🔥 0 siku mfululizo
📖 Sura ndefu — imegawanywa sehemu ndogo (118 Aya)
📚 Sura Zote
30%
🎤 Gusa ikoni ya maikrofoni 🎙️ karibu na aya yoyote ili kujirekodi, kisha sikiliza na ulinganishe na qari.
0/118
23:1 🔁 0/5
قَدۡ أَفۡلَحَ ٱلۡمُؤۡمِنُونَ  ۝١
Qad aflahal mu`minoon
HAKIKA wamefanikiwa Waumini,
🎤 Rekodi yako:
23:2 🔁 0/5
ٱلَّذِينَ هُمۡ فِي صَلَاتِهِمۡ خَٰشِعُونَ  ۝٢
Allazeena hum fee Salaatihim khaashi`oon
Ambao ni wanyenyekevu katika Sala zao,
🎤 Rekodi yako:
23:3 🔁 0/5
وَٱلَّذِينَ هُمۡ عَنِ ٱللَّغۡوِ مُعۡرِضُونَ  ۝٣
Wallazeena hum `anillaghwimu`ridoon
Na ambao hujiepusha na mambo ya upuuzi,
🎤 Rekodi yako:
23:4 🔁 0/5
وَٱلَّذِينَ هُمۡ لِلزَّكَوٰةِ فَٰعِلُونَ  ۝٤
Wallazeena hum liz Zakaati faa`iloon
Na ambao wanatoa Zaka,
🎤 Rekodi yako:
23:5 🔁 0/5
وَٱلَّذِينَ هُمۡ لِفُرُوجِهِمۡ حَٰفِظُونَ  ۝٥
Wallazeena hum lifuroo jihim haafizoon
Na ambao wanazilinda tupu zao,
🎤 Rekodi yako:
23:6 🔁 0/5
إِلَّا عَلَىٰٓ أَزۡوَٰجِهِمۡ أَوۡ مَا مَلَكَتۡ أَيۡمَٰنُهُمۡ فَإِنَّهُمۡ غَيۡرُ مَلُومِينَ  ۝٦
Illaa `alaaa azwaajihim aw maa malakat aimaanuhum fa innahum ghairu maloomeen
Isipo kuwa kwa wake zao au kwa iliyo wamiliki mikono yao ya kulia. Kwani hao si wenye kulaumiwa.
🎤 Rekodi yako:
23:7 🔁 0/5
فَمَنِ ٱبۡتَغَىٰ وَرَآءَ ذَٰلِكَ فَأُوْلَٰٓئِكَ هُمُ ٱلۡعَادُونَ  ۝٧
Famanib taghaa waraaa`a zaalika fa ulaaa`ika humul `aadoon
Lakini anaye taka kinyume cha haya, basi hao ndio warukao mipaka.
🎤 Rekodi yako:
23:8 🔁 0/5
وَٱلَّذِينَ هُمۡ لِأَمَٰنَٰتِهِمۡ وَعَهۡدِهِمۡ رَٰعُونَ  ۝٨
Wallazeena hum li amaanaatihim wa `ahdihim raa`oon
Na ambao wanazitimiza amana zao na ahadi zao,
🎤 Rekodi yako:
23:9 🔁 0/5
وَٱلَّذِينَ هُمۡ عَلَىٰ صَلَوَٰتِهِمۡ يُحَافِظُونَ  ۝٩
Wallazeena hum `alaa Salawaatihim yuhaafizoon
Na ambao Sala zao wanazihifadhi -
🎤 Rekodi yako:
23:10 🔁 0/5
أُوْلَٰٓئِكَ هُمُ ٱلۡوَٰرِثُونَ  ۝١٠
Ulaaa`ika humul waarisoon
Hao ndio warithi,
🎤 Rekodi yako:
23:11 🔁 0/5
ٱلَّذِينَ يَرِثُونَ ٱلۡفِرۡدَوۡسَ هُمۡ فِيهَا خَٰلِدُونَ  ۝١١
Allazeena yarisoonal Firdawsa hum feehaa khaalidoon
Ambao watairithi Pepo ya Firdausi, wadumu humo.
🎤 Rekodi yako:
23:12 🔁 0/5
وَلَقَدۡ خَلَقۡنَا ٱلۡإِنسَٰنَ مِن سُلَٰلَةٍ مِّن طِينٍ  ۝١٢
Wa laqad khalaqnal insaana min sulaalatim minteen
Na kwa yakini tumemuumba mtu kutokana na asli ya udongo.
🎤 Rekodi yako:
23:13 🔁 0/5
ثُمَّ جَعَلۡنَٰهُ نُطۡفَةً فِي قَرَارٍ مَّكِينٍ  ۝١٣
Summa ja`alnaahu nutfatan fee qaraarim makeen
Kisha tukamjaalia awe tone ya mbegu ya uzazi katika kalio madhubuti.
🎤 Rekodi yako:
23:14 🔁 0/5
ثُمَّ خَلَقۡنَا ٱلنُّطۡفَةَ عَلَقَةً فَخَلَقۡنَا ٱلۡعَلَقَةَ مُضۡغَةً فَخَلَقۡنَا ٱلۡمُضۡغَةَ عِظَٰمًا فَكَسَوۡنَا ٱلۡعِظَٰمَ لَحۡمًا ثُمَّ أَنشَأۡنَٰهُ خَلۡقًا ءَاخَرَۚ فَتَبَارَكَ ٱللَّهُ أَحۡسَنُ ٱلۡخَٰلِقِينَ  ۝١٤
Summa khalaqnan nutfata `alaqatan fakhalaqnal `alaqata mudghatan fakhalaq nal mudghata `izaaman fakasawnal `izaama lahman summa anshaanaahu khalqan aakhar; fatabaarakal laahu ahsanul khaaliqeen
Kisha tukaiumba tone kuwa damu iliyo ganda, na tukaiumba damu kuwa pande la nyama, kisha tukaliumba pande la nyama kuwa mifupa, na mifupa tukaivika nyama. Kisha tukamfanya kiumbe mwengine. Basi ametukuka Mwenyezi Mungu Mbora wa waumbaji.
🎤 Rekodi yako:
23:15 🔁 0/5
ثُمَّ إِنَّكُم بَعۡدَ ذَٰلِكَ لَمَيِّتُونَ  ۝١٥
Summa innakum ba`da zaalika la maaiyitoon
Kisha hakika nyinyi baada ya hayo mtakufa.
🎤 Rekodi yako:
23:16 🔁 0/5
ثُمَّ إِنَّكُمۡ يَوۡمَ ٱلۡقِيَٰمَةِ تُبۡعَثُونَ  ۝١٦
Summa innakum Yawmal Qiyaamati tub`asoon
Kisha hakika nyinyi Siku ya Kiyama mtafufuliwa.
🎤 Rekodi yako:
23:17 🔁 0/5
وَلَقَدۡ خَلَقۡنَا فَوۡقَكُمۡ سَبۡعَ طَرَآئِقَ وَمَا كُنَّا عَنِ ٱلۡخَلۡقِ غَٰفِلِينَ  ۝١٧
Wa laqad khalaqnaa fawqakum sab`a taraaa`iqa wa maa kunnaa `anil khalqi ghaafileen
Na kwa yakini tumeziumba juu yenu njia saba. Nasi hatukuwa wenye kughafilika na viumbe.
🎤 Rekodi yako:
23:18 🔁 0/5
وَأَنزَلۡنَا مِنَ ٱلسَّمَآءِ مَآءَۢ بِقَدَرٍ فَأَسۡكَنَّٰهُ فِي ٱلۡأَرۡضِۖ وَإِنَّا عَلَىٰ ذَهَابِۭ بِهِۦ لَقَٰدِرُونَ  ۝١٨
Wa anzalnaa minas samaaa`i maaa`am biqadarin fa-askannaahu fil ardi wa innaa `alaa zahaabim bihee laqaa diroon
Na tumeteremsha kutoka mbinguni maji kwa kiasi na tukayatuliza katika ardhi. Na hakika Sisi tunaweza kuyaondoa.
