسۡتَسۡلِمُونَ  ۝٢٦
Bal humul Yawma mustaslimoon
Bali hii leo, watasalimu amri.
🎤 Rekodi yako:
37:27 🔁 0/5
وَأَقۡبَلَ بَعۡضُهُمۡ عَلَىٰ بَعۡضٍ يَتَسَآءَلُونَ  ۝٢٧
Wa aqbala ba`duhum `alaa ba`diny yatasaaa`aloon
Watakabiliana wao kwa wao kuulizana.
🎤 Rekodi yako:
37:28 🔁 0/5
قَالُوٓاْ إِنَّكُمۡ كُنتُمۡ تَأۡتُونَنَا عَنِ ٱلۡيَمِينِ  ۝٢٨
Qaalooo innakum kuntum taatoonanaa `anil yameen
Watasema: Kwa hakika nyinyi mlikuwa mkitujia upande wa kulia.
🎤 Rekodi yako:
37:29 🔁 0/5
قَالُواْ بَل لَّمۡ تَكُونُواْ مُؤۡمِنِينَ  ۝٢٩
Qaaloo bal lam takoonoo mu`mineen
Watasema (wakubwa): Bali nyinyi wenyewe hamkuwa Waumini.
🎤 Rekodi yako:
37:30 🔁 0/5
وَمَا كَانَ لَنَا عَلَيۡكُم مِّن سُلۡطَٰنِۭۖ بَلۡ كُنتُمۡ قَوۡمًا طَٰغِينَ  ۝٣٠
Wa maa kaana lanaa `alaikum min sultaanim bal kuntum qawman taagheen
Sisi hatukuwa na mamlaka juu yenu, bali nyinyi wenyewe mlikuwa wapotovu.
🎤 Rekodi yako:
37:31 🔁 0/5
فَحَقَّ عَلَيۡنَا قَوۡلُ رَبِّنَآۖ إِنَّا لَذَآئِقُونَ  ۝٣١
Fahaqqa `alainaa qawlu Rabbinaaa innaa lazaaa`iqoon
Basi hukumu ya Mola wetu Mlezi imekwisha tuthibitikia. Hakika bila ya shaka tutaonja tu adhabu.
🎤 Rekodi yako:
37:32 🔁 0/5
فَأَغۡوَيۡنَٰكُمۡ إِنَّا كُنَّا غَٰوِينَ  ۝٣٢
Fa aghwainaakum innaa kunnaa ghaaween
Tulikupotezeni kwa sababu sisi wenyewe tulikuwa wapotovu.
🎤 Rekodi yako:
37:33 🔁 0/5
فَإِنَّهُمۡ يَوۡمَئِذٍ فِي ٱلۡعَذَابِ مُشۡتَرِكُونَ  ۝٣٣
Fa innahum Yawma`izin fil`azaabi mushtarikoon
Basi wao kwa hakika siku hiyo watashirikiana katika adhabu pamoja.
🎤 Rekodi yako:
37:34 🔁 0/5
إِنَّا كَذَٰلِكَ نَفۡعَلُ بِٱلۡمُجۡرِمِينَ  ۝٣٤
Innaa kazaalika naf`alu bil mujrimeen
Hivyo ndivyo tutakavyo wafanyia wakosefu.
🎤 Rekodi yako:
37:35 🔁 0/5
إِنَّهُمۡ كَانُوٓاْ إِذَا قِيلَ لَهُمۡ لَآ إِلَٰهَ إِلَّا ٱللَّهُ يَسۡتَكۡبِرُونَ  ۝٣٥
Innahum kaanooo izaa qeela lahum laaa ilaaha illal laahu yastakbiroon
Wao walipo kuwa wakiambiwa La ilaha illa 'Llahu Hapana mungu ila Mwenyezi Mungu tu, wakijivuna.
🎤 Rekodi yako:
37:36 🔁 0/5
وَيَقُولُونَ أَئِنَّا لَتَارِكُوٓاْ ءَالِهَتِنَا لِشَاعِرٍ مَّجۡنُونِۭ  ۝٣٦
Wa yaqooloona a`innaa lataarikooo aalihatinaa lishaa`irim majnoon
Na wakisema: Hivyo sisi tuiache miungu yetu kwa ajili ya huyu mtunga mashairi mwendawazimu?
🎤 Rekodi yako:
37:37 🔁 0/5
بَلۡ جَآءَ بِٱلۡحَقِّ وَصَدَّقَ ٱلۡمُرۡسَلِينَ  ۝٣٧
bal jaaa`a bilhaqqi wa saddaqal mursaleen
Bali huyu amekuja kwa Haki, na amewasadikisha Mitume.
🎤 Rekodi yako:
37:38 🔁 0/5
إِنَّكُمۡ لَذَآئِقُواْ ٱلۡعَذَابِ ٱلۡأَلِيمِ  ۝٣٨
Innakum lazaaa`iqul `azaabil aleem
Hakika nyinyi bila ya shaka mtaionja adhabu chungu.
🎤 Rekodi yako:
37:39 🔁 0/5
وَمَا تُجۡزَوۡنَ إِلَّا مَا كُنتُمۡ تَعۡمَلُونَ  ۝٣٩
Wa maa tujzawna illaa maa kuntum ta`maloon
Wala hamlipwi ila hayo mliyo kuwa mkiyafanya.
🎤 Rekodi yako:
37:40 🔁 0/5
إِلَّا عِبَادَ ٱللَّهِ ٱلۡمُخۡلَصِينَ  ۝٤٠
Illaa `ibaadal laahil mukhlaseen
Isipo kuwa waja wa Mwenyezi Mungu walio khitariwa.
🎤 Rekodi yako:
37:41 🔁 0/5
أُوْلَٰٓئِكَ لَهُمۡ رِزۡقٌ مَّعۡلُومٌ  ۝٤١
Ulaaa`ika lahum rizqum ma`loom
Hao ndio watakao pata riziki maalumu,
🎤 Rekodi yako:
37:42 🔁 0/5
فَوَٰكِهُ وَهُم مُّكۡرَمُونَ  ۝٤٢
Fa waakihu wa hum mukramoon
Matunda, nao watahishimiwa.
🎤 Rekodi yako:
37:43 🔁 0/5
فِي جَنَّٰتِ ٱلنَّعِيمِ  ۝٤٣
Fee jannaatin Na`eem
Katika Bustani za neema.
🎤 Rekodi yako:
37:44 🔁 0/5
عَلَىٰ سُرُرٍ مُّتَقَٰبِلِينَ  ۝٤٤
Alaa sururim mutaqaa bileen
Wako juu ya viti wamekabiliana.
