Surah Al-Waqiah with Swahili

  1. Surah mp3
  2. More
  3. Swahili
The Holy Quran | Quran translation | Language Swahili | Surah Waqiah | الواقعة - Ayat Count 96 - The number of the surah in moshaf: 56 - The meaning of the surah in English: The Inevitable, The Event.

إِذَا وَقَعَتِ الْوَاقِعَةُ(1)

 Litakapo tukia hilo Tukio

لَيْسَ لِوَقْعَتِهَا كَاذِبَةٌ(2)

 Hapana cha kukanusha kutukia kwake.

خَافِضَةٌ رَّافِعَةٌ(3)

 Literemshalo linyanyualo,

إِذَا رُجَّتِ الْأَرْضُ رَجًّا(4)

 Itakapo tikiswa ardhi kwa mtikiso,

وَبُسَّتِ الْجِبَالُ بَسًّا(5)

 Na milima itapo sagwasagwa,

فَكَانَتْ هَبَاءً مُّنبَثًّا(6)

 Iwe mavumbi yanayo peperushwa,

وَكُنتُمْ أَزْوَاجًا ثَلَاثَةً(7)

 Na nyinyi mtakuwa namna tatu:-

فَأَصْحَابُ الْمَيْمَنَةِ مَا أَصْحَابُ الْمَيْمَنَةِ(8)

 Basi watakuwepo wa kuliani; je, ni wepi wa kuliani?

وَأَصْحَابُ الْمَشْأَمَةِ مَا أَصْحَابُ الْمَشْأَمَةِ(9)

 Na wa kushotoni; je, ni wepi wa kushotoni?

وَالسَّابِقُونَ السَّابِقُونَ(10)

 Na wa mbele watakuwa mbele.

أُولَٰئِكَ الْمُقَرَّبُونَ(11)

 Hao ndio watakao karibishwa

فِي جَنَّاتِ النَّعِيمِ(12)

 Katika Bustani zenye neema.

ثُلَّةٌ مِّنَ الْأَوَّلِينَ(13)

 Fungu kubwa katika wa mwanzo,

وَقَلِيلٌ مِّنَ الْآخِرِينَ(14)

 Na wachache katika wa mwisho.

عَلَىٰ سُرُرٍ مَّوْضُونَةٍ(15)

 Watakuwa juu ya viti vya fakhari vilivyo tonewa.

مُّتَّكِئِينَ عَلَيْهَا مُتَقَابِلِينَ(16)

 Wakiviegemea wakielekeana.

يَطُوفُ عَلَيْهِمْ وِلْدَانٌ مُّخَلَّدُونَ(17)

 Wakitumikiwa na wavulana wa ujana wa milele,

بِأَكْوَابٍ وَأَبَارِيقَ وَكَأْسٍ مِّن مَّعِينٍ(18)

 Kwa vikombe na mabirika na bilauri za vinywaji kutoka chemchem safi.

لَّا يُصَدَّعُونَ عَنْهَا وَلَا يُنزِفُونَ(19)

 Hawataumwa kichwa kwa vinywaji hivyo wala hawatoleweshwa.

وَفَاكِهَةٍ مِّمَّا يَتَخَيَّرُونَ(20)

 Na matunda wayapendayo,

وَلَحْمِ طَيْرٍ مِّمَّا يَشْتَهُونَ(21)

 Na nyama za ndege kama wanavyo tamani.

وَحُورٌ عِينٌ(22)

 Na Mahurulaini,

كَأَمْثَالِ اللُّؤْلُؤِ الْمَكْنُونِ(23)

 Walio kama mfano wa lulu zilio hifadhiwa.

جَزَاءً بِمَا كَانُوا يَعْمَلُونَ(24)

 Ni malipo kwa waliyo kuwa wakiyatenda.

لَا يَسْمَعُونَ فِيهَا لَغْوًا وَلَا تَأْثِيمًا(25)

 Humo hawatasikia porojo wala maneno ya dhambi,

إِلَّا قِيلًا سَلَامًا سَلَامًا(26)

 Isipo kuwa maneno ya Salama, Salama.

وَأَصْحَابُ الْيَمِينِ مَا أَصْحَابُ الْيَمِينِ(27)

 Na wale wa mkono wa kulia, ni yepi yatakuwa ya wa kuliani?

فِي سِدْرٍ مَّخْضُودٍ(28)

 Katika mikunazi isiyo na miba,

وَطَلْحٍ مَّنضُودٍ(29)

 Na migomba iliyo pangiliwa,

وَظِلٍّ مَّمْدُودٍ(30)

 Na kivuli kilicho tanda,

وَمَاءٍ مَّسْكُوبٍ(31)

 Na maji yanayo miminika,

وَفَاكِهَةٍ كَثِيرَةٍ(32)

 Na matunda mengi,

لَّا مَقْطُوعَةٍ وَلَا مَمْنُوعَةٍ(33)

 Hayatindikii wala hayakatazwi,

وَفُرُشٍ مَّرْفُوعَةٍ(34)

 Na matandiko yaliyo nyanyuliwa.

إِنَّا أَنشَأْنَاهُنَّ إِنشَاءً(35)

 Hakika Sisi tutawaumba (Mahurulaini) upya,

فَجَعَلْنَاهُنَّ أَبْكَارًا(36)

 Na tutawafanya vijana,

عُرُبًا أَتْرَابًا(37)

 Wanapendana na waume zao, hirimu moja.