🎤 Rekodi yako:
23:19 🔁 0/5
فَأَنشَأۡنَا لَكُم بِهِۦ جَنَّٰتٍ مِّن نَّخِيلٍ وَأَعۡنَٰبٍ لَّكُمۡ فِيهَا فَوَٰكِهُ كَثِيرَةٌ وَمِنۡهَا تَأۡكُلُونَ  ۝١٩
Fa anshaanaa lakum bihee Jannaatim min nakheelinw wa a`naab; lakum feehaa fawaakihu kaseeratunw wa minhaa taakuloon
Kwa maji hayo tukakufanyieni bustani za mitende na mizabibu, mnapata humo matunda mengi, na katika hayo mnakula;
🎤 Rekodi yako:
23:20 🔁 0/5
وَشَجَرَةً تَخۡرُجُ مِن طُورِ سَيۡنَآءَ تَنۢبُتُ بِٱلدُّهۡنِ وَصِبۡغٍ لِّلۡأٓكِلِينَ  ۝٢٠
Wa shajaratan takhruju min Toori Sainaaa`a tambutu bidduhni wa sibghil lil aakileen
Na mti utokao katika mlima wa Sinai, unatoa mafuta na kuwa kitoweo kwa walao.
🎤 Rekodi yako:
23:21 🔁 0/5
وَإِنَّ لَكُمۡ فِي ٱلۡأَنۡعَٰمِ لَعِبۡرَةًۖ نُّسۡقِيكُم مِّمَّا فِي بُطُونِهَا وَلَكُمۡ فِيهَا مَنَٰفِعُ كَثِيرَةٌ وَمِنۡهَا تَأۡكُلُونَ  ۝٢١
Wa inna lakum fil an`aami la`ibrah; nusqeekum mimmaa fee butoonihaa wa lakum feehaa manaafi`u kaseeratunw wa minhaa taakuloon
Na hakika mnayo mazingatio makubwa katika nyama hoa - tunakunywesheni katika vile viliomo matumboni mwao, na nyinyi mnapata katika hao manufaa mengi, na pia mnawala.
🎤 Rekodi yako:
23:22 🔁 0/5
وَعَلَيۡهَا وَعَلَى ٱلۡفُلۡكِ تُحۡمَلُونَ  ۝٢٢
Wa `alaihaa wa`alal fulki tuhmaloon
Na juu yao na juu ya marikebu mnabebwa.
🎤 Rekodi yako:
23:23 🔁 0/5
وَلَقَدۡ أَرۡسَلۡنَا نُوحًا إِلَىٰ قَوۡمِهِۦ فَقَالَ يَٰقَوۡمِ ٱعۡبُدُواْ ٱللَّهَ مَا لَكُم مِّنۡ إِلَٰهٍ غَيۡرُهُۥٓۚ أَفَلَا تَتَّقُونَ  ۝٢٣
Wa laqad arsalnaa Noohan ilaa qawmihee faqaala yaa qawmi`budul laaha maa lakum min ilahin ghairuhoo afalaa tattaqoon
Na hakika tulimtuma Nuhu kwa watu wake, akasema: Enyi watu wangu! Muabuduni Mwenyezi Mungu. Nyinyi hamna mungu asiye kuwa Yeye. Basi je! Hamwogopi?
🎤 Rekodi yako:
23:24 🔁 0/5
فَقَالَ ٱلۡمَلَؤُاْ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ مِن قَوۡمِهِۦ مَا هَٰذَآ إِلَّا بَشَرٌ مِّثۡلُكُمۡ يُرِيدُ أَن يَتَفَضَّلَ عَلَيۡكُمۡ وَلَوۡ شَآءَ ٱللَّهُ لَأَنزَلَ مَلَٰٓئِكَةً مَّا سَمِعۡنَا بِهَٰذَا فِيٓ ءَابَآئِنَا ٱلۡأَوَّلِينَ  ۝٢٤
Faqaalal mala`ul lazeena kafaroo min qawmihee maa haazaaa illaa basharum mislukum yureedu ai yatafaddala `alaikum wa law shaaa`al laahu la anzala malaaa`ikatam maa sami`naa bihaazaa feee aabaaa`inal awwaleen
Walisema wale wakuu walio kufuru katika watu wake: Huyu si chochote ila ni mtu tu kama nyinyi. Anataka kujipa ubora juu yenu. Na lau kuwa Mwenyezi Mungu amependa basi yakini angeli teremsha Malaika. Hatukusikia haya kwa baba zetu wa zamani.
🎤 Rekodi yako:
23:25 🔁 0/5
إِنۡ هُوَ إِلَّا رَجُلُۢ بِهِۦ جِنَّةٌ فَتَرَبَّصُواْ بِهِۦ حَتَّىٰ حِينٍ  ۝٢٥
In huwa illaa rajulum bihee jinnatun fatarabbasoo bihee hattan heen
Huyu si lolote ila ni mtu mwenye wazimu. Basi mngojeeni tu kwa muda.
🎤 Rekodi yako:
23:26 🔁 0/5
قَالَ رَبِّ ٱنصُرۡنِي بِمَا كَذَّبُونِ  ۝٢٦
Qaala Rabbin surnee bimaa kazzaboon
Akasema (Nuhu): Mola wangu Mlezi! Ninusuru kwa kuwa wamenikanusha.
🎤 Rekodi yako:
23:27 🔁 0/5
فَأَوۡحَيۡنَآ إِلَيۡهِ أَنِ ٱصۡنَعِ ٱلۡفُلۡكَ بِأَعۡيُنِنَا وَوَحۡيِنَا فَإِذَا جَآءَ أَمۡرُنَا وَفَارَ ٱلتَّنُّورُ فَٱسۡلُكۡ فِيهَا مِن كُلٍّ زَوۡجَيۡنِ ٱثۡنَيۡنِ وَأَهۡلَكَ إِلَّا مَن سَبَقَ عَلَيۡهِ ٱلۡقَوۡلُ مِنۡهُمۡۖ وَلَا تُخَٰطِبۡنِي فِي ٱلَّذِينَ ظَلَمُوٓاْ إِنَّهُم مُّغۡرَقُونَ  ۝٢٧
Fa awhainaaa ilaihi anis na`il fulka bi a`yuninaa wa wahyinaa fa izaa jaaa`a amrunaa wa faarat tannooru fasluk feehaa min kullin zawjainis naini wa ahlaka illaa man sabaqa `alaihil qawlu minhum wa laa tukhaat ibnee fil lazeena zalamooo innaahum mughraqoon
Tukampa wahyi: Unda jahazi mbele ya macho yetu na uwongozi wetu! Basi itapo fika amri yetu na ikafurika tanuri, hapo waingize ndani yake wa kila namna dume na jike, na ahali zako, isipo kuwa yule ambaye katika wao juu yake imekwisha tangulia kauli. Wala usinitajie hao walio dhulumu. Kwani hao bila ya shaka watazamishwa.
🎤 Rekodi yako:
23:28 🔁 0/5
فَإِذَا ٱسۡتَوَيۡتَ أَنتَ وَمَن مَّعَكَ عَلَى ٱلۡفُلۡكِ فَقُلِ ٱلۡحَمۡدُ لِلَّهِ ٱلَّذِي نَجَّىٰنَا مِنَ ٱلۡقَوۡمِ ٱلظَّٰلِمِينَ  ۝٢٨
Fa izas tawaita ata wa mam ma`aka `alal fulki faqulil hamdu lillaahil lazee najjaanaa minal qawmiz zalimeen
Basi utakapo tulia wewe na walio pamoja nawe humo marikebuni, sema: Alhamdulillahi Sifa zote njema ni za Mwenyezi Mungu, aliye tuokoa na watu madhaalimu!
