🔥 0 siku mfululizo
📖 Sura ndefu — imegawanywa sehemu ndogo (59 Aya)
📚 Sura Zote
30%
🎤 Gusa ikoni ya maikrofoni 🎙️ karibu na aya yoyote ili kujirekodi, kisha sikiliza na ulinganishe na qari.
0/59
44:1 🔁 0/5
حمٓ  ۝١
Haa Meeem
H'a Mim
🎤 Rekodi yako:
44:2 🔁 0/5
وَٱلۡكِتَٰبِ ٱلۡمُبِينِ  ۝٢
Wal Kitaabil Mubeen
Naapa kwa Kitabu kinacho bainisha,
🎤 Rekodi yako:
44:3 🔁 0/5
إِنَّآ أَنزَلۡنَٰهُ فِي لَيۡلَةٍ مُّبَٰرَكَةٍۚ إِنَّا كُنَّا مُنذِرِينَ  ۝٣
Innaaa anzalnaahu fee lailatim mubaarakah; innaa kunnaa munzireen
Hakika tumekiteremsha katika usiku ulio barikiwa. Hakika Sisi ni Waonyaji.
🎤 Rekodi yako:
44:4 🔁 0/5
فِيهَا يُفۡرَقُ كُلُّ أَمۡرٍ حَكِيمٍ  ۝٤
Feehaa yufraqu kullu amrin hakeem
Katika usiku huu hubainishwa kila jambo la hikima,
🎤 Rekodi yako:
44:5 🔁 0/5
أَمۡرًا مِّنۡ عِندِنَآۚ إِنَّا كُنَّا مُرۡسِلِينَ  ۝٥
Amram min `indinaaa; innaa kunnaa mursileen
Jambo litokalo kwetu. Hakika Sisi ndio wenye kutuma.
🎤 Rekodi yako:
44:6 🔁 0/5
رَحۡمَةً مِّن رَّبِّكَۚ إِنَّهُۥ هُوَ ٱلسَّمِيعُ ٱلۡعَلِيمُ  ۝٦
Rahmatam mir rabbik; innahoo Huwas Samee`ul `Aleem
Ni rehema itokayo kwa Mola wako Mlezi. Hakika Yeye ni Mwenye kusikia Mwenye kujua.
🎤 Rekodi yako:
44:7 🔁 0/5
رَبِّ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضِ وَمَا بَيۡنَهُمَآۖ إِن كُنتُم مُّوقِنِينَ  ۝٧
Rabbis samaawaati wal ardi wa maa bainahumaa; in kuntum mooqineen
Mola Mlezi wa mbingu na ardhi na vilio baina yao, ikiwa nyinyi mna yakini.
🎤 Rekodi yako:
44:8 🔁 0/5
لَآ إِلَٰهَ إِلَّا هُوَ يُحۡيِۦ وَيُمِيتُۖ رَبُّكُمۡ وَرَبُّ ءَابَآئِكُمُ ٱلۡأَوَّلِينَ  ۝٨
Laaa ilaaha illaa Huwa yuhyee wa yumeetu Rabbukum wa Rabbu aabaaa`ikumul awwaleen
Hakuna mungu ila Yeye; anahuisha na anafisha- Mola Mlezi wenu na Mola Mlezi wa baba zenu wa mwanzo.
🎤 Rekodi yako:
44:9 🔁 0/5
بَلۡ هُمۡ فِي شَكٍّ يَلۡعَبُونَ  ۝٩
Bal hum fee shakkiny yal`aboon
Lakini wao wanacheza katika shaka.
🎤 Rekodi yako:
44:10 🔁 0/5
فَٱرۡتَقِبۡ يَوۡمَ تَأۡتِي ٱلسَّمَآءُ بِدُخَانٍ مُّبِينٍ  ۝١٠
Fartaqib Yawma taatis samaaa`u bidukhaanim mubeen
Basi ingoje siku ambayo mbingu zitakapo leta moshi ulio dhaahiri,
🎤 Rekodi yako:
44:11 🔁 0/5
يَغۡشَى ٱلنَّاسَۖ هَٰذَا عَذَابٌ أَلِيمٌ  ۝١١
Yaghshan naasa haazaa `azaabun aleem
Utakao wafunika watu: Hii ni adhabu chungu!
