Sura Al-Fajr kwa Kiarabu na Kiswahili

Soma Sura Al-Fajr na tafsiri kamili ya Kiswahili, maandishi na usomaji wa sauti. Tafsiri aya kwa aya. (30 Aya — مكية). Al-Fajr Sikiliza, Al-Fajr Tafsiri, Al-Fajr mp3, Al-Fajr pdf.

Soma na Sikiliza Sura Al-Fajr

🎧 Aya
M Mishary Rashid Alafasy
M Mahmoud Khalil Al-Husary
A Abdurrahman As-Sudais
M Mohamed Siddiq Al-Minshawi
A Abdul Basit Abdul Samad
A Ali Al-Hudhaify
A Ahmed ibn Ali al-Ajamy
A Abu Bakr Ash-Shaatree
M Muhammad Ayyoub
A Abdullah Basfar
A Abdullah Al-Juhani
M Maher Al Muaiqly
x1
وَالْفَجْرِ ۝١
📖 Tafsiri Aya 1
Naapa kwa alfajiri,
وَلَيَالٍ عَشْرٍ ۝٢
📖 Tafsiri Aya 2
Na kwa masiku kumi,
وَالشَّفْعِ وَالْوَتْرِ ۝٣
📖 Tafsiri Aya 3
Na kwa viwili viwili na kimoja kimoja,
وَاللَّيْلِ إِذَا يَسْرِ ۝٤
📖 Tafsiri Aya 4
Na kwa usiku unapo pita,
هَلْ فِي ذَٰلِكَ قَسَمٌ لِّذِي حِجْرٍ ۝٥
📖 Tafsiri Aya 5
Je! Hapana katika haya kiapo kwa mwenye akili?
أَلَمْ تَرَ كَيْفَ فَعَلَ رَبُّكَ بِعَادٍ ۝٦
📖 Tafsiri Aya 6
Kwani hukuona jinsi Mola wako Mlezi alivyo wafanya kina A'di?
إِرَمَ ذَاتِ الْعِمَادِ ۝٧
📖 Tafsiri Aya 7
Wa Iram, wenye majumba marefu?
الَّتِي لَمْ يُخْلَقْ مِثْلُهَا فِي الْبِلَادِ ۝٨
📖 Tafsiri Aya 8
Ambao haukuumbwa mfano wake katika nchi?
وَثَمُودَ الَّذِينَ جَابُوا الصَّخْرَ بِالْوَادِ ۝٩
📖 Tafsiri Aya 9
Na Thamudi walio chonga majabali huko bondeni?
وَفِرْعَوْنَ ذِي الْأَوْتَادِ ۝١٠
📖 Tafsiri Aya 10
Na Firauni mwenye vigingi?
الَّذِينَ طَغَوْا فِي الْبِلَادِ ۝١١
📖 Tafsiri Aya 11
Ambao walifanya jeuri katika nchi?
فَأَكْثَرُوا فِيهَا الْفَسَادَ ۝١٢
📖 Tafsiri Aya 12
Wakakithirisha humo ufisadi?
فَصَبَّ عَلَيْهِمْ رَبُّكَ سَوْطَ عَذَابٍ ۝١٣
📖 Tafsiri Aya 13
Basi Mola wako Mlezi aliwapiga mjeledi wa adhabu.
إِنَّ رَبَّكَ لَبِالْمِرْصَادِ ۝١٤
📖 Tafsiri Aya 14
Hakika Mola wako Mlezi yupo kwenye mavizio anawavizia.
فَأَمَّا الْإِنسَانُ إِذَا مَا ابْتَلَاهُ رَبُّهُ فَأَكْرَمَهُ وَنَعَّمَهُ فَيَقُولُ رَبِّي أَكْرَمَنِ ۝١٥
📖 Tafsiri Aya 15
Ama mtu anapo jaribiwa na Mola wake Mlezi, akamkirimu na akamneemesha, husema: Mola wangu Mlezi amenikirimu!