🎤 Rekodi yako:
23:29 🔁 0/5
وَقُل رَّبِّ أَنزِلۡنِي مُنزَلًا مُّبَارَكًا وَأَنتَ خَيۡرُ ٱلۡمُنزِلِينَ  ۝٢٩
Wa qur Rabbi anzilnee munzalam mubaarakanw wa Anta khairul munzileen
Na sema: Mola wangu Mlezi! Niteremshe mteremsho wenye baraka, na Wewe ni Mbora wa wateremshaji.
🎤 Rekodi yako:
23:30 🔁 0/5
إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَأٓيَٰتٍ وَإِن كُنَّا لَمُبۡتَلِينَ  ۝٣٠
Inna fee zaalika la Aayaatinw wa in kunnaa lamubtaleen
Hakika katika hayo yapo mazingatio. Na kwa yakini Sisi ni wenye kuwafanyia mtihani.
🎤 Rekodi yako:
23:31 🔁 0/5
ثُمَّ أَنشَأۡنَا مِنۢ بَعۡدِهِمۡ قَرۡنًا ءَاخَرِينَ  ۝٣١
Summaa anshaana mim ba`dihim qarnan aakhareen
Kisha baada yao tukaanzisha kizazi kingine.
🎤 Rekodi yako:
23:32 🔁 0/5
فَأَرۡسَلۡنَا فِيهِمۡ رَسُولًا مِّنۡهُمۡ أَنِ ٱعۡبُدُواْ ٱللَّهَ مَا لَكُم مِّنۡ إِلَٰهٍ غَيۡرُهُۥٓۚ أَفَلَا تَتَّقُونَ  ۝٣٢
Fa arsalnaa feehim Rasoolam minhum ani`budul laaha maa lakum min ilaahin ghairuhoo afalaa tattaqoon
Tukawapelekea Mtume miongoni mwao, kuwaambia: Muabuduni Mwenyezi Mungu! Hamna mungu asiye kuwa Yeye. Jee, hamwogopi?
🎤 Rekodi yako:
23:33 🔁 0/5
وَقَالَ ٱلۡمَلَأُ مِن قَوۡمِهِ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ وَكَذَّبُواْ بِلِقَآءِ ٱلۡأٓخِرَةِ وَأَتۡرَفۡنَٰهُمۡ فِي ٱلۡحَيَوٰةِ ٱلدُّنۡيَا مَا هَٰذَآ إِلَّا بَشَرٌ مِّثۡلُكُمۡ يَأۡكُلُ مِمَّا تَأۡكُلُونَ مِنۡهُ وَيَشۡرَبُ مِمَّا تَشۡرَبُونَ  ۝٣٣
Wa qaalal mala-u min qawmihil lazeena kafaroo wa kazzaboo bi liqaaa`il Aakhirati wa atrafnaahum fil hayaatid dunyaa maa haazaaa illaa basharum mislukum yaakulu mimmaa taakuloona minhu wa yashrabu mimmaa tashraboon
Na wakubwa katika watu wake walio kufuru na wakakanusha mkutano wa Akhera, na tukawadekeza kwa starehe katika maisha ya dunia, walisema: Huyu si chochote ila ni binaadamu kama nyinyi; anakula mlacho, na anakunywa mnywacho.
🎤 Rekodi yako:
23:34 🔁 0/5
وَلَئِنۡ أَطَعۡتُم بَشَرًا مِّثۡلَكُمۡ إِنَّكُمۡ إِذًا لَّخَٰسِرُونَ  ۝٣٤
Wa la`in at`atum basharam mislakum innakum izal lakhaasiroon
Na nyinyi mkimt'ii mtu kama nyinyi basi hakika mtakuwa khasarani.
🎤 Rekodi yako:
23:35 🔁 0/5
أَيَعِدُكُمۡ أَنَّكُمۡ إِذَا مِتُّمۡ وَكُنتُمۡ تُرَابًا وَعِظَٰمًا أَنَّكُم مُّخۡرَجُونَ  ۝٣٥
A-Ya`idukum annakum izaa mittum wa kuntum turaabanw wa izaaman annakum mukhrajoon
Hivyo anakuahidini ati ya kwamba mtakapo kufa na mkawa udongo na mifupa kuwa mtatolewa?
🎤 Rekodi yako:
23:36 🔁 0/5
۞ هَيۡهَاتَ هَيۡهَاتَ لِمَا تُوعَدُونَ  ۝٣٦
Haihaata haihaata limaa too`adoon
Hayawi! Hayawi hayo mnayo ahidiwa.
🎤 Rekodi yako:
23:37 🔁 0/5
إِنۡ هِيَ إِلَّا حَيَاتُنَا ٱلدُّنۡيَا نَمُوتُ وَنَحۡيَا وَمَا نَحۡنُ بِمَبۡعُوثِينَ  ۝٣٧
In hiya illaa hayaatunad dunyaa namootu wa nahyaa wa maa nahnu bimab`ooseen
Hapana ila uhai wetu wa duniani tu, tunakufa na kuishi basi. Wala sisi hatutafufuliwa.
🎤 Rekodi yako:
23:38 🔁 0/5
إِنۡ هُوَ إِلَّا رَجُلٌ ٱفۡتَرَىٰ عَلَى ٱللَّهِ كَذِبًا وَمَا نَحۡنُ لَهُۥ بِمُؤۡمِنِينَ  ۝٣٨
In huwa illaa rajulunif taraa `alal laahi kazibanw wa maa nahnuu lahoo bimu`mineen
Huyu si lolote ila ni mtu anaye mzulia Mwenyezi Mungu uwongo, wala sisi sio wa kumuamini.
🎤 Rekodi yako:
23:39 🔁 0/5
قَالَ رَبِّ ٱنصُرۡنِي بِمَا كَذَّبُونِ  ۝٣٩
Qaala Rabbin surnee bimaa kazzaboon
Akasema: Mola wangu Mlezi! Ninusuru kwa sababu wananikanusha.
🎤 Rekodi yako:
23:40 🔁 0/5
قَالَ عَمَّا قَلِيلٍ لَّيُصۡبِحُنَّ نَٰدِمِينَ  ۝٤٠
Qaala `ammaa qaleelil la yusbihunna naadimeen
(Mwenyezi Mungu) akasema: Baada ya muda mchache watakuwa wenye kujuta.
🎤 Rekodi yako:
23:41 🔁 0/5
فَأَخَذَتۡهُمُ ٱلصَّيۡحَةُ بِٱلۡحَقِّ فَجَعَلۡنَٰهُمۡ غُثَآءًۚ فَبُعۡدًا لِّلۡقَوۡمِ ٱلظَّٰلِمِينَ  ۝٤١
Fa akhazat humus saihatu bilhaqqi faja`alnaahum ghusaaa`aa; fabu;dal lilqaw miz zaalimeen
Basi ukawanyakua ukelele kwa haki, na tukawafanya kama takataka zinazo elea juu ya maji. Ikapotelea mbali kaumu ya madhaalimu!
🎤 Rekodi yako:
23:42 🔁 0/5
ثُمَّ أَنشَأۡنَا مِنۢ بَعۡدِهِمۡ قُرُونًا ءَاخَرِينَ  ۝٤٢
Summa anshaanaa mim ba`dihim quroonan aakhareen
Kisha tukaleta baada yao vizazi vingine.
🎤 Rekodi yako:
23:43 🔁 0/5
مَا تَسۡبِقُ مِنۡ أُمَّةٍ أَجَلَهَا وَمَا يَسۡتَـٔۡخِرُونَ  ۝٤٣
Maa tasbiqu min ummatin ajalahaa wa maa yastaakhiroon
Hapana umma uwezao kutanguliza ajali yake wala kuikawiza.
