PDF —
59 Aya Makka PDF
Built right in your browser — download starts automatically

Sura Ad-Dukhan pdf — Pakua (Kiswahili)

Sura Ad-Dukhan pdf Kiswahili — Pakua Sura Ad-Dukhan Tafsiri. Sura Ad-Dukhan (Makka) 59 Aya.



59 Aya · Makka · Kiswahili
bismillah
ﭑﭒ
44:1 H'a Mim
ﭓﭔﭕ
44:2 Naapa kwa Kitabu kinacho bainisha,
ﭖﭗﭘﭙﭚﭛﭜﭝﭞﭟ
44:3 Hakika tumekiteremsha katika usiku ulio barikiwa. Hakika Sisi ni Waonyaji.
ﭠﭡﭢﭣﭤﭥ
44:4 Katika usiku huu hubainishwa kila jambo la hikima,
ﭦﭧﭨﭩﭪﭫﭬﭭ
44:5 Jambo litokalo kwetu. Hakika Sisi ndio wenye kutuma.
ﭮﭯﭰﭱﭲﭳﭴﭵﭶ
44:6 Ni rehema itokayo kwa Mola wako Mlezi. Hakika Yeye ni Mwenye kusikia Mwenye kujua.
ﭷﭸﭹﭺﭻﭼﭽﭾﭿﮀ
44:7 Mola Mlezi wa mbingu na ardhi na vilio baina yao, ikiwa nyinyi mna yakini.
ﮁﮂﮃﮄﮅﮆﮇﮈﮉﮊﮋﮌ
44:8 Hakuna mungu ila Yeye; anahuisha na anafisha- Mola Mlezi wenu na Mola Mlezi wa baba zenu wa mwanzo.
ﮍﮎﮏﮐﮑﮒ
44:9 Lakini wao wanacheza katika shaka.
ﮓﮔﮕﮖﮗﮘﮙ
44:10 Basi ingoje siku ambayo mbingu zitakapo leta moshi ulio dhaahiri,
ﮚﮛﮜﮝﮞﮟﮠ
44:11 Utakao wafunika watu: Hii ni adhabu chungu!
ﮡﮢﮣﮤﮥﮦﮧ
44:12 Mola wetu Mlezi! Tuondolee adhabu hii. Hakika tutaamini.
ﮨﮩﮪﮫﮬﮭﮮﮯ
44:13 Nini faida ya kukumbuka kwao? Na alikwisha wafikia Mtume mwenye kubainisha.
ﮰﮱﯓﯔﯕﯖﯗ
44:14 Na wao wakamgeuzia uso, na wakasema: Huyu amefunzwa, naye ni mwendawazimu.
ﯘﯙﯚﯛﯜﯝﯞﯟ
44:15 Hakika sisi tutaiondoa adhabu kidogo, lakini nyinyi kwa yakini mtarejea vile vile!
ﯠﯡﯢﯣﯤﯥﯦ
44:16 Siku tutayo yashambulia mashambulio makubwa, bila ya shaka Sisi ni wenye kutesa.
ﯧﯨﯩﯪﯫﯬﯭﯮﯯﯰ
44:17 Na hakika kabla ya hawa tuliwafanyia mtihani watu wa Firauni, na aliwafikia Mtume Mtukufu.
ﯱﯲﯳﯴﯵﯶﯷﯸﯹﯺﯻ
44:18 Akasema: Nipeni waja wa Mwenyezi Mungu; kwa hakika mimi kwenu ni Mtume Muaminifu.
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖﭗﭘﭙﭚﭛ
44:19 Na msimfanyie kiburi Mwenyezi Mungu; hakika mimi nitakuleteeni uthibitisho ulio wazi.
ﭜﭝﭞﭟﭠﭡﭢ
44:20 Nami najikinga kwa Mola wangu Mlezi na ndiye Mola wenu Mlezi pia, ili msinipige mawe.
ﭣﭤﭥﭦﭧﭨ
44:21 Na ikiwa hamniamini, basi jitengeni nami.
ﭩﭪﭫﭬﭭﭮﭯ
44:22 Ndipo akamwomba Mola wake Mlezi: Hakika watu hawa ni wakosefu.
ﭰﭱﭲﭳﭴﭵ
44:23 Mwenyezi Mungu akasema: Basi nenda na waja wangu usiku. Kwa yakini mtafuatwa.
ﭶﭷﭸﭹﭺﭻﭼﭽ
44:24 Na iache bahari vivyo hivyo imeachana, hakika wao hao ni jeshi litakalo zamishwa.
ﭾﭿﮀﮁﮂﮃ
44:25 Mabustani mangapi, na chemchem ngapi waliziacha!
ﮄﮅﮆﮇ
44:26 Na mimea na vyeo vitukufu!
ﮈﮉﮊﮋﮌ
44:27 Na neema walizo kuwa wakijistareheshea!
ﮍﮎﮏﮐﮑﮒ
