Sura Al-Mu'minun
PDF —
Built right in your browser — download starts automatically
Sura Al-Mu'minun pdf — Pakua (Kiswahili)
Sura Al-Mu'minun pdf Kiswahili — Pakua Sura Al-Mu'minun Tafsiri. Al-Mu'minun (Makka) 118 Aya.
Related
- Al-Mu'minun TafsiriKiswahili
- Al-Mu'minun mp3Sikiliza
- Quran Index Kiswahili114
More Sura PDF
Sura Al-Mu'minun

ﭑﭒﭓﭔ
HAKIKA wamefanikiwa Waumini,
ﭕﭖﭗﭘﭙﭚ
Ambao ni wanyenyekevu katika Sala zao,
ﭛﭜﭝﭞﭟﭠ
Na ambao hujiepusha na mambo ya upuuzi,
ﭡﭢﭣﭤﭥ
Na ambao wanatoa Zaka,
ﭦﭧﭨﭩﭪ
Na ambao wanazilinda tupu zao,
ﭫﭬﭭﭮﭯﭰﭱﭲﭳﭴﭵ
Isipo kuwa kwa wake zao au kwa iliyo wamiliki mikono yao ya kulia. Kwani hao si wenye kulaumiwa.
ﭶﭷﭸﭹﭺﭻﭼﭽ
Lakini anaye taka kinyume cha haya, basi hao ndio warukao mipaka.
ﭾﭿﮀﮁﮂﮃ
Na ambao wanazitimiza amana zao na ahadi zao,
ﮄﮅﮆﮇﮈﮉ
Na ambao Sala zao wanazihifadhi -
ﮊﮋﮌﮍ
Hao ndio warithi,
ﮎﮏﮐﮑﮒﮓﮔ
Ambao watairithi Pepo ya Firdausi, wadumu humo.
ﮕﮖﮗﮘﮙﮚﮛﮜ
Na kwa yakini tumemuumba mtu kutokana na asli ya udongo.
ﮝﮞﮟﮠﮡﮢﮣ
Kisha tukamjaalia awe tone ya mbegu ya uzazi katika kalio madhubuti.
ﮤﮥﮦﮧﮨﮩﮪﮫﮬﮭﮮﮯﮰﮱﯓﯔﯕﯖﯗﯘﯙﯚﯛ
Kisha tukaiumba tone kuwa damu iliyo ganda, na tukaiumba damu kuwa pande la nyama, kisha tukaliumba pande la nyama kuwa mifupa, na mifupa tukaivika nyama. Kisha tukamfanya kiumbe mwengine. Basi ametukuka Mwenyezi Mungu Mbora wa waumbaji.
ﯜﯝﯞﯟﯠﯡ
Kisha hakika nyinyi baada ya hayo mtakufa.
ﯢﯣﯤﯥﯦﯧ
Kisha hakika nyinyi Siku ya Kiyama mtafufuliwa.
ﯨﯩﯪﯫﯬﯭﯮﯯﯰﯱﯲ
Na kwa yakini tumeziumba juu yenu njia saba. Nasi hatukuwa wenye kughafilika na viumbe.
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖﭗﭘﭙﭚﭛﭜﭝﭞﭟ
Na tumeteremsha kutoka mbinguni maji kwa kiasi na tukayatuliza katika ardhi. Na hakika Sisi tunaweza kuyaondoa.
ﭠﭡﭢﭣﭤﭥﭦﭧﭨﭩﭪﭫﭬﭭ
Kwa maji hayo tukakufanyieni bustani za mitende na mizabibu, mnapata humo matunda mengi, na katika hayo mnakula;
ﭮﭯﭰﭱﭲﭳﭴﭵﭶﭷ
Na mti utokao katika mlima wa Sinai, unatoa mafuta na kuwa kitoweo kwa walao.
ﭸﭹﭺﭻﭼﭽﭾﭿﮀﮁﮂﮃﮄﮅﮆﮇﮈ
Na hakika mnayo mazingatio makubwa katika nyama hoa - tunakunywesheni katika vile viliomo matumboni mwao, na nyinyi mnapata katika hao manufaa mengi, na pia mnawala.
