Surah Al-Mutaffifin with Swahili

  1. Surah mp3
  2. More
  3. Swahili
The Holy Quran | Quran translation | Language Swahili | Surah Mutaffifin | المطففين - Ayat Count 36 - The number of the surah in moshaf: 83 - The meaning of the surah in English: The Dealers in Fraud - The Cheats.

وَيْلٌ لِّلْمُطَفِّفِينَ(1)

 Ole wao hao wapunjao!

الَّذِينَ إِذَا اكْتَالُوا عَلَى النَّاسِ يَسْتَوْفُونَ(2)

 Ambao wanapo jipimia kwa watu hudai watimiziwe.

وَإِذَا كَالُوهُمْ أَو وَّزَنُوهُمْ يُخْسِرُونَ(3)

 Na wao wanapo wapimia watu kwa kipimo au mizani hupunguza.

أَلَا يَظُنُّ أُولَٰئِكَ أَنَّهُم مَّبْعُوثُونَ(4)

 Kwani hawadhani hao kwamba watafufuliwa

لِيَوْمٍ عَظِيمٍ(5)

 Katika Siku iliyo kuu,

يَوْمَ يَقُومُ النَّاسُ لِرَبِّ الْعَالَمِينَ(6)

 Siku watapo msimamia watu Mola Mlezi wa walimwengu wote?

كَلَّا إِنَّ كِتَابَ الْفُجَّارِ لَفِي سِجِّينٍ(7)

 Hasha! Hakika maandiko ya wakosefu bila ya shaka yamo katika Sijjin.

وَمَا أَدْرَاكَ مَا سِجِّينٌ(8)

 Unajua nini Sijjin?

كِتَابٌ مَّرْقُومٌ(9)

 Kitabu kilicho andikwa.

وَيْلٌ يَوْمَئِذٍ لِّلْمُكَذِّبِينَ(10)

 Ole wao siku hiyo kwa wanao kadhibisha!

الَّذِينَ يُكَذِّبُونَ بِيَوْمِ الدِّينِ(11)

 Ambao wanaikadhibisha Siku ya Malipo.

وَمَا يُكَذِّبُ بِهِ إِلَّا كُلُّ مُعْتَدٍ أَثِيمٍ(12)

 Wala haikadhibishi ila kila mwenye kuruka mipaka, mwenye dhambi.

إِذَا تُتْلَىٰ عَلَيْهِ آيَاتُنَا قَالَ أَسَاطِيرُ الْأَوَّلِينَ(13)

 Anapo somewa Aya zetu husema: Ni visa vya watu wa kale!

كَلَّا ۖ بَلْ ۜ رَانَ عَلَىٰ قُلُوبِهِم مَّا كَانُوا يَكْسِبُونَ(14)

 Hasha! Bali yametia kutu juu ya nyoyo zao hao walio kuwa wakiyachuma.

كَلَّا إِنَّهُمْ عَن رَّبِّهِمْ يَوْمَئِذٍ لَّمَحْجُوبُونَ(15)

 Hasha! Hakika hao siku hiyo bila ya shaka watazuiliwa na neema za Mola wao Mlezi.

ثُمَّ إِنَّهُمْ لَصَالُو الْجَحِيمِ(16)

 Kisha wataingia Motoni!

ثُمَّ يُقَالُ هَٰذَا الَّذِي كُنتُم بِهِ تُكَذِّبُونَ(17)

 Kisha waambiwe: Haya ndiyo mliyo kuwa mkiyakadhabisha.

كَلَّا إِنَّ كِتَابَ الْأَبْرَارِ لَفِي عِلِّيِّينَ(18)

 Hasha! Hakika maandiko ya watu wema bila ya shaka yamo katika I'liyyin.

وَمَا أَدْرَاكَ مَا عِلِّيُّونَ(19)

 Na nini kitakacho kujuvya nini I'liyyin?

كِتَابٌ مَّرْقُومٌ(20)

 Kitabu kilicho andikwa.

يَشْهَدُهُ الْمُقَرَّبُونَ(21)

 Wanakishuhudia walio karibishwa.

إِنَّ الْأَبْرَارَ لَفِي نَعِيمٍ(22)

 Hakika watu wema bila ya shaka watakuwa katika neema.

عَلَى الْأَرَائِكِ يَنظُرُونَ(23)

 Wakae juu ya viti vya enzi wakiangalia.