وَأَمَّا إِذَا مَا ابْتَلَاهُ فَقَدَرَ عَلَيْهِ رِزْقَهُ فَيَقُولُ رَبِّي أَهَانَنِ ۝١٦
📖 Tafsiri Aya 16
Na ama anapo mjaribu akampunguzia riziki yake, husema: Mola wangu Mlezi amenitia unyonge!
كَلَّا ۖ بَل لَّا تُكْرِمُونَ الْيَتِيمَ ۝١٧
📖 Tafsiri Aya 17
Sivyo hivyo! Bali nyinyi hamuwakirimu mayatima,
وَلَا تَحَاضُّونَ عَلَىٰ طَعَامِ الْمِسْكِينِ ۝١٨
📖 Tafsiri Aya 18
Wala hamhimizani kulisha masikini;
وَتَأْكُلُونَ التُّرَاثَ أَكْلًا لَّمًّا ۝١٩
📖 Tafsiri Aya 19
Na mnakula urithi kwa ulaji wa pupa,
وَتُحِبُّونَ الْمَالَ حُبًّا جَمًّا ۝٢٠
📖 Tafsiri Aya 20
Na mnapenda mali pendo la kupita kiasi.
كَلَّا إِذَا دُكَّتِ الْأَرْضُ دَكًّا دَكًّا ۝٢١
📖 Tafsiri Aya 21
Sivyo hivyo! Itakapo vunjwa ardhi vipande vipande,
وَجَاءَ رَبُّكَ وَالْمَلَكُ صَفًّا صَفًّا ۝٢٢
📖 Tafsiri Aya 22
Na akaja Mola wako Mlezi na Malaika safu safu,
وَجِيءَ يَوْمَئِذٍ بِجَهَنَّمَ ۚ يَوْمَئِذٍ يَتَذَكَّرُ الْإِنسَانُ وَأَنَّىٰ لَهُ الذِّكْرَىٰ ۝٢٣
📖 Tafsiri Aya 23
Na ikaletwa Jahannamu siku hiyo, siku hiyo mtu atakumbuka! Lakini kukumbuka huko kutamfaa nini?
يَقُولُ يَا لَيْتَنِي قَدَّمْتُ لِحَيَاتِي ۝٢٤
📖 Tafsiri Aya 24
Atasema: Laiti ningeli jitangulizia kwa uhai wangu!
فَيَوْمَئِذٍ لَّا يُعَذِّبُ عَذَابَهُ أَحَدٌ ۝٢٥
📖 Tafsiri Aya 25
Basi siku hiyo hataadhibu yeyote namna ya kuadhibu kwake.
وَلَا يُوثِقُ وَثَاقَهُ أَحَدٌ ۝٢٦
📖 Tafsiri Aya 26
Wala hatafunga yeyote kama kufunga kwake.
يَا أَيَّتُهَا النَّفْسُ الْمُطْمَئِنَّةُ ۝٢٧
📖 Tafsiri Aya 27
Ewe nafsi iliyo tua!
ارْجِعِي إِلَىٰ رَبِّكِ رَاضِيَةً مَّرْضِيَّةً ۝٢٨
📖 Tafsiri Aya 28
Rejea kwa Mola wako Mlezi umeridhika, na umemridhisha.
فَادْخُلِي فِي عِبَادِي ۝٢٩
📖 Tafsiri Aya 29
Basi ingia miongoni mwa waja wangu,
وَادْخُلِي جَنَّتِي ۝٣٠
📖 Tafsiri Aya 30
Na ingia katika Pepo yangu.
← 88 Al-Fajr (89/114) 90 →
Soma Sura Al-Fajr kwa Kiswahili – Tafsiri na Sauti

89الفجر Al-Fajr 📚 30 Aya مكية



Kurani Tukufu


Tuesday, August 18, 2026

Usitusahau katika dua zako njema