Sura Ar-Rahman kwa Kiarabu na Kiswahili

Soma Sura Ar-Rahman na tafsiri kamili ya Kiswahili, maandishi na usomaji wa sauti. Tafsiri aya kwa aya. (78 Aya — مدنية). Ar-Rahman Sikiliza, Ar-Rahman Tafsiri, Ar-Rahman mp3, Ar-Rahman pdf.

Soma na Sikiliza Sura Ar-Rahman

🎧 Aya
M Mishary Rashid Alafasy
M Mahmoud Khalil Al-Husary
A Abdurrahman As-Sudais
M Mohamed Siddiq Al-Minshawi
A Abdul Basit Abdul Samad
A Ali Al-Hudhaify
A Ahmed ibn Ali al-Ajamy
A Abu Bakr Ash-Shaatree
M Muhammad Ayyoub
A Abdullah Basfar
A Abdullah Al-Juhani
M Maher Al Muaiqly
x1
الرَّحْمَٰنُ ۝١
📖 Tafsiri Aya 1
Arrah'man, Mwingi wa Rehema
عَلَّمَ الْقُرْآنَ ۝٢
📖 Tafsiri Aya 2
Amefundisha Qur'ani.
خَلَقَ الْإِنسَانَ ۝٣
📖 Tafsiri Aya 3
Amemuumba mwanaadamu,
عَلَّمَهُ الْبَيَانَ ۝٤
📖 Tafsiri Aya 4
Akamfundisha kubaini.
الشَّمْسُ وَالْقَمَرُ بِحُسْبَانٍ ۝٥
📖 Tafsiri Aya 5
Jua na mwezi huenda kwa hisabu.
وَالنَّجْمُ وَالشَّجَرُ يَسْجُدَانِ ۝٦
📖 Tafsiri Aya 6
Na mimea yenye kutambaa, na miti, inanyenyekea.
وَالسَّمَاءَ رَفَعَهَا وَوَضَعَ الْمِيزَانَ ۝٧
📖 Tafsiri Aya 7
Na mbingu ameziinua, na ameweka mizani,
أَلَّا تَطْغَوْا فِي الْمِيزَانِ ۝٨
📖 Tafsiri Aya 8
Ili msidhulumu katika mizani.
وَأَقِيمُوا الْوَزْنَ بِالْقِسْطِ وَلَا تُخْسِرُوا الْمِيزَانَ ۝٩
📖 Tafsiri Aya 9
Na wekeni mizani kwa haki, wala msipunje katika mizani.
وَالْأَرْضَ وَضَعَهَا لِلْأَنَامِ ۝١٠
📖 Tafsiri Aya 10
Na ardhi ameiweka kwa ajili ya viumbe.
فِيهَا فَاكِهَةٌ وَالنَّخْلُ ذَاتُ الْأَكْمَامِ ۝١١
📖 Tafsiri Aya 11
Humo yamo matunda na mitende yenye mafumba.
وَالْحَبُّ ذُو الْعَصْفِ وَالرَّيْحَانُ ۝١٢
📖 Tafsiri Aya 12
Na nafaka zenye makapi, na rehani.
فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ ۝١٣
📖 Tafsiri Aya 13
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha
خَلَقَ الْإِنسَانَ مِن صَلْصَالٍ كَالْفَخَّارِ ۝١٤
📖 Tafsiri Aya 14
Amemuumba mtu kwa udongo wa kinamo..
وَخَلَقَ الْجَانَّ مِن مَّارِجٍ مِّن نَّارٍ ۝١٥
📖 Tafsiri Aya 15
Na akawaumba majini kwa ulimi wa moto.
فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ ۝١٦
📖 Tafsiri Aya 16
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha
رَبُّ الْمَشْرِقَيْنِ وَرَبُّ الْمَغْرِبَيْنِ ۝١٧
📖 Tafsiri Aya 17
Mola Mlezi wa mashariki mbili na wa magharibi mbili.
فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ ۝١٨
📖 Tafsiri Aya 18
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
مَرَجَ الْبَحْرَيْنِ يَلْتَقِيَانِ ۝١٩
📖 Tafsiri Aya 19
Anaziendesha bahari mbili zikutane;
بَيْنَهُمَا بَرْزَخٌ لَّا يَبْغِيَانِ ۝٢٠
📖 Tafsiri Aya 20
Baina yao kipo kizuizi, zisiingiliane.
فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ ۝٢١
📖 Tafsiri Aya 21
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
يَخْرُجُ مِنْهُمَا اللُّؤْلُؤُ وَالْمَرْجَانُ ۝٢٢
📖 Tafsiri Aya 22
Katika hizo bahari mbili zinatoka lulu na marijani.
فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ ۝٢٣
📖 Tafsiri Aya 23
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
وَلَهُ الْجَوَارِ الْمُنشَآتُ فِي الْبَحْرِ كَالْأَعْلَامِ ۝٢٤
📖 Tafsiri Aya 24
Na ni vyake Yeye hivi viendavyo baharini vilivyo undwa kama vilima.
فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ ۝٢٥
📖 Tafsiri Aya 25
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
كُلُّ مَنْ عَلَيْهَا فَانٍ ۝٢٦
📖 Tafsiri Aya 26
Kila kilioko juu yake kitatoweka.
وَيَبْقَىٰ وَجْهُ رَبِّكَ ذُو الْجَلَالِ وَالْإِكْرَامِ ۝٢٧
📖 Tafsiri Aya 27
Na atabakia Mwenyewe Mola wako Mlezi Mwenye utukufu na ukarimu.
فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ ۝٢٨
📖 Tafsiri Aya 28
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
يَسْأَلُهُ مَن فِي السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ ۚ كُلَّ يَوْمٍ هُوَ فِي شَأْنٍ ۝٢٩
📖 Tafsiri Aya 29
Vinamwomba Yeye vilivyomo katika mbingu na ardhi. Kila siku Yeye yumo katika mambo.
فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ ۝٣٠
📖 Tafsiri Aya 30
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
سَنَفْرُغُ لَكُمْ أَيُّهَ الثَّقَلَانِ ۝٣١
📖 Tafsiri Aya 31
Tutakuhisabuni enyi makundi mawili.
فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ ۝٣٢
📖 Tafsiri Aya 32
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
يَا مَعْشَرَ الْجِنِّ وَالْإِنسِ إِنِ اسْتَطَعْتُمْ أَن تَنفُذُوا مِنْ أَقْطَارِ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ فَانفُذُوا ۚ لَا تَنفُذُونَ إِلَّا بِسُلْطَانٍ ۝٣٣
📖 Tafsiri Aya 33
Enyi makundi ya majini na watu! Mkiweza kupenya kwenye mbingu na ardhi, basi penyeni! Hamtapenya ila kwa kupewa madaraka.
فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ ۝٣٤
📖 Tafsiri Aya 34
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
يُرْسَلُ عَلَيْكُمَا شُوَاظٌ مِّن نَّارٍ وَنُحَاسٌ فَلَا تَنتَصِرَانِ ۝٣٥
📖 Tafsiri Aya 35
Mtapelekewa muwako wa moto na shaba; wala hamtashinda.
فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ ۝٣٦
📖 Tafsiri Aya 36
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
فَإِذَا انشَقَّتِ السَّمَاءُ فَكَانَتْ وَرْدَةً كَالدِّهَانِ ۝٣٧
📖 Tafsiri Aya 37
Itakapo pasuka mbingu ikawa nyekundu kama mafuta.
فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ ۝٣٨
📖 Tafsiri Aya 38
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
فَيَوْمَئِذٍ لَّا يُسْأَلُ عَن ذَنبِهِ إِنسٌ وَلَا جَانٌّ ۝٣٩
📖 Tafsiri Aya 39
Siku hiyo hataulizwa dhambi zake mtu wala jini.
فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ ۝٤٠
📖 Tafsiri Aya 40
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
يُعْرَفُ الْمُجْرِمُونَ بِسِيمَاهُمْ فَيُؤْخَذُ بِالنَّوَاصِي وَالْأَقْدَامِ ۝٤١
📖 Tafsiri Aya 41
Watajuulikana wakosefu kwa alama zao, basi watashikwa kwa nywele zao za utosini na kwa miguu.
فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ ۝٤٢
📖 Tafsiri Aya 42
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
هَٰذِهِ جَهَنَّمُ الَّتِي يُكَذِّبُ بِهَا الْمُجْرِمُونَ ۝٤٣
📖 Tafsiri Aya 43
Hii ndiyo Jahannamu ambayo wakosefu wakiikanusha.
يَطُوفُونَ بَيْنَهَا وَبَيْنَ حَمِيمٍ آنٍ ۝٤٤
📖 Tafsiri Aya 44
Watakuwa wakizunguka baina ya hiyo na maji ya moto yanayo chemka.
فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ ۝٤٥
📖 Tafsiri Aya 45
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
وَلِمَنْ خَافَ مَقَامَ رَبِّهِ جَنَّتَانِ ۝٤٦
📖 Tafsiri Aya 46
Na mwenye kuogopa kusimamishwa mbele ya Mola wake Mlezi atapata Bustani mbili.
فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ ۝٤٧
📖 Tafsiri Aya 47
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
ذَوَاتَا أَفْنَانٍ ۝٤٨
📖 Tafsiri Aya 48
Bustani zenye matawi yaliyo tanda.
فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ ۝٤٩
📖 Tafsiri Aya 49
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
فِيهِمَا عَيْنَانِ تَجْرِيَانِ ۝٥٠
📖 Tafsiri Aya 50
Ndani yake zimo chemchem mbili zinazo pita.
فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ ۝٥١
📖 Tafsiri Aya 51
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
فِيهِمَا مِن كُلِّ فَاكِهَةٍ زَوْجَانِ ۝٥٢
📖 Tafsiri Aya 52
Humo katika kila matunda zimo namna mbili.
فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ ۝٥٣
📖 Tafsiri Aya 53
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
مُتَّكِئِينَ عَلَىٰ فُرُشٍ بَطَائِنُهَا مِنْ إِسْتَبْرَقٍ ۚ وَجَنَى الْجَنَّتَيْنِ دَانٍ ۝٥٤
📖 Tafsiri Aya 54
Wawe wameegemea matandiko yenye bit'ana ya hariri nzito; na matunda ya Bustani hizo yapo karibu.
فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ ۝٥٥
📖 Tafsiri Aya 55
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
فِيهِنَّ قَاصِرَاتُ الطَّرْفِ لَمْ يَطْمِثْهُنَّ إِنسٌ قَبْلَهُمْ وَلَا جَانٌّ ۝٥٦
📖 Tafsiri Aya 56
Humo watakuwamo wanawake watulizao macho yao; hajawagusa mtu kabla yao wala jini.
فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ ۝٥٧
📖 Tafsiri Aya 57
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
كَأَنَّهُنَّ الْيَاقُوتُ وَالْمَرْجَانُ ۝٥٨
📖 Tafsiri Aya 58
Kama kwamba wao ni yakuti na marijani.
فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ ۝٥٩
📖 Tafsiri Aya 59
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha.
هَلْ جَزَاءُ الْإِحْسَانِ إِلَّا الْإِحْسَانُ ۝٦٠
📖 Tafsiri Aya 60
Ati yaweza kuwa malipo ya ihsani ila ihsani?
فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ ۝٦١
📖 Tafsiri Aya 61
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
وَمِن دُونِهِمَا جَنَّتَانِ ۝٦٢
📖 Tafsiri Aya 62
Na zaidi ya hizo zipo Bustani nyengine mbili.
فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ ۝٦٣
📖 Tafsiri Aya 63
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
مُدْهَامَّتَانِ ۝٦٤
📖 Tafsiri Aya 64
Za kijani kibivu.
فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ ۝٦٥
📖 Tafsiri Aya 65
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
فِيهِمَا عَيْنَانِ نَضَّاخَتَانِ ۝٦٦
📖 Tafsiri Aya 66
Na chemchem mbili zinazo furika.
فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ ۝٦٧
📖 Tafsiri Aya 67
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
فِيهِمَا فَاكِهَةٌ وَنَخْلٌ وَرُمَّانٌ ۝٦٨
📖 Tafsiri Aya 68
Imo humo miti ya matunda, na mitende na mikomamanga.
فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ ۝٦٩
📖 Tafsiri Aya 69
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
فِيهِنَّ خَيْرَاتٌ حِسَانٌ ۝٧٠
📖 Tafsiri Aya 70
Humo wamo wanawake wema wazuri.
فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ ۝٧١
📖 Tafsiri Aya 71
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
حُورٌ مَّقْصُورَاتٌ فِي الْخِيَامِ ۝٧٢
📖 Tafsiri Aya 72
Wanawake wazuri wanao tawishwa katika makhema.
فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ ۝٧٣
📖 Tafsiri Aya 73
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
لَمْ يَطْمِثْهُنَّ إِنسٌ قَبْلَهُمْ وَلَا جَانٌّ ۝٧٤
📖 Tafsiri Aya 74
Hajawagusa mtu wala jini kabla yao.
فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ ۝٧٥
📖 Tafsiri Aya 75
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
مُتَّكِئِينَ عَلَىٰ رَفْرَفٍ خُضْرٍ وَعَبْقَرِيٍّ حِسَانٍ ۝٧٦
📖 Tafsiri Aya 76
Wameegemea juu ya matakia ya kijani na mazulia mazuri.
فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ ۝٧٧
📖 Tafsiri Aya 77
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
تَبَارَكَ اسْمُ رَبِّكَ ذِي الْجَلَالِ وَالْإِكْرَامِ ۝٧٨
📖 Tafsiri Aya 78
Limetukuka jina la Mola wako Mlezi Mwenye utukufu na ukarimu.
← 54 Ar-Rahman (55/114) 56 →
Soma Sura Ar-Rahman kwa Kiswahili – Tafsiri na Sauti

55الرحمن Ar-Rahman 📚 78 Aya مدنية



Kurani Tukufu


Tuesday, August 18, 2026

Usitusahau katika dua zako njema