🎤 Rekodi yako:
23:44 🔁 0/5
ثُمَّ أَرۡسَلۡنَا رُسُلَنَا تَتۡرَاۖ كُلَّ مَا جَآءَ أُمَّةً رَّسُولُهَا كَذَّبُوهُۖ فَأَتۡبَعۡنَا بَعۡضَهُم بَعۡضًا وَجَعَلۡنَٰهُمۡ أَحَادِيثَۚ فَبُعۡدًا لِّقَوۡمٍ لَّا يُؤۡمِنُونَ  ۝٤٤
Summa arsalnaa Rusulanaa tatraa kulla maa jaaa`a ummatar Rasooluhaa kazzabooh; fa atba`naa ba`dahum ba`danw wa ja`alnaahum ahaadees; fabu`dal liqawmil laa yu`minoon
Kisha tukawatuma Mitume wetu, mmoja baada ya mmoja. Kila umma alipo wafikia Mtume wao walimkanusha. Tukawafuatanisha hawa baada ya hawa, na tukawafanya ni hadithi za kusimuliwa. Wakapotelea mbali watu wasio amini.
🎤 Rekodi yako:
23:45 🔁 0/5
ثُمَّ أَرۡسَلۡنَا مُوسَىٰ وَأَخَاهُ هَٰرُونَ بِـَٔايَٰتِنَا وَسُلۡطَٰنٍ مُّبِينٍ  ۝٤٥
Summa arsalnaa Moosaa wa akhaahu Haaroona bi Aayaatinaa wa sultaanim mubeen
Kisha tukamtuma Musa na nduguye, Haaruni, pamoja na ishara zetu na hoja zilizo wazi.
🎤 Rekodi yako:
23:46 🔁 0/5
إِلَىٰ فِرۡعَوۡنَ وَمَلَإِيْهِۦ فَٱسۡتَكۡبَرُواْ وَكَانُواْ قَوۡمًا عَالِينَ  ۝٤٦
Ilaa Fir`awna wa mala`ihee fastakbaroo wa kaanoo qawman `aaleem
Kumwendea Firauni na wakuu wake. Lakini walijivuna, nao walikuwa watu majeuri.
🎤 Rekodi yako:
23:47 🔁 0/5
فَقَالُوٓاْ أَنُؤۡمِنُ لِبَشَرَيۡنِ مِثۡلِنَا وَقَوۡمُهُمَا لَنَا عَٰبِدُونَ  ۝٤٧
Faqaaloo annu`minu libasharaini mislinaa wa qawmuhumaa lanaa `aabidoon
Wakasema: Je, tuwaamini wanaadamu wawili hawa kama sisi, na ambao watu wao ni watumwa wetu?
🎤 Rekodi yako:
23:48 🔁 0/5
فَكَذَّبُوهُمَا فَكَانُواْ مِنَ ٱلۡمُهۡلَكِينَ  ۝٤٨
Fakazzaboohumaa fakaanoo minal mmuhlakeen
Basi wakawakanusha, na wakawa miongoni mwa walio angamizwa.
🎤 Rekodi yako:
23:49 🔁 0/5
وَلَقَدۡ ءَاتَيۡنَا مُوسَى ٱلۡكِتَٰبَ لَعَلَّهُمۡ يَهۡتَدُونَ  ۝٤٩
Wa laqad aatainaa Moosal Kitaaba la`allahum yahtadoon
Na hakika tulimpa Musa Kitabu ili wapate kuongoka.
🎤 Rekodi yako:
23:50 🔁 0/5
وَجَعَلۡنَا ٱبۡنَ مَرۡيَمَ وَأُمَّهُۥٓ ءَايَةً وَءَاوَيۡنَٰهُمَآ إِلَىٰ رَبۡوَةٍ ذَاتِ قَرَارٍ وَمَعِينٍ  ۝٥٠
Wa ja`alnab na Maryama wa ummahooo aayatannw wa aawainaahumaaa ilaa rabwatin zaati qaraarinw wa ma`een
Na tukamfanya mwana wa Mariamu na mama yake kuwa ni Ishara, na tukawapa makimbilio kwenda mahali palipo inuka penye utulivu na chemchem za maji.
🎤 Rekodi yako:
23:51 🔁 0/5
يَٰٓأَيُّهَا ٱلرُّسُلُ كُلُواْ مِنَ ٱلطَّيِّبَٰتِ وَٱعۡمَلُواْ صَٰلِحًاۖ إِنِّي بِمَا تَعۡمَلُونَ عَلِيمٌ  ۝٥١
Yaaa aiyuhar Rusulu kuloo minat taiyibaati wa`maloo saalihan innee bimaa ta`maloona `Aleem
Enyi Mitume! Kuleni vyakula vizuri na tendeni mema. Hakika Mimi ni Mjuzi wa mnayo yatenda.
🎤 Rekodi yako:
23:52 🔁 0/5
وَإِنَّ هَٰذِهِۦٓ أُمَّتُكُمۡ أُمَّةً وَٰحِدَةً وَأَنَا۠ رَبُّكُمۡ فَٱتَّقُونِ  ۝٥٢
Wa inna haaziheee ummatukum ummatanw waahidatanw wa Ana Rabbukum fattaqoon
Na kwa yakini huu Umma wenu ni Umma mmoja, na Mimi ni Mola wenu Mlezi, basi nicheni Mimi.
🎤 Rekodi yako:
23:53 🔁 0/5
فَتَقَطَّعُوٓاْ أَمۡرَهُم بَيۡنَهُمۡ زُبُرًاۖ كُلُّ حِزۡبِۭ بِمَا لَدَيۡهِمۡ فَرِحُونَ  ۝٥٣
Fataqatta`ooo amrahum bainahum zuburaa; kullu hizbim bimaa ladaihim farihoon
Lakini walikatiana jambo lao mapande mbali mbali. Kila kundi likifurahia kwa waliyo nayo.
🎤 Rekodi yako:
23:54 🔁 0/5
فَذَرۡهُمۡ فِي غَمۡرَتِهِمۡ حَتَّىٰ حِينٍ  ۝٥٤
Fazarhum fee ghamratihim hattaa heen
Basi waache katika ghafla yao kwa muda.
🎤 Rekodi yako:
23:55 🔁 0/5
أَيَحۡسَبُونَ أَنَّمَا نُمِدُّهُم بِهِۦ مِن مَّالٍ وَبَنِينَ  ۝٥٥
A-yahsaboona annnamaa numiduhum bihee mimmaalinw wa baneen
Je! Wanadhani ya kuwa kwa vile tunavyo wapa mali na watoto
🎤 Rekodi yako:
23:56 🔁 0/5
نُسَارِعُ لَهُمۡ فِي ٱلۡخَيۡرَٰتِۚ بَل لَّا يَشۡعُرُونَ  ۝٥٦
Nusaari`u lahum fil khairaat; bal laa yash`uroon
Ndio tunawahimizia kheri? Lakini wenyewe hawatambui.
🎤 Rekodi yako:
23:57 🔁 0/5
إِنَّ ٱلَّذِينَ هُم مِّنۡ خَشۡيَةِ رَبِّهِم مُّشۡفِقُونَ  ۝٥٧
Innal lazeena hum min khashyati Rabbihim mushfiqoon
Kwa hakika hao ambao kwa kumwogopa Mola wao Mlezi wananyenyekea,
🎤 Rekodi yako:
23:58 🔁 0/5
وَٱلَّذِينَ هُم بِـَٔايَٰتِ رَبِّهِمۡ يُؤۡمِنُونَ  ۝٥٨
Wallazeena hum bi Aayaati Rabbihim yu`minoon
Na wale ambao Ishara za Mola wao Mlezi wanaziamini,
🎤 Rekodi yako:
23:59 🔁 0/5
وَٱلَّذِينَ هُم بِرَبِّهِمۡ لَا يُشۡرِكُونَ  ۝٥٩
Wallazeena hum bi Rabbihim laa yushrikoon
Na wale ambao Mola wao Mlezi hawamshirikishi,
🎤 Rekodi yako:
23:60 🔁 0/5
وَٱلَّذِينَ يُؤۡتُونَ مَآ ءَاتَواْ وَّقُلُوبُهُمۡ وَجِلَةٌ أَنَّهُمۡ إِلَىٰ رَبِّهِمۡ رَٰجِعُونَ  ۝٦٠
Wallazeena yu`toona maaa aataw wa quloobuhum wajilatun annahum ilaa Rabbihim raaji`oon
Na wale ambao wanatoa walicho pewa, na hali nyoyo zao zinagopa kwa kuwa watarejea kwa Mola wao Mlezi,
🎤 Rekodi yako:
23:61 🔁 0/5
أُوْلَٰٓئِكَ يُسَٰرِعُونَ فِي ٱلۡخَيۡرَٰتِ وَهُمۡ لَهَا سَٰبِقُونَ  ۝٦١
Ulaaa`ika yusaari`oona fil khairaati wa hum lahaa saabiqoon
Basi wote hao ndio wanao kimbilia katika mambo ya kheri, na ndio watakao tangulia kuyafikia.