🎤 Rekodi yako:
37:45 🔁 0/5
يُطَافُ عَلَيۡهِم بِكَأۡسٍ مِّن مَّعِينِۭ  ۝٤٥
Yutaafu `alaihim bikaasim mim ma`een
Wanazungushiwa kikombe chenye kinywaji cha chemchem
🎤 Rekodi yako:
37:46 🔁 0/5
بَيۡضَآءَ لَذَّةٍ لِّلشَّٰرِبِينَ  ۝٤٦
Baidaaa`a laz zatil lish shaaribeen
Kinywaji cheupe, kitamu kwa wanywao.
🎤 Rekodi yako:
37:47 🔁 0/5
لَا فِيهَا غَوۡلٌ وَلَا هُمۡ عَنۡهَا يُنزَفُونَ  ۝٤٧
Laa feehaa ghawlunw wa laa hum `anhaa yunzafoon
Hakina madhara, wala hakiwaleweshi.
🎤 Rekodi yako:
37:48 🔁 0/5
وَعِندَهُمۡ قَٰصِرَٰتُ ٱلطَّرۡفِ عِينٌ  ۝٤٨
Wa `indahum qaasiraatut tarfi `een
Na watakuwa nao wanawake wenye macho ya staha mazuri.
🎤 Rekodi yako:
37:49 🔁 0/5
كَأَنَّهُنَّ بَيۡضٌ مَّكۡنُونٌ  ۝٤٩
Ka annahunna baidum maknoon
Hao wanawake kama mayai yaliyo hifadhika.
🎤 Rekodi yako:
37:50 🔁 0/5
فَأَقۡبَلَ بَعۡضُهُمۡ عَلَىٰ بَعۡضٍ يَتَسَآءَلُونَ  ۝٥٠
Fa aqbala ba`duhum `alaa badiny yatasaaa `aloon
Waingie kuulizana wenyewe kwa wenyewe.
🎤 Rekodi yako:
37:51 🔁 0/5
قَالَ قَآئِلٌ مِّنۡهُمۡ إِنِّي كَانَ لِي قَرِينٌ  ۝٥١
Qaala qaaa`ilum minhum innee kaana lee qareen
Aseme msemaji mmoja miongoni mwao: Hakika mimi nalikuwa na rafiki
🎤 Rekodi yako:
37:52 🔁 0/5
يَقُولُ أَءِنَّكَ لَمِنَ ٱلۡمُصَدِّقِينَ  ۝٥٢
Yaqoolu a`innnaka laminal musaddiqeen
Aliye kuwa akinambia: Hivyo wewe ni katika wanao sadiki
🎤 Rekodi yako:
37:53 🔁 0/5
أَءِذَا مِتۡنَا وَكُنَّا تُرَابًا وَعِظَٰمًا أَءِنَّا لَمَدِينُونَ  ۝٥٣
A-izaa mitnaa wa kunnaa turaabanw wa `izaaman `ainnaa lamadeenoon
Ati tukisha kufa tukawa udongo na mafupa, ndio tutalipwa na kuhisabiwa?
🎤 Rekodi yako:
37:54 🔁 0/5
قَالَ هَلۡ أَنتُم مُّطَّلِعُونَ  ۝٥٤
Qaala hal antum muttali`oon
Atasema: Je! Nyie mnawaona?
🎤 Rekodi yako:
37:55 🔁 0/5
فَٱطَّلَعَ فَرَءَاهُ فِي سَوَآءِ ٱلۡجَحِيمِ  ۝٥٥
Fattala`a fara aahu fee sawaaa`il Jaheem
Basi atachungulia amwone katikati ya Jahannamu.
🎤 Rekodi yako:
37:56 🔁 0/5
قَالَ تَٱللَّهِ إِن كِدتَّ لَتُرۡدِينِ  ۝٥٦
Qaala tallaahi in kitta laturdeen
Atasema: Wallahi! Ulikaribia kunipoteza.
🎤 Rekodi yako:
37:57 🔁 0/5
وَلَوۡلَا نِعۡمَةُ رَبِّي لَكُنتُ مِنَ ٱلۡمُحۡضَرِينَ  ۝٥٧
Wa law laa ni`matu Rabbee lakuntu minal muhdareen
Na lau kuwa si neema ya Mola wangu Mlezi bila ya shaka ningeli kuwa miongoni mwa walio hudhurishwa.
🎤 Rekodi yako:
37:58 🔁 0/5
أَفَمَا نَحۡنُ بِمَيِّتِينَ  ۝٥٨
Afamaa nahnu bimaiyiteen
Je! Sisi hatutakufa,
🎤 Rekodi yako:
37:59 🔁 0/5
إِلَّا مَوۡتَتَنَا ٱلۡأُولَىٰ وَمَا نَحۡنُ بِمُعَذَّبِينَ  ۝٥٩
Illa mawtatanal oola wa maa nahnu bimu`azzabeen
Isipo kuwa kifo chetu cha kwanza? Wala sisi hatutaadhibiwa.
🎤 Rekodi yako:
37:60 🔁 0/5
إِنَّ هَٰذَا لَهُوَ ٱلۡفَوۡزُ ٱلۡعَظِيمُ  ۝٦٠
Inna haazaa falya`ma lil`aamiloon
Hakika huku bila ya shaka ndiko kufuzu kukubwa.
🎤 Rekodi yako:
37:61 🔁 0/5
لِمِثۡلِ هَٰذَا فَلۡيَعۡمَلِ ٱلۡعَٰمِلُونَ  ۝٦١
Limisli haaza falya`ma lil `aamiloon
Kwa mfano wa haya nawatende watendao.
🎤 Rekodi yako:
37:62 🔁 0/5
أَذَٰلِكَ خَيۡرٌ نُّزُلًا أَمۡ شَجَرَةُ ٱلزَّقُّومِ  ۝٦٢
Azaalika khairun nuzulan am shajaratuz Zaqqom
Je! Kukaribishwa hivi si ndio bora, au mti wa Zaqqum?
🎤 Rekodi yako:
37:63 🔁 0/5
إِنَّا جَعَلۡنَٰهَا فِتۡنَةً لِّلظَّٰلِمِينَ  ۝٦٣
Innaa ja`alnaahaa fitnatal lizzaalimeen
Hakika Sisi tumeufanya huo kuwa ni mateso kwa walio dhulumu.
🎤 Rekodi yako:
37:64 🔁 0/5
إِنَّهَا شَجَرَةٌ تَخۡرُجُ فِيٓ أَصۡلِ ٱلۡجَحِيمِ  ۝٦٤
Innahaa shajaratun takhruju feee aslil Jaheem
Hakika huo ni mti unao toka katikati ya Jahannamu.