🎤 Rekodi yako:
44:12 🔁 0/5
رَّبَّنَا ٱكۡشِفۡ عَنَّا ٱلۡعَذَابَ إِنَّا مُؤۡمِنُونَ  ۝١٢
Rabbanak shif `annal `azaaba innaa mu`minoon
Mola wetu Mlezi! Tuondolee adhabu hii. Hakika tutaamini.
🎤 Rekodi yako:
44:13 🔁 0/5
أَنَّىٰ لَهُمُ ٱلذِّكۡرَىٰ وَقَدۡ جَآءَهُمۡ رَسُولٌ مُّبِينٌ  ۝١٣
Annaa lahumuz zikraa wa qad jaaa`ahum Rasoolum mubeen
Nini faida ya kukumbuka kwao? Na alikwisha wafikia Mtume mwenye kubainisha.
🎤 Rekodi yako:
44:14 🔁 0/5
ثُمَّ تَوَلَّوۡاْ عَنۡهُ وَقَالُواْ مُعَلَّمٌ مَّجۡنُونٌ  ۝١٤
Summaa tawallaw `anhu wa qaaloo mu`allamum majnoon
Na wao wakamgeuzia uso, na wakasema: Huyu amefunzwa, naye ni mwendawazimu.
🎤 Rekodi yako:
44:15 🔁 0/5
إِنَّا كَاشِفُواْ ٱلۡعَذَابِ قَلِيلًاۚ إِنَّكُمۡ عَآئِدُونَ  ۝١٥
Innaa kaashiful `azaabi qaleelaa; innakum `aaa`indoon
Hakika sisi tutaiondoa adhabu kidogo, lakini nyinyi kwa yakini mtarejea vile vile!
🎤 Rekodi yako:
44:16 🔁 0/5
يَوۡمَ نَبۡطِشُ ٱلۡبَطۡشَةَ ٱلۡكُبۡرَىٰٓ إِنَّا مُنتَقِمُونَ  ۝١٦
Yawma nabtishul batsha tal kubraa innaa muntaqimoon
Siku tutayo yashambulia mashambulio makubwa, bila ya shaka Sisi ni wenye kutesa.
🎤 Rekodi yako:
44:17 🔁 0/5
۞ وَلَقَدۡ فَتَنَّا قَبۡلَهُمۡ قَوۡمَ فِرۡعَوۡنَ وَجَآءَهُمۡ رَسُولٌ كَرِيمٌ  ۝١٧
Wa laqad fatannaa qablahum qawma Fir`awna wa jaaa`ahum Rasoolun kareem
Na hakika kabla ya hawa tuliwafanyia mtihani watu wa Firauni, na aliwafikia Mtume Mtukufu.
🎤 Rekodi yako:
44:18 🔁 0/5
أَنۡ أَدُّوٓاْ إِلَيَّ عِبَادَ ٱللَّهِۖ إِنِّي لَكُمۡ رَسُولٌ أَمِينٌ  ۝١٨
An addooo ilaiya `ibaadal laahi innee lakum Rasoolun ameen
Akasema: Nipeni waja wa Mwenyezi Mungu; kwa hakika mimi kwenu ni Mtume Muaminifu.
🎤 Rekodi yako:
44:19 🔁 0/5
وَأَن لَّا تَعۡلُواْ عَلَى ٱللَّهِۖ إِنِّيٓ ءَاتِيكُم بِسُلۡطَٰنٍ مُّبِينٍ  ۝١٩
Wa al laa ta`loo `alal laahi innee aateekum bisultaanim mubeen
Na msimfanyie kiburi Mwenyezi Mungu; hakika mimi nitakuleteeni uthibitisho ulio wazi.