🎤 Rekodi yako:
23:62 🔁 0/5
وَلَا نُكَلِّفُ نَفۡسًا إِلَّا وُسۡعَهَاۚ وَلَدَيۡنَا كِتَٰبٌ يَنطِقُ بِٱلۡحَقِّ وَهُمۡ لَا يُظۡلَمُونَ  ۝٦٢
Wa laa nukallifu nafsan illaa wus`ahaa wa ladainaa kitaabuny yantiqu bilhaqqi w ahum la yuzlamoon
Na hatuilazimishi nafsi ila kwa kadri ya uwezo wake. Na tunacho kitabu kisemacho kweli. Nao hawatadhulumiwa.
🎤 Rekodi yako:
23:63 🔁 0/5
بَلۡ قُلُوبُهُمۡ فِي غَمۡرَةٍ مِّنۡ هَٰذَا وَلَهُمۡ أَعۡمَٰلٌ مِّن دُونِ ذَٰلِكَ هُمۡ لَهَا عَٰمِلُونَ  ۝٦٣
Bal quloobuhum fee ghamratim min haazaa wa lahum a`maalum min dooni zaalika hum lahaa `aamiloon
Lakini nyoyo zao zimeghafilika na hayo, na wanavyo vitendo vinginevyo wanavyo vifanya.
🎤 Rekodi yako:
23:64 🔁 0/5
حَتَّىٰٓ إِذَآ أَخَذۡنَا مُتۡرَفِيهِم بِٱلۡعَذَابِ إِذَا هُمۡ يَجۡـَٔرُونَ  ۝٦٤
Hattaaa izaaa akhznaa mutrafeehim bil`azaabi izaa hum yaj`aroon
Hata tutakapo watia katika adhabu wale walio dekezwa kwa starehe kati yao, hapo ndipo watapo yayatika.
🎤 Rekodi yako:
23:65 🔁 0/5
لَا تَجۡـَٔرُواْ ٱلۡيَوۡمَۖ إِنَّكُم مِّنَّا لَا تُنصَرُونَ  ۝٦٥
Laa taj`arul yawma innakum minnaa laa tunsaroon
Msiyayatike leo! Hakika nyinyi hamtanusurika nasi.
🎤 Rekodi yako:
23:66 🔁 0/5
قَدۡ كَانَتۡ ءَايَٰتِي تُتۡلَىٰ عَلَيۡكُمۡ فَكُنتُمۡ عَلَىٰٓ أَعۡقَٰبِكُمۡ تَنكِصُونَ  ۝٦٦
Qad kaanat Aayaatee tutlaa `alaikum fakuntum `alaaa a`qaabikum tankisoon
Hakika zilikuwa Aya zangu mkisomewa, nanyi mkirudi nyuma juu ya visigino vyenu,
🎤 Rekodi yako:
23:67 🔁 0/5
مُسۡتَكۡبِرِينَ بِهِۦ سَٰمِرًا تَهۡجُرُونَ  ۝٦٧
Mustakbireena bihee saamiran tahjuroon
Na huku mkitakabari na usiku mkiizungumza (Qur'ani) kwa dharau.
🎤 Rekodi yako:
23:68 🔁 0/5
أَفَلَمۡ يَدَّبَّرُواْ ٱلۡقَوۡلَ أَمۡ جَآءَهُم مَّا لَمۡ يَأۡتِ ءَابَآءَهُمُ ٱلۡأَوَّلِينَ  ۝٦٨
Afalam yaddabbarrul qawla am jaaa`ahum maa lam yaati aabaaa`ahumul awwaleen
Je, hawakuifikiri kauli, au yamewajia yasiyo wafikia baba zao wa zamani?
🎤 Rekodi yako:
23:69 🔁 0/5
أَمۡ لَمۡ يَعۡرِفُواْ رَسُولَهُمۡ فَهُمۡ لَهُۥ مُنكِرُونَ  ۝٦٩
Am lam ya`rifoo Rasoolahum fahum lahoo munkiroon
Au hawakumjua Mtume wao, ndio maana wanamkataa?
🎤 Rekodi yako:
23:70 🔁 0/5
أَمۡ يَقُولُونَ بِهِۦ جِنَّةُۢۚ بَلۡ جَآءَهُم بِٱلۡحَقِّ وَأَكۡثَرُهُمۡ لِلۡحَقِّ كَٰرِهُونَ  ۝٧٠
Am yaqooloona bihee jinnnah; bal jaaa`ahum bilhaqqi wa aksaruhum lil haqqi kaarihoon
Au wanasema: Ana wazimu? Bali amewajia kwa Haki, na wengi wao wanaichukia Haki.
🎤 Rekodi yako:
23:71 🔁 0/5
وَلَوِ ٱتَّبَعَ ٱلۡحَقُّ أَهۡوَآءَهُمۡ لَفَسَدَتِ ٱلسَّمَٰوَٰتُ وَٱلۡأَرۡضُ وَمَن فِيهِنَّۚ بَلۡ أَتَيۡنَٰهُم بِذِكۡرِهِمۡ فَهُمۡ عَن ذِكۡرِهِم مُّعۡرِضُونَ  ۝٧١
Wa lawit taba`al haqqu ahwaaa`ahum lafasadatis samaawaatu wal ardu wa man feehinnn; bal atainaahum bizikrihim fahum `an zikrihim mu`ridon
Na lau kuwa Haki ingeli fuata matamanio yao, basi zingeli haribika mbingu na ardhi na waliomo ndani. Bali tumewaletea ukumbusho wao, nao wanajitenga mbali na ukumbusho wao.
🎤 Rekodi yako:
23:72 🔁 0/5
أَمۡ تَسۡـَٔلُهُمۡ خَرۡجًا فَخَرَاجُ رَبِّكَ خَيۡرٌۖ وَهُوَ خَيۡرُ ٱلرَّٰزِقِينَ  ۝٧٢
Am tas`aluhum kharjan fakharaaju Rabbika khairunw wa Huwa khairur raaziqeen
Au unawaomba ujira? Lakini ujira wa Mola wako Mlezi ni bora, na Yeye ndiye Mbora wa wanao ruzuku.
🎤 Rekodi yako:
23:73 🔁 0/5
وَإِنَّكَ لَتَدۡعُوهُمۡ إِلَىٰ صِرَٰطٍ مُّسۡتَقِيمٍ  ۝٧٣
Wa innaka latad`oohum ilaa Siraatim Mustaqeem
Na kwa yakini wewe unawaita kwenye Njia Iliyo Nyooka.
🎤 Rekodi yako:
23:74 🔁 0/5
وَإِنَّ ٱلَّذِينَ لَا يُؤۡمِنُونَ بِٱلۡأٓخِرَةِ عَنِ ٱلصِّرَٰطِ لَنَٰكِبُونَ  ۝٧٤
Wa innnal lazeena laa yu`minoona bil Aakhirati `anis siraati lanaakiboon
Na hakika wale wasio iamini Akhera wanajitenga na Njia hiyo.
