Sura Al-Waqi'a kwa Kiarabu na Kiswahili

Soma Sura Al-Waqi'a na tafsiri kamili ya Kiswahili, maandishi na usomaji wa sauti. Tafsiri aya kwa aya. (96 Aya — مكية). Al-Waqi'a Sikiliza, Al-Waqi'a Tafsiri, Al-Waqi'a mp3, Al-Waqi'a pdf.

Soma na Sikiliza Sura Al-Waqi'a

🎧 Aya
M Mishary Rashid Alafasy
M Mahmoud Khalil Al-Husary
A Abdurrahman As-Sudais
M Mohamed Siddiq Al-Minshawi
A Abdul Basit Abdul Samad
A Ali Al-Hudhaify
A Ahmed ibn Ali al-Ajamy
A Abu Bakr Ash-Shaatree
M Muhammad Ayyoub
A Abdullah Basfar
A Abdullah Al-Juhani
M Maher Al Muaiqly
x1
إِذَا وَقَعَتِ الْوَاقِعَةُ ۝١
📖 Tafsiri Aya 1
Litakapo tukia hilo Tukio
لَيْسَ لِوَقْعَتِهَا كَاذِبَةٌ ۝٢
📖 Tafsiri Aya 2
Hapana cha kukanusha kutukia kwake.
خَافِضَةٌ رَّافِعَةٌ ۝٣
📖 Tafsiri Aya 3
Literemshalo linyanyualo,
إِذَا رُجَّتِ الْأَرْضُ رَجًّا ۝٤
📖 Tafsiri Aya 4
Itakapo tikiswa ardhi kwa mtikiso,
وَبُسَّتِ الْجِبَالُ بَسًّا ۝٥
📖 Tafsiri Aya 5
Na milima itapo sagwasagwa,
فَكَانَتْ هَبَاءً مُّنبَثًّا ۝٦
📖 Tafsiri Aya 6
Iwe mavumbi yanayo peperushwa,
وَكُنتُمْ أَزْوَاجًا ثَلَاثَةً ۝٧
📖 Tafsiri Aya 7
Na nyinyi mtakuwa namna tatu:-
فَأَصْحَابُ الْمَيْمَنَةِ مَا أَصْحَابُ الْمَيْمَنَةِ ۝٨
📖 Tafsiri Aya 8
Basi watakuwepo wa kuliani; je, ni wepi wa kuliani?
وَأَصْحَابُ الْمَشْأَمَةِ مَا أَصْحَابُ الْمَشْأَمَةِ ۝٩
📖 Tafsiri Aya 9
Na wa kushotoni; je, ni wepi wa kushotoni?
وَالسَّابِقُونَ السَّابِقُونَ ۝١٠
📖 Tafsiri Aya 10
Na wa mbele watakuwa mbele.
أُولَٰئِكَ الْمُقَرَّبُونَ ۝١١
📖 Tafsiri Aya 11
Hao ndio watakao karibishwa
فِي جَنَّاتِ النَّعِيمِ ۝١٢
📖 Tafsiri Aya 12
Katika Bustani zenye neema.
ثُلَّةٌ مِّنَ الْأَوَّلِينَ ۝١٣
📖 Tafsiri Aya 13
Fungu kubwa katika wa mwanzo,
وَقَلِيلٌ مِّنَ الْآخِرِينَ ۝١٤
📖 Tafsiri Aya 14
Na wachache katika wa mwisho.
عَلَىٰ سُرُرٍ مَّوْضُونَةٍ ۝١٥
📖 Tafsiri Aya 15
Watakuwa juu ya viti vya fakhari vilivyo tonewa.
مُّتَّكِئِينَ عَلَيْهَا مُتَقَابِلِينَ ۝١٦
📖 Tafsiri Aya 16
Wakiviegemea wakielekeana.
يَطُوفُ عَلَيْهِمْ وِلْدَانٌ مُّخَلَّدُونَ ۝١٧
📖 Tafsiri Aya 17
Wakitumikiwa na wavulana wa ujana wa milele,
بِأَكْوَابٍ وَأَبَارِيقَ وَكَأْسٍ مِّن مَّعِينٍ ۝١٨
📖 Tafsiri Aya 18
Kwa vikombe na mabirika na bilauri za vinywaji kutoka chemchem safi.