🎤 Rekodi yako:
37:65 🔁 0/5
طَلۡعُهَا كَأَنَّهُۥ رُءُوسُ ٱلشَّيَٰطِينِ  ۝٦٥
Tal`uhaa ka annahoo ru`oosush Shayaateen
Mashada ya matunda yake kama kwamba vichwa vya mashet'ani.
🎤 Rekodi yako:
37:66 🔁 0/5
فَإِنَّهُمۡ لَأٓكِلُونَ مِنۡهَا فَمَالِـُٔونَ مِنۡهَا ٱلۡبُطُونَ  ۝٦٦
Fa innahum la aakiloona minhaa famaali`oona minhal butoon
Basi hakika bila ya shaka hao watayala hayo, na wajaze matumbo.
🎤 Rekodi yako:
37:67 🔁 0/5
ثُمَّ إِنَّ لَهُمۡ عَلَيۡهَا لَشَوۡبًا مِّنۡ حَمِيمٍ  ۝٦٧
Summa inna lahum `alaihaa lashawbam min hameem
Kisha juu yake wanyweshwe mchanganyo wa maji yamoto yaliyo chemka.
🎤 Rekodi yako:
37:68 🔁 0/5
ثُمَّ إِنَّ مَرۡجِعَهُمۡ لَإِلَى ٱلۡجَحِيمِ  ۝٦٨
Summa inna marji`ahum la ilal Jaheem
Kisha hakika marejeo yao bila ya shaka yatakuwa kwenye Jahannamu.
🎤 Rekodi yako:
37:69 🔁 0/5
إِنَّهُمۡ أَلۡفَوۡاْ ءَابَآءَهُمۡ ضَآلِّينَ  ۝٦٩
Innahum alfaw aabaaa`ahum daaalleen
Hakika waliwakuta baba zao wamepotea.
🎤 Rekodi yako:
37:70 🔁 0/5
فَهُمۡ عَلَىٰٓ ءَاثَٰرِهِمۡ يُهۡرَعُونَ  ۝٧٠
Fahum `alaa aasaarihim yuhra`oon
Na wao wakafanya haraka kufuata nyayo zao.
🎤 Rekodi yako:
37:71 🔁 0/5
وَلَقَدۡ ضَلَّ قَبۡلَهُمۡ أَكۡثَرُ ٱلۡأَوَّلِينَ  ۝٧١
Wa laqad dalla qablahum aksarul awwaleen
Na bila ya shaka walikwisha potea kabla yao wengi wa watu wa zamani.
🎤 Rekodi yako:
37:72 🔁 0/5
وَلَقَدۡ أَرۡسَلۡنَا فِيهِم مُّنذِرِينَ  ۝٧٢
Wa laqad arsalnaa feehim munzireen
Na Sisi hakika tuliwapelekea waonyaji.
🎤 Rekodi yako:
37:73 🔁 0/5
فَٱنظُرۡ كَيۡفَ كَانَ عَٰقِبَةُ ٱلۡمُنذَرِينَ  ۝٧٣
Fanzur kaifa kaana `aaqibatul munzareen
Basi hebu angalia ulikuwaje mwisho wa walio onywa.
🎤 Rekodi yako:
37:74 🔁 0/5
إِلَّا عِبَادَ ٱللَّهِ ٱلۡمُخۡلَصِينَ  ۝٧٤
Illaa `ibaadal laahil mukhlaseen
Isipo kuwa waja wa Mwenyezi Mungu walio khitariwa.
🎤 Rekodi yako:
37:75 🔁 0/5
وَلَقَدۡ نَادَىٰنَا نُوحٌ فَلَنِعۡمَ ٱلۡمُجِيبُونَ  ۝٧٥
Wa laqad naadaanaa Noohun falani`mal mujeeboon
Na hakika Nuhu alitwita, na Sisi ni bora wa waitikiaji.
🎤 Rekodi yako:
37:76 🔁 0/5
وَنَجَّيۡنَٰهُ وَأَهۡلَهُۥ مِنَ ٱلۡكَرۡبِ ٱلۡعَظِيمِ  ۝٧٦
Wa jajainaahu wa ahlahoo minal karbil `azeem
Na tulimwokoa yeye na ahali zake kutokana na msiba mkubwa.
🎤 Rekodi yako:
37:77 🔁 0/5
وَجَعَلۡنَا ذُرِّيَّتَهُۥ هُمُ ٱلۡبَاقِينَ  ۝٧٧
Wa ja`alnaa zurriyyatahoo hummul baaqeen
Na tuliwajaalia dhuriya zake ndio wenye kubakia.
🎤 Rekodi yako:
37:78 🔁 0/5
وَتَرَكۡنَا عَلَيۡهِ فِي ٱلۡأٓخِرِينَ  ۝٧٨
Wa taraknaa `alaihi fil aakhireen
Na tukamwachia (sifa njema) kwa walio kuja baadaye.
🎤 Rekodi yako:
37:79 🔁 0/5
سَلَٰمٌ عَلَىٰ نُوحٍ فِي ٱلۡعَٰلَمِينَ  ۝٧٩
Salaamun `alaa Noohin fil `aalameen
Iwe salama kwa Nuhu ulimwenguni kote!
🎤 Rekodi yako:
37:80 🔁 0/5
إِنَّا كَذَٰلِكَ نَجۡزِي ٱلۡمُحۡسِنِينَ  ۝٨٠
Innaa kazaalika najzil muhsineen
Kwa hakika hivi ndivyo tunavyo walipa wanao fanya mema.
🎤 Rekodi yako:
37:81 🔁 0/5
إِنَّهُۥ مِنۡ عِبَادِنَا ٱلۡمُؤۡمِنِينَ  ۝٨١
Innahoo min `ibaadinal mu`mineen
Hakika yeye ni katika waja wetu walio amini.
🎤 Rekodi yako:
37:82 🔁 0/5
ثُمَّ أَغۡرَقۡنَا ٱلۡأٓخَرِينَ  ۝٨٢
Summa aghraqnal aakhareen
Kisha tukawazamisha wale wengine.
🎤 Rekodi yako:
37:83 🔁 0/5
۞ وَإِنَّ مِن شِيعَتِهِۦ لَإِبۡرَٰهِيمَ  ۝٨٣
Wa ina min shee`atihee la Ibraaheem
Na hakika Ibrahim alikuwa katika kundi lake,
🎤 Rekodi yako:
37:84 🔁 0/5
إِذۡ جَآءَ رَبَّهُۥ بِقَلۡبٍ سَلِيمٍ  ۝٨٤
Iz jaaa`a Rabbahoo bi qalbin saleem
Alipo mjia Mola wake Mlezi kwa moyo mzima.
🎤 Rekodi yako:
37:85 🔁 0/5
إِذۡ قَالَ لِأَبِيهِ وَقَوۡمِهِۦ مَاذَا تَعۡبُدُونَ  ۝٨٥
Iz qaala li abeehi wa qawmihee maazaa ta`budoon
Alimwambia baba yake na watu wake: Mnaabudu nini?