🎤 Rekodi yako:
23:75 🔁 0/5
۞ وَلَوۡ رَحِمۡنَٰهُمۡ وَكَشَفۡنَا مَا بِهِم مِّن ضُرٍّ لَّلَجُّواْ فِي طُغۡيَٰنِهِمۡ يَعۡمَهُونَ  ۝٧٥
Wa law rahimnaahum wa kashafnaa maa bihim min durril lalajjoo fee tughyaanihim ya`mahoon
Na lau tungeli warehemu na tukawaondolea shida waliyo nayo bila ya shaka wangeli endelea katika upotofu wao vile vile, wakitangatanga.
🎤 Rekodi yako:
23:76 🔁 0/5
وَلَقَدۡ أَخَذۡنَٰهُم بِٱلۡعَذَابِ فَمَا ٱسۡتَكَانُواْ لِرَبِّهِمۡ وَمَا يَتَضَرَّعُونَ  ۝٧٦
Wa laqad akhaznaahum bil`azaabi famastakaanoo li Rabbihim wa maa yatadarra`oon
Na hakika tuliwatia adhabu kali; lakini hawakuelekea kwa Mola wao Mlezi wala hawakunyenyekea.
🎤 Rekodi yako:
23:77 🔁 0/5
حَتَّىٰٓ إِذَا فَتَحۡنَا عَلَيۡهِم بَابًا ذَا عَذَابٍ شَدِيدٍ إِذَا هُمۡ فِيهِ مُبۡلِسُونَ  ۝٧٧
Hattaaa izaa fatahnaa `alaihim baaban zaa `azaabin shadeedin izaa hum feehi mublisoon
Mpaka tulipo wafungulia mlango wa adhabu kali, hapo ndipo wakawa wenye kukata tamaa.
🎤 Rekodi yako:
23:78 🔁 0/5
وَهُوَ ٱلَّذِيٓ أَنشَأَ لَكُمُ ٱلسَّمۡعَ وَٱلۡأَبۡصَٰرَ وَٱلۡأَفۡـِٔدَةَۚ قَلِيلًا مَّا تَشۡكُرُونَ  ۝٧٨
Wa Huwal lazeee ansha a-lakumus sam`a wal absaara wal af`idah; qaleelam maa tashkuroon
Na Yeye ndiye aliye kuumbieni kusikia na kuona na nyoyo za kufahamu. Ni kuchache mno kushukuru kwenu.
🎤 Rekodi yako:
23:79 🔁 0/5
وَهُوَ ٱلَّذِي ذَرَأَكُمۡ فِي ٱلۡأَرۡضِ وَإِلَيۡهِ تُحۡشَرُونَ  ۝٧٩
Wa Huwal lazee zara akum fil ardi wa ilaihi tuhsharoon
Na Yeye ndiye aliye kuenezeni katika ardhi, na kwake Yeye mtakusanywa.
🎤 Rekodi yako:
23:80 🔁 0/5
وَهُوَ ٱلَّذِي يُحۡيِۦ وَيُمِيتُ وَلَهُ ٱخۡتِلَٰفُ ٱلَّيۡلِ وَٱلنَّهَارِۚ أَفَلَا تَعۡقِلُونَ  ۝٨٠
Wa Huwal lazee yuhyee wa yumeetu wa lahukh tilaaful laili wannahaar; afalaa ta`qiloon
Na Yeye ndiye anaye huisha na kufisha, na yake Yeye mabadiliko ya usiku na mchana. Basi je! Hamfahamu?
🎤 Rekodi yako:
23:81 🔁 0/5
بَلۡ قَالُواْ مِثۡلَ مَا قَالَ ٱلۡأَوَّلُونَ  ۝٨١
Bal qaaloo misla maa qaalal awwaloon
Bali wanasema kama walivyo sema watu wa kwanza.
🎤 Rekodi yako:
23:82 🔁 0/5
قَالُوٓاْ أَءِذَا مِتۡنَا وَكُنَّا تُرَابًا وَعِظَٰمًا أَءِنَّا لَمَبۡعُوثُونَ  ۝٨٢
Qaalooo `a-izaa mitnaa wa kunnaa turaabanw wa `izaaman `a-innaa lamab `oosoon
Walisema: Je! Tukisha kufa tukawa udongo na mifupa ndio tutafufuliwa?
🎤 Rekodi yako:
23:83 🔁 0/5
لَقَدۡ وُعِدۡنَا نَحۡنُ وَءَابَآؤُنَا هَٰذَا مِن قَبۡلُ إِنۡ هَٰذَآ إِلَّآ أَسَٰطِيرُ ٱلۡأَوَّلِينَ  ۝٨٣
Laqad wu`idnaa nahnu wa aabaaa`unaa haazaa min qablu in haazaaa illaaa asaateerul awwaleen
Tuliahidiwa haya sisi na baba zetu zamani. Hayakuwa haya ila ni visa vya uwongo vya watu wa zamani.
🎤 Rekodi yako:
23:84 🔁 0/5
قُل لِّمَنِ ٱلۡأَرۡضُ وَمَن فِيهَآ إِن كُنتُمۡ تَعۡلَمُونَ  ۝٨٤
Qul limanil ardu wa man feehaaa in kuntum ta`lamoon
Sema: Ni ya nani ardhi na viliomo ndani yake, kama nyinyi mnajua?
🎤 Rekodi yako:
23:85 🔁 0/5
سَيَقُولُونَ لِلَّهِۚ قُلۡ أَفَلَا تَذَكَّرُونَ  ۝٨٥
Sa-yaqooloona lillaah; qul afalaa tazakkkaroon
Watasema: Ni vya Mwenyezi Mungu! Sema: Basi, je, hamkumbuki?
🎤 Rekodi yako:
23:86 🔁 0/5
قُلۡ مَن رَّبُّ ٱلسَّمَٰوَٰتِ ٱلسَّبۡعِ وَرَبُّ ٱلۡعَرۡشِ ٱلۡعَظِيمِ  ۝٨٦
Qul mar Rabbus samaawaatis sab`i wa Rabbul `Arshil `Azeem
Sema: Ni nani Mola Mlezi wa mbingu saba na Mola Mlezi wa A'rshi Kuu?
🎤 Rekodi yako:
23:87 🔁 0/5
سَيَقُولُونَ لِلَّهِۚ قُلۡ أَفَلَا تَتَّقُونَ  ۝٨٧
Sa yaqooloona lillaah; qul afalaa tattaqoon
Watasema: Ni vya Mwenyezi Mungu. Sema: Basi je, hamwogopi?
🎤 Rekodi yako:
23:88 🔁 0/5
قُلۡ مَنۢ بِيَدِهِۦ مَلَكُوتُ كُلِّ شَيۡءٍ وَهُوَ يُجِيرُ وَلَا يُجَارُ عَلَيۡهِ إِن كُنتُمۡ تَعۡلَمُونَ  ۝٨٨
Qul mam bi yadihee malakootu kulli shai`inw wa Huwa yujeeru wa laa yujaaru `alaihi in kuntum ta`lamoon
Sema: Ni nani mkononi mwake umo Ufalme wa kila kitu, naye ndiye anaye linda, wala hakilindwi asicho taka, kama mnajua?
🎤 Rekodi yako:
23:89 🔁 0/5
سَيَقُولُونَ لِلَّهِۚ قُلۡ فَأَنَّىٰ تُسۡحَرُونَ  ۝٨٩
Sa yaqooloona lillaah; qul fa annaa tus haroon
Watasema: (Ufalme huo) ni wa Mwenyezi Mungu. Sema: Basi vipi mnadanganyika?
