PDF —
59 Aya Makka PDF
Built right in your browser — download starts automatically

Sura Ad-Dukhan pdf — Pakua (Kiswahili)

Sura Ad-Dukhan pdf Kiswahili — Pakua Sura Ad-Dukhan Tafsiri. Ad-Dukhan (Makka) 59 Aya.



59 Aya · Makka · Kiswahili
bismillah
ﭑﭒ
H'a Mim
ﭓﭔﭕ
Naapa kwa Kitabu kinacho bainisha,
ﭖﭗﭘﭙﭚﭛﭜﭝﭞﭟ
Hakika tumekiteremsha katika usiku ulio barikiwa. Hakika Sisi ni Waonyaji.
ﭠﭡﭢﭣﭤﭥ
Katika usiku huu hubainishwa kila jambo la hikima,
ﭦﭧﭨﭩﭪﭫﭬﭭ
Jambo litokalo kwetu. Hakika Sisi ndio wenye kutuma.
ﭮﭯﭰﭱﭲﭳﭴﭵﭶ
Ni rehema itokayo kwa Mola wako Mlezi. Hakika Yeye ni Mwenye kusikia Mwenye kujua.
ﭷﭸﭹﭺﭻﭼﭽﭾﭿﮀ
Mola Mlezi wa mbingu na ardhi na vilio baina yao, ikiwa nyinyi mna yakini.
ﮁﮂﮃﮄﮅﮆﮇﮈﮉﮊﮋﮌ
Hakuna mungu ila Yeye; anahuisha na anafisha- Mola Mlezi wenu na Mola Mlezi wa baba zenu wa mwanzo.
ﮍﮎﮏﮐﮑﮒ
Lakini wao wanacheza katika shaka.
ﮓﮔﮕﮖﮗﮘﮙ
Basi ingoje siku ambayo mbingu zitakapo leta moshi ulio dhaahiri,
ﮚﮛﮜﮝﮞﮟﮠ
Utakao wafunika watu: Hii ni adhabu chungu!
ﮡﮢﮣﮤﮥﮦﮧ
Mola wetu Mlezi! Tuondolee adhabu hii. Hakika tutaamini.
ﮨﮩﮪﮫﮬﮭﮮﮯ
Nini faida ya kukumbuka kwao? Na alikwisha wafikia Mtume mwenye kubainisha.
ﮰﮱﯓﯔﯕﯖﯗ
Na wao wakamgeuzia uso, na wakasema: Huyu amefunzwa, naye ni mwendawazimu.
ﯘﯙﯚﯛﯜﯝﯞﯟ
Hakika sisi tutaiondoa adhabu kidogo, lakini nyinyi kwa yakini mtarejea vile vile!
ﯠﯡﯢﯣﯤﯥﯦ
Siku tutayo yashambulia mashambulio makubwa, bila ya shaka Sisi ni wenye kutesa.
ﯧﯨﯩﯪﯫﯬﯭﯮﯯﯰ
Na hakika kabla ya hawa tuliwafanyia mtihani watu wa Firauni, na aliwafikia Mtume Mtukufu.
ﯱﯲﯳﯴﯵﯶﯷﯸﯹﯺﯻ
Akasema: Nipeni waja wa Mwenyezi Mungu; kwa hakika mimi kwenu ni Mtume Muaminifu.
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖﭗﭘﭙﭚﭛ
Na msimfanyie kiburi Mwenyezi Mungu; hakika mimi nitakuleteeni uthibitisho ulio wazi.
ﭜﭝﭞﭟﭠﭡﭢ
Nami najikinga kwa Mola wangu Mlezi na ndiye Mola wenu Mlezi pia, ili msinipige mawe.
ﭣﭤﭥﭦﭧﭨ
Na ikiwa hamniamini, basi jitengeni nami.
ﭩﭪﭫﭬﭭﭮﭯ
Ndipo akamwomba Mola wake Mlezi: Hakika watu hawa ni wakosefu.
ﭰﭱﭲﭳﭴﭵ
Mwenyezi Mungu akasema: Basi nenda na waja wangu usiku. Kwa yakini mtafuatwa.
ﭶﭷﭸﭹﭺﭻﭼﭽ
Na iache bahari vivyo hivyo imeachana, hakika wao hao ni jeshi litakalo zamishwa.
ﭾﭿﮀﮁﮂﮃ
Mabustani mangapi, na chemchem ngapi waliziacha!
ﮄﮅﮆﮇ
Na mimea na vyeo vitukufu!
ﮈﮉﮊﮋﮌ
Na neema walizo kuwa wakijistareheshea!