🎤 Rekodi yako:
37:86 🔁 0/5
أَئِفۡكًا ءَالِهَةً دُونَ ٱللَّهِ تُرِيدُونَ  ۝٨٦
A`ifkan aalihatan doonal laahi tureedoon
Kwa kuzua tu mnataka miungu mingine badala ya Mwenyezi Mungu?
🎤 Rekodi yako:
37:87 🔁 0/5
فَمَا ظَنُّكُم بِرَبِّ ٱلۡعَٰلَمِينَ  ۝٨٧
Famaa zannukum bi Rabbil`aalameen
Mnamdhania nini Mola Mlezi wa walimwengu wote?
🎤 Rekodi yako:
37:88 🔁 0/5
فَنَظَرَ نَظۡرَةً فِي ٱلنُّجُومِ  ۝٨٨
Fanazara nazratan finnujoom
Kisha akapiga jicho kutazama nyota.
🎤 Rekodi yako:
37:89 🔁 0/5
فَقَالَ إِنِّي سَقِيمٌ  ۝٨٩
Faqaala inee saqeem
Akasema: Hakika mimi ni mgonjwa!
🎤 Rekodi yako:
37:90 🔁 0/5
فَتَوَلَّوۡاْ عَنۡهُ مُدۡبِرِينَ  ۝٩٠
Fatawallaw `anhu mudbireen
Nao wakamwacha, wakampa kisogo.
🎤 Rekodi yako:
37:91 🔁 0/5
فَرَاغَ إِلَىٰٓ ءَالِهَتِهِمۡ فَقَالَ أَلَا تَأۡكُلُونَ  ۝٩١
Faraagha ilaaa aalihatihim faqaala alaa taakuloon
Basi akaiendea miungu yao kwa siri, akaiambia: Mbona hamli?
🎤 Rekodi yako:
37:92 🔁 0/5
مَا لَكُمۡ لَا تَنطِقُونَ  ۝٩٢
Maa lakum laa tantiqoon
Mna nini hata hamsemi?
🎤 Rekodi yako:
37:93 🔁 0/5
فَرَاغَ عَلَيۡهِمۡ ضَرۡبَۢا بِٱلۡيَمِينِ  ۝٩٣
Faraagha `alaihim darbam bilyameen
Kisha akaigeukia kuipiga kwa mkono wa kulia.
🎤 Rekodi yako:
37:94 🔁 0/5
فَأَقۡبَلُوٓاْ إِلَيۡهِ يَزِفُّونَ  ۝٩٤
Fa aqbalooo ilaihi yaziffoon
Basi wakamjia upesi upesi.
🎤 Rekodi yako:
37:95 🔁 0/5
قَالَ أَتَعۡبُدُونَ مَا تَنۡحِتُونَ  ۝٩٥
Qaala ata`budoona maa tanhitoon
Akasema: Hivyo mnaviabudu vitu mnavyo vichonga wenyewe?
🎤 Rekodi yako:
37:96 🔁 0/5
وَٱللَّهُ خَلَقَكُمۡ وَمَا تَعۡمَلُونَ  ۝٩٦
Wallaahu khalaqakum wa maa ta`maloon
Na hali Mwenyezi Mungu ndiye aliye kuumbeni nyinyi na hivyo mnavyo vifanya!
🎤 Rekodi yako:
37:97 🔁 0/5
قَالُواْ ٱبۡنُواْ لَهُۥ بُنۡيَٰنًا فَأَلۡقُوهُ فِي ٱلۡجَحِيمِ  ۝٩٧
Qaalub noo lahoo bun yaanan fa alqoohu fil jaheem
Wakasema: Mjengeeni jengo, na kisha mtupeni motoni humo!
🎤 Rekodi yako:
37:98 🔁 0/5
فَأَرَادُواْ بِهِۦ كَيۡدًا فَجَعَلۡنَٰهُمُ ٱلۡأَسۡفَلِينَ  ۝٩٨
Fa araadoo bihee kaidan faja `alnaahumul asfaleen
Basi walitaka kumfanyia vitimbi, lakini tukawafanya wao ndio wa chini.
🎤 Rekodi yako:
37:99 🔁 0/5
وَقَالَ إِنِّي ذَاهِبٌ إِلَىٰ رَبِّي سَيَهۡدِينِ  ۝٩٩
Wa qaala innee zaahibun ilaa Rabbee sa yahdeen
Na akasema: Hakika mimi nahama, nakwenda kwa Mola wangu Mlezi; Yeye ataniongoa.
🎤 Rekodi yako:
37:100 🔁 0/5
رَبِّ هَبۡ لِي مِنَ ٱلصَّٰلِحِينَ  ۝١٠٠
Rabbi hab lee minas saaliheen
Ewe Mola wangu Mlezi! Nitunukie aliye miongoni mwa watenda mema.
🎤 Rekodi yako:
37:101 🔁 0/5
فَبَشَّرۡنَٰهُ بِغُلَٰمٍ حَلِيمٍ  ۝١٠١
Fabashsharnaahu bighulaamin haleem
Basi tukambashiria mwana aliye mpole.
🎤 Rekodi yako:
37:102 🔁 0/5
فَلَمَّا بَلَغَ مَعَهُ ٱلسَّعۡيَ قَالَ يَٰبُنَيَّ إِنِّيٓ أَرَىٰ فِي ٱلۡمَنَامِ أَنِّيٓ أَذۡبَحُكَ فَٱنظُرۡ مَاذَا تَرَىٰۚ قَالَ يَٰٓأَبَتِ ٱفۡعَلۡ مَا تُؤۡمَرُۖ سَتَجِدُنِيٓ إِن شَآءَ ٱللَّهُ مِنَ ٱلصَّٰبِرِينَ  ۝١٠٢
Falamma balagha ma`a hus sa`ya qaala yaa buniya inneee araa fil manaami anneee azbahuka fanzur maazaa taraa; qaala yaaa abatif `al maa tu`maru satajidunee in shaaa`allaahu minas saabireen
Basi alipo fika makamo ya kwenda na kurudi pamoja naye, alimwambia: Ewe mwanangu! Hakika mimi nimeona usingizini kuwa ninakuchinja. Basi angalia wewe, waonaje? Akasema: Ewe baba yangu! Tenda unavyo amrishwa, utanikuta mimi, Inshallah, katika wanao subiri.
🎤 Rekodi yako:
37:103 🔁 0/5
فَلَمَّآ أَسۡلَمَا وَتَلَّهُۥ لِلۡجَبِينِ  ۝١٠٣
Falammaaa aslamaa wa tallahoo liljabeen
Basi wote wawili walipo jisalimisha, na akamlaza juu ya kipaji.