🎤 Rekodi yako:
44:20 🔁 0/5
وَإِنِّي عُذۡتُ بِرَبِّي وَرَبِّكُمۡ أَن تَرۡجُمُونِ  ۝٢٠
Wa innee `uztu bi Rabbee wa rabbikum an tarjumoon
Nami najikinga kwa Mola wangu Mlezi na ndiye Mola wenu Mlezi pia, ili msinipige mawe.
🎤 Rekodi yako:
44:21 🔁 0/5
وَإِن لَّمۡ تُؤۡمِنُواْ لِي فَٱعۡتَزِلُونِ  ۝٢١
Wa il lam tu`minoo lee fa`taziloon
Na ikiwa hamniamini, basi jitengeni nami.
🎤 Rekodi yako:
44:22 🔁 0/5
فَدَعَا رَبَّهُۥٓ أَنَّ هَٰٓؤُلَآءِ قَوۡمٌ مُّجۡرِمُونَ  ۝٢٢
Fada`aa rabbahooo anna haaa`ulaaa`i qawmum mujrimoon
Ndipo akamwomba Mola wake Mlezi: Hakika watu hawa ni wakosefu.
🎤 Rekodi yako:
44:23 🔁 0/5
فَأَسۡرِ بِعِبَادِي لَيۡلًا إِنَّكُم مُّتَّبَعُونَ  ۝٢٣
Fa asri bi`ibaadee lailan innakum muttaba`oon
Mwenyezi Mungu akasema: Basi nenda na waja wangu usiku. Kwa yakini mtafuatwa.
🎤 Rekodi yako:
44:24 🔁 0/5
وَٱتۡرُكِ ٱلۡبَحۡرَ رَهۡوًاۖ إِنَّهُمۡ جُندٌ مُّغۡرَقُونَ  ۝٢٤
Watrukil bahra rahwan innahum jundum mughraqoon
Na iache bahari vivyo hivyo imeachana, hakika wao hao ni jeshi litakalo zamishwa.
🎤 Rekodi yako:
44:25 🔁 0/5
كَمۡ تَرَكُواْ مِن جَنَّٰتٍ وَعُيُونٍ  ۝٢٥
Kam tarakoo min jannaatinw wa `uyoon
Mabustani mangapi, na chemchem ngapi waliziacha!
🎤 Rekodi yako:
44:26 🔁 0/5
وَزُرُوعٍ وَمَقَامٍ كَرِيمٍ  ۝٢٦
Wa zuroo`inw wa maqaa min kareem
Na mimea na vyeo vitukufu!
🎤 Rekodi yako:
44:27 🔁 0/5
وَنَعۡمَةٍ كَانُواْ فِيهَا فَٰكِهِينَ  ۝٢٧
Wa na`matin kaanoo feehaa faakiheen
Na neema walizo kuwa wakijistareheshea!
🎤 Rekodi yako:
44:28 🔁 0/5
كَذَٰلِكَۖ وَأَوۡرَثۡنَٰهَا قَوۡمًا ءَاخَرِينَ  ۝٢٨
Kazaalika wa awrasnaahaa qawman aakhareen
Ndio hivyo! Na tukawarithisha haya watu wenginewe.
🎤 Rekodi yako:
44:29 🔁 0/5
فَمَا بَكَتۡ عَلَيۡهِمُ ٱلسَّمَآءُ وَٱلۡأَرۡضُ وَمَا كَانُواْ مُنظَرِينَ  ۝٢٩
Famaa bakat `alaihimus samaaa`u wal ardu wa maa kaanoo munzareen
La mbingu wala ardhi hazikuwalilia, wala hawakupewa muhula.
