Sura Ad-Dukhan pdf — Pakua (Kiswahili)
Sura Ad-Dukhan pdf Kiswahili — Pakua Sura Ad-Dukhan Tafsiri. Sura Ad-Dukhan (Makka) 59 Aya.
Related
- Sura Ad-Dukhan TafsiriKiswahili
- Sura Ad-Dukhan mp3Sikiliza
- Quran Index Kiswahili114
More Sura PDF
Sura Ad-Dukhan

ﭑﭒ
44:1
H'a Mim
ﭓﭔﭕ
44:2
Naapa kwa Kitabu kinacho bainisha,
ﭖﭗﭘﭙﭚﭛﭜﭝﭞﭟ
44:3
Hakika tumekiteremsha katika usiku ulio barikiwa. Hakika Sisi ni Waonyaji.
ﭠﭡﭢﭣﭤﭥ
44:4
Katika usiku huu hubainishwa kila jambo la hikima,
ﭦﭧﭨﭩﭪﭫﭬﭭ
44:5
Jambo litokalo kwetu. Hakika Sisi ndio wenye kutuma.
ﭮﭯﭰﭱﭲﭳﭴﭵﭶ
44:6
Ni rehema itokayo kwa Mola wako Mlezi. Hakika Yeye ni Mwenye kusikia Mwenye kujua.
ﭷﭸﭹﭺﭻﭼﭽﭾﭿﮀ
44:7
Mola Mlezi wa mbingu na ardhi na vilio baina yao, ikiwa nyinyi mna yakini.
ﮁﮂﮃﮄﮅﮆﮇﮈﮉﮊﮋﮌ
44:8
Hakuna mungu ila Yeye; anahuisha na anafisha- Mola Mlezi wenu na Mola Mlezi wa baba zenu wa mwanzo.
ﮍﮎﮏﮐﮑﮒ
44:9
Lakini wao wanacheza katika shaka.
ﮓﮔﮕﮖﮗﮘﮙ
44:10
Basi ingoje siku ambayo mbingu zitakapo leta moshi ulio dhaahiri,
ﮚﮛﮜﮝﮞﮟﮠ
44:11
Utakao wafunika watu: Hii ni adhabu chungu!
ﮡﮢﮣﮤﮥﮦﮧ
44:12
Mola wetu Mlezi! Tuondolee adhabu hii. Hakika tutaamini.
ﮨﮩﮪﮫﮬﮭﮮﮯ
44:13
Nini faida ya kukumbuka kwao? Na alikwisha wafikia Mtume mwenye kubainisha.
ﮰﮱﯓﯔﯕﯖﯗ
44:14
Na wao wakamgeuzia uso, na wakasema: Huyu amefunzwa, naye ni mwendawazimu.
ﯘﯙﯚﯛﯜﯝﯞﯟ
44:15
Hakika sisi tutaiondoa adhabu kidogo, lakini nyinyi kwa yakini mtarejea vile vile!
ﯠﯡﯢﯣﯤﯥﯦ
44:16
Siku tutayo yashambulia mashambulio makubwa, bila ya shaka Sisi ni wenye kutesa.
ﯧﯨﯩﯪﯫﯬﯭﯮﯯﯰ
44:17
Na hakika kabla ya hawa tuliwafanyia mtihani watu wa Firauni, na aliwafikia Mtume Mtukufu.
ﯱﯲﯳﯴﯵﯶﯷﯸﯹﯺﯻ
44:18
Akasema: Nipeni waja wa Mwenyezi Mungu; kwa hakika mimi kwenu ni Mtume Muaminifu.
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖﭗﭘﭙﭚﭛ
44:19
Na msimfanyie kiburi Mwenyezi Mungu; hakika mimi nitakuleteeni uthibitisho ulio wazi.
ﭜﭝﭞﭟﭠﭡﭢ
44:20
Nami najikinga kwa Mola wangu Mlezi na ndiye Mola wenu Mlezi pia, ili msinipige mawe.
ﭣﭤﭥﭦﭧﭨ
44:21
Na ikiwa hamniamini, basi jitengeni nami.
ﭩﭪﭫﭬﭭﭮﭯ
44:22
Ndipo akamwomba Mola wake Mlezi: Hakika watu hawa ni wakosefu.
ﭰﭱﭲﭳﭴﭵ
44:23
Mwenyezi Mungu akasema: Basi nenda na waja wangu usiku. Kwa yakini mtafuatwa.
ﭶﭷﭸﭹﭺﭻﭼﭽ
44:24
Na iache bahari vivyo hivyo imeachana, hakika wao hao ni jeshi litakalo zamishwa.
ﭾﭿﮀﮁﮂﮃ
44:25
Mabustani mangapi, na chemchem ngapi waliziacha!
ﮄﮅﮆﮇ
44:26
Na mimea na vyeo vitukufu!
ﮈﮉﮊﮋﮌ
44:27
Na neema walizo kuwa wakijistareheshea!