ﮉﮊﮋﮌﮍ
Na juu yao na juu ya marikebu mnabebwa.
ﮎﮏﮐﮑﮒﮓﮔﮕﮖﮗﮘﮙﮚﮛﮜﮝﮞﮟ
Na hakika tulimtuma Nuhu kwa watu wake, akasema: Enyi watu wangu! Muabuduni Mwenyezi Mungu. Nyinyi hamna mungu asiye kuwa Yeye. Basi je! Hamwogopi?
ﮠﮡﮢﮣﮤﮥﮦﮧﮨﮩﮪﮫﮬﮭﮮﮯﮰﮱﯓﯔﯕﯖﯗﯘﯙﯚﯛ
Walisema wale wakuu walio kufuru katika watu wake: Huyu si chochote ila ni mtu tu kama nyinyi. Anataka kujipa ubora juu yenu. Na lau kuwa Mwenyezi Mungu amependa basi yakini angeli teremsha Malaika. Hatukusikia haya kwa baba zetu wa zamani.
ﯜﯝﯞﯟﯠﯡﯢﯣﯤﯥﯦ
Huyu si lolote ila ni mtu mwenye wazimu. Basi mngojeeni tu kwa muda.
ﯧﯨﯩﯪﯫﯬ
Akasema (Nuhu): Mola wangu Mlezi! Ninusuru kwa kuwa wamenikanusha.
ﯭﯮﯯﯰﯱﯲﯳﯴﯵﯶﯷﯸﯹﯺﯻﯼﯽﯾﯿﰀﰁﰂﰃﰄﰅﰆﰇﰈﰉﰊﰋﰌﰍﰎ
Tukampa wahyi: Unda jahazi mbele ya macho yetu na uwongozi wetu! Basi itapo fika amri yetu na ikafurika tanuri, hapo waingize ndani yake wa kila namna dume na jike, na ahali zako, isipo kuwa yule ambaye katika wao juu yake imekwisha tangulia kauli. Wala usinitajie hao walio dhulumu. Kwani hao bila ya shaka watazamishwa.
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖﭗﭘﭙﭚﭛﭜﭝﭞﭟﭠ
Basi utakapo tulia wewe na walio pamoja nawe humo marikebuni, sema: Alhamdulillahi Sifa zote njema ni za Mwenyezi Mungu, aliye tuokoa na watu madhaalimu!
ﭡﭢﭣﭤﭥﭦﭧﭨﭩ
Na sema: Mola wangu Mlezi! Niteremshe mteremsho wenye baraka, na Wewe ni Mbora wa wateremshaji.
ﭪﭫﭬﭭﭮﭯﭰﭱ
Hakika katika hayo yapo mazingatio. Na kwa yakini Sisi ni wenye kuwafanyia mtihani.
ﭲﭳﭴﭵﭶﭷﭸ
Kisha baada yao tukaanzisha kizazi kingine.
ﭹﭺﭻﭼﭽﭾﭿﮀﮁﮂﮃﮄﮅﮆﮇﮈ
Tukawapelekea Mtume miongoni mwao, kuwaambia: Muabuduni Mwenyezi Mungu! Hamna mungu asiye kuwa Yeye. Jee, hamwogopi?
ﮉﮊﮋﮌﮍﮎﮏﮐﮑﮒﮓﮔﮕﮖﮗﮘﮙﮚﮛﮜﮝﮞﮟﮠﮡﮢ
Na wakubwa katika watu wake walio kufuru na wakakanusha mkutano wa Akhera, na tukawadekeza kwa starehe katika maisha ya dunia, walisema: Huyu si chochote ila ni binaadamu kama nyinyi; anakula mlacho, na anakunywa mnywacho.
ﮣﮤﮥﮦﮧﮨﮩﮪ
Na nyinyi mkimt'ii mtu kama nyinyi basi hakika mtakuwa khasarani.
ﮫﮬﮭﮮﮯﮰﮱﯓﯔﯕ
Hivyo anakuahidini ati ya kwamba mtakapo kufa na mkawa udongo na mifupa kuwa mtatolewa?
ﯖﯗﯘﯙﯚﯛ
Hayawi! Hayawi hayo mnayo ahidiwa.