🎤 Rekodi yako:
37:104 🔁 0/5
وَنَٰدَيۡنَٰهُ أَن يَٰٓإِبۡرَٰهِيمُ  ۝١٠٤
Wa naadainaahu ai yaaaa Ibraheem
Tulimwita: Ewe Ibrahim!
🎤 Rekodi yako:
37:105 🔁 0/5
قَدۡ صَدَّقۡتَ ٱلرُّءۡيَآۚ إِنَّا كَذَٰلِكَ نَجۡزِي ٱلۡمُحۡسِنِينَ  ۝١٠٥
Qad saddaqtar ru`yaa; innaa kazaalika najzil muhsineen
Umekwisha itimiliza ndoto. Hakika hivi ndivyo tunavyo walipa wanao tenda mema.
🎤 Rekodi yako:
37:106 🔁 0/5
إِنَّ هَٰذَا لَهُوَ ٱلۡبَلَٰٓؤُاْ ٱلۡمُبِينُ  ۝١٠٦
Inna haazaa lahuwal balaaa`ul mubeen
Hakika haya ni majaribio yaliyo dhaahiri.
🎤 Rekodi yako:
37:107 🔁 0/5
وَفَدَيۡنَٰهُ بِذِبۡحٍ عَظِيمٍ  ۝١٠٧
Wa fadainaahu bizibhin `azeem
Basi tukamtolea fidia kwa dhabihu mtukufu.
🎤 Rekodi yako:
37:108 🔁 0/5
وَتَرَكۡنَا عَلَيۡهِ فِي ٱلۡأٓخِرِينَ  ۝١٠٨
Wa taraknaa `alaihi fil aakhireen
Na tukamwachia (sifa njema) kwa watu walio kuja baadaye.
🎤 Rekodi yako:
37:109 🔁 0/5
سَلَٰمٌ عَلَىٰٓ إِبۡرَٰهِيمَ  ۝١٠٩
Salaamun `alaaa Ibraaheem
Iwe salama kwa Ibrahim!
🎤 Rekodi yako:
37:110 🔁 0/5
كَذَٰلِكَ نَجۡزِي ٱلۡمُحۡسِنِينَ  ۝١١٠
Kazaalika najzil muhsineen
Hivi ndivyo tunavyo walipa wanao fanya mema.
🎤 Rekodi yako:
37:111 🔁 0/5
إِنَّهُۥ مِنۡ عِبَادِنَا ٱلۡمُؤۡمِنِينَ  ۝١١١
Innahoo min `ibaadinal mu`mineen
Hakika yeye ni katika waja wetu walio amini.
🎤 Rekodi yako:
37:112 🔁 0/5
وَبَشَّرۡنَٰهُ بِإِسۡحَٰقَ نَبِيًّا مِّنَ ٱلصَّٰلِحِينَ  ۝١١٢
Wa bashsharnaahu bi Ishaaqa Nabiyayam minas saaliheen
Na tukambashiria kuzaliwa Is-haqa, naye ni Nabii miongoni mwa watu wema.
🎤 Rekodi yako:
37:113 🔁 0/5
وَبَٰرَكۡنَا عَلَيۡهِ وَعَلَىٰٓ إِسۡحَٰقَۚ وَمِن ذُرِّيَّتِهِمَا مُحۡسِنٌ وَظَالِمٌ لِّنَفۡسِهِۦ مُبِينٌ  ۝١١٣
Wa baaraknaa `alaihi wa `alaaa Ishaaq; wa min zurriyya tihimaa muhsinunw wa zaalimul linafshihee mubeen
Na tukambarikia yeye na Is-haqa. Na miongoni mwa dhuriya zao walitokea wema na wenye kudhulumu nafsi zao waziwazi.
🎤 Rekodi yako:
37:114 🔁 0/5
وَلَقَدۡ مَنَنَّا عَلَىٰ مُوسَىٰ وَهَٰرُونَ  ۝١١٤
Wa laqad mananna alaa Moosaa wa Haaroon
Na kwa hakika tuliwafanyia hisani Musa na Haruni.
🎤 Rekodi yako:
37:115 🔁 0/5
وَنَجَّيۡنَٰهُمَا وَقَوۡمَهُمَا مِنَ ٱلۡكَرۡبِ ٱلۡعَظِيمِ  ۝١١٥
Wa najjainaahumaa wa qawmahumaa minal karbil `azeem
Na tukawaokoa wao na watu wao kutokana na dhiki kubwa.
🎤 Rekodi yako:
37:116 🔁 0/5
وَنَصَرۡنَٰهُمۡ فَكَانُواْ هُمُ ٱلۡغَٰلِبِينَ  ۝١١٦
Wa nasarnaahum fakaanoo humul ghaalibeen
Na tukawanusuru; na wakawa wao ndio wenye kushinda.
🎤 Rekodi yako:
37:117 🔁 0/5
وَءَاتَيۡنَٰهُمَا ٱلۡكِتَٰبَ ٱلۡمُسۡتَبِينَ  ۝١١٧
Wa aatainaahumal Kitaabal mustabeen
Na tukawapa wawili hao Kitabu kinacho bainisha.
🎤 Rekodi yako:
37:118 🔁 0/5
وَهَدَيۡنَٰهُمَا ٱلصِّرَٰطَ ٱلۡمُسۡتَقِيمَ  ۝١١٨
Wa hadainaahumus Siraatal Mustaqeem
Na tukawaongoa kwenye Njia Iliyo Nyooka.
🎤 Rekodi yako:
37:119 🔁 0/5
وَتَرَكۡنَا عَلَيۡهِمَا فِي ٱلۡأٓخِرِينَ  ۝١١٩
Wa taraknaa `alaihimaa fil aakhireen
Na tukawaachia (sifa njema) katika watu walio kuja baadaye.
🎤 Rekodi yako:
37:120 🔁 0/5
سَلَٰمٌ عَلَىٰ مُوسَىٰ وَهَٰرُونَ  ۝١٢٠
Salaamun `alaa Moosaa wa Haaroon
Iwe salama kwa Musa na Haruni!
🎤 Rekodi yako:
37:121 🔁 0/5
إِنَّا كَذَٰلِكَ نَجۡزِي ٱلۡمُحۡسِنِينَ  ۝١٢١
Innaa kazaalika najzil muhsineen
Hakika hivyo ndivyo tunavyo walipa walio wema.
🎤 Rekodi yako:
37:122 🔁 0/5
إِنَّهُمَا مِنۡ عِبَادِنَا ٱلۡمُؤۡمِنِينَ  ۝١٢٢
Innahumaa min `ibaadinal mu`mineen
Hakika wawili hao ni katika waja wetu walio amini.