ﮍﮎﮏﮐﮑﮒ
44:28
Ndio hivyo! Na tukawarithisha haya watu wenginewe.
ﮓﮔﮕﮖﮗﮘﮙﮚﮛ
44:29
La mbingu wala ardhi hazikuwalilia, wala hawakupewa muhula.
ﮜﮝﮞﮟﮠﮡﮢﮣ
44:30
Na bila ya shaka tuliwaokoa Wana wa Israili katika adhabu ya kuwadhalilisha,
ﮤﮥﮦﮧﮨﮩﮪﮫﮬ
44:31
Ya Firauni. Hakika yeye alikuwa jeuri katika wenye kupindukia mipaka.
ﮭﮮﮯﮰﮱﯓﯔ
44:32
Na tuliwakhiari kwa ujuzi wetu kuliko walimwengu wenginewe.
ﯕﯖﯗﯘﯙﯚﯛﯜ
44:33
Na tukawapa katika ishara zenye majaribio yaliyo wazi.
ﯝﯞﯟﯠ
44:34
Hakika hawa wanasema:
ﯡﯢﯣﯤﯥﯦﯧﯨﯩ
44:35
Hapana ila kufa kwetu mara ya kwanza tu, wala sisi hatufufuliwi.
ﯪﯫﯬﯭﯮﯯ
44:36
Basi warudisheni baba zetu, ikiwa nyinyi mnasema kweli.
ﯰﯱﯲﯳﯴﯵﯶﯷﯸﯹﯺﯻﯼﯽ
44:37
Je! Ni wao bora au watu wa Tubbaa' na walio kuwa kabla yao? Tuliwaangamiza. Hakika hao walikuwa wakosefu.
ﯾﯿﰀﰁﰂﰃﰄﰅ
44:38
Na hatukuziumba mbingu na ardhi na vilivyomo baina yake kwa mchezo.
ﰆﰇﰈﰉﰊﰋﰌﰍﰎ
44:39
Hatukuviumba hivyo ila kwa Haki, lakini wengi wao hawajui.
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖ
44:40
Hakika siku ya Uamuzi ni wakati ulio wekwa kwa wao wote.
ﭗﭘﭙﭚﭛﭜﭝﭞﭟﭠﭡ
44:41
Siku ambayo rafiki hatamfaa rafiki yake kwa chochote, wala hawatanusuriwa.
ﭢﭣﭤﭥﭦﭧﭨﭩﭪ
44:42
Isipo kuwa atakaye mrehemu Mwenyezi Mungu. Hakika Yeye ndiye Mwenye nguvu, Mwenye kurehemu.
ﭫﭬﭭﭮ
44:43
Hakika Mti wa Zaqqum,
ﭯﭰﭱ
44:44
Ni chakula cha mwenye dhambi.
ﭲﭳﭴﭵﭶ
44:45
Kama shaba iliyo yayushwa, hutokota matumboni
ﭷﭸﭹ
44:46
Kama kutokota kwa maji ya moto.
ﭺﭻﭼﭽﭾﭿ
44:47
(Itasemwa:) Mkamateni na mtupeni katikati ya Jahannamu!
ﮀﮁﮂﮃﮄﮅﮆﮇ
44:48
Kisha mmwagieni juu ya kichwa chake adhabu ya maji yanayo chemka.
ﮈﮉﮊﮋﮌﮍ
44:49
Onja! Ati wewe ndiye mwenye nguvu, mtukufu!
ﮎﮏﮐﮑﮒﮓﮔ
44:50
Hakika haya ndiyo mliyo kuwa mkiyatilia shaka.
ﮕﮖﮗﮘﮙﮚ
44:51
Hakika wachamngu watakuwa katika mahali pa amani,
ﮛﮜﮝﮞ
44:52
Katika mabustani na chemchem,
ﮟﮠﮡﮢﮣﮤ
44:53
Watavaa hariri nyepesi na hariri nzito wakikabiliana,
ﮥﮦﮧﮨﮩ
44:54
Hivi ndivyo itakavyo kuwa, na tutawaoza mahurilaini.
ﮪﮫﮬﮭﮮﮯ
44:55
Humo watataka kila aina ya matunda, na wakae kwa amani.
ﮰﮱﯓﯔﯕﯖﯗﯘﯙﯚﯛﯜ
44:56
Humo hawataonja mauti ila mauti yale ya kwanza, na (Mwenyezi Mungu) atawalinda na adhabu ya Jahannamu,
ﯝﯞﯟﯠﯡﯢﯣﯤﯥ
44:57
Kuwa ni fadhila zitokazo kwa Mola wako Mlezi. Huko ndiko kufuzu kukubwa.
ﯦﯧﯨﯩﯪﯫ
44:58
Basi tumeifanya nyepesi hii Qur'ani kwa ulimi wako, ili wapate kukumbuka.
ﯬﯭﯮﯯ
44:59
Ngoja tu, na wao wangoje pia.
Kurani Tukufu
Wednesday, September 9, 2026
Usitusahau katika dua zako njema