ﯜﯝﯞﯟﯠﯡﯢﯣﯤﯥﯦ
Hapana ila uhai wetu wa duniani tu, tunakufa na kuishi basi. Wala sisi hatutafufuliwa.
ﯧﯨﯩﯪﯫﯬﯭﯮﯯﯰﯱﯲﯳ
Huyu si lolote ila ni mtu anaye mzulia Mwenyezi Mungu uwongo, wala sisi sio wa kumuamini.
ﯴﯵﯶﯷﯸﯹ
Akasema: Mola wangu Mlezi! Ninusuru kwa sababu wananikanusha.
ﯺﯻﯼﯽﯾﯿ
(Mwenyezi Mungu) akasema: Baada ya muda mchache watakuwa wenye kujuta.
ﰀﰁﰂﰃﰄﰅﰆﰇﰈﰉ
Basi ukawanyakua ukelele kwa haki, na tukawafanya kama takataka zinazo elea juu ya maji. Ikapotelea mbali kaumu ya madhaalimu!
ﰊﰋﰌﰍﰎﰏﰐ
Kisha tukaleta baada yao vizazi vingine.
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖﭗﭘ
Hapana umma uwezao kutanguliza ajali yake wala kuikawiza.
ﭙﭚﭛﭜﭝﭞﭟﭠﭡﭢﭣﭤﭥﭦﭧﭨﭩﭪﭫﭬﭭﭮﭯ
Kisha tukawatuma Mitume wetu, mmoja baada ya mmoja. Kila umma alipo wafikia Mtume wao walimkanusha. Tukawafuatanisha hawa baada ya hawa, na tukawafanya ni hadithi za kusimuliwa. Wakapotelea mbali watu wasio amini.
ﭰﭱﭲﭳﭴﭵﭶﭷﭸ
Kisha tukamtuma Musa na nduguye, Haaruni, pamoja na ishara zetu na hoja zilizo wazi.
ﭹﭺﭻﭼﭽﭾﭿﮀ
Kumwendea Firauni na wakuu wake. Lakini walijivuna, nao walikuwa watu majeuri.
ﮁﮂﮃﮄﮅﮆﮇﮈ
Wakasema: Je, tuwaamini wanaadamu wawili hawa kama sisi, na ambao watu wao ni watumwa wetu?
ﮉﮊﮋﮌﮍ
Basi wakawakanusha, na wakawa miongoni mwa walio angamizwa.
ﮎﮏﮐﮑﮒﮓﮔ
Na hakika tulimpa Musa Kitabu ili wapate kuongoka.
ﮕﮖﮗﮘﮙﮚﮛﮜﮝﮞﮟﮠ
Na tukamfanya mwana wa Mariamu na mama yake kuwa ni Ishara, na tukawapa makimbilio kwenda mahali palipo inuka penye utulivu na chemchem za maji.
ﮡﮢﮣﮤﮥﮦﮧﮨﮩﮪﮫﮬﮭ
Enyi Mitume! Kuleni vyakula vizuri na tendeni mema. Hakika Mimi ni Mjuzi wa mnayo yatenda.
ﮮﮯﮰﮱﯓﯔﯕﯖﯗ
Na kwa yakini huu Umma wenu ni Umma mmoja, na Mimi ni Mola wenu Mlezi, basi nicheni Mimi.
ﯘﯙﯚﯛﯜﯝﯞﯟﯠﯡﯢ
Lakini walikatiana jambo lao mapande mbali mbali. Kila kundi likifurahia kwa waliyo nayo.
ﯣﯤﯥﯦﯧﯨ
Basi waache katika ghafla yao kwa muda.
ﯩﯪﯫﯬﯭﯮﯯﯰ
Je! Wanadhani ya kuwa kwa vile tunavyo wapa mali na watoto
ﯱﯲﯳﯴﯵﯶﯷﯸﯹ
Ndio tunawahimizia kheri? Lakini wenyewe hawatambui.
ﯺﯻﯼﯽﯾﯿﰀﰁ
Kwa hakika hao ambao kwa kumwogopa Mola wao Mlezi wananyenyekea,
ﰂﰃﰄﰅﰆﰇ
Na wale ambao Ishara za Mola wao Mlezi wanaziamini,
ﰈﰉﰊﰋﰌﰍ
Na wale ambao Mola wao Mlezi hawamshirikishi,
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖﭗﭘﭙﭚﭛ
Na wale ambao wanatoa walicho pewa, na hali nyoyo zao zinagopa kwa kuwa watarejea kwa Mola wao Mlezi,
ﭜﭝﭞﭟﭠﭡﭢﭣ
Basi wote hao ndio wanao kimbilia katika mambo ya kheri, na ndio watakao tangulia kuyafikia.
ﭤﭥﭦﭧﭨﭩﭪﭫﭬﭭﭮﭯﭰﭱ
Na hatuilazimishi nafsi ila kwa kadri ya uwezo wake. Na tunacho kitabu kisemacho kweli. Nao hawatadhulumiwa.
ﭲﭳﭴﭵﭶﭷﭸﭹﭺﭻﭼﭽﭾﭿﮀ
Lakini nyoyo zao zimeghafilika na hayo, na wanavyo vitendo vinginevyo wanavyo vifanya.
ﮁﮂﮃﮄﮅﮆﮇﮈﮉ
Hata tutakapo watia katika adhabu wale walio dekezwa kwa starehe kati yao, hapo ndipo watapo yayatika.
ﮊﮋﮌﮍﮎﮏﮐﮑﮒ
Msiyayatike leo! Hakika nyinyi hamtanusurika nasi.
ﮓﮔﮕﮖﮗﮘﮙﮚﮛﮜ
Hakika zilikuwa Aya zangu mkisomewa, nanyi mkirudi nyuma juu ya visigino vyenu,
ﮝﮞﮟﮠﮡ
Na huku mkitakabari na usiku mkiizungumza (Qur'ani) kwa dharau.
ﮢﮣﮤﮥﮦﮧﮨﮩﮪﮫﮬ
Je, hawakuifikiri kauli, au yamewajia yasiyo wafikia baba zao wa zamani?
ﮭﮮﮯﮰﮱﯓﯔﯕ
Au hawakumjua Mtume wao, ndio maana wanamkataa?
ﯖﯗﯘﯙﯚﯛﯜﯝﯞﯟﯠﯡ
Au wanasema: Ana wazimu? Bali amewajia kwa Haki, na wengi wao wanaichukia Haki.
ﯢﯣﯤﯥﯦﯧﯨﯩﯪﯫﯬﯭﯮﯯﯰﯱﯲﯳ
Na lau kuwa Haki ingeli fuata matamanio yao, basi zingeli haribika mbingu na ardhi na waliomo ndani. Bali tumewaletea ukumbusho wao, nao wanajitenga mbali na ukumbusho wao.
ﯴﯵﯶﯷﯸﯹﯺﯻﯼﯽﯾ
Au unawaomba ujira? Lakini ujira wa Mola wako Mlezi ni bora, na Yeye ndiye Mbora wa wanao ruzuku.
ﯿﰀﰁﰂﰃﰄ
Na kwa yakini wewe unawaita kwenye Njia Iliyo Nyooka.
ﰅﰆﰇﰈﰉﰊﰋﰌﰍ
Na hakika wale wasio iamini Akhera wanajitenga na Njia hiyo.
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖﭗﭘﭙﭚﭛﭜﭝ
Na lau tungeli warehemu na tukawaondolea shida waliyo nayo bila ya shaka wangeli endelea katika upotofu wao vile vile, wakitangatanga.
ﭞﭟﭠﭡﭢﭣﭤﭥﭦ
Na hakika tuliwatia adhabu kali; lakini hawakuelekea kwa Mola wao Mlezi wala hawakunyenyekea.
ﭧﭨﭩﭪﭫﭬﭭﭮﭯﭰﭱﭲﭳ
Mpaka tulipo wafungulia mlango wa adhabu kali, hapo ndipo wakawa wenye kukata tamaa.
ﭴﭵﭶﭷﭸﭹﭺﭻﭼﭽﭾﭿ
Na Yeye ndiye aliye kuumbieni kusikia na kuona na nyoyo za kufahamu. Ni kuchache mno kushukuru kwenu.