لَّا يُصَدَّعُونَ عَنْهَا وَلَا يُنزِفُونَ ۝١٩
📖 Tafsiri Aya 19
Hawataumwa kichwa kwa vinywaji hivyo wala hawatoleweshwa.
وَفَاكِهَةٍ مِّمَّا يَتَخَيَّرُونَ ۝٢٠
📖 Tafsiri Aya 20
Na matunda wayapendayo,
وَلَحْمِ طَيْرٍ مِّمَّا يَشْتَهُونَ ۝٢١
📖 Tafsiri Aya 21
Na nyama za ndege kama wanavyo tamani.
وَحُورٌ عِينٌ ۝٢٢
📖 Tafsiri Aya 22
Na Mahurulaini,
كَأَمْثَالِ اللُّؤْلُؤِ الْمَكْنُونِ ۝٢٣
📖 Tafsiri Aya 23
Walio kama mfano wa lulu zilio hifadhiwa.
جَزَاءً بِمَا كَانُوا يَعْمَلُونَ ۝٢٤
📖 Tafsiri Aya 24
Ni malipo kwa waliyo kuwa wakiyatenda.
لَا يَسْمَعُونَ فِيهَا لَغْوًا وَلَا تَأْثِيمًا ۝٢٥
📖 Tafsiri Aya 25
Humo hawatasikia porojo wala maneno ya dhambi,
إِلَّا قِيلًا سَلَامًا سَلَامًا ۝٢٦
📖 Tafsiri Aya 26
Isipo kuwa maneno ya Salama, Salama.
وَأَصْحَابُ الْيَمِينِ مَا أَصْحَابُ الْيَمِينِ ۝٢٧
📖 Tafsiri Aya 27
Na wale wa mkono wa kulia, ni yepi yatakuwa ya wa kuliani?
فِي سِدْرٍ مَّخْضُودٍ ۝٢٨
📖 Tafsiri Aya 28
Katika mikunazi isiyo na miba,
وَطَلْحٍ مَّنضُودٍ ۝٢٩
📖 Tafsiri Aya 29
Na migomba iliyo pangiliwa,
وَظِلٍّ مَّمْدُودٍ ۝٣٠
📖 Tafsiri Aya 30
Na kivuli kilicho tanda,
وَمَاءٍ مَّسْكُوبٍ ۝٣١
📖 Tafsiri Aya 31
Na maji yanayo miminika,
وَفَاكِهَةٍ كَثِيرَةٍ ۝٣٢
📖 Tafsiri Aya 32
Na matunda mengi,
لَّا مَقْطُوعَةٍ وَلَا مَمْنُوعَةٍ ۝٣٣
📖 Tafsiri Aya 33
Hayatindikii wala hayakatazwi,
وَفُرُشٍ مَّرْفُوعَةٍ ۝٣٤
📖 Tafsiri Aya 34
Na matandiko yaliyo nyanyuliwa.
إِنَّا أَنشَأْنَاهُنَّ إِنشَاءً ۝٣٥
📖 Tafsiri Aya 35
Hakika Sisi tutawaumba (Mahurulaini) upya,
فَجَعَلْنَاهُنَّ أَبْكَارًا ۝٣٦
📖 Tafsiri Aya 36
Na tutawafanya vijana,
عُرُبًا أَتْرَابًا ۝٣٧
📖 Tafsiri Aya 37
Wanapendana na waume zao, hirimu moja.
لِّأَصْحَابِ الْيَمِينِ ۝٣٨
📖 Tafsiri Aya 38
Kwa ajili ya watu wa kuliani.
ثُلَّةٌ مِّنَ الْأَوَّلِينَ ۝٣٩
📖 Tafsiri Aya 39
Fungu kubwa katika wa mwanzo,
وَثُلَّةٌ مِّنَ الْآخِرِينَ ۝٤٠
📖 Tafsiri Aya 40
Na fungu kubwa katika wa mwisho.
وَأَصْحَابُ الشِّمَالِ مَا أَصْحَابُ الشِّمَالِ ۝٤١
📖 Tafsiri Aya 41
Na watu wa kushotoni; je ni yepi ya wa kushotoni?
فِي سَمُومٍ وَحَمِيمٍ ۝٤٢
📖 Tafsiri Aya 42
Katika upepo wa moto, na maji yanayo chemka,
وَظِلٍّ مِّن يَحْمُومٍ ۝٤٣
📖 Tafsiri Aya 43
Na kivuli cha moshi mweusi,
لَّا بَارِدٍ وَلَا كَرِيمٍ ۝٤٤
📖 Tafsiri Aya 44
Si cha kuburudisha wala kustarehesha.
إِنَّهُمْ كَانُوا قَبْلَ ذَٰلِكَ مُتْرَفِينَ ۝٤٥
📖 Tafsiri Aya 45
Hakika hao walikuwa kabla ya haya wakiishi maisha ya anasa.
وَكَانُوا يُصِرُّونَ عَلَى الْحِنثِ الْعَظِيمِ ۝٤٦
📖 Tafsiri Aya 46
Na walikuwa wakishikilia kufanya madhambi makubwa,
وَكَانُوا يَقُولُونَ أَئِذَا مِتْنَا وَكُنَّا تُرَابًا وَعِظَامًا أَإِنَّا لَمَبْعُوثُونَ ۝٤٧
📖 Tafsiri Aya 47
Na walikuwa wakisema: Tutakapo kufa na tukawa udongo na mafupa, ati ndio tutafufuliwa?
أَوَآبَاؤُنَا الْأَوَّلُونَ ۝٤٨
📖 Tafsiri Aya 48
Au baba zetu wa zamani?
قُلْ إِنَّ الْأَوَّلِينَ وَالْآخِرِينَ ۝٤٩
📖 Tafsiri Aya 49
Sema: Hakika wa zamani na wa mwisho
لَمَجْمُوعُونَ إِلَىٰ مِيقَاتِ يَوْمٍ مَّعْلُومٍ ۝٥٠
📖 Tafsiri Aya 50
Bila ya shaka watakusanywa kwa wakati wa siku maalumu.
ثُمَّ إِنَّكُمْ أَيُّهَا الضَّالُّونَ الْمُكَذِّبُونَ ۝٥١
📖 Tafsiri Aya 51
Kisha nyinyi, mlio potea, mnao kanusha,
لَآكِلُونَ مِن شَجَرٍ مِّن زَقُّومٍ ۝٥٢
📖 Tafsiri Aya 52
Kwa yakini mtakula mti wa Zaqqumu.
فَمَالِئُونَ مِنْهَا الْبُطُونَ ۝٥٣
📖 Tafsiri Aya 53
Na kwa mti huo mtajaza matumbo.
فَشَارِبُونَ عَلَيْهِ مِنَ الْحَمِيمِ ۝٥٤
📖 Tafsiri Aya 54
Na juu yake mtakunywa maji yanayo chemka.
فَشَارِبُونَ شُرْبَ الْهِيمِ ۝٥٥
📖 Tafsiri Aya 55
Tena mtakunywa kama wanavyo kunywa ngamia wenye kiu.
هَٰذَا نُزُلُهُمْ يَوْمَ الدِّينِ ۝٥٦
📖 Tafsiri Aya 56
Hiyo ndiyo karamu yao Siku ya Malipo.
نَحْنُ خَلَقْنَاكُمْ فَلَوْلَا تُصَدِّقُونَ ۝٥٧
📖 Tafsiri Aya 57
Sisi tumekuumbeni; basi hamsadiki?
أَفَرَأَيْتُم مَّا تُمْنُونَ ۝٥٨
📖 Tafsiri Aya 58
Je! Mnaiona mbegu ya uzazi mnayo idondokeza?
أَأَنتُمْ تَخْلُقُونَهُ أَمْ نَحْنُ الْخَالِقُونَ ۝٥٩
📖 Tafsiri Aya 59
Je! Mnaiumba nyinyi, au ni Sisi ndio Waumbaji?
نَحْنُ قَدَّرْنَا بَيْنَكُمُ الْمَوْتَ وَمَا نَحْنُ بِمَسْبُوقِينَ ۝٦٠
📖 Tafsiri Aya 60
Sisi tumekuwekeeni mauti; na wala Sisi hatushindwi
عَلَىٰ أَن نُّبَدِّلَ أَمْثَالَكُمْ وَنُنشِئَكُمْ فِي مَا لَا تَعْلَمُونَ ۝٦١
📖 Tafsiri Aya 61
Kuwaleta wengine badala yenu na kukuumbeni nyinyi kwa umbo msilo lijua.
وَلَقَدْ عَلِمْتُمُ النَّشْأَةَ الْأُولَىٰ فَلَوْلَا تَذَكَّرُونَ ۝٦٢
📖 Tafsiri Aya 62
Na bila ya shaka mlikwisha jua umbo la kwanza, basi kwa nini hamkumbuki?
أَفَرَأَيْتُم مَّا تَحْرُثُونَ ۝٦٣
📖 Tafsiri Aya 63
Je! Mnaona makulima mnayo yapanda?
أَأَنتُمْ تَزْرَعُونَهُ أَمْ نَحْنُ الزَّارِعُونَ ۝٦٤
📖 Tafsiri Aya 64
Je! Ni nyinyi mnayo yaotesha au ni Sisi ndio wenye kuotesha?
لَوْ نَشَاءُ لَجَعَلْنَاهُ حُطَامًا فَظَلْتُمْ تَفَكَّهُونَ ۝٦٥
📖 Tafsiri Aya 65
Tungeli taka tungeli yafanya yakawa mapepe, mkabaki mnastaajabu,
إِنَّا لَمُغْرَمُونَ ۝٦٦
📖 Tafsiri Aya 66
Mkisema: Hakika sisi tumegharimika;
بَلْ نَحْنُ مَحْرُومُونَ ۝٦٧
📖 Tafsiri Aya 67
Bali sisi tumenyimwa.
أَفَرَأَيْتُمُ الْمَاءَ الَّذِي تَشْرَبُونَ ۝٦٨
📖 Tafsiri Aya 68
Je! Mnayaona maji mnayo yanywa?
أَأَنتُمْ أَنزَلْتُمُوهُ مِنَ الْمُزْنِ أَمْ نَحْنُ الْمُنزِلُونَ ۝٦٩
📖 Tafsiri Aya 69
Je! Ni nyinyi mnayo yateremsha kutoka mawinguni au ni Sisi ndio wenye kuyateremsha?
لَوْ نَشَاءُ جَعَلْنَاهُ أُجَاجًا فَلَوْلَا تَشْكُرُونَ ۝٧٠
📖 Tafsiri Aya 70
Tungeli penda tungeli yafanya ya chumvi. Basi mbona hamshukuru?
أَفَرَأَيْتُمُ النَّارَ الَّتِي تُورُونَ ۝٧١
📖 Tafsiri Aya 71
Je! Mnauona moto mnao uwasha?
أَأَنتُمْ أَنشَأْتُمْ شَجَرَتَهَا أَمْ نَحْنُ الْمُنشِئُونَ ۝٧٢
📖 Tafsiri Aya 72
Ni nyinyi mlio uumba mti wake au Sisi ndio Waumbaji?
نَحْنُ جَعَلْنَاهَا تَذْكِرَةً وَمَتَاعًا لِّلْمُقْوِينَ ۝٧٣
📖 Tafsiri Aya 73
Sisi tumeufanya uwe ni ukumbusho na manufaa kwa walioko nyikani.
فَسَبِّحْ بِاسْمِ رَبِّكَ الْعَظِيمِ ۝٧٤
📖 Tafsiri Aya 74
Basi litakase jina la Mola wako Mlezi aliye Mkuu.
۞ فَلَا أُقْسِمُ بِمَوَاقِعِ النُّجُومِ ۝٧٥
📖 Tafsiri Aya 75
Basi naapa kwa maanguko ya nyota,
وَإِنَّهُ لَقَسَمٌ لَّوْ تَعْلَمُونَ عَظِيمٌ ۝٧٦
📖 Tafsiri Aya 76
Na hakika bila ya shaka hichi ni kiapo kikubwa, laiti mngeli jua!
إِنَّهُ لَقُرْآنٌ كَرِيمٌ ۝٧٧
📖 Tafsiri Aya 77
Hakika hii bila ya shaka ni Qur'ani Tukufu,
فِي كِتَابٍ مَّكْنُونٍ ۝٧٨
📖 Tafsiri Aya 78
Katika Kitabu kilicho hifadhiwa.