🎤 Rekodi yako:
37:123 🔁 0/5
وَإِنَّ إِلۡيَاسَ لَمِنَ ٱلۡمُرۡسَلِينَ  ۝١٢٣
Wa inna Ilyaasa laminal mursaleen
Na hakika Ilyas bila ya shaka alikuwa miongoni mwa Mitume.
🎤 Rekodi yako:
37:124 🔁 0/5
إِذۡ قَالَ لِقَوۡمِهِۦٓ أَلَا تَتَّقُونَ  ۝١٢٤
Iz qaala liqawmiheee alaa tattaqoon
Alipo waambia watu wake: Hamwogopi?
🎤 Rekodi yako:
37:125 🔁 0/5
أَتَدۡعُونَ بَعۡلًا وَتَذَرُونَ أَحۡسَنَ ٱلۡخَٰلِقِينَ  ۝١٢٥
Atad`oona Ba`lanw wa tazaroona ahsanal khaaliqeen
Mnamwomba Baa'li na mnamwacha Mbora wa waumbaji,
🎤 Rekodi yako:
37:126 🔁 0/5
ٱللَّهَ رَبَّكُمۡ وَرَبَّ ءَابَآئِكُمُ ٱلۡأَوَّلِينَ  ۝١٢٦
Allaaha Rabbakum wa Rabba aabaaa`ikumul awwaleen
Mwenyezi Mungu, Mola Mlezi wenu na Mola Mlezi wa baba zenu wa zamani?
🎤 Rekodi yako:
37:127 🔁 0/5
فَكَذَّبُوهُ فَإِنَّهُمۡ لَمُحۡضَرُونَ  ۝١٢٧
Fakazzaboohu fa inna hum lamuhdaroon
Wakamkadhibisha. Basi kwa hakika watahudhurishwa;
🎤 Rekodi yako:
37:128 🔁 0/5
إِلَّا عِبَادَ ٱللَّهِ ٱلۡمُخۡلَصِينَ  ۝١٢٨
Illaa `ibaadal laahil mukhlaseen
Isipo kuwa waja wa Mwenyezi Mungu walio safishwa.
🎤 Rekodi yako:
37:129 🔁 0/5
وَتَرَكۡنَا عَلَيۡهِ فِي ٱلۡأٓخِرِينَ  ۝١٢٩
Wa taraknaa `alaihi fil aakhireen
Na tumemwachia (sifa nzuri) kwa walio kuja baadaye.
🎤 Rekodi yako:
37:130 🔁 0/5
سَلَٰمٌ عَلَىٰٓ إِلۡ يَاسِينَ  ۝١٣٠
Salaamun `alaaa Ilyaaseen
Iwe salama kwa Ilyas.
🎤 Rekodi yako:
37:131 🔁 0/5
إِنَّا كَذَٰلِكَ نَجۡزِي ٱلۡمُحۡسِنِينَ  ۝١٣١
Innaa kazaalika najzil muhsineen
Hakika hivyo ndivyo tunavyo walipa walio wema.
🎤 Rekodi yako:
37:132 🔁 0/5
إِنَّهُۥ مِنۡ عِبَادِنَا ٱلۡمُؤۡمِنِينَ  ۝١٣٢
Innahoo min `ibaadinal mu`mineen
Hakika yeye ni katika waja wetu walio amini.
🎤 Rekodi yako:
37:133 🔁 0/5
وَإِنَّ لُوطًا لَّمِنَ ٱلۡمُرۡسَلِينَ  ۝١٣٣
Wa inna Lootal laminal mursaleen
Na hakika Lut'i bila ya shaka ni miongoni mwa Mitume.
🎤 Rekodi yako:
37:134 🔁 0/5
إِذۡ نَجَّيۡنَٰهُ وَأَهۡلَهُۥٓ أَجۡمَعِينَ  ۝١٣٤
Iz najjainaahu wa ahlahooo ajma`een
Tulipo mwokoa yeye na ahali zake wote,
🎤 Rekodi yako:
37:135 🔁 0/5
إِلَّا عَجُوزًا فِي ٱلۡغَٰبِرِينَ  ۝١٣٥
Illaa `ajoozan fil ghaabireen
Isipo kuwa mwanamke mkongwe katika wale walio bakia nyuma.
🎤 Rekodi yako:
37:136 🔁 0/5
ثُمَّ دَمَّرۡنَا ٱلۡأٓخَرِينَ  ۝١٣٦
Summa dammarnal aakhareen
Kisha tukawaangamiza wale wengineo.
🎤 Rekodi yako:
37:137 🔁 0/5
وَإِنَّكُمۡ لَتَمُرُّونَ عَلَيۡهِم مُّصۡبِحِينَ  ۝١٣٧
Wa innakum latamurroona `alaihim musbiheen
Na hakika nyinyi mnawapitia wakati wa asubuhi,
🎤 Rekodi yako:
37:138 🔁 0/5
وَبِٱلَّيۡلِۚ أَفَلَا تَعۡقِلُونَ  ۝١٣٨
Wa billail; afalaa ta`qiloon
Na usiku. Basi je! Hamyatii akilini?
🎤 Rekodi yako:
37:139 🔁 0/5
وَإِنَّ يُونُسَ لَمِنَ ٱلۡمُرۡسَلِينَ  ۝١٣٩
Wa inna Yoonusa laminal mursaleen
Na hakika Yunus alikuwa miongoni mwa Mitume.
🎤 Rekodi yako:
37:140 🔁 0/5
إِذۡ أَبَقَ إِلَى ٱلۡفُلۡكِ ٱلۡمَشۡحُونِ  ۝١٤٠
Iz abaqa ilal fulkil mash hoon
Alipo kimbia katika jahazi lilio sheheni.
🎤 Rekodi yako:
37:141 🔁 0/5
فَسَاهَمَ فَكَانَ مِنَ ٱلۡمُدۡحَضِينَ  ۝١٤١
Fasaahama fakaana minal mudhadeen
Akaingia katika kupigiwa kura, na akawa katika walio shindwa.
🎤 Rekodi yako:
37:142 🔁 0/5
فَٱلۡتَقَمَهُ ٱلۡحُوتُ وَهُوَ مُلِيمٌ  ۝١٤٢
Faltaqamahul hootu wa huwa muleem
Samaki akammeza hali ya kuwa ni mwenye kulaumiwa.