🎤 Rekodi yako:
44:30 🔁 0/5
وَلَقَدۡ نَجَّيۡنَا بَنِيٓ إِسۡرَٰٓءِيلَ مِنَ ٱلۡعَذَابِ ٱلۡمُهِينِ  ۝٣٠
Wa laqad najjainaa Baneee Israaa`eela minal`azaabil muheen
Na bila ya shaka tuliwaokoa Wana wa Israili katika adhabu ya kuwadhalilisha,
🎤 Rekodi yako:
44:31 🔁 0/5
مِن فِرۡعَوۡنَۚ إِنَّهُۥ كَانَ عَالِيًا مِّنَ ٱلۡمُسۡرِفِينَ  ۝٣١
Min Fir`awn; innahoo kaana `aaliyam minal musrifeen
Ya Firauni. Hakika yeye alikuwa jeuri katika wenye kupindukia mipaka.
🎤 Rekodi yako:
44:32 🔁 0/5
وَلَقَدِ ٱخۡتَرۡنَٰهُمۡ عَلَىٰ عِلۡمٍ عَلَى ٱلۡعَٰلَمِينَ  ۝٣٢
Wa laqadikh tarnaahum `alaa `ilmin `alal `aalameen
Na tuliwakhiari kwa ujuzi wetu kuliko walimwengu wenginewe.
🎤 Rekodi yako:
44:33 🔁 0/5
وَءَاتَيۡنَٰهُم مِّنَ ٱلۡأٓيَٰتِ مَا فِيهِ بَلَٰٓؤٌاْ مُّبِينٌ  ۝٣٣
Wa aatainaahum minal aayaati maa feehi balaaa`um mubeen
Na tukawapa katika ishara zenye majaribio yaliyo wazi.
🎤 Rekodi yako:
44:34 🔁 0/5
إِنَّ هَٰٓؤُلَآءِ لَيَقُولُونَ  ۝٣٤
Inna haaa`ulaaa`i la yaqooloon
Hakika hawa wanasema:
🎤 Rekodi yako:
44:35 🔁 0/5
إِنۡ هِيَ إِلَّا مَوۡتَتُنَا ٱلۡأُولَىٰ وَمَا نَحۡنُ بِمُنشَرِينَ  ۝٣٥
In hiya illaa mawtatunal oolaa wa maa nahnu bimun shareen
Hapana ila kufa kwetu mara ya kwanza tu, wala sisi hatufufuliwi.
🎤 Rekodi yako:
44:36 🔁 0/5
فَأۡتُواْ بِـَٔابَآئِنَآ إِن كُنتُمۡ صَٰدِقِينَ  ۝٣٦
Faatoo bi aabaaa`inaaa inkuntum saadiqeen
Basi warudisheni baba zetu, ikiwa nyinyi mnasema kweli.
🎤 Rekodi yako:
44:37 🔁 0/5
أَهُمۡ خَيۡرٌ أَمۡ قَوۡمُ تُبَّعٍ وَٱلَّذِينَ مِن قَبۡلِهِمۡ أَهۡلَكۡنَٰهُمۡۚ إِنَّهُمۡ كَانُواْ مُجۡرِمِينَ  ۝٣٧
Ahum khayrun am qawmu Tubba`inw wallazeena min qablihim; ahlaknaahum innahum kaanoo mujrimeen
Je! Ni wao bora au watu wa Tubbaa' na walio kuwa kabla yao? Tuliwaangamiza. Hakika hao walikuwa wakosefu.
🎤 Rekodi yako:
44:38 🔁 0/5
وَمَا خَلَقۡنَا ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضَ وَمَا بَيۡنَهُمَا لَٰعِبِينَ  ۝٣٨
Wa maa khalaqnas samaawaati wal arda wa maa baina humaa laa`ibeen
Na hatukuziumba mbingu na ardhi na vilivyomo baina yake kwa mchezo.
🎤 Rekodi yako:
44:39 🔁 0/5
مَا خَلَقۡنَٰهُمَآ إِلَّا بِٱلۡحَقِّ وَلَٰكِنَّ أَكۡثَرَهُمۡ لَا يَعۡلَمُونَ  ۝٣٩
Maa khalaqnaahumaaa illaa bilhaqqi wa laakinna aksarahum laa ya`lamoon
Hatukuviumba hivyo ila kwa Haki, lakini wengi wao hawajui.