تَعْرِفُ فِي وُجُوهِهِمْ نَضْرَةَ النَّعِيمِ(24)

 Utatambua katika nyuso zao mng'aro wa neema,

يُسْقَوْنَ مِن رَّحِيقٍ مَّخْتُومٍ(25)

 Watanyweshwa kinywaji safi kiliyo tiwa muhuri,

خِتَامُهُ مِسْكٌ ۚ وَفِي ذَٰلِكَ فَلْيَتَنَافَسِ الْمُتَنَافِسُونَ(26)

 Muhuri wake ni miski. Na katika hayo washindanie wenye kushindana.

وَمِزَاجُهُ مِن تَسْنِيمٍ(27)

 Na mchanganyiko wake ni Tasniim,

عَيْنًا يَشْرَبُ بِهَا الْمُقَرَّبُونَ(28)

 Chemchem watakayo inywa walio kurubishwa.

إِنَّ الَّذِينَ أَجْرَمُوا كَانُوا مِنَ الَّذِينَ آمَنُوا يَضْحَكُونَ(29)

 Kwa hakika wale walio kuwa wakosefu walikuwa wakiwacheka walio amini.

وَإِذَا مَرُّوا بِهِمْ يَتَغَامَزُونَ(30)

 Na wanapo pita karibu yao wakikonyezana.

وَإِذَا انقَلَبُوا إِلَىٰ أَهْلِهِمُ انقَلَبُوا فَكِهِينَ(31)

 Na wanapo rudi kwa watu wao hurudi nao wamefurahi.

وَإِذَا رَأَوْهُمْ قَالُوا إِنَّ هَٰؤُلَاءِ لَضَالُّونَ(32)

 Na wanapo waona husema: Hakika hawa ndio khasa walio potea.

وَمَا أُرْسِلُوا عَلَيْهِمْ حَافِظِينَ(33)

 Na wao hawakutumwa wawe walinzi juu yao.

فَالْيَوْمَ الَّذِينَ آمَنُوا مِنَ الْكُفَّارِ يَضْحَكُونَ(34)

 Basi leo walio amini ndio watawacheka makafiri,

عَلَى الْأَرَائِكِ يَنظُرُونَ(35)

 Nao wako juu ya viti vya enzi wakiangalia.

هَلْ ثُوِّبَ الْكُفَّارُ مَا كَانُوا يَفْعَلُونَ(36)

 Je! makafiri wamelipwa malipo ya yale waliyo kuwa wakiyatenda?


More surahs in Swahili:


Al-Baqarah Al-'Imran An-Nisa'
Al-Ma'idah Yusuf Ibrahim
Al-Hijr Al-Kahf Maryam
Al-Hajj Al-Qasas Al-'Ankabut
As-Sajdah Ya Sin Ad-Dukhan
Al-Fath Al-Hujurat Qaf
An-Najm Ar-Rahman Al-Waqi'ah
Al-Hashr Al-Mulk Al-Haqqah
Al-Inshiqaq Al-A'la Al-Ghashiyah

Download surah Al-Mutaffifin with the voice of the most famous Quran reciters :

surah Al-Mutaffifin mp3 : choose the reciter to listen and download the chapter Al-Mutaffifin Complete with high quality
surah Al-Mutaffifin Ahmed El Agamy
Ahmed Al Ajmy
surah Al-Mutaffifin Bandar Balila
Bandar Balila
surah Al-Mutaffifin Khalid Al Jalil
Khalid Al Jalil
surah Al-Mutaffifin Saad Al Ghamdi
Saad Al Ghamdi
surah Al-Mutaffifin Saud Al Shuraim
Saud Al Shuraim
surah Al-Mutaffifin Abdul Basit Abdul Samad
Abdul Basit
surah Al-Mutaffifin Abdul Rashid Sufi
Abdul Rashid Sufi
surah Al-Mutaffifin Abdullah Basfar
Abdullah Basfar
surah Al-Mutaffifin Abdullah Awwad Al Juhani
Abdullah Al Juhani
surah Al-Mutaffifin Fares Abbad
Fares Abbad
surah Al-Mutaffifin Maher Al Muaiqly
Maher Al Muaiqly
surah Al-Mutaffifin Muhammad Siddiq Al Minshawi
Al Minshawi
surah Al-Mutaffifin Al Hosary
Al Hosary
surah Al-Mutaffifin Al-afasi
Mishari Al-afasi
surah Al-Mutaffifin Yasser Al Dosari
Yasser Al Dosari


Tuesday, May 7, 2024

لا تنسنا من دعوة صالحة بظهر الغيب