🎤 Rekodi yako:
37:143 🔁 0/5
فَلَوۡلَآ أَنَّهُۥ كَانَ مِنَ ٱلۡمُسَبِّحِينَ  ۝١٤٣
Falaw laaa annahoo kaana minal musabbiheen
Na ingeli kuwa hakuwa katika wanao mtakasa Mwenyezi Mungu,
🎤 Rekodi yako:
37:144 🔁 0/5
لَلَبِثَ فِي بَطۡنِهِۦٓ إِلَىٰ يَوۡمِ يُبۡعَثُونَ  ۝١٤٤
Lalabisa fee batniheee ilaa Yawmi yub`asoon
Bila ya shaka angeli kaa ndani yake mpaka siku ya kufufuliwa.
🎤 Rekodi yako:
37:145 🔁 0/5
۞ فَنَبَذۡنَٰهُ بِٱلۡعَرَآءِ وَهُوَ سَقِيمٌ  ۝١٤٥
Fanabaznaahu bil`araaa`i wa huwa saqeem
Lakini tulimtupa ufukweni patupu, hali yu mgonjwa.
🎤 Rekodi yako:
37:146 🔁 0/5
وَأَنۢبَتۡنَا عَلَيۡهِ شَجَرَةً مِّن يَقۡطِينٍ  ۝١٤٦
Wa ambatnaa `alaihi shajaratam mai yaqteen
Na tukauotesha juu yake mmea wa kabila ya mung'unye.
🎤 Rekodi yako:
37:147 🔁 0/5
وَأَرۡسَلۡنَٰهُ إِلَىٰ مِاْئَةِ أَلۡفٍ أَوۡ يَزِيدُونَ  ۝١٤٧
Wa arsalnaahu ilaa mi`ati alfin aw yazeedoon
Na tulimtuma kwa watu laki moja au zaidi.
🎤 Rekodi yako:
37:148 🔁 0/5
فَـَٔامَنُواْ فَمَتَّعۡنَٰهُمۡ إِلَىٰ حِينٍ  ۝١٤٨
Fa aamanoo famatta` naahum ilaa heen
Basi wakaamini, na tukawastarehesha kwa muda.
🎤 Rekodi yako:
37:149 🔁 0/5
فَٱسۡتَفۡتِهِمۡ أَلِرَبِّكَ ٱلۡبَنَاتُ وَلَهُمُ ٱلۡبَنُونَ  ۝١٤٩
Fastaftihim ali Rabbikal banaatu wa lahumul banoon
Basi waulize: Ati Mola wako Mlezi ndiye mwenye watoto wa kike, na wao wanao watoto wa kiume?
🎤 Rekodi yako:
37:150 🔁 0/5
أَمۡ خَلَقۡنَا ٱلۡمَلَٰٓئِكَةَ إِنَٰثًا وَهُمۡ شَٰهِدُونَ  ۝١٥٠
Am khalaqnal malaaa`i kata inaasanw wa hm shaahidoon
Au tumewaumba Malaika kuwa ni wanawake, na wao wakashuhudia?
🎤 Rekodi yako:
37:151 🔁 0/5
أَلَآ إِنَّهُم مِّنۡ إِفۡكِهِمۡ لَيَقُولُونَ  ۝١٥١
Alaaa innahum min ifkihim la yaqooloon
Ati ni kwa uzushi wao ndio wanasema:
🎤 Rekodi yako:
37:152 🔁 0/5
وَلَدَ ٱللَّهُ وَإِنَّهُمۡ لَكَٰذِبُونَ  ۝١٥٢
Waladal laahu wa innhum lakaaziboon
Mwenyezi Mungu amezaa! Ama hakika bila ya shaka hao ni waongo!
🎤 Rekodi yako:
37:153 🔁 0/5
أَصۡطَفَى ٱلۡبَنَاتِ عَلَى ٱلۡبَنِينَ  ۝١٥٣
Astafal banaati `alal baneen
Ati amekhiari watoto wa kike kuliko wanaume?
🎤 Rekodi yako:
37:154 🔁 0/5
مَا لَكُمۡ كَيۡفَ تَحۡكُمُونَ  ۝١٥٤
Maa lakum kaifa tahkumoon
Mna nini? Mnahukumu vipi nyinyi?
🎤 Rekodi yako:
37:155 🔁 0/5
أَفَلَا تَذَكَّرُونَ  ۝١٥٥
Afalaa tazakkaroon
Hamkumbuki?
🎤 Rekodi yako:
37:156 🔁 0/5
أَمۡ لَكُمۡ سُلۡطَٰنٌ مُّبِينٌ  ۝١٥٦
Am lakum sultaanum mubeen
Au mnayo hoja iliyo wazi?
🎤 Rekodi yako:
37:157 🔁 0/5
فَأۡتُواْ بِكِتَٰبِكُمۡ إِن كُنتُمۡ صَٰدِقِينَ  ۝١٥٧
Faatoo bi Kitaabikum in kuntum saadiqeen
Basi leteni Kitabu chenu kama mnasema kweli.
🎤 Rekodi yako:
37:158 🔁 0/5
وَجَعَلُواْ بَيۡنَهُۥ وَبَيۡنَ ٱلۡجِنَّةِ نَسَبًاۚ وَلَقَدۡ عَلِمَتِ ٱلۡجِنَّةُ إِنَّهُمۡ لَمُحۡضَرُونَ  ۝١٥٨
Wa ja`aloo bainahoo wa bainal jinnati nasabaa; wa laqad `alimatil jinnatu innahum lamuhdaroon
Na wameweka makhusiano ya nasaba baina yake na majini; na majini wamekwisha jua bila ya shaka kuwa wao watahudhurishwa.
🎤 Rekodi yako:
37:159 🔁 0/5
سُبۡحَٰنَ ٱللَّهِ عَمَّا يَصِفُونَ  ۝١٥٩
Subhaanal laahi `ammaa yasifoon
Subhana 'Llah Ametakasika Mwenyezi Mungu na hayo wanayo msingizia.
🎤 Rekodi yako:
37:160 🔁 0/5
إِلَّا عِبَادَ ٱللَّهِ ٱلۡمُخۡلَصِينَ  ۝١٦٠
Illaa `ibaadal laahil mukhlaseen
Isipo kuwa waja wa Mwenyezi Mungu walio safishwa.
🎤 Rekodi yako:
37:161 🔁 0/5
فَإِنَّكُمۡ وَمَا تَعۡبُدُونَ  ۝١٦١
Fa innakum wa maa ta`ubdoon
Basi hakika nyinyi na mnao waabudu
🎤 Rekodi yako:
37:162 🔁 0/5
مَآ أَنتُمۡ عَلَيۡهِ بِفَٰتِنِينَ  ۝١٦٢
Maaa antum `alaihi befaaatineen
Hamwezi kuwapoteza
🎤 Rekodi yako:
37:163 🔁 0/5
إِلَّا مَنۡ هُوَ صَالِ ٱلۡجَحِيمِ  ۝١٦٣
Illaa man huwa saalil jaheem
Isipo kuwa yule atakaye ingia Motoni.