🎤 Rekodi yako:
44:40 🔁 0/5
إِنَّ يَوۡمَ ٱلۡفَصۡلِ مِيقَٰتُهُمۡ أَجۡمَعِينَ  ۝٤٠
Inna yawmal fasli meeqaatuhum ajma`een
Hakika siku ya Uamuzi ni wakati ulio wekwa kwa wao wote.
🎤 Rekodi yako:
44:41 🔁 0/5
يَوۡمَ لَا يُغۡنِي مَوۡلًى عَن مَّوۡلًى شَيۡـًٔا وَلَا هُمۡ يُنصَرُونَ  ۝٤١
Yawma laa yughnee mawlan `am mawlan shai`anw wa laa hum yunsaroon
Siku ambayo rafiki hatamfaa rafiki yake kwa chochote, wala hawatanusuriwa.
🎤 Rekodi yako:
44:42 🔁 0/5
إِلَّا مَن رَّحِمَ ٱللَّهُۚ إِنَّهُۥ هُوَ ٱلۡعَزِيزُ ٱلرَّحِيمُ  ۝٤٢
Illaa mar rahimal laah` innahoo huwal `azeezur raheem
Isipo kuwa atakaye mrehemu Mwenyezi Mungu. Hakika Yeye ndiye Mwenye nguvu, Mwenye kurehemu.
🎤 Rekodi yako:
44:43 🔁 0/5
إِنَّ شَجَرَتَ ٱلزَّقُّومِ  ۝٤٣
Inna shajarataz zaqqoom
Hakika Mti wa Zaqqum,
🎤 Rekodi yako:
44:44 🔁 0/5
طَعَامُ ٱلۡأَثِيمِ  ۝٤٤
Ta`aamul aseem
Ni chakula cha mwenye dhambi.
🎤 Rekodi yako:
44:45 🔁 0/5
كَٱلۡمُهۡلِ يَغۡلِي فِي ٱلۡبُطُونِ  ۝٤٥
Kalmuhli yaghlee filbutoon
Kama shaba iliyo yayushwa, hutokota matumboni
🎤 Rekodi yako:
44:46 🔁 0/5
كَغَلۡيِ ٱلۡحَمِيمِ  ۝٤٦
Kaghalyil hameem
Kama kutokota kwa maji ya moto.
🎤 Rekodi yako:
44:47 🔁 0/5
خُذُوهُ فَٱعۡتِلُوهُ إِلَىٰ سَوَآءِ ٱلۡجَحِيمِ  ۝٤٧
Khuzoohu fa`tiloohu ilaa sawaaa`il Jaheem
(Itasemwa:) Mkamateni na mtupeni katikati ya Jahannamu!
🎤 Rekodi yako:
44:48 🔁 0/5
ثُمَّ صُبُّواْ فَوۡقَ رَأۡسِهِۦ مِنۡ عَذَابِ ٱلۡحَمِيمِ  ۝٤٨
Summa subboo fawqa raasihee min `azaabil hameem
Kisha mmwagieni juu ya kichwa chake adhabu ya maji yanayo chemka.
🎤 Rekodi yako:
44:49 🔁 0/5
ذُقۡ إِنَّكَ أَنتَ ٱلۡعَزِيزُ ٱلۡكَرِيمُ  ۝٤٩
Zuq innaka antal `azeezul kareem
Onja! Ati wewe ndiye mwenye nguvu, mtukufu!
🎤 Rekodi yako:
44:50 🔁 0/5
إِنَّ هَٰذَا مَا كُنتُم بِهِۦ تَمۡتَرُونَ  ۝٥٠
Inna haazaa maa kuntum bihee tamtaroon
Hakika haya ndiyo mliyo kuwa mkiyatilia shaka.