لِّأَصْحَابِ الْيَمِينِ(38)

 Kwa ajili ya watu wa kuliani.

ثُلَّةٌ مِّنَ الْأَوَّلِينَ(39)

 Fungu kubwa katika wa mwanzo,

وَثُلَّةٌ مِّنَ الْآخِرِينَ(40)

 Na fungu kubwa katika wa mwisho.

وَأَصْحَابُ الشِّمَالِ مَا أَصْحَابُ الشِّمَالِ(41)

 Na watu wa kushotoni; je ni yepi ya wa kushotoni?

فِي سَمُومٍ وَحَمِيمٍ(42)

 Katika upepo wa moto, na maji yanayo chemka,

وَظِلٍّ مِّن يَحْمُومٍ(43)

 Na kivuli cha moshi mweusi,

لَّا بَارِدٍ وَلَا كَرِيمٍ(44)

 Si cha kuburudisha wala kustarehesha.

إِنَّهُمْ كَانُوا قَبْلَ ذَٰلِكَ مُتْرَفِينَ(45)

 Hakika hao walikuwa kabla ya haya wakiishi maisha ya anasa.

وَكَانُوا يُصِرُّونَ عَلَى الْحِنثِ الْعَظِيمِ(46)

 Na walikuwa wakishikilia kufanya madhambi makubwa,

وَكَانُوا يَقُولُونَ أَئِذَا مِتْنَا وَكُنَّا تُرَابًا وَعِظَامًا أَإِنَّا لَمَبْعُوثُونَ(47)

 Na walikuwa wakisema: Tutakapo kufa na tukawa udongo na mafupa, ati ndio tutafufuliwa?

أَوَآبَاؤُنَا الْأَوَّلُونَ(48)

 Au baba zetu wa zamani?

قُلْ إِنَّ الْأَوَّلِينَ وَالْآخِرِينَ(49)

 Sema: Hakika wa zamani na wa mwisho

لَمَجْمُوعُونَ إِلَىٰ مِيقَاتِ يَوْمٍ مَّعْلُومٍ(50)

 Bila ya shaka watakusanywa kwa wakati wa siku maalumu.

ثُمَّ إِنَّكُمْ أَيُّهَا الضَّالُّونَ الْمُكَذِّبُونَ(51)

 Kisha nyinyi, mlio potea, mnao kanusha,

لَآكِلُونَ مِن شَجَرٍ مِّن زَقُّومٍ(52)

 Kwa yakini mtakula mti wa Zaqqumu.

فَمَالِئُونَ مِنْهَا الْبُطُونَ(53)

 Na kwa mti huo mtajaza matumbo.

فَشَارِبُونَ عَلَيْهِ مِنَ الْحَمِيمِ(54)

 Na juu yake mtakunywa maji yanayo chemka.

فَشَارِبُونَ شُرْبَ الْهِيمِ(55)

 Tena mtakunywa kama wanavyo kunywa ngamia wenye kiu.

هَٰذَا نُزُلُهُمْ يَوْمَ الدِّينِ(56)

 Hiyo ndiyo karamu yao Siku ya Malipo.

نَحْنُ خَلَقْنَاكُمْ فَلَوْلَا تُصَدِّقُونَ(57)

 Sisi tumekuumbeni; basi hamsadiki?

أَفَرَأَيْتُم مَّا تُمْنُونَ(58)

 Je! Mnaiona mbegu ya uzazi mnayo idondokeza?

أَأَنتُمْ تَخْلُقُونَهُ أَمْ نَحْنُ الْخَالِقُونَ(59)

 Je! Mnaiumba nyinyi, au ni Sisi ndio Waumbaji?

نَحْنُ قَدَّرْنَا بَيْنَكُمُ الْمَوْتَ وَمَا نَحْنُ بِمَسْبُوقِينَ(60)

 Sisi tumekuwekeeni mauti; na wala Sisi hatushindwi

عَلَىٰ أَن نُّبَدِّلَ أَمْثَالَكُمْ وَنُنشِئَكُمْ فِي مَا لَا تَعْلَمُونَ(61)

 Kuwaleta wengine badala yenu na kukuumbeni nyinyi kwa umbo msilo lijua.

وَلَقَدْ عَلِمْتُمُ النَّشْأَةَ الْأُولَىٰ فَلَوْلَا تَذَكَّرُونَ(62)

 Na bila ya shaka mlikwisha jua umbo la kwanza, basi kwa nini hamkumbuki?

أَفَرَأَيْتُم مَّا تَحْرُثُونَ(63)

 Je! Mnaona makulima mnayo yapanda?

أَأَنتُمْ تَزْرَعُونَهُ أَمْ نَحْنُ الزَّارِعُونَ(64)

 Je! Ni nyinyi mnayo yaotesha au ni Sisi ndio wenye kuotesha?

لَوْ نَشَاءُ لَجَعَلْنَاهُ حُطَامًا فَظَلْتُمْ تَفَكَّهُونَ(65)

 Tungeli taka tungeli yafanya yakawa mapepe, mkabaki mnastaajabu,

إِنَّا لَمُغْرَمