🔥 0 siku mfululizo
📖 Sura ndefu — imegawanywa sehemu ndogo (99 Aya)
📚 Sura Zote
30%
🎤 Gusa ikoni ya maikrofoni 🎙️ karibu na aya yoyote ili kujirekodi, kisha sikiliza na ulinganishe na qari.
0/99
15:1 🔁 0/5
الٓرۚ تِلۡكَ ءَايَٰتُ ٱلۡكِتَٰبِ وَقُرۡءَانٍ مُّبِينٍ  ۝١
Alif-Laaam-Raa; tilka Aayaatul Kitaabi wa Qur-aa-nim Mubeen
Alif Lam Ra. (A. L. R). Hizi ni Aya za Kitabu na Qur'ani inayo bainisha.
🎤 Rekodi yako:
15:2 🔁 0/5
رُّبَمَا يَوَدُّ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ لَوۡ كَانُواْ مُسۡلِمِينَ  ۝٢
Rubamaa yawaddul lazeena kafaroo law kaanoo muslimeen
HUENDA ikawa walio kufuru wakatamani wange kuwa Waislamu.
🎤 Rekodi yako:
15:3 🔁 0/5
ذَرۡهُمۡ يَأۡكُلُواْ وَيَتَمَتَّعُواْ وَيُلۡهِهِمُ ٱلۡأَمَلُۖ فَسَوۡفَ يَعۡلَمُونَ  ۝٣
Zarhum yaakuloo wa tatamatta`oo wa yulhihimul amalu fasawfa ya`lamoon
Waache wale, na wastarehe, na iwazuge tamaa. Watakuja jua.
🎤 Rekodi yako:
15:4 🔁 0/5
وَمَآ أَهۡلَكۡنَا مِن قَرۡيَةٍ إِلَّا وَلَهَا كِتَابٌ مَّعۡلُومٌ  ۝٤
Wa maaa ahlaknaa min qaryatin illaa wa lahaa kitaabum ma`loom
Na hatukuuangamiza mji wowote ule ila ulikuwa na muda wake maalumu.
🎤 Rekodi yako:
15:5 🔁 0/5
مَّا تَسۡبِقُ مِنۡ أُمَّةٍ أَجَلَهَا وَمَا يَسۡتَـٔۡخِرُونَ  ۝٥
Maa tasbiqu min ummatin ajalahaa wa maa yastaakhiroon
Hawawezi watu wowote kuitangulia ajali yao, wala kuchelewa.
🎤 Rekodi yako:
15:6 🔁 0/5
وَقَالُواْ يَٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِي نُزِّلَ عَلَيۡهِ ٱلذِّكۡرُ إِنَّكَ لَمَجۡنُونٌ  ۝٦
Wa qaaloo yaaa aiyuhal lazee nuzzila `alaihiz Zikru innaka lamajnoon
Na walisema: Ewe uliyeteremshiwa Ukumbusho! Hakika wewe ni mwendawazimu.
🎤 Rekodi yako:
15:7 🔁 0/5
لَّوۡمَا تَأۡتِينَا بِٱلۡمَلَٰٓئِكَةِ إِن كُنتَ مِنَ ٱلصَّٰدِقِينَ  ۝٧
Law maa taateenaa bil malaaa`ikati in kunta minas saadiqeen
Mbona hutuletei Malaika ikiwa wewe ni miongoni mwa wasemao kweli?
🎤 Rekodi yako:
15:8 🔁 0/5
مَا نُنَزِّلُ ٱلۡمَلَٰٓئِكَةَ إِلَّا بِٱلۡحَقِّ وَمَا كَانُوٓاْ إِذًا مُّنظَرِينَ  ۝٨
Maa nunazzilul malaaa`i kata illaa bilhaqqi wa maa kaanooo izam munzareen
Sisi hatuwateremshi Malaika ila kwa sababu ya haki, na hapo hawatapewa muhula.
🎤 Rekodi yako:
15:9 🔁 0/5
إِنَّا نَحۡنُ نَزَّلۡنَا ٱلذِّكۡرَ وَإِنَّا لَهُۥ لَحَٰفِظُونَ  ۝٩
Innaa Nahnu nazalnaz Zikra wa Innaa lahoo lahaa fizoon
Hakika Sisi ndio tulio teremsha Ukumbusho huu, na hakika Sisi ndio tutao ulinda.
🎤 Rekodi yako:
15:10 🔁 0/5
وَلَقَدۡ أَرۡسَلۡنَا مِن قَبۡلِكَ فِي شِيَعِ ٱلۡأَوَّلِينَ  ۝١٠
Wa laqad arsalnaa min qablika fee shiya`il awwaleen
Na hakika tulikwisha watumia Mitume mataifa ya mwanzo.
🎤 Rekodi yako:
15:11 🔁 0/5
وَمَا يَأۡتِيهِم مِّن رَّسُولٍ إِلَّا كَانُواْ بِهِۦ يَسۡتَهۡزِءُونَ  ۝١١
Wa maa yaateehim mir Rasoolin illaa kaanoo bihee yastahzi`oon
Na hakuwafikia Mtume ila walimkejeli.
🎤 Rekodi yako:
15:12 🔁 0/5
كَذَٰلِكَ نَسۡلُكُهُۥ فِي قُلُوبِ ٱلۡمُجۡرِمِينَ  ۝١٢
kazaalika naslukuhoo fee quloobil mujrimeen
Na kama hivi ndivyo tunavyo ingiza katika nyoyo za wakosefu.
🎤 Rekodi yako:
15:13 🔁 0/5
لَا يُؤۡمِنُونَ بِهِۦ وَقَدۡ خَلَتۡ سُنَّةُ ٱلۡأَوَّلِينَ  ۝١٣
Laa yu`minoona bihee wa qad khalat sunnatul awwaleen
Hawayaamini haya, na hali ya kuwa umekwisha wapitia mfano wa watu wa kale.
🎤 Rekodi yako:
15:14 🔁 0/5
وَلَوۡ فَتَحۡنَا عَلَيۡهِم بَابًا مِّنَ ٱلسَّمَآءِ فَظَلُّواْ فِيهِ يَعۡرُجُونَ  ۝١٤
Wa law fatahnaa `alaihim baabam minas samaaa`i fazaloo feehi ya`rujoon
Na lau tungeli wafungulia mlango wa mbingu, wakawa wanapanda,
🎤 Rekodi yako:
15:15 🔁 0/5
لَقَالُوٓاْ إِنَّمَا سُكِّرَتۡ أَبۡصَٰرُنَا بَلۡ نَحۡنُ قَوۡمٌ مَّسۡحُورُونَ  ۝١٥
Laqaaloo innamaa sukkirat absaarunaa bal nahnu qawmum mashooroon
Basi wangeli sema: Macho yetu yamelevywa, bali sisi wenyewe tumerogwa.
🎤 Rekodi yako:
15:16 🔁 0/5
وَلَقَدۡ جَعَلۡنَا فِي ٱلسَّمَآءِ بُرُوجًا وَزَيَّنَّٰهَا لِلنَّٰظِرِينَ  ۝١٦
Wa laqad ja`alnaa fissamaaa`i buroojanw wa zaiyannaahaa linnaazireen
Na hakika tumeweka katika mbingu vituo vya sayari, na tumezipamba kwa wenye kuangalia.
🎤 Rekodi yako:
15:17 🔁 0/5
وَحَفِظۡنَٰهَا مِن كُلِّ شَيۡطَٰنٍ رَّجِيمٍ  ۝١٧
Wa hafiznaahaa min kulli Shaitaanir rajeem
Na tumezilinda na kila shetani afukuzwaye.
🎤 Rekodi yako:
15:18 🔁 0/5
إِلَّا مَنِ ٱسۡتَرَقَ ٱلسَّمۡعَ فَأَتۡبَعَهُۥ شِهَابٌ مُّبِينٌ  ۝١٨
Illaa manis taraqas sam`a fa atba`ahoo shihaabum mubeen
Isipo kuwa mwenye kusikiliza kwa kuibia, naye hufuatwa na kijinga cha moto kinacho onekana.
🎤 Rekodi yako:
15:19 🔁 0/5
وَٱلۡأَرۡضَ مَدَدۡنَٰهَا وَأَلۡقَيۡنَا فِيهَا رَوَٰسِيَ وَأَنۢبَتۡنَا فِيهَا مِن كُلِّ شَيۡءٍ مَّوۡزُونٍ  ۝١٩
Wal arda madadnaahaa wa alqainaa feehaa rawaasiya wa ambatnaa feehaa min kulli shai`im mawzoon
Na ardhi tumeitandaza na humo tumeweka milima, na tumeotesha kila kitu kwa kiasi chake.
🎤 Rekodi yako:
15:20 🔁 0/5
وَجَعَلۡنَا لَكُمۡ فِيهَا مَعَٰيِشَ وَمَن لَّسۡتُمۡ لَهُۥ بِرَٰزِقِينَ  ۝٢٠
Wa ja`alnaa lakum feehaa ma`aayisha wa mal lastum lahoo biraaziqeen
Na tumekujaalieni humo vitu vya maisha yenu, na ya hao ambao nyinyi sio wenye kuwaruzuku.
🎤 Rekodi yako:
15:21 🔁 0/5
وَإِن مِّن شَيۡءٍ إِلَّا عِندَنَا خَزَآئِنُهُۥ وَمَا نُنَزِّلُهُۥٓ إِلَّا بِقَدَرٍ مَّعۡلُومٍ  ۝٢١
Wa im min shai`in illaa `indanaa khazaaa `inuhoo wa maa nunazziluhooo illaa biqadarim ma`loom
Na hakuna chochote ila asili yake inatokana na Sisi; wala hatukiteremshi ila kwa kipimo maalumu.
🎤 Rekodi yako:
15:22 🔁 0/5
وَأَرۡسَلۡنَا ٱلرِّيَٰحَ لَوَٰقِحَ فَأَنزَلۡنَا مِنَ ٱلسَّمَآءِ مَآءً فَأَسۡقَيۡنَٰكُمُوهُ وَمَآ أَنتُمۡ لَهُۥ بِخَٰزِنِينَ  ۝٢٢
Wa arsalnar riyaaha la waaqiha fa anzalnaa minas samaaa`i maaa`an fa asqai naakumoohu wa maaa antum lahoo bikhaazineen
Na tunazipeleka pepo za kupandishia, na tunateremsha kutoka mbinguni maji, kisha tukakunywesheni maji hayo. Wala si nyinyi mnayo yaweka.
🎤 Rekodi yako:
15:23 🔁 0/5
وَإِنَّا لَنَحۡنُ نُحۡيِۦ وَنُمِيتُ وَنَحۡنُ ٱلۡوَٰرِثُونَ  ۝٢٣
Wa innnaa la nahnu nuhyee wa numeetu wa nahnul waarisoon
Na Sisi ndio tunao huisha na tunao fisha. Na Sisi ndio Warithi.
🎤 Rekodi yako:
15:24 🔁 0/5
وَلَقَدۡ عَلِمۡنَا ٱلۡمُسۡتَقۡدِمِينَ مِنكُمۡ وَلَقَدۡ عَلِمۡنَا ٱلۡمُسۡتَـٔۡخِرِينَ  ۝٢٤
Wa la qad `alimnal mustaqdimeena minkum wa laqad `alimnal mustaakhireen
Na tunawajua walio tangulia katika nyinyi, na tunawajua walio taakhari.
🎤 Rekodi yako:
15:25 🔁 0/5
وَإِنَّ رَبَّكَ هُوَ يَحۡشُرُهُمۡۚ إِنَّهُۥ حَكِيمٌ عَلِيمٌ  ۝٢٥
Wa inna Rabbaka Huwa yahshuruhum; innahoo Hakeem `Aleem
Na hakika Mola wako Mlezi ndiye atakaye wakusanya. Hakika Yeye ni Mwenye hikima na Mjuzi.
🎤 Rekodi yako:
15:26 🔁 0/5
وَلَقَدۡ خَلَقۡنَا ٱلۡإِنسَٰنَ مِن صَلۡصَٰلٍ مِّنۡ حَمَإٍ مَّسۡنُونٍ  ۝٢٦
Wa laqad khalaqnal insaana min salsaalim min hama im masnoon
Na tulimuumba mtu kwa udongo unao toa sauti, unao tokana na matope yaliyo tiwa sura.
🎤 Rekodi yako:
15:27 🔁 0/5
وَٱلۡجَآنَّ خَلَقۡنَٰهُ مِن قَبۡلُ مِن نَّارِ ٱلسَّمُومِ  ۝٢٧
Waljaaanna khalaqnaahu min qablu min naaris samoom
Na majini tuliwaumba kabla kwa moto wa upepo umoto.
🎤 Rekodi yako:
15:28 🔁 0/5
وَإِذۡ قَالَ رَبُّكَ لِلۡمَلَٰٓئِكَةِ إِنِّي خَٰلِقُۢ بَشَرًا مِّن صَلۡصَٰلٍ مِّنۡ حَمَإٍ مَّسۡنُونٍ  ۝٢٨
Wa iz qaala Rabbuka lilmalaaa` ikati innee khaaliqum basharam min salsaalim min hama im masnoon
Na Mola wako Mlezi alipo waambia Malaika: Hakika Mimi nitamuumba mtu kwa udongo unao toa sauti, unao tokana na matope yaliyo tiwa sura.
🎤 Rekodi yako:
15:29 🔁 0/5
فَإِذَا سَوَّيۡتُهُۥ وَنَفَخۡتُ فِيهِ مِن رُّوحِي فَقَعُواْ لَهُۥ سَٰجِدِينَ  ۝٢٩
Fa izaa sawwaituhoo wa nafakhtu feehi mir roohee faqa`oo lahoo saajideen
Basi nitakapo mkamilisha na nikampulizia roho yangu, basi mumwangukie kumsujudia.
🎤 Rekodi yako:
15:30 🔁 0/5
فَسَجَدَ ٱلۡمَلَٰٓئِكَةُ كُلُّهُمۡ أَجۡمَعُونَ  ۝٣٠
Fasajadal malaaa`ikatu kulluhum ajma`oon
Basi Malaika wote pamoja walimsujudia,
🎤 Rekodi yako:
15:31 🔁 0/5
إِلَّآ إِبۡلِيسَ أَبَىٰٓ أَن يَكُونَ مَعَ ٱلسَّٰجِدِينَ  ۝٣١
Illaaa ibleesa abaaa ai yakoona ma`as saajideen
Isipo kuwa Iblisi. Yeye alikataa kuwa pamoja na walio sujudu.
🎤 Rekodi yako:
15:32 🔁 0/5
قَالَ يَٰٓإِبۡلِيسُ مَا لَكَ أَلَّا تَكُونَ مَعَ ٱلسَّٰجِدِينَ  ۝٣٢
Qaala yaaa Ibleesu maa laka allaa takoona ma`as saajideen
(Mwenyezi Mungu) akasema: Ewe Iblisi! Una nini hata hukuwa pamoja na walio sujudu?
🎤 Rekodi yako:
15:33 🔁 0/5
قَالَ لَمۡ أَكُن لِّأَسۡجُدَ لِبَشَرٍ خَلَقۡتَهُۥ مِن صَلۡصَٰلٍ مِّنۡ حَمَإٍ مَّسۡنُونٍ  ۝٣٣
Qaala lam akul li asjuda libasharin khalaqtahoo min salsaalim min hama im masnoon
Akasema: Haiwi mimi nimsujudie mtu uliye muumba kwa udongo unao toa sauti, unao tokana na matope yenye sura.
🎤 Rekodi yako:
15:34 🔁 0/5
قَالَ فَٱخۡرُجۡ مِنۡهَا فَإِنَّكَ رَجِيمٌ  ۝٣٤
Qaala fakhruj minhaa fa innaka rajeem
(Mwenyezi Mungu) akasema: Basi toka humo, kwani hakika wewe ni maluuni!
🎤 Rekodi yako:
15:35 🔁 0/5
وَإِنَّ عَلَيۡكَ ٱللَّعۡنَةَ إِلَىٰ يَوۡمِ ٱلدِّينِ  ۝٣٥
Wa inna `alikal la`nata ilaa Yawmid Deen
Na hakika juu yako ipo laana mpaka Siku ya Malipo.
🎤 Rekodi yako:
15:36 🔁 0/5
قَالَ رَبِّ فَأَنظِرۡنِيٓ إِلَىٰ يَوۡمِ يُبۡعَثُونَ  ۝٣٦
Qaala Rabbi fa anzirneee ilaa Yawmi yub`asoon
Akasema (Iblisi): Mola wangu Mlezi! Nipe muhula mpaka siku watapo fufuliwa.
🎤 Rekodi yako:
15:37 🔁 0/5
قَالَ فَإِنَّكَ مِنَ ٱلۡمُنظَرِينَ  ۝٣٧
Qaala fa innaka minal munzareen
(Mwenyezi Mungu) akasema: Hakika wewe ni katika walio pewa muhula
🎤 Rekodi yako:
15:38 🔁 0/5
إِلَىٰ يَوۡمِ ٱلۡوَقۡتِ ٱلۡمَعۡلُومِ  ۝٣٨
Ilaa Yawmil waqtil ma`loom
Mpaka siku ya wakati maalumu.
🎤 Rekodi yako:
15:39 🔁 0/5
قَالَ رَبِّ بِمَآ أَغۡوَيۡتَنِي لَأُزَيِّنَنَّ لَهُمۡ فِي ٱلۡأَرۡضِ وَلَأُغۡوِيَنَّهُمۡ أَجۡمَعِينَ  ۝٣٩
Qaala Rabbi bimaaa aghwaitanee la uzayyinaana lahum fil ardi wa la ughwiyan nahum ajma`een
Akasema: Mola wangu Mlezi! Ilivyo kuwa umenitia makosani, basi nahakikisha nitawazaini hapa duniani na nitawapoteza wote,
🎤 Rekodi yako:
15:40 🔁 0/5
إِلَّا عِبَادَكَ مِنۡهُمُ ٱلۡمُخۡلَصِينَ  ۝٤٠
Illaa `ibaadaka minhumul mukhlaseen
Ila waja wako walio safika.
🎤 Rekodi yako:
15:41 🔁 0/5
قَالَ هَٰذَا صِرَٰطٌ عَلَيَّ مُسۡتَقِيمٌ  ۝٤١
Qaala haaza Siraatun `alaiya Mustaqeem
Akasema: Hii Njia ya kujia kwangu Iliyo Nyooka.
🎤 Rekodi yako:
15:42 🔁 0/5
إِنَّ عِبَادِي لَيۡسَ لَكَ عَلَيۡهِمۡ سُلۡطَٰنٌ إِلَّا مَنِ ٱتَّبَعَكَ مِنَ ٱلۡغَاوِينَ  ۝٤٢
Inna `ibaadee laisa laka `alaihim sultaanun illaa manittaba`aka minal ghaaween
Hakika waja wangu, wewe hutakuwa na mamlaka juu yao, isipo kuwa wale wapotofu walio kufuata.
🎤 Rekodi yako:
15:43 🔁 0/5
وَإِنَّ جَهَنَّمَ لَمَوۡعِدُهُمۡ أَجۡمَعِينَ  ۝٤٣
Wa inna jahannama lamaw`iduhum ajma`een
Na bila shaka Jahannamu ndipo pahali pao walipo ahidiwa wote.
🎤 Rekodi yako:
15:44 🔁 0/5
لَهَا سَبۡعَةُ أَبۡوَٰبٍ لِّكُلِّ بَابٍ مِّنۡهُمۡ جُزۡءٌ مَّقۡسُومٌ  ۝٤٤
Lahaa sab`atu abwaab; likulli baabim minhum juz`um maqsoom
Ina milango saba; na kwa kila mlango iko sehemu walio tengewa.
🎤 Rekodi yako:
15:45 🔁 0/5
إِنَّ ٱلۡمُتَّقِينَ فِي جَنَّٰتٍ وَعُيُونٍ  ۝٤٥
Innal muttaqeena fee Jannaatinw wa `uyoon
Hakika wachamngu watakuwa katika Mabustani na chemchem.
🎤 Rekodi yako:
15:46 🔁 0/5
ٱدۡخُلُوهَا بِسَلَٰمٍ ءَامِنِينَ  ۝٤٦
Udkhuloohaa bisalaamin aamineen
(Wataambiwa:) Ingieni kwa salama na amani.
🎤 Rekodi yako:
15:47 🔁 0/5
وَنَزَعۡنَا مَا فِي صُدُورِهِم مِّنۡ غِلٍّ إِخۡوَٰنًا عَلَىٰ سُرُرٍ مُّتَقَٰبِلِينَ  ۝٤٧
Wa naza`naa ma fee sudoorihim min ghillin ikhwaanan `alaa sururim mutaqaabileen
Na tutaondoa chuki iliyo kuwamo vifuani mwao, wawe ndugu juu ya viti vya enzi wameelekeana.
🎤 Rekodi yako:
15:48 🔁 0/5
لَا يَمَسُّهُمۡ فِيهَا نَصَبٌ وَمَا هُم مِّنۡهَا بِمُخۡرَجِينَ  ۝٤٨
Laa yamas suhum feehaa nasabunw wa maa hum minhaa bimukhrajeen
Humo hayatawagusa machofu, wala hawatatolewa humo.
🎤 Rekodi yako:
15:49 🔁 0/5
۞ نَبِّئۡ عِبَادِيٓ أَنِّيٓ أَنَا ٱلۡغَفُورُ ٱلرَّحِيمُ  ۝٤٩
Nabbi` `ibaadeee annneee anal Ghafoorur Raheem
Waambie waja wangu ya kwamba Mimi ndiye Mwenye kusamehe, Mwenye kurehemu.
🎤 Rekodi yako:
15:50 🔁 0/5
وَأَنَّ عَذَابِي هُوَ ٱلۡعَذَابُ ٱلۡأَلِيمُ  ۝٥٠
Wa anna `azaabee uwal `azaabul aleem
Na kwamba adhabu yangu ndio adhabu iliyo chungu!
🎤 Rekodi yako:
15:51 🔁 0/5
وَنَبِّئۡهُمۡ عَن ضَيۡفِ إِبۡرَٰهِيمَ  ۝٥١
Wa nabbi`hum `an daifi Ibraaheem
Na uwape khabari za wageni wa Ibrahim.
🎤 Rekodi yako:
15:52 🔁 0/5
إِذۡ دَخَلُواْ عَلَيۡهِ فَقَالُواْ سَلَٰمًا قَالَ إِنَّا مِنكُمۡ وَجِلُونَ  ۝٥٢
Iz dakhaloo `alaihi faqaaloo salaaman qaala innaa minkum wajiloon
Walipo ingia kwake na wakasema: Salama! Yeye akasema: Hakika sisi tunakuogopeni.
🎤 Rekodi yako:
15:53 🔁 0/5
قَالُواْ لَا تَوۡجَلۡ إِنَّا نُبَشِّرُكَ بِغُلَٰمٍ عَلِيمٍ  ۝٥٣
Qaaloo la tawjal innaa nubashshiruka bighulaamin `aleem
Wakasema: Usiogope. Sisi tunakubashiria kijana mwenye ujuzi.
🎤 Rekodi yako:
15:54 🔁 0/5
قَالَ أَبَشَّرۡتُمُونِي عَلَىٰٓ أَن مَّسَّنِيَ ٱلۡكِبَرُ فَبِمَ تُبَشِّرُونَ  ۝٥٤
Qaala abashshartumoonee `alaaa am massaniyal kibaru fabima tubashshiroon
Akasema: Mnanibashiria nami uzee umenishika! Basi kwa njia gani mnanibashiria?
🎤 Rekodi yako:
15:55 🔁 0/5
قَالُواْ بَشَّرۡنَٰكَ بِٱلۡحَقِّ فَلَا تَكُن مِّنَ ٱلۡقَٰنِطِينَ  ۝٥٥
Qaaloo bashsharnaaka bilhaqqi falaa takum minal qaaniteen
Wakasema: Tunakubashiria kwa haki; basi usiwe miongoni mwa wanao kata tamaa.
🎤 Rekodi yako:
15:56 🔁 0/5
قَالَ وَمَن يَقۡنَطُ مِن رَّحۡمَةِ رَبِّهِۦٓ إِلَّا ٱلضَّآلُّونَ  ۝٥٦
Qaala wa mai yaqnatu mir rahmati Rabbiheee illad daaaloon
Akasema: Na nani anaye kata tamaa na rehema ya Mola wake Mlezi ila wale walio potea?
🎤 Rekodi yako:
15:57 🔁 0/5
قَالَ فَمَا خَطۡبُكُمۡ أَيُّهَا ٱلۡمُرۡسَلُونَ  ۝٥٧
Qaala famaa khatbukum aiyuhal mursaloon
Akasema: Hebu nini amri yenu, enyi wajumbe?
🎤 Rekodi yako:
15:58 🔁 0/5
قَالُوٓاْ إِنَّآ أُرۡسِلۡنَآ إِلَىٰ قَوۡمٍ مُّجۡرِمِينَ  ۝٥٨
Qaaloo innaaa ursilnaaa ilaa qawmim mujrimeen
Wakasema: Hakika sisi tumetumwa kwa kaumu ya wakosefu!
🎤 Rekodi yako:
15:59 🔁 0/5
إِلَّآ ءَالَ لُوطٍ إِنَّا لَمُنَجُّوهُمۡ أَجۡمَعِينَ  ۝٥٩
Illaaa Aala Loot; innaa lamunajjoohum ajma`een
Isipo kuwa walio mfuata Luut'i. Bila ya shaka sisi tutawaokoa hao wote.
🎤 Rekodi yako:
15:60 🔁 0/5
إِلَّا ٱمۡرَأَتَهُۥ قَدَّرۡنَآ إِنَّهَا لَمِنَ ٱلۡغَٰبِرِينَ  ۝٦٠
Illam ra atahoo qaddarnaaa innahaa laminal ghaabireen
Ila mkewe. Tunakadiria huyo atakuwa miongoni watao bakia nyuma.
🎤 Rekodi yako:
15:61 🔁 0/5
فَلَمَّا جَآءَ ءَالَ لُوطٍ ٱلۡمُرۡسَلُونَ  ۝٦١
Falamma jaaa`a Aala Lootinil mursaloon
Basi wale wajumbe walipo fika kwa Luut'i,
🎤 Rekodi yako:
15:62 🔁 0/5
قَالَ إِنَّكُمۡ قَوۡمٌ مُّنكَرُونَ  ۝٦٢
Qaala innakum qawmum munkaroon
Alisema (Luut'i): Hakika nyinyi ni watu msio juulikana.
🎤 Rekodi yako:
15:63 🔁 0/5
قَالُواْ بَلۡ جِئۡنَٰكَ بِمَا كَانُواْ فِيهِ يَمۡتَرُونَ  ۝٦٣
Qaaloo bal ji`naaka bimaa kaanoo feehi yamtaroon
Wakasema: Bali sisi tumekuletea yale waliyo kuwa wakiyafanyia shaka.
🎤 Rekodi yako:
15:64 🔁 0/5
وَأَتَيۡنَٰكَ بِٱلۡحَقِّ وَإِنَّا لَصَٰدِقُونَ  ۝٦٤
Wa atainaaka bilhaqqi wa innaa lasaadiqoon
Na tumefika kwako kwa Haki, na hakika sisi tunasema kweli.
🎤 Rekodi yako:
15:65 🔁 0/5
فَأَسۡرِ بِأَهۡلِكَ بِقِطۡعٍ مِّنَ ٱلَّيۡلِ وَٱتَّبِعۡ أَدۡبَٰرَهُمۡ وَلَا يَلۡتَفِتۡ مِنكُمۡ أَحَدٌ وَٱمۡضُواْ حَيۡثُ تُؤۡمَرُونَ  ۝٦٥
Fa asri bi ahlika biqit`im minal laili wattabi` adbaarahum wa laa yaltafit minkum ahadunw wamdoo haisu tu`maroon
Basi ondoka na ahli zako usiku ungalipo, nawe ufuate nyuma yao, wala yeyote kati yenu asigeuke nyuma. Na mwende mnapo amrishwa.
🎤 Rekodi yako:
15:66 🔁 0/5
وَقَضَيۡنَآ إِلَيۡهِ ذَٰلِكَ ٱلۡأَمۡرَ أَنَّ دَابِرَ هَٰٓؤُلَآءِ مَقۡطُوعٌ مُّصۡبِحِينَ  ۝٦٦
Wa qadainaaa ilaihi zaalikal amra anna daabira haaa`ulaaa`i maqtoo`um musbiheen
Na tukamfunulia hukumu hiyo, ya kwamba hata wa mwisho wao hao ikifika asubuhi atakuwa kesha katiliwa mbali.
🎤 Rekodi yako:
15:67 🔁 0/5
وَجَآءَ أَهۡلُ ٱلۡمَدِينَةِ يَسۡتَبۡشِرُونَ  ۝٦٧
Wa jaaa`a ahlul madeenati yastabshiroon
Na wakaja watu wa mji ule nao furahani.
🎤 Rekodi yako:
15:68 🔁 0/5
قَالَ إِنَّ هَٰٓؤُلَآءِ ضَيۡفِي فَلَا تَفۡضَحُونِ  ۝٦٨
Qaala inna haaa`ulaaa`i daifee falaa tafdahoon
Akasema: Hakika hawa wageni wangu, basi msinifedheheshe.
🎤 Rekodi yako:
15:69 🔁 0/5
وَٱتَّقُواْ ٱللَّهَ وَلَا تُخۡزُونِ  ۝٦٩
Wattaqul laaha wa laa tukhzoon
Na mcheni Mwenyezi Mungu, wala msinihizi.
🎤 Rekodi yako:
15:70 🔁 0/5
قَالُوٓاْ أَوَلَمۡ نَنۡهَكَ عَنِ ٱلۡعَٰلَمِينَ  ۝٧٠
Qaalooo awalam nanhaka `anil `aalameen
Wakasema: Sisi hatukukukataza usimkaribishe yeyote?
🎤 Rekodi yako:
15:71 🔁 0/5
قَالَ هَٰٓؤُلَآءِ بَنَاتِيٓ إِن كُنتُمۡ فَٰعِلِينَ  ۝٧١
Qaala haaa`ulaaa`i banaateee in kuntum faa`ileen
Akasema: Hawa binti zangu, ikiwa nyinyi ni watendaji.
🎤 Rekodi yako:
15:72 🔁 0/5
لَعَمۡرُكَ إِنَّهُمۡ لَفِي سَكۡرَتِهِمۡ يَعۡمَهُونَ  ۝٧٢
La`amruka innahum lafee sakratihim ya`mahoon
Naapa kwa umri wako! Hakika hao walikuwa katika ulevi wao, wakihangaika ovyo.
🎤 Rekodi yako:
15:73 🔁 0/5
فَأَخَذَتۡهُمُ ٱلصَّيۡحَةُ مُشۡرِقِينَ  ۝٧٣
Fa akhazat humus saihatu mushriqeen
Ukelele ukawatwaa wakipambaukiwa.
🎤 Rekodi yako:
15:74 🔁 0/5
فَجَعَلۡنَا عَٰلِيَهَا سَافِلَهَا وَأَمۡطَرۡنَا عَلَيۡهِمۡ حِجَارَةً مِّن سِجِّيلٍ  ۝٧٤
Faja`alnaa `aaliyahaa saafilahaa wa amtamaa `alaihim hijaaratam min sjijjeel
Na tukaigeuza nchi juu chini, na tukawanyeshea mvua ya mawe ya udongo wa Motoni.
🎤 Rekodi yako:
15:75 🔁 0/5
إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَأٓيَٰتٍ لِّلۡمُتَوَسِّمِينَ  ۝٧٥
Inna fee zaalika la Aayaatil lilmutawassimeen
Hakika katika hayo zipo ishara kwa waaguzi.
🎤 Rekodi yako:
15:76 🔁 0/5
وَإِنَّهَا لَبِسَبِيلٍ مُّقِيمٍ  ۝٧٦
Wa innahaa labi sabeelim muqeem
Na miji hii ipo kwenye njia inayo pitiwa.
🎤 Rekodi yako:
15:77 🔁 0/5
إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَأٓيَةً لِّلۡمُؤۡمِنِينَ  ۝٧٧
Inna fee zaalika la Aayatal lilmu`mineen
Hakika katika hayo ipo ishara kwa Waumini.
🎤 Rekodi yako:
15:78 🔁 0/5
وَإِن كَانَ أَصۡحَٰبُ ٱلۡأَيۡكَةِ لَظَٰلِمِينَ  ۝٧٨
Wa in kaana Ashaabul Aikati lazaalimeen
Na hakika watu wa Kichakani walikuwa wenye kudhulumu.
🎤 Rekodi yako:
15:79 🔁 0/5
فَٱنتَقَمۡنَا مِنۡهُمۡ وَإِنَّهُمَا لَبِإِمَامٍ مُّبِينٍ  ۝٧٩
Fantaqamnaa minhum wa innahumaa labi imaamim mubeen
Kwa hivyo tukawaadhibu. Na nchi mbili hizi ziko kwenye njia ilio wazi.
🎤 Rekodi yako:
15:80 🔁 0/5
وَلَقَدۡ كَذَّبَ أَصۡحَٰبُ ٱلۡحِجۡرِ ٱلۡمُرۡسَلِينَ  ۝٨٠
Wa laqad kazzaba ashaabul Hijril mursaleen
Na bila ya shaka wakaazi wa Hijr waliwakanusha Mitume.
🎤 Rekodi yako:
15:81 🔁 0/5
وَءَاتَيۡنَٰهُمۡ ءَايَٰتِنَا فَكَانُواْ عَنۡهَا مُعۡرِضِينَ  ۝٨١
Wa aatainaahum Aayaatinaa fakaanoo `anhaa mu`rideen
Na tuliwapa ishara zetu, nao wakazipuuza.
🎤 Rekodi yako:
15:82 🔁 0/5
وَكَانُواْ يَنۡحِتُونَ مِنَ ٱلۡجِبَالِ بُيُوتًا ءَامِنِينَ  ۝٨٢
Wa kaanoo yanhitoona minal jibaali buyootan aamineen
Nao walikuwa wakichonga majumba katika milima kwa amani.
🎤 Rekodi yako:
15:83 🔁 0/5
فَأَخَذَتۡهُمُ ٱلصَّيۡحَةُ مُصۡبِحِينَ  ۝٨٣
Fa akhazat humus saihatu musbiheen
Basi ukelele ukawatwaa asubuhi.
🎤 Rekodi yako:
15:84 🔁 0/5
فَمَآ أَغۡنَىٰ عَنۡهُم مَّا كَانُواْ يَكۡسِبُونَ  ۝٨٤
Famaaa aghnaa `anhum maa kaanoo yaksiboon
Hayakuwafaa waliyo kuwa wakiyachuma.
🎤 Rekodi yako:
15:85 🔁 0/5
وَمَا خَلَقۡنَا ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضَ وَمَا بَيۡنَهُمَآ إِلَّا بِٱلۡحَقِّۗ وَإِنَّ ٱلسَّاعَةَ لَأٓتِيَةٌۖ فَٱصۡفَحِ ٱلصَّفۡحَ ٱلۡجَمِيلَ  ۝٨٥
Wa maa khalaqnas samaawaati wal arda wa maa bainahumaaa illaa bilhaqq; wa innas Saa`ata la aatiyatun fasfahis safhal jameel
Na hatukuziumba mbingu na ardhi na vilivyomo ndani yake ila kwa ajili ya Haki. Na hakika Kiyama kitafika. Basi samehe msamaha mzuri.
🎤 Rekodi yako:
15:86 🔁 0/5
إِنَّ رَبَّكَ هُوَ ٱلۡخَلَّٰقُ ٱلۡعَلِيمُ  ۝٨٦
Inna Rabbaka Huwal khallaaqul `aleem
Hakika Mola wako Mlezi ndiye Muumbaji Mjuzi.
🎤 Rekodi yako:
15:87 🔁 0/5
وَلَقَدۡ ءَاتَيۡنَٰكَ سَبۡعًا مِّنَ ٱلۡمَثَانِي وَٱلۡقُرۡءَانَ ٱلۡعَظِيمَ  ۝٨٧
Wa laqad aatainaaka sab`am mnal masaanee wal Qur-aanal `azeem
Na tumekupa Aya saba zinazo somwa mara kwa mara, na Qur'ani Tukufu.
🎤 Rekodi yako:
15:88 🔁 0/5
لَا تَمُدَّنَّ عَيۡنَيۡكَ إِلَىٰ مَا مَتَّعۡنَا بِهِۦٓ أَزۡوَٰجًا مِّنۡهُمۡ وَلَا تَحۡزَنۡ عَلَيۡهِمۡ وَٱخۡفِضۡ جَنَاحَكَ لِلۡمُؤۡمِنِينَ  ۝٨٨
Laa tamuddanna `ainaika ilaa maa matta `naa biheee azwaajam minhum wa laa tahzan `alaihim wakhfid janaahaka lilmu `mineen
Usivitumbulie macho yako vitu tulivyo waneemesha makundi fulani kati yao, wala usiwahuzunikie. Na wainamishie bawa lako (la huruma) Waumini.
🎤 Rekodi yako:
15:89 🔁 0/5
وَقُلۡ إِنِّيٓ أَنَا ٱلنَّذِيرُ ٱلۡمُبِينُ  ۝٨٩
Wa qul inneee anan nazeerul mubeen
Na sema: Hakika mimi ni mwonyaji mwenye kubainisha.
🎤 Rekodi yako:
15:90 🔁 0/5
كَمَآ أَنزَلۡنَا عَلَى ٱلۡمُقۡتَسِمِينَ  ۝٩٠
Kamaaa anzalnaa `alal muqtasimeen
Kama hivyo tuliwateremshia walio gawa,
🎤 Rekodi yako:
15:91 🔁 0/5
ٱلَّذِينَ جَعَلُواْ ٱلۡقُرۡءَانَ عِضِينَ  ۝٩١
Allazeena ja`alul Quraana`ideen
Ambao wakaifanya Qur'ani vipande vipande.
🎤 Rekodi yako:
15:92 🔁 0/5
فَوَرَبِّكَ لَنَسۡـَٔلَنَّهُمۡ أَجۡمَعِينَ  ۝٩٢
Fawa Rabbika lanas`a lannahum ajma`een
Basi Naapa kwa Mola wako Mlezi! Tutawahoji wote,
🎤 Rekodi yako:
15:93 🔁 0/5
عَمَّا كَانُواْ يَعۡمَلُونَ  ۝٩٣
Ammaa kaanoo ya`maloon
Kwa waliyo kuwa wakiyatenda.
🎤 Rekodi yako:
15:94 🔁 0/5
فَٱصۡدَعۡ بِمَا تُؤۡمَرُ وَأَعۡرِضۡ عَنِ ٱلۡمُشۡرِكِينَ  ۝٩٤
Fasda` bimaa tu`maru wa a`rid anil mushrikeen
Basi wewe yatangaze uliyo amrishwa, na jitenge na washirikina.
🎤 Rekodi yako:
15:95 🔁 0/5
إِنَّا كَفَيۡنَٰكَ ٱلۡمُسۡتَهۡزِءِينَ  ۝٩٥
Innaa kafainaakal mustahzi`een
Hakika Sisi tunatosha kukukinga na wanao kejeli.
🎤 Rekodi yako:
15:96 🔁 0/5
ٱلَّذِينَ يَجۡعَلُونَ مَعَ ٱللَّهِ إِلَٰهًا ءَاخَرَۚ فَسَوۡفَ يَعۡلَمُونَ  ۝٩٦
Allazeena yaj`aloona ma`al laahi ilaahan aakhar; fasawfa ya`lamoon
Hao wanao fanya kuwa pamoja na Mwenyezi Mungu yupo mungu mwingine. Basi, watakuja jua!
🎤 Rekodi yako:
15:97 🔁 0/5
وَلَقَدۡ نَعۡلَمُ أَنَّكَ يَضِيقُ صَدۡرُكَ بِمَا يَقُولُونَ  ۝٩٧
Wa laqad na`lamu annak yadeequ sadruka bimaa yaqooloon
Na Sisi tunajua kwa hakika kuwa wewe kifua chako kinaona dhiki kwa hayo wayasemayo.
🎤 Rekodi yako:
15:98 🔁 0/5
فَسَبِّحۡ بِحَمۡدِ رَبِّكَ وَكُن مِّنَ ٱلسَّٰجِدِينَ  ۝٩٨
Fasbbih bihamdi Rabbika wa kum minas saajideen
Basi mtakase Mola wako Mlezi kwa kumhimidi, na uwe miongoni wanao msujudia.
🎤 Rekodi yako:
15:99 🔁 0/5
وَٱعۡبُدۡ رَبَّكَ حَتَّىٰ يَأۡتِيَكَ ٱلۡيَقِينُ  ۝٩٩
Wa`bud Rabbaka hattaa yaatiyakal yaqeen
Na muabudu Mola wako Mlezi mpaka ikufikie Yakini.
🎤 Rekodi yako:
💡 Gusa neno lililofichwa ili lionekane kwa muda — maendeleo yako yanahifadhiwa kiotomatiki.

🎉
🎊 Hongera! Umemaliza Kuhifadhi
Mishary Rashid Alafasy
Mahmoud Khalil Al-Husary
Abdurrahman As-Sudais
Mohamed Siddiq Al-Minshawi
Abdul Basit Abdul Samad
Ali Al-Hudhaify
Ahmed ibn Ali al-Ajamy
Abu Bakr Ash-Shaatree
Muhammad Ayyoub
Abdullah Basfar
Abdullah Al-Juhani
Maher Al Muaiqly
0:00
0:00
-

Kurani Tukufu


Tuesday, August 18, 2026

Usitusahau katika dua zako njema