لَّا يَمَسُّهُ إِلَّا الْمُطَهَّرُونَ ۝٧٩
📖 Tafsiri Aya 79
Hapana akigusaye ila walio takaswa.
تَنزِيلٌ مِّن رَّبِّ الْعَالَمِينَ ۝٨٠
📖 Tafsiri Aya 80
Ni uteremsho unao toka kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.
أَفَبِهَٰذَا الْحَدِيثِ أَنتُم مُّدْهِنُونَ ۝٨١
📖 Tafsiri Aya 81
Ni maneno haya ndiyo nyinyi mnayapuuza?
وَتَجْعَلُونَ رِزْقَكُمْ أَنَّكُمْ تُكَذِّبُونَ ۝٨٢
📖 Tafsiri Aya 82
Na badala ya kushukuru kwa riziki yenu mnafanya kuwa mnakadhibisha?
فَلَوْلَا إِذَا بَلَغَتِ الْحُلْقُومَ ۝٨٣
📖 Tafsiri Aya 83
Yawaje basi itakapo fika roho kwenye koo,
وَأَنتُمْ حِينَئِذٍ تَنظُرُونَ ۝٨٤
📖 Tafsiri Aya 84
Na nyinyi wakati huo mnatazama!
وَنَحْنُ أَقْرَبُ إِلَيْهِ مِنكُمْ وَلَٰكِن لَّا تُبْصِرُونَ ۝٨٥
📖 Tafsiri Aya 85
Na Sisi tuko karibu zaidi naye kuliko nyinyi.
فَلَوْلَا إِن كُنتُمْ غَيْرَ مَدِينِينَ ۝٨٦
📖 Tafsiri Aya 86
Na lau kuwa nyinyi hamumo katika mamlaka yangu,
تَرْجِعُونَهَا إِن كُنتُمْ صَادِقِينَ ۝٨٧
📖 Tafsiri Aya 87
Kwanini hamuirudishi hiyo roho, ikiwa nyinyi mnasema kweli?
فَأَمَّا إِن كَانَ مِنَ الْمُقَرَّبِينَ ۝٨٨
📖 Tafsiri Aya 88
Basi akiwa miongoni mwa walio karibishwa,
فَرَوْحٌ وَرَيْحَانٌ وَجَنَّتُ نَعِيمٍ ۝٨٩
📖 Tafsiri Aya 89
Basi ni raha, na manukato, na Bustani zenye neema.
وَأَمَّا إِن كَانَ مِنْ أَصْحَابِ الْيَمِينِ ۝٩٠
📖 Tafsiri Aya 90
Na akiwa katika watu wa upande wa kulia,
فَسَلَامٌ لَّكَ مِنْ أَصْحَابِ الْيَمِينِ ۝٩١
📖 Tafsiri Aya 91
Basi ni Salamu kwako uliye miongoni mwa watu wa upande wa kulia.
وَأَمَّا إِن كَانَ مِنَ الْمُكَذِّبِينَ الضَّالِّينَ ۝٩٢
📖 Tafsiri Aya 92
Na ama akiwa katika walio kadhibisha wapotovu,
فَنُزُلٌ مِّنْ حَمِيمٍ ۝٩٣
📖 Tafsiri Aya 93
Basi karamu yake ni maji yanayo chemka,
وَتَصْلِيَةُ جَحِيمٍ ۝٩٤
📖 Tafsiri Aya 94
Na kutiwa Motoni.
إِنَّ هَٰذَا لَهُوَ حَقُّ الْيَقِينِ ۝٩٥
📖 Tafsiri Aya 95
Hakika hii ndiyo haki yenye yakini.
فَسَبِّحْ بِاسْمِ رَبِّكَ الْعَظِيمِ ۝٩٦
📖 Tafsiri Aya 96
Basi litakase jina la Mola wako Mlezi aliye Mkubwa.
← 55 Al-Waqi'a (56/114) 57 →
Soma Sura Al-Waqi'a kwa Kiswahili – Tafsiri na Sauti

56الواقعة Al-Waqi'ah 📚 96 Aya مكية



Kurani Tukufu


Tuesday, August 18, 2026

Usitusahau katika dua zako njema