ﮍﮎﮏﮐﮑﮒ
Ndio hivyo! Na tukawarithisha haya watu wenginewe.
ﮓﮔﮕﮖﮗﮘﮙﮚﮛ
La mbingu wala ardhi hazikuwalilia, wala hawakupewa muhula.
ﮜﮝﮞﮟﮠﮡﮢﮣ
Na bila ya shaka tuliwaokoa Wana wa Israili katika adhabu ya kuwadhalilisha,
ﮤﮥﮦﮧﮨﮩﮪﮫﮬ
Ya Firauni. Hakika yeye alikuwa jeuri katika wenye kupindukia mipaka.
ﮭﮮﮯﮰﮱﯓﯔ
Na tuliwakhiari kwa ujuzi wetu kuliko walimwengu wenginewe.
ﯕﯖﯗﯘﯙﯚﯛﯜ
Na tukawapa katika ishara zenye majaribio yaliyo wazi.
ﯝﯞﯟﯠ
Hakika hawa wanasema:
ﯡﯢﯣﯤﯥﯦﯧﯨﯩ
Hapana ila kufa kwetu mara ya kwanza tu, wala sisi hatufufuliwi.
ﯪﯫﯬﯭﯮﯯ
Basi warudisheni baba zetu, ikiwa nyinyi mnasema kweli.
ﯰﯱﯲﯳﯴﯵﯶﯷﯸﯹﯺﯻﯼﯽ
Je! Ni wao bora au watu wa Tubbaa' na walio kuwa kabla yao? Tuliwaangamiza. Hakika hao walikuwa wakosefu.
ﯾﯿﰀﰁﰂﰃﰄﰅ
Na hatukuziumba mbingu na ardhi na vilivyomo baina yake kwa mchezo.
ﰆﰇﰈﰉﰊﰋﰌﰍﰎ
Hatukuviumba hivyo ila kwa Haki, lakini wengi wao hawajui.
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖ
Hakika siku ya Uamuzi ni wakati ulio wekwa kwa wao wote.
ﭗﭘﭙﭚﭛﭜﭝﭞﭟﭠﭡ
Siku ambayo rafiki hatamfaa rafiki yake kwa chochote, wala hawatanusuriwa.
ﭢﭣﭤﭥﭦﭧﭨﭩﭪ
Isipo kuwa atakaye mrehemu Mwenyezi Mungu. Hakika Yeye ndiye Mwenye nguvu, Mwenye kurehemu.
ﭫﭬﭭﭮ
Hakika Mti wa Zaqqum,
ﭯﭰﭱ
Ni chakula cha mwenye dhambi.
ﭲﭳﭴﭵﭶ
Kama shaba iliyo yayushwa, hutokota matumboni
ﭷﭸﭹ
Kama kutokota kwa maji ya moto.
ﭺﭻﭼﭽﭾﭿ
(Itasemwa:) Mkamateni na mtupeni katikati ya Jahannamu!
ﮀﮁﮂﮃﮄﮅﮆﮇ
Kisha mmwagieni juu ya kichwa chake adhabu ya maji yanayo chemka.
ﮈﮉﮊﮋﮌﮍ
Onja! Ati wewe ndiye mwenye nguvu, mtukufu!
ﮎﮏﮐﮑﮒﮓﮔ
Hakika haya ndiyo mliyo kuwa mkiyatilia shaka.
ﮕﮖﮗﮘﮙﮚ
Hakika wachamngu watakuwa katika mahali pa amani,
ﮛﮜﮝﮞ
Katika mabustani na chemchem,
ﮟﮠﮡﮢﮣﮤ
Watavaa hariri nyepesi na hariri nzito wakikabiliana,
ﮥﮦﮧﮨﮩ
Hivi ndivyo itakavyo kuwa, na tutawaoza mahurilaini.
ﮪﮫﮬﮭﮮﮯ
Humo watataka kila aina ya matunda, na wakae kwa amani.
ﮰﮱﯓﯔﯕﯖﯗﯘﯙﯚﯛﯜ
Humo hawataonja mauti ila mauti yale ya kwanza, na (Mwenyezi Mungu) atawalinda na adhabu ya Jahannamu,
ﯝﯞﯟﯠﯡﯢﯣﯤﯥ
Kuwa ni fadhila zitokazo kwa Mola wako Mlezi. Huko ndiko kufuzu kukubwa.
ﯦﯧﯨﯩﯪﯫ
Basi tumeifanya nyepesi hii Qur'ani kwa ulimi wako, ili wapate kukumbuka.
ﯬﯭﯮﯯ
Ngoja tu, na wao wangoje pia.

Kurani Tukufu


Tuesday, August 18, 2026

Usitusahau katika dua zako njema