🎤 Rekodi yako:
23:90 🔁 0/5
بَلۡ أَتَيۡنَٰهُم بِٱلۡحَقِّ وَإِنَّهُمۡ لَكَٰذِبُونَ  ۝٩٠
Bal atainaahum bil haqqi wa innahum lakaaziboon
Bali tumewaletea Haki, na kwa yakini hao ni waongo.
🎤 Rekodi yako:
23:91 🔁 0/5
مَا ٱتَّخَذَ ٱللَّهُ مِن وَلَدٍ وَمَا كَانَ مَعَهُۥ مِنۡ إِلَٰهٍۚ إِذًا لَّذَهَبَ كُلُّ إِلَٰهِۭ بِمَا خَلَقَ وَلَعَلَا بَعۡضُهُمۡ عَلَىٰ بَعۡضٍۚ سُبۡحَٰنَ ٱللَّهِ عَمَّا يَصِفُونَ  ۝٩١
Mat takhazal laahu minw waladinw wa maa kaana ma`ahoo min ilaah; izal lazahaba kullu ilaahim bimaa khalaqa wa la`alaa ba`duhum `alaa ba`d; Subhaannal laahi `ammaa yasifoon
Mwenyezi Mungu hana mwana yeyote, wala hanaye mungu mwengine. Inge kuwa hivyo basi kila mungu angeli chukua alivyo umba, na baadhi yao wangeli washinda wengine. Mwenyezi Mungu ameepukana na sifa wanazo msifu.
🎤 Rekodi yako:
23:92 🔁 0/5
عَٰلِمِ ٱلۡغَيۡبِ وَٱلشَّهَٰدَةِ فَتَعَٰلَىٰ عَمَّا يُشۡرِكُونَ  ۝٩٢
Aalimil Ghaibi wash shahhaadati fata`aalaa `ammaa yushrikoon
Mjuzi wa siri na dhaahiri, na ametukuka juu ya hayo wanayo mshirikisha nayo.
🎤 Rekodi yako:
23:93 🔁 0/5
قُل رَّبِّ إِمَّا تُرِيَنِّي مَا يُوعَدُونَ  ۝٩٣
Qur Rabbi immmaa turiyannee maa yoo`adoon
Sema: Mola wangu Mlezi! Ukinionyesha adhabu waliyo ahidiwa,
🎤 Rekodi yako:
23:94 🔁 0/5
رَبِّ فَلَا تَجۡعَلۡنِي فِي ٱلۡقَوۡمِ ٱلظَّٰلِمِينَ  ۝٩٤
Rabbi falaa taj`alnee fil qawmiz zaalimeen
Mola wangu Mlezi! Usinijaalie katika watu madhaalimu hao.
🎤 Rekodi yako:
23:95 🔁 0/5
وَإِنَّا عَلَىٰٓ أَن نُّرِيَكَ مَا نَعِدُهُمۡ لَقَٰدِرُونَ  ۝٩٥
Wa innaa `alaaa an nuriyaka maa na`iduhum laqaadiroon
Na hakika Sisi ni waweza wa kukuonyeshsa tuliyo waahidi.
🎤 Rekodi yako:
23:96 🔁 0/5
ٱدۡفَعۡ بِٱلَّتِي هِيَ أَحۡسَنُ ٱلسَّيِّئَةَۚ نَحۡنُ أَعۡلَمُ بِمَا يَصِفُونَ  ۝٩٦
Idfa` billate hiya ahsanus saiyi`ah; nahnu a`lamu bimaa yasifoon
Kinga maovu kwa kutenda yaliyo mema zaidi. Sisi tunajua wayasemayo.
🎤 Rekodi yako:
23:97 🔁 0/5
وَقُل رَّبِّ أَعُوذُ بِكَ مِنۡ هَمَزَٰتِ ٱلشَّيَٰطِينِ  ۝٩٧
Wa qur Rabbi a`oozu bika min hamazaatish Shayaateen
Na sema: Mola wangu Mlezi! Najikinga kwako na wasiwasi wa mashet'ani.
🎤 Rekodi yako:
23:98 🔁 0/5
وَأَعُوذُ بِكَ رَبِّ أَن يَحۡضُرُونِ  ۝٩٨
Wa a`oozu bika Rabbi ai-yahduroon
Na najikinga kwako, Mola wangu Mlezi, wasinikaribie.
🎤 Rekodi yako:
23:99 🔁 0/5
حَتَّىٰٓ إِذَا جَآءَ أَحَدَهُمُ ٱلۡمَوۡتُ قَالَ رَبِّ ٱرۡجِعُونِ  ۝٩٩
Hattaaa izaa jaaa`a ahada humul mawtu qaala Rabbir ji`oon
Mpaka yanapo mfikia mmoja wao mauti, husema: Mola wangu Mlezi! Nirudishe.
🎤 Rekodi yako:
23:100 🔁 0/5
لَعَلِّيٓ أَعۡمَلُ صَٰلِحًا فِيمَا تَرَكۡتُۚ كـَلَّآۚ إِنَّهَا كَلِمَةٌ هُوَ قَآئِلُهَاۖ وَمِن وَرَآئِهِم بَرۡزَخٌ إِلَىٰ يَوۡمِ يُبۡعَثُونَ  ۝١٠٠
La`alleee a`malu saalihan feemaa taraktu kallaa; innahaa kalimatun huwa qaaa`iluhaa wa minw waraaa`him barzakhun ilaa Yawmi yub`asoon
Ili nitende mema sasa badala ya yale niliyo yaacha. Wapi! Hii ni kauli aisemayo yeye tu. Na nyuma yao kipo kizuizi mpaka siku watapo fufuliwa.
🎤 Rekodi yako:
23:101 🔁 0/5
فَإِذَا نُفِخَ فِي ٱلصُّورِ فَلَآ أَنسَابَ بَيۡنَهُمۡ يَوۡمَئِذٍ وَلَا يَتَسَآءَلُونَ  ۝١٠١
Fa izaa nufikha fis Soori falaaa ansaaba bainahum yawma`izinw wa laa yatasaaa`aloon
Basi litapo pulizwa baragumu hapo hautakuwapo ujamaa baina yao siku hiyo, wala hawataulizana.
🎤 Rekodi yako:
23:102 🔁 0/5
فَمَن ثَقُلَتۡ مَوَٰزِينُهُۥ فَأُوْلَٰٓئِكَ هُمُ ٱلۡمُفۡلِحُونَ  ۝١٠٢
Faman saqulat mawaazee nuhoo fa ulaaa`ika humul muflihoon
Ama wale ambao mizani zao zitakuwa nzito, hao ndio wenye kufanikiwa.
🎤 Rekodi yako:
23:103 🔁 0/5
وَمَنۡ خَفَّتۡ مَوَٰزِينُهُۥ فَأُوْلَٰٓئِكَ ٱلَّذِينَ خَسِرُوٓاْ أَنفُسَهُمۡ فِي جَهَنَّمَ خَٰلِدُونَ  ۝١٠٣
Wa man khaffat mawaa zeenuhoo fa ulaaa`ikal lazeena khasiroon anfusahum fee Jahannnama khaalidoon
Na wale ambao mizani zao zitakuwa nyepesi, hao ndio walio zitia khasarani nafsi zao, na katika Jahannamu watadumu.
🎤 Rekodi yako:
23:104 🔁 0/5
تَلۡفَحُ وُجُوهَهُمُ ٱلنَّارُ وَهُمۡ فِيهَا كَٰلِحُونَ  ۝١٠٤
Talfahu wujoohahumun Naaru wa hum feehaa kaalihood
Moto utababua nyuso zao, nao watakuwa na nyuso zilizo kunjana.
🎤 Rekodi yako:
23:105 🔁 0/5
أَلَمۡ تَكُنۡ ءَايَٰتِي تُتۡلَىٰ عَلَيۡكُمۡ فَكُنتُم بِهَا تُكَذِّبُونَ  ۝١٠٥
Alam takun Aayaatee tutlaa `alaikum fakuntum bihaa tukazziboon
Je! Hazikuwa Aya zangu mkisomewa, na nyinyi mkizikanusha?