44:28 Ndio hivyo! Na tukawarithisha haya watu wenginewe.
ﮓﮔﮕﮖﮗﮘﮙﮚﮛ
44:29 La mbingu wala ardhi hazikuwalilia, wala hawakupewa muhula.
ﮜﮝﮞﮟﮠﮡﮢﮣ
44:30 Na bila ya shaka tuliwaokoa Wana wa Israili katika adhabu ya kuwadhalilisha,
ﮤﮥﮦﮧﮨﮩﮪﮫﮬ
44:31 Ya Firauni. Hakika yeye alikuwa jeuri katika wenye kupindukia mipaka.
ﮭﮮﮯﮰﮱﯓﯔ
44:32 Na tuliwakhiari kwa ujuzi wetu kuliko walimwengu wenginewe.
ﯕﯖﯗﯘﯙﯚﯛﯜ
44:33 Na tukawapa katika ishara zenye majaribio yaliyo wazi.
ﯝﯞﯟﯠ
44:34 Hakika hawa wanasema:
ﯡﯢﯣﯤﯥﯦﯧﯨﯩ
44:35 Hapana ila kufa kwetu mara ya kwanza tu, wala sisi hatufufuliwi.
ﯪﯫﯬﯭﯮﯯ
44:36 Basi warudisheni baba zetu, ikiwa nyinyi mnasema kweli.
ﯰﯱﯲﯳﯴﯵﯶﯷﯸﯹﯺﯻﯼﯽ
44:37 Je! Ni wao bora au watu wa Tubbaa' na walio kuwa kabla yao? Tuliwaangamiza. Hakika hao walikuwa wakosefu.
ﯾﯿﰀﰁﰂﰃﰄﰅ
44:38 Na hatukuziumba mbingu na ardhi na vilivyomo baina yake kwa mchezo.
ﰆﰇﰈﰉﰊﰋﰌﰍﰎ
44:39 Hatukuviumba hivyo ila kwa Haki, lakini wengi wao hawajui.
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖ
44:40 Hakika siku ya Uamuzi ni wakati ulio wekwa kwa wao wote.
ﭗﭘﭙﭚﭛﭜﭝﭞﭟﭠﭡ
44:41 Siku ambayo rafiki hatamfaa rafiki yake kwa chochote, wala hawatanusuriwa.
ﭢﭣﭤﭥﭦﭧﭨﭩﭪ
44:42 Isipo kuwa atakaye mrehemu Mwenyezi Mungu. Hakika Yeye ndiye Mwenye nguvu, Mwenye kurehemu.
ﭫﭬﭭﭮ
44:43 Hakika Mti wa Zaqqum,
ﭯﭰﭱ
44:44 Ni chakula cha mwenye dhambi.
ﭲﭳﭴﭵﭶ
44:45 Kama shaba iliyo yayushwa, hutokota matumboni
ﭷﭸﭹ
44:46 Kama kutokota kwa maji ya moto.
ﭺﭻﭼﭽﭾﭿ
44:47 (Itasemwa:) Mkamateni na mtupeni katikati ya Jahannamu!
ﮀﮁﮂﮃﮄﮅﮆﮇ
44:48 Kisha mmwagieni juu ya kichwa chake adhabu ya maji yanayo chemka.
ﮈﮉﮊﮋﮌﮍ
44:49 Onja! Ati wewe ndiye mwenye nguvu, mtukufu!
ﮎﮏﮐﮑﮒﮓﮔ
44:50 Hakika haya ndiyo mliyo kuwa mkiyatilia shaka.
ﮕﮖﮗﮘﮙﮚ
44:51 Hakika wachamngu watakuwa katika mahali pa amani,
ﮛﮜﮝﮞ
44:52 Katika mabustani na chemchem,
ﮟﮠﮡﮢﮣﮤ
44:53 Watavaa hariri nyepesi na hariri nzito wakikabiliana,
ﮥﮦﮧﮨﮩ
44:54 Hivi ndivyo itakavyo kuwa, na tutawaoza mahurilaini.
ﮪﮫﮬﮭﮮﮯ
44:55 Humo watataka kila aina ya matunda, na wakae kwa amani.
ﮰﮱﯓﯔﯕﯖﯗﯘﯙﯚﯛﯜ
44:56 Humo hawataonja mauti ila mauti yale ya kwanza, na (Mwenyezi Mungu) atawalinda na adhabu ya Jahannamu,
ﯝﯞﯟﯠﯡﯢﯣﯤﯥ
44:57 Kuwa ni fadhila zitokazo kwa Mola wako Mlezi. Huko ndiko kufuzu kukubwa.
ﯦﯧﯨﯩﯪﯫ
44:58 Basi tumeifanya nyepesi hii Qur'ani kwa ulimi wako, ili wapate kukumbuka.
ﯬﯭﯮﯯ
44:59 Ngoja tu, na wao wangoje pia.

Kurani Tukufu


Wednesday, September 9, 2026

Usitusahau katika dua zako njema