🔥 0 siku mfululizo
📖 Sura ndefu — imegawanywa sehemu ndogo (45 Aya)
0/45
50:1
🔁 0/5
قٓۚ وَٱلۡقُرۡءَانِ ٱلۡمَجِيدِ ١
Qaaaf; wal Qur aanil Majeed
Qaaf. Naapa kwa Qur'ani tukufu!
🎤 Rekodi yako:
50:2
🔁 0/5
بَلۡ عَجِبُوٓاْ أَن جَآءَهُم مُّنذِرٌ مِّنۡهُمۡ فَقَالَ ٱلۡكَٰفِرُونَ هَٰذَا شَيۡءٌ عَجِيبٌ ٢
Bal `ajibooo an jaa`ahum munzirum minhum faqaalal kaafiroona haazaa shai`un `ajeeb
Bali wanastaajabu kwamba amewafikia mwonyaji kutoka miongoni mwao, na wakasema makafiri: Hili ni jambo la ajabu!
🎤 Rekodi yako:
50:3
🔁 0/5
أَءِذَا مِتۡنَا وَكُنَّا تُرَابًاۖ ذَٰلِكَ رَجۡعُۢ بَعِيدٌ ٣
A-izaa mitnaa wa kunnaa turaaban zaalika raj`um ba`eed
Ati tukifa na tukawa udongo...? Kurejea huko kuko mbali!
🎤 Rekodi yako:
50:4
🔁 0/5
قَدۡ عَلِمۡنَا مَا تَنقُصُ ٱلۡأَرۡضُ مِنۡهُمۡۖ وَعِندَنَا كِتَٰبٌ حَفِيظُۢ ٤
Qad `alimnaa maa tanqu-sul-ardu minhum wa `indanaa Kitaabun Hafeez
Hakika Sisi tunajua kiasi cha kila kinacho punguzwa na ardhi kutokana nao. Na kwetu kipo Kitabu kinacho hifadhi yote.
🎤 Rekodi yako:
50:5
🔁 0/5
بَلۡ كَذَّبُواْ بِٱلۡحَقِّ لَمَّا جَآءَهُمۡ فَهُمۡ فِيٓ أَمۡرٍ مَّرِيجٍ ٥
Bal kazzaboo bilhaqqi lammaa jaaa`ahum fahum feee amrim mareej
Lakini waliikanusha Haki ilipo wajia; kwa hivyo wamo katika mambo ya mkorogo.
🎤 Rekodi yako:
50:6
🔁 0/5
أَفَلَمۡ يَنظُرُوٓاْ إِلَى ٱلسَّمَآءِ فَوۡقَهُمۡ كَيۡفَ بَنَيۡنَٰهَا وَزَيَّنَّٰهَا وَمَا لَهَا مِن فُرُوجٍ ٦
Afalam yanzurooo ilas samaaa`i fawqahum kaifa banainaahaa wa zaiyannaahaa wa maa lahaa min furooj
Je! Hawaangalii mbingu zilizo juu yao! Vipi tulivyo zijenga, na tukazipamba. Wala hazina nyufa.
🎤 Rekodi yako:
50:7
🔁 0/5
وَٱلۡأَرۡضَ مَدَدۡنَٰهَا وَأَلۡقَيۡنَا فِيهَا رَوَٰسِيَ وَأَنۢبَتۡنَا فِيهَا مِن كُلِّ زَوۡجِۭ بَهِيجٍ ٧
Wal arda madadnaahaa wa alqainaa feehaa rawaasiya wa ambatnaa feehaa min kulli zawjim baheej
Na ardhi tumeitandaza na tukaiwekea milima, na tukaiotesha mimea mizuri ya kila namna.
🎤 Rekodi yako:
50:8
🔁 0/5
تَبۡصِرَةً وَذِكۡرَىٰ لِكُلِّ عَبۡدٍ مُّنِيبٍ ٨
Tabsiratanw wa zikraa likulli `abdim muneeb
Yawe haya ni kifumbua macho na ukumbusho kwa kila mja mwenye kuelekea.
🎤 Rekodi yako:
50:9
🔁 0/5
وَنَزَّلۡنَا مِنَ ٱلسَّمَآءِ مَآءً مُّبَٰرَكًا فَأَنۢبَتۡنَا بِهِۦ جَنَّٰتٍ وَحَبَّ ٱلۡحَصِيدِ ٩
Wa nazzalnaa minas samaaa`i maaa`am mubaarakan fa ambatnaa bihee jannaatinw wa habbal haseed
Na tumeteremsha kutoka mbinguni maji yaliyo barikiwa, na kwa hayo tukaotesha mabustani na nafaka za kuvunwa.
🎤 Rekodi yako:
50:10
🔁 0/5
وَٱلنَّخۡلَ بَاسِقَٰتٍ لَّهَا طَلۡعٌ نَّضِيدٌ ١٠
Wannakhla baasiqaatil laha tal`un nadeed
Na mitende mirefu yenye makole yaliyo zaa kwa wingi,
🎤 Rekodi yako:
50:11
🔁 0/5
رِّزۡقًا لِّلۡعِبَادِۖ وَأَحۡيَيۡنَا بِهِۦ بَلۡدَةً مَّيۡتًاۚ كَذَٰلِكَ ٱلۡخُرُوجُ ١١
Rizqal lil`ibaad, wa ahyainaa bihee baldatam maitaa; kazaalikal khurooj
Ili iwe ni riziki kwa waja wangu. Na tukaifufua kwa maji nchi iliyo kuwa imekufa. Kama hivyo ndivyo utakavyo kuwa ufufuaji.
🎤 Rekodi yako:
50:12
🔁 0/5
كَذَّبَتۡ قَبۡلَهُمۡ قَوۡمُ نُوحٍ وَأَصۡحَٰبُ ٱلرَّسِّ وَثَمُودُ ١٢
Kazzabat qablahum qawmu Noohinw wa Ashaabur Rassi wa Samood
Kabla yao walikadhibisha kaumu ya Nuhu na wakaazi wa Rassi na Thamudi.
🎤 Rekodi yako:
50:13
🔁 0/5
وَعَادٌ وَفِرۡعَوۡنُ وَإِخۡوَٰنُ لُوطٍ ١٣
Wa `Aadunw wa Fir`awnu wikhwaanu loot
Na A'di na Firauni na kaumu ya Lut'i.
🎤 Rekodi yako:
50:14
🔁 0/5
وَأَصۡحَٰبُ ٱلۡأَيۡكَةِ وَقَوۡمُ تُبَّعٍۚ كُلٌّ كَذَّبَ ٱلرُّسُلَ فَحَقَّ وَعِيدِ ١٤
Wa Ashaabul Aykati wa qawmu Tubba`; kullun kazzabar Rusula fahaqqa wa`eed
Na wakaazi wa Machakani, na watu wa Tubbaa'. Wote hao waliwakanusha Mitume, kwa hivyo onyo likathibitika juu yao.
🎤 Rekodi yako:
50:15
🔁 0/5
أَفَعَيِينَا بِٱلۡخَلۡقِ ٱلۡأَوَّلِۚ بَلۡ هُمۡ فِي لَبۡسٍ مِّنۡ خَلۡقٍ جَدِيدٍ ١٥
Afa`a yeenaa bilkhalqil awwal; bal hum fee labsim min khalqin jadeed
Kwani tulichoka kwa kuumba mara ya kwanza. Bali wao wamo katika shaka tu juu ya umbo jipya.
🎤 Rekodi yako:
50:16
🔁 0/5
وَلَقَدۡ خَلَقۡنَا ٱلۡإِنسَٰنَ وَنَعۡلَمُ مَا تُوَسۡوِسُ بِهِۦ نَفۡسُهُۥۖ وَنَحۡنُ أَقۡرَبُ إِلَيۡهِ مِنۡ حَبۡلِ ٱلۡوَرِيدِ ١٦
Wa laqad khalaqnal insaana wa na`lamu maa tuwaswisu bihee nafsuhoo wa Nahnu aqrabu ilaihi min hablil wareed
Na hakika tumemuumba mtu, nasi tunayajua yanayo mpitikia katika nafsi yake. Na Sisi tuko karibu naye kuliko mshipa wa shingoni mwake.
🎤 Rekodi yako:
50:17
🔁 0/5
إِذۡ يَتَلَقَّى ٱلۡمُتَلَقِّيَانِ عَنِ ٱلۡيَمِينِ وَعَنِ ٱلشِّمَالِ قَعِيدٌ ١٧
Iz yatalaqqal mutalaqqi yaani `anil yameeni wa `anish shimaali qa`eed
Wanapo pokea wapokeaji wawili, wanao kaa kuliani na kushotoni.
🎤 Rekodi yako:
50:18
🔁 0/5
مَّا يَلۡفِظُ مِن قَوۡلٍ إِلَّا لَدَيۡهِ رَقِيبٌ عَتِيدٌ ١٨
Maa yalfizu min qawlin illaa ladaihi raqeebun `ateed
Hatamki neno ila karibu yake yupo mwangalizi tayari.
🎤 Rekodi yako:
50:19
🔁 0/5
وَجَآءَتۡ سَكۡرَةُ ٱلۡمَوۡتِ بِٱلۡحَقِّۖ ذَٰلِكَ مَا كُنتَ مِنۡهُ تَحِيدُ ١٩
Wa jaaa`at kullu nafsim ma`ahaa saaa`iqunw wa shaheed
Na uchungu wa kutoka roho utamjia kwa haki. Hayo ndiyo uliyo kuwa ukiyakimbia.
🎤 Rekodi yako:
50:20
🔁 0/5
وَنُفِخَ فِي ٱلصُّورِۚ ذَٰلِكَ يَوۡمُ ٱلۡوَعِيدِ ٢٠
Wa nufikha fis Soor; zaalika yawmul wa`eed
Na litapulizwa baragumu. Hiyo ndiyo Siku ya Miadi.
🎤 Rekodi yako:
50:21
🔁 0/5
وَجَآءَتۡ كُلُّ نَفۡسٍ مَّعَهَا سَآئِقٌ وَشَهِيدٌ ٢١
Wa jaaa`at kullu nafsim ma`ahaa saaa`iqunw wa shaheed
Na kila nafsi itakuja na pamoja nayo mchungaji na shahidi.
🎤 Rekodi yako:
50:22
🔁 0/5
لَّقَدۡ كُنتَ فِي غَفۡلَةٍ مِّنۡ هَٰذَا فَكَشَفۡنَا عَنكَ غِطَآءَكَ فَبَصَرُكَ ٱلۡيَوۡمَ حَدِيدٌ ٢٢
Laqad kunta fee ghaf latim min haazaa fakashafnaa `anka ghitaaa`aka fabasarukal yawma hadeed
(Aambiwe): Kwa hakika ulikuwa umeghafilika na haya; basi leo tumekuondolea pazia lako, na kwa hivyo kuona kwako leo ni kukali.
🎤 Rekodi yako:
50:23
🔁 0/5
وَقَالَ قَرِينُهُۥ هَٰذَا مَا لَدَيَّ عَتِيدٌ ٢٣
Wa qaala qareenuhoo haazaa maa ladaiya `ateed
Na mwenzake atasema: Huyu niliye naye mimi kesha tayarishwa.
🎤 Rekodi yako:
50:24
🔁 0/5
أَلۡقِيَا فِي جَهَنَّمَ كُلَّ كَفَّارٍ عَنِيدٍ ٢٤
Alqiyaa fee Jahannama kulla kaffaarin `aneed
Mtupeni katika Jahannamu kila kafiri mwenye inda,
🎤 Rekodi yako:
50:25
🔁 0/5
مَّنَّاعٍ لِّلۡخَيۡرِ مُعۡتَدٍ مُّرِيبٍ ٢٥
Mannaa`il lilkhayri mu`tadim mureeb
Akatazaye kheri, arukaye mipaka, mwenye kutia shaka,
🎤 Rekodi yako:
50:26
🔁 0/5
ٱلَّذِي جَعَلَ مَعَ ٱللَّهِ إِلَٰهًا ءَاخَرَ فَأَلۡقِيَاهُ فِي ٱلۡعَذَابِ ٱلشَّدِيدِ ٢٦
Allazee ja`ala ma`al laahi ilaahan aakhara fa alqiyaahu fil`azaabish shadeed
Aliye weka mungu mwengine pamoja na Mwenyezi Mungu. Basi mtupeni katika adhabu kali.
🎤 Rekodi yako:
50:27
🔁 0/5
۞ قَالَ قَرِينُهُۥ رَبَّنَا مَآ أَطۡغَيۡتُهُۥ وَلَٰكِن كَانَ فِي ضَلَٰلِۭ بَعِيدٍ ٢٧
Qaala qareenuhoo Rabbanaa maaa atghaituhoo wa laakin kaana fee dalaahim ba`eed
Mwenzake aseme: Ee Mola wetu Mlezi! Sikumpoteza mimi, bali yeye mwenyewe alikuwa katika upotovu wa mbali.
🎤 Rekodi yako:
50:28
🔁 0/5
قَالَ لَا تَخۡتَصِمُواْ لَدَيَّ وَقَدۡ قَدَّمۡتُ إِلَيۡكُم بِٱلۡوَعِيدِ ٢٨
Qaala laa takhtasimoo ladaayya wa qad qaddamtu ilaikum bilwa`eed
(Mwenyezi Mungu) aseme: Msigombane mbele yangu. Nilikuleteeni mbele onyo langu.
🎤 Rekodi yako:
50:29
🔁 0/5
مَا يُبَدَّلُ ٱلۡقَوۡلُ لَدَيَّ وَمَآ أَنَا۠ بِظَلَّٰمٍ لِّلۡعَبِيدِ ٢٩
Maa yubaddalul qawlu ladaiya wa maaa ana bizal laamil lil`abeed
Mbele yangu haibadilishwi kauli, wala Mimi siwadhulumu waja wangu.
🎤 Rekodi yako:
50:30
🔁 0/5
يَوۡمَ نَقُولُ لِجَهَنَّمَ هَلِ ٱمۡتَلَأۡتِ وَتَقُولُ هَلۡ مِن مَّزِيدٍ ٣٠
Yawma naqoolu li`jahannama halim talaati wa taqoolu hal mim mazeed
Siku tutapo iambia Jahannamu: Je! Umejaa? Nayo itasema: Je! Kuna ziada?
🎤 Rekodi yako:
50:31
🔁 0/5
وَأُزۡلِفَتِ ٱلۡجَنَّةُ لِلۡمُتَّقِينَ غَيۡرَ بَعِيدٍ ٣١
Wa uzlifatil jannatu lil muttaqeena ghaira ba`eed
Na Pepo italetwa karibu kwa ajili ya wachamngu, haitakuwa mbali.
🎤 Rekodi yako:
50:32
🔁 0/5
هَٰذَا مَا تُوعَدُونَ لِكُلِّ أَوَّابٍ حَفِيظٍ ٣٢
Haaza maa too`adoona likulli awwaabin hafeez
Haya ndiyo mnayo ahidiwa kwa kila mwenye kurejea kwa Mwenyezi Mungu na akajilinda.
🎤 Rekodi yako:
50:33
🔁 0/5
مَّنۡ خَشِيَ ٱلرَّحۡمَٰنَ بِٱلۡغَيۡبِ وَجَآءَ بِقَلۡبٍ مُّنِيبٍ ٣٣
Man khashiyar Rahmaana bilghaibi wa jaaa`a biqalbim muneeb
Mwenye kumwogopa Mwingi wa Rehema hali kuwa hamwoni, na akaja kwa moyo ulio elekea-
🎤 Rekodi yako:
50:34
🔁 0/5
ٱدۡخُلُوهَا بِسَلَٰمٍۖ ذَٰلِكَ يَوۡمُ ٱلۡخُلُودِ ٣٤
Udkhuloohaa bisalaamin zaalika yawmul khulood
(Ataambiwa) ingieni kwa salama. Hiyo ndiyo siku ya daima dawamu.
🎤 Rekodi yako:
50:35
🔁 0/5
لَهُم مَّا يَشَآءُونَ فِيهَا وَلَدَيۡنَا مَزِيدٌ ٣٥
Lahum maa yashaaa`oona feehaa wa ladainaa mazeed
Humo watapata wakitakacho, na kwetu yako ya ziada.
🎤 Rekodi yako:
50:36
🔁 0/5
وَكَمۡ أَهۡلَكۡنَا قَبۡلَهُم مِّن قَرۡنٍ هُمۡ أَشَدُّ مِنۡهُم بَطۡشًا فَنَقَّبُواْ فِي ٱلۡبِلَٰدِ هَلۡ مِن مَّحِيصٍ ٣٦
Wa kam ahlaknaa qablahum min qarnin hum ashaddu minhum batshan fanaqqaboo fil bilaad, hal mim mahees
Na kaumu ngapi tuliziangamiza kabla yao walio kuwa na nguvu zaidi kuliko hawa! Nao walitanga tanga katika nchi nyingi. Je! Walipata pa kukimbilia?
🎤 Rekodi yako:
50:37
🔁 0/5
إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَذِكۡرَىٰ لِمَن كَانَ لَهُۥ قَلۡبٌ أَوۡ أَلۡقَى ٱلسَّمۡعَ وَهُوَ شَهِيدٌ ٣٧
Inna fee zaalika lazikraa liman kaana lahoo qalbun aw alqas sam`a wa huwa shaheed
Hakika katika hayo upo ukumbusho kwa mwenye moyo au akatega sikio naye yupo anashuhudia.
🎤 Rekodi yako:
50:38
🔁 0/5
وَلَقَدۡ خَلَقۡنَا ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضَ وَمَا بَيۡنَهُمَا فِي سِتَّةِ أَيَّامٍ وَمَا مَسَّنَا مِن لُّغُوبٍ ٣٨
Wa laqad khalaqnas samaawaati wal arda wa maa bainahumaa fee sittati ayyaamin wa maa massanaa mil lughoob
Na bila ya shaka Sisi tumeziumba mbingu na ardhi na vilio baina yao mnamo siku sita; na wala hayakutugusa machofu.
🎤 Rekodi yako:
50:39
🔁 0/5
فَٱصۡبِرۡ عَلَىٰ مَا يَقُولُونَ وَسَبِّحۡ بِحَمۡدِ رَبِّكَ قَبۡلَ طُلُوعِ ٱلشَّمۡسِ وَقَبۡلَ ٱلۡغُرُوبِ ٣٩
Fasbir `alaa maa yaqooloona wa sabbih bihamdi Rabbika qabla tuloo`ish shamsi wa qablal ghuroob
Basi vumilia kwa hayo wasemayo, na mtakase kwa kumsifu Mola wako Mlezi kabla ya kuchomoza jua na kabla ya kuchwa.
🎤 Rekodi yako:
50:40
🔁 0/5
وَمِنَ ٱلَّيۡلِ فَسَبِّحۡهُ وَأَدۡبَٰرَ ٱلسُّجُودِ ٤٠
Wa minal laili fasabbih hu wa adbaaras sujood
Na katika usiku pia mtakase, na baada ya kusujudu.
🎤 Rekodi yako:
50:41
🔁 0/5
وَٱسۡتَمِعۡ يَوۡمَ يُنَادِ ٱلۡمُنَادِ مِن مَّكَانٍ قَرِيبٍ ٤١
Wastami` yawma yunaa dil munaadi mim makaanin qareeb
Na sikiliza siku atapo nadi mwenye kunadi kutoka pahala karibu.
🎤 Rekodi yako:
50:42
🔁 0/5
يَوۡمَ يَسۡمَعُونَ ٱلصَّيۡحَةَ بِٱلۡحَقِّۚ ذَٰلِكَ يَوۡمُ ٱلۡخُرُوجِ ٤٢
Yawma yasmaoonas sai hata bilhaqq zaalika yawmul khurooj
Siku watakapo sikia ukelele wa haki. Hiyo ndiyo siku ya kufufuka.
🎤 Rekodi yako:
50:43
🔁 0/5
إِنَّا نَحۡنُ نُحۡيِۦ وَنُمِيتُ وَإِلَيۡنَا ٱلۡمَصِيرُ ٤٣
Innaa Nahnu nuhyee wa numeetu wa ilainal maseer
Hakika Sisi tunahuisha na tunafisha, na kwetu Sisi ndio marejeo.
🎤 Rekodi yako:
50:44
🔁 0/5
يَوۡمَ تَشَقَّقُ ٱلۡأَرۡضُ عَنۡهُمۡ سِرَاعًاۚ ذَٰلِكَ حَشۡرٌ عَلَيۡنَا يَسِيرٌ ٤٤
Yawma tashaqqaqul ardu `anhum siraa`aa; zaalika hashrun `alainaa yaseer
Siku itapo wapasukia ardhi mbio mbio! Mkusanyo huo kwetu ni mwepesi.
🎤 Rekodi yako:
50:45
🔁 0/5
نَّحۡنُ أَعۡلَمُ بِمَا يَقُولُونَۖ وَمَآ أَنتَ عَلَيۡهِم بِجَبَّارٍۖ فَذَكِّرۡ بِٱلۡقُرۡءَانِ مَن يَخَافُ وَعِيدِ ٤٥
Nahnu a`lamu bimaa yaqooloona wa maaa anta `alihim bijabbaarin fazakkir bil quraani many yakhaafu wa`eed
Sisi tunajua kabisa wayasemayo. Wala wewe si mwenye kuwatawalia kwa ujabari. Basi mkumbushe kwa Qur'ani anaye liogopa onyo.
🎤 Rekodi yako:
💡 Gusa neno lililofichwa ili lionekane kwa muda — maendeleo yako yanahifadhiwa kiotomatiki.
العربيةEnglishBahasa IndonesiaTürkçeРусскийفارسیFrançaisاردوবাংলাDeutschEspañol中文हिन्दीPortuguêsItalianoภาษาไทยPolskiNederlandsShqipKiswahiliO'zbekதமிழ்MelayuBosanskiSoomaaliAzərbaycanکوردی한국어日本語SvenskaDanskNorskپښتوമലയാളംසිංහලTamazightHausaአማርኛБългарскиТоҷикӣҚазақшаFilipinoسنڌيYorùbáFulfuldeТатарчаئۇيغۇرچەКыргызчаਪੰਜਾਬੀJawaతెలుగుမြန်မာગુજરાતીOromoमराठीTiếng ViệtMalagasyНохчийнWolofދިވެހިಕನ್ನಡУкраїнськаΕλληνικάქართულიខ្មែរدریQafar afMaranaoनेपाली
Kurani Tukufu
Tuesday, August 18, 2026
Usitusahau katika dua zako njema







