Surah Al Imran aya 140 , Swahili translation of the meaning Ayah.
﴿إِن يَمْسَسْكُمْ قَرْحٌ فَقَدْ مَسَّ الْقَوْمَ قَرْحٌ مِّثْلُهُ ۚ وَتِلْكَ الْأَيَّامُ نُدَاوِلُهَا بَيْنَ النَّاسِ وَلِيَعْلَمَ اللَّهُ الَّذِينَ آمَنُوا وَيَتَّخِذَ مِنكُمْ شُهَدَاءَ ۗ وَاللَّهُ لَا يُحِبُّ الظَّالِمِينَ﴾
[ آل عمران: 140]
Kama yamekupateni majaraha, basi na hao watu wengine yamewapata majaraha mfano wa haya. Na siku za namna hii tunaweletea watu kwa zamu, ili Mwenyezi Mungu awapambanue walio amini na awateuwe miongoni mwenu mashahidi. Na Mwenyezi Mungu hawapendi madhaalimu;
Surah Al Imran in SwahiliSwahili Translation - Al-Barwani
English - Sahih International
If a wound should touch you - there has already touched the [opposing] people a wound similar to it. And these days [of varying conditions] We alternate among the people so that Allah may make evident those who believe and [may] take to Himself from among you martyrs - and Allah does not like the wrongdoers -
Tafsiri ya maana yake kwenye lugha ya Kiswahili
Kama yamekupateni majaraha, basi na hao watu wengine yamewapata majaraha mfano wa haya. Na siku za namna hii tunaweletea watu kwa zamu, ili Mwenyezi Mungu awapambanue walio amini na awateuwe miongoni mwenu mashahidi. Na Mwenyezi Mungu hawapendi madhaalimu;
Ingawa katika vita vya Uhud wameuwawa au kujuruhiwa vibaya baadhi yenu na kwa hayo mkaathirika nafsi zenu, lakini msilegee na kuhuzunika. Kwani hao makhasimu zenu yaliwapata kama hayo katika vita vya Badri. Nyakati za ushindi huendeshwa na Mwenyezi Mungu kwa watu kama apendavyo, pengine hawa hushinda, na pengine hawa, ili awatie mtihani na kuwajaribu Waumini, awateuwe wenye kusimama imara juu ya Imani yao, na apate kuwatukuza baadhi yao kwa kuwafisha mashahidi katika Sabili Llahi. Na Mwenyezi Mungu hawapendi washirikina wenye kudhulumu na wangashinda kwa kusaidiwa na wengineo.
English | Türkçe | Indonesia |
Русский | Français | فارسی |
تفسير | Bengali | Urdu |
Ayats from Quran in Swahili
- Kisha nyinyi kwa nyinyi mnauwana, na mnawatoa baadhi yenu majumbani kwao, mkisaidiana kwa dhambi na
- Na atakaye ubadilisha wasia baada ya kuusikia, basi dhambi yake ni juu ya wale watakao
- Wanao shika Sala, na wanatoa Zaka, nao wana yakini na Akhera.
- Kwani hawakuona ya kwamba Mwenyezi Mungu aliye umba mbingu na ardhi ni Mwenye kuweza kuumba
- Na pale tulipomweka Ibrahim pahala penye ile Nyumba tukamwambia: Usinishirikishe na chochote; na isafishe Nyumba
- Mali yangu hayakunifaa kitu.
- Akasema (Iblisi): Naapa kwa utukufu wako, bila ya shaka nitawapoteza wote,
- Bali Saa ya Kiyama ndio miadi yao, na Saa hiyo ni nzito zaidi na chungu
- Basi tukamrudisha kwa mama yake ili macho yake yaburudike, wala asihuzunike. Na ajue ya kwamba
- Wakasema: Ukorofi wenu mnao wenyewe! Je! Ni kwa kuwa mnakumbushwa? Ama nyinyi ni watu walio
Quran Surah in Swahili :
Download Surah Al Imran with the voice of the most famous Quran reciters :
Surah Al Imran mp3 : choose the reciter to listen and download the chapter Al Imran Complete with high quality
Ahmed Al Ajmy
Bandar Balila
Khalid Al Jalil
Saad Al Ghamdi
Saud Al Shuraim
Abdul Basit
Abdul Rashid Sufi
Abdullah Basfar
Abdullah Al Juhani
Fares Abbad
Maher Al Muaiqly
Al Minshawi
Al Hosary
Mishari Al-afasi
Yasser Al Dosari
Please remember us in your sincere prayers