🎤 Rekodi yako:
44:51 🔁 0/5
إِنَّ ٱلۡمُتَّقِينَ فِي مَقَامٍ أَمِينٍ  ۝٥١
Innal muttaqeena fee maqaamin ameen
Hakika wachamngu watakuwa katika mahali pa amani,
🎤 Rekodi yako:
44:52 🔁 0/5
فِي جَنَّٰتٍ وَعُيُونٍ  ۝٥٢
Fee jannaatinw wa `uyoon
Katika mabustani na chemchem,
🎤 Rekodi yako:
44:53 🔁 0/5
يَلۡبَسُونَ مِن سُندُسٍ وَإِسۡتَبۡرَقٍ مُّتَقَٰبِلِينَ  ۝٥٣
Yalbasoona min sundusinw wa istbraqim mutaqaabileen
Watavaa hariri nyepesi na hariri nzito wakikabiliana,
🎤 Rekodi yako:
44:54 🔁 0/5
كَذَٰلِكَ وَزَوَّجۡنَٰهُم بِحُورٍ عِينٍ  ۝٥٤
Kazaalika wa zawwajnaahum bihoorin `een
Hivi ndivyo itakavyo kuwa, na tutawaoza mahurilaini.
🎤 Rekodi yako:
44:55 🔁 0/5
يَدۡعُونَ فِيهَا بِكُلِّ فَٰكِهَةٍ ءَامِنِينَ  ۝٥٥
Yad`oona feehaa bikulli faakihatin aamineen
Humo watataka kila aina ya matunda, na wakae kwa amani.
🎤 Rekodi yako:
44:56 🔁 0/5
لَا يَذُوقُونَ فِيهَا ٱلۡمَوۡتَ إِلَّا ٱلۡمَوۡتَةَ ٱلۡأُولَىٰۖ وَوَقَىٰهُمۡ عَذَابَ ٱلۡجَحِيمِ  ۝٥٦
Laa yazooqoona feehal mawtaa illal mawtatal oolaa wa qaqaahum `azaabal jaheem
Humo hawataonja mauti ila mauti yale ya kwanza, na (Mwenyezi Mungu) atawalinda na adhabu ya Jahannamu,
🎤 Rekodi yako:
44:57 🔁 0/5
فَضۡلًا مِّن رَّبِّكَۚ ذَٰلِكَ هُوَ ٱلۡفَوۡزُ ٱلۡعَظِيمُ  ۝٥٧
Fadlam mir rabbik; zaalika huwal fawzul `azeem
Kuwa ni fadhila zitokazo kwa Mola wako Mlezi. Huko ndiko kufuzu kukubwa.
🎤 Rekodi yako:
44:58 🔁 0/5
فَإِنَّمَا يَسَّرۡنَٰهُ بِلِسَانِكَ لَعَلَّهُمۡ يَتَذَكَّرُونَ  ۝٥٨
Fa innamaa yassarnaahu bilisaanika la`allahum yatazakkaroon
Basi tumeifanya nyepesi hii Qur'ani kwa ulimi wako, ili wapate kukumbuka.
🎤 Rekodi yako:
44:59 🔁 0/5
فَٱرۡتَقِبۡ إِنَّهُم مُّرۡتَقِبُونَ  ۝٥٩
Fartaqib innahum murta qiboon
Ngoja tu, na wao wangoje pia.
🎤 Rekodi yako:
💡 Gusa neno lililofichwa ili lionekane kwa muda — maendeleo yako yanahifadhiwa kiotomatiki.

🎉
🎊 Hongera! Umemaliza Kuhifadhi
Mishary Rashid Alafasy
Mahmoud Khalil Al-Husary
Abdurrahman As-Sudais
Mohamed Siddiq Al-Minshawi
Abdul Basit Abdul Samad
Ali Al-Hudhaify
Ahmed ibn Ali al-Ajamy
Abu Bakr Ash-Shaatree
Muhammad Ayyoub
Abdullah Basfar
Abdullah Al-Juhani
Maher Al Muaiqly
0:00
0:00
-

Kurani Tukufu


Tuesday, August 18, 2026

Usitusahau katika dua zako njema