🎤 Rekodi yako:
37:164 🔁 0/5
وَمَا مِنَّآ إِلَّا لَهُۥ مَقَامٌ مَّعۡلُومٌ  ۝١٦٤
Wa maa minnasa illaa lahoo maqaamum ma`loom
Na hapana katika sisi ila anapo mahali pake maalumu.
🎤 Rekodi yako:
37:165 🔁 0/5
وَإِنَّا لَنَحۡنُ ٱلصَّآفُّونَ  ۝١٦٥
Wa innaa llanah nus saaffoon
Na hakika bila ya shaka sisi ndio wajipangao safu.
🎤 Rekodi yako:
37:166 🔁 0/5
وَإِنَّا لَنَحۡنُ ٱلۡمُسَبِّحُونَ  ۝١٦٦
Wa innaa lanah nul musabbihoon
Na hakika sisi ndio wenye kusabihi kutakasa.
🎤 Rekodi yako:
37:167 🔁 0/5
وَإِن كَانُواْ لَيَقُولُونَ  ۝١٦٧
Wa in kaanoo la yaqooloon
Na walikuwapo walio kuwa wakisema:
🎤 Rekodi yako:
37:168 🔁 0/5
لَوۡ أَنَّ عِندَنَا ذِكۡرًا مِّنَ ٱلۡأَوَّلِينَ  ۝١٦٨
Law anna `indana zikram minal awwaleen
Tungeli kuwa na Ukumbusho kama wa watu wa zamani,
🎤 Rekodi yako:
37:169 🔁 0/5
لَكُنَّا عِبَادَ ٱللَّهِ ٱلۡمُخۡلَصِينَ  ۝١٦٩
Lakunna `ibaadal laahil mukhlaseen
Bila ya shaka tungeli kuwa ni waja wa Mwenyezi Mungu wenye ikhlasi.
🎤 Rekodi yako:
37:170 🔁 0/5
فَكَفَرُواْ بِهِۦۖ فَسَوۡفَ يَعۡلَمُونَ  ۝١٧٠
Fakafaroo bihee fasawfa ya`lamoon
Lakini waliukataa. Basi watakuja jua.
🎤 Rekodi yako:
37:171 🔁 0/5
وَلَقَدۡ سَبَقَتۡ كَلِمَتُنَا لِعِبَادِنَا ٱلۡمُرۡسَلِينَ  ۝١٧١
Wa laqad sabaqat Kalimatunaa li`ibaadinal mursa leen
Na bila ya shaka neno letu lilikwisha tangulia kwa waja wetu walio tumwa.
🎤 Rekodi yako:
37:172 🔁 0/5
إِنَّهُمۡ لَهُمُ ٱلۡمَنصُورُونَ  ۝١٧٢
Innaa hum lahumul mansooroon
Ya kuwa wao bila ya shaka ndio watakao nusuriwa.
🎤 Rekodi yako:
37:173 🔁 0/5
وَإِنَّ جُندَنَا لَهُمُ ٱلۡغَٰلِبُونَ  ۝١٧٣
Wa inna jundana lahumul ghaaliboon
Na kwamba jeshi letu ndilo litakalo shinda.
🎤 Rekodi yako:
37:174 🔁 0/5
فَتَوَلَّ عَنۡهُمۡ حَتَّىٰ حِينٍ  ۝١٧٤
Fatawalla `anhum hatta heen
Basi waachilie mbali kwa muda.
🎤 Rekodi yako:
37:175 🔁 0/5
وَأَبۡصِرۡهُمۡ فَسَوۡفَ يُبۡصِرُونَ  ۝١٧٥
Wa absirhum fasawfa yubsiroon
Na watazame, nao wataona.
🎤 Rekodi yako:
37:176 🔁 0/5
أَفَبِعَذَابِنَا يَسۡتَعۡجِلُونَ  ۝١٧٦
Afabi`azaabinaa yasta`jiloon
Je! Wanaihimiza adhabu yetu?
🎤 Rekodi yako:
37:177 🔁 0/5
فَإِذَا نَزَلَ بِسَاحَتِهِمۡ فَسَآءَ صَبَاحُ ٱلۡمُنذَرِينَ  ۝١٧٧
Fa izaa nazala bisaahatihim fasaaa`a sabaahul munzareen
Basi itakapo shuka uwanjani kwao, itakuwa asubuhi mbaya kwa walio onywa.
🎤 Rekodi yako:
37:178 🔁 0/5
وَتَوَلَّ عَنۡهُمۡ حَتَّىٰ حِينٍ  ۝١٧٨
Wa tawalla `anhum hattaa heen
Na waache kwa muda.
🎤 Rekodi yako:
37:179 🔁 0/5
وَأَبۡصِرۡ فَسَوۡفَ يُبۡصِرُونَ  ۝١٧٩
Wa absir fasawfa yubsiroon
Na tazama, na wao wataona.
🎤 Rekodi yako:
37:180 🔁 0/5
سُبۡحَٰنَ رَبِّكَ رَبِّ ٱلۡعِزَّةِ عَمَّا يَصِفُونَ  ۝١٨٠
Subhaana Rabbika Rabbil `izzati `amma yasifoon
Subhana Rabbi'l'Izzat Ametakasika Mola Mlezi Mwenye enzi na yale wanayo mzulia.
🎤 Rekodi yako:
37:181 🔁 0/5
وَسَلَٰمٌ عَلَى ٱلۡمُرۡسَلِينَ  ۝١٨١
Wa salaamun `alalmursaleen
Na Salamu juu ya Mitume.
🎤 Rekodi yako:
37:182 🔁 0/5
وَٱلۡحَمۡدُ لِلَّهِ رَبِّ ٱلۡعَٰلَمِينَ  ۝١٨٢
Walhamdu lillaahi Rabbil `aalameen
Na sifa njema zote ni za Mwenyezi Mungu Mola Mlezi wa walimwengu wote.
🎤 Rekodi yako:
💡 Gusa neno lililofichwa ili lionekane kwa muda — maendeleo yako yanahifadhiwa kiotomatiki.

🎉
🎊 Hongera! Umemaliza Kuhifadhi
Mishary Rashid Alafasy
Mahmoud Khalil Al-Husary
Abdurrahman As-Sudais
Mohamed Siddiq Al-Minshawi
Abdul Basit Abdul Samad
Ali Al-Hudhaify
Ahmed ibn Ali al-Ajamy
Abu Bakr Ash-Shaatree
Muhammad Ayyoub
Abdullah Basfar
Abdullah Al-Juhani
Maher Al Muaiqly
0:00
0:00
-

Kurani Tukufu


Tuesday, August 18, 2026

Usitusahau katika dua zako njema