🎤 Rekodi yako:
23:106 🔁 0/5
قَالُواْ رَبَّنَا غَلَبَتۡ عَلَيۡنَا شِقۡوَتُنَا وَكُنَّا قَوۡمًا ضَآلِّينَ  ۝١٠٦
Qaaloo Rabbanaa ghalabat `alainaa shiqwatunaa wa kunnaa qawman daaalleen
Mola wetu Mlezi! Tulizidiwa na uovu wetu na tukawa watu tulio potea.
🎤 Rekodi yako:
23:107 🔁 0/5
رَبَّنَآ أَخۡرِجۡنَا مِنۡهَا فَإِنۡ عُدۡنَا فَإِنَّا ظَٰلِمُونَ  ۝١٠٧
Rabbanaa akhrijnaa minhaa fa in `udnaa fa innaa zaalimoon
Mola wetu Mlezi! Tutoe humu Motoni. Na tufanyapo tena basi kweli sisi ni wenye kudhulumu.
🎤 Rekodi yako:
23:108 🔁 0/5
قَالَ ٱخۡسَـُٔواْ فِيهَا وَلَا تُكَلِّمُونِ  ۝١٠٨
Qaalakh sa`oo feehaa wa laa tukallimoon
Atasema Mwenyezi Mungu: Tokomeeni humo, wala msinisemeze.
🎤 Rekodi yako:
23:109 🔁 0/5
إِنَّهُۥ كَانَ فَرِيقٌ مِّنۡ عِبَادِي يَقُولُونَ رَبَّنَآ ءَامَنَّا فَٱغۡفِرۡ لَنَا وَٱرۡحَمۡنَا وَأَنتَ خَيۡرُ ٱلرَّٰحِمِينَ  ۝١٠٩
Innahoo kaana fareequm min `ibaadee yaqooloona Rabbanaaa aamannaa faghfir lanaa warhamnaa wa Anta khairur raahimeen
Bila ya shaka lilikuwapo kundi katika waja wangu likisema: Mola wetu Mlezi! Tumeamini; basi tusamehe na uturehemu, nawe ndiwe Mbora wa wanao rehemu.
🎤 Rekodi yako:
23:110 🔁 0/5
فَٱتَّخَذۡتُمُوهُمۡ سِخۡرِيًّا حَتَّىٰٓ أَنسَوۡكُمۡ ذِكۡرِي وَكُنتُم مِّنۡهُمۡ تَضۡحَكُونَ  ۝١١٠
Fattakhaztumoohum sikhriyyan hattaaa ansawkum zikree wa kuntum minhum tadhakoon
Lakini nyinyi mliwakejeli hata wakakusahaulisheni kunikumbuka, na mlikuwa mkiwacheka.
🎤 Rekodi yako:
23:111 🔁 0/5
إِنِّي جَزَيۡتُهُمُ ٱلۡيَوۡمَ بِمَا صَبَرُوٓاْ أَنَّهُمۡ هُمُ ٱلۡفَآئِزُونَ  ۝١١١
Inee jazaituhumul Yawma bimaa sabarooo annahum humul faaa`izoon
Hakika Mimi leo nimewalipa kwa vile walivyo subiri. Bila ya shaka hao ndio wenye kufuzu.
🎤 Rekodi yako:
23:112 🔁 0/5
قَٰلَ كَمۡ لَبِثۡتُمۡ فِي ٱلۡأَرۡضِ عَدَدَ سِنِينَ  ۝١١٢
Qaala kam labistum fil ardi `adada sineen
Atasema: Mlikaa muda gani katika ardhi kwa hisabu ya miaka?
🎤 Rekodi yako:
23:113 🔁 0/5
قَالُواْ لَبِثۡنَا يَوۡمًا أَوۡ بَعۡضَ يَوۡمٍ فَسۡـَٔلِ ٱلۡعَآدِّينَ  ۝١١٣
Qaaloo labisnaa yawman aw ba`da yawmin fas`alil `aaaddeen
Watasema: Tulikaa siku moja au sehemu ya siku. Basi waulize wanao weka hisabu.
🎤 Rekodi yako:
23:114 🔁 0/5
قَٰلَ إِن لَّبِثۡتُمۡ إِلَّا قَلِيلًاۖ لَّوۡ أَنَّكُمۡ كُنتُمۡ تَعۡلَمُونَ  ۝١١٤
Qaala il labistum illaa qaleelal law annakum kuntum ta`lamoon
Atasema: Nyinyi hamkukaa huko duniani ila kidogo, laiti ingeli kuwa mnajua.
🎤 Rekodi yako:
23:115 🔁 0/5
أَفَحَسِبۡتُمۡ أَنَّمَا خَلَقۡنَٰكُمۡ عَبَثًا وَأَنَّكُمۡ إِلَيۡنَا لَا تُرۡجَعُونَ  ۝١١٥
Afahsibtum annamaa khalaqnaakum `abasanw wa annakum ilainaa laa turja`oon
Je! Mlidhani ya kwamba tulikuumbeni bure na ya kwamba nyinyi kwetu hamtarudishwa?
🎤 Rekodi yako:
23:116 🔁 0/5
فَتَعَٰلَى ٱللَّهُ ٱلۡمَلِكُ ٱلۡحَقُّۖ لَآ إِلَٰهَ إِلَّا هُوَ رَبُّ ٱلۡعَرۡشِ ٱلۡكَرِيمِ  ۝١١٦
Fata`aalal laahul Malikul Haqq; laaa ilaaha illaa Huwa Rabbul `Arshil Kareem
Ametukuka Mwenyezi Mungu, Mfalme wa Haki, hapana mungu ila Yeye, Mola Mlezi wa A'rshi Tukufu.
🎤 Rekodi yako:
23:117 🔁 0/5
وَمَن يَدۡعُ مَعَ ٱللَّهِ إِلَٰهًا ءَاخَرَ لَا بُرۡهَٰنَ لَهُۥ بِهِۦ فَإِنَّمَا حِسَابُهُۥ عِندَ رَبِّهِۦٓۚ إِنَّهُۥ لَا يُفۡلِحُ ٱلۡكَٰفِرُونَ  ۝١١٧
Wa mai yad`u ma`allaahi ilaahan aakhara laa burhaana lahoo bihee fa innnamaa hisaabuhoo `inda Rabbih; innahoo laa yuflihul kaafiroon
Na anaye muomba - pamoja na Mwenyezi Mungu - mungu mwenginewe hana ushahidi wa hili; basi bila ya shaka hisabu yake iko kwa Mola wake Mlezi. Kwa hakika makafiri hawafanikiwi.
🎤 Rekodi yako:
23:118 🔁 0/5
وَقُل رَّبِّ ٱغۡفِرۡ وَٱرۡحَمۡ وَأَنتَ خَيۡرُ ٱلرَّٰحِمِينَ  ۝١١٨
Wa qur Rabbigh fir warham wa Anta khairur raahimeen
Nawe sema: Mola wangu Mlezi! Samehe na urehemu nawe ni Mbora wa wanao rehemu.
🎤 Rekodi yako:
💡 Gusa neno lililofichwa ili lionekane kwa muda — maendeleo yako yanahifadhiwa kiotomatiki.

🎉
🎊 Hongera! Umemaliza Kuhifadhi
Mishary Rashid Alafasy
Mahmoud Khalil Al-Husary
Abdurrahman As-Sudais
Mohamed Siddiq Al-Minshawi
Abdul Basit Abdul Samad
Ali Al-Hudhaify
Ahmed ibn Ali al-Ajamy
Abu Bakr Ash-Shaatree
Muhammad Ayyoub
Abdullah Basfar
Abdullah Al-Juhani
Maher Al Muaiqly
0:00
0:00
-

Kurani Tukufu


Tuesday, August 18, 2026

Usitusahau katika dua zako njema