ﮀﮁﮂﮃﮄﮅﮆﮇ
Na Yeye ndiye aliye kuenezeni katika ardhi, na kwake Yeye mtakusanywa.
ﮈﮉﮊﮋﮌﮍﮎﮏﮐﮑﮒﮓ
Na Yeye ndiye anaye huisha na kufisha, na yake Yeye mabadiliko ya usiku na mchana. Basi je! Hamfahamu?
ﮔﮕﮖﮗﮘﮙﮚ
Bali wanasema kama walivyo sema watu wa kwanza.
ﮛﮜﮝﮞﮟﮠﮡﮢﮣ
Walisema: Je! Tukisha kufa tukawa udongo na mifupa ndio tutafufuliwa?
ﮤﮥﮦﮧﮨﮩﮪﮫﮬﮭﮮﮯﮰ
Tuliahidiwa haya sisi na baba zetu zamani. Hayakuwa haya ila ni visa vya uwongo vya watu wa zamani.
ﮱﯓﯔﯕﯖﯗﯘﯙﯚ
Sema: Ni ya nani ardhi na viliomo ndani yake, kama nyinyi mnajua?
ﯛﯜﯝﯞﯟﯠﯡ
Watasema: Ni vya Mwenyezi Mungu! Sema: Basi, je, hamkumbuki?
ﯢﯣﯤﯥﯦﯧﯨﯩﯪ
Sema: Ni nani Mola Mlezi wa mbingu saba na Mola Mlezi wa A'rshi Kuu?
ﯫﯬﯭﯮﯯﯰﯱ
Watasema: Ni vya Mwenyezi Mungu. Sema: Basi je, hamwogopi?
ﯲﯳﯴﯵﯶﯷﯸﯹﯺﯻﯼﯽﯾﯿﰀ
Sema: Ni nani mkononi mwake umo Ufalme wa kila kitu, naye ndiye anaye linda, wala hakilindwi asicho taka, kama mnajua?
ﰁﰂﰃﰄﰅﰆﰇ
Watasema: (Ufalme huo) ni wa Mwenyezi Mungu. Sema: Basi vipi mnadanganyika?
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖ
Bali tumewaletea Haki, na kwa yakini hao ni waongo.
ﭗﭘﭙﭚﭛﭜﭝﭞﭟﭠﭡﭢﭣﭤﭥﭦﭧﭨﭩﭪﭫﭬﭭﭮﭯﭰﭱ
Mwenyezi Mungu hana mwana yeyote, wala hanaye mungu mwengine. Inge kuwa hivyo basi kila mungu angeli chukua alivyo umba, na baadhi yao wangeli washinda wengine. Mwenyezi Mungu ameepukana na sifa wanazo msifu.
ﭲﭳﭴﭵﭶﭷﭸ
Mjuzi wa siri na dhaahiri, na ametukuka juu ya hayo wanayo mshirikisha nayo.
ﭹﭺﭻﭼﭽﭾﭿ
Sema: Mola wangu Mlezi! Ukinionyesha adhabu waliyo ahidiwa,
ﮀﮁﮂﮃﮄﮅﮆ
Mola wangu Mlezi! Usinijaalie katika watu madhaalimu hao.
ﮇﮈﮉﮊﮋﮌﮍﮎ
Na hakika Sisi ni waweza wa kukuonyeshsa tuliyo waahidi.
ﮏﮐﮑﮒﮓﮔﮕﮖﮗﮘﮙ
Kinga maovu kwa kutenda yaliyo mema zaidi. Sisi tunajua wayasemayo.
ﮚﮛﮜﮝﮞﮟﮠﮡ
Na sema: Mola wangu Mlezi! Najikinga kwako na wasiwasi wa mashet'ani.
ﮢﮣﮤﮥﮦﮧ
Na najikinga kwako, Mola wangu Mlezi, wasinikaribie.
ﮨﮩﮪﮫﮬﮭﮮﮯﮰ
Mpaka yanapo mfikia mmoja wao mauti, husema: Mola wangu Mlezi! Nirudishe.
ﮱﯓﯔﯕﯖﯗﯘﯙﯚﯛﯜﯝﯞﯟﯠﯡﯢﯣﯤﯥ
Ili nitende mema sasa badala ya yale niliyo yaacha. Wapi! Hii ni kauli aisemayo yeye tu. Na nyuma yao kipo kizuizi mpaka siku watapo fufuliwa.
ﯦﯧﯨﯩﯪﯫﯬﯭﯮﯯﯰ
Basi litapo pulizwa baragumu hapo hautakuwapo ujamaa baina yao siku hiyo, wala hawataulizana.
ﯱﯲﯳﯴﯵﯶﯷ
Ama wale ambao mizani zao zitakuwa nzito, hao ndio wenye kufanikiwa.
ﯸﯹﯺﯻﯼﯽﯾﯿﰀﰁﰂ
Na wale ambao mizani zao zitakuwa nyepesi, hao ndio walio zitia khasarani nafsi zao, na katika Jahannamu watadumu.
ﰃﰄﰅﰆﰇﰈﰉ
Moto utababua nyuso zao, nao watakuwa na nyuso zilizo kunjana.
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖﭗﭘﭙ
Je! Hazikuwa Aya zangu mkisomewa, na nyinyi mkizikanusha?
ﭚﭛﭜﭝﭞﭟﭠﭡﭢ
Mola wetu Mlezi! Tulizidiwa na uovu wetu na tukawa watu tulio potea.
ﭣﭤﭥﭦﭧﭨﭩﭪ
Mola wetu Mlezi! Tutoe humu Motoni. Na tufanyapo tena basi kweli sisi ni wenye kudhulumu.
ﭫﭬﭭﭮﭯﭰ
Atasema Mwenyezi Mungu: Tokomeeni humo, wala msinisemeze.
ﭱﭲﭳﭴﭵﭶﭷﭸﭹﭺﭻﭼﭽﭾﭿ
Bila ya shaka lilikuwapo kundi katika waja wangu likisema: Mola wetu Mlezi! Tumeamini; basi tusamehe na uturehemu, nawe ndiwe Mbora wa wanao rehemu.
ﮀﮁﮂﮃﮄﮅﮆﮇﮈ
Lakini nyinyi mliwakejeli hata wakakusahaulisheni kunikumbuka, na mlikuwa mkiwacheka.
ﮉﮊﮋﮌﮍﮎﮏﮐﮑ
Hakika Mimi leo nimewalipa kwa vile walivyo subiri. Bila ya shaka hao ndio wenye kufuzu.
ﮒﮓﮔﮕﮖﮗﮘﮙ
Atasema: Mlikaa muda gani katika ardhi kwa hisabu ya miaka?
ﮚﮛﮜﮝﮞﮟﮠﮡﮢ
Watasema: Tulikaa siku moja au sehemu ya siku. Basi waulize wanao weka hisabu.
ﮣﮤﮥﮦﮧﮨﮩﮪﮫﮬﮭ
Atasema: Nyinyi hamkukaa huko duniani ila kidogo, laiti ingeli kuwa mnajua.
ﮮﮯﮰﮱﯓﯔﯕﯖﯗ
Je! Mlidhani ya kwamba tulikuumbeni bure na ya kwamba nyinyi kwetu hamtarudishwa?
ﯘﯙﯚﯛﯜﯝﯞﯟﯠﯡﯢﯣﯤ
Ametukuka Mwenyezi Mungu, Mfalme wa Haki, hapana mungu ila Yeye, Mola Mlezi wa A'rshi Tukufu.
ﯥﯦﯧﯨﯩﯪﯫﯬﯭﯮﯯﯰﯱﯲﯳﯴﯵﯶﯷﯸ
Na anaye muomba - pamoja na Mwenyezi Mungu - mungu mwenginewe hana ushahidi wa hili; basi bila ya shaka hisabu yake iko kwa Mola wake Mlezi. Kwa hakika makafiri hawafanikiwi.
ﯹﯺﯻﯼﯽﯾﯿﰀ
Nawe sema: Mola wangu Mlezi! Samehe na urehemu nawe ni Mbora wa wanao rehemu.
Kurani Tukufu
Tuesday, August 18, 2026
Usitusahau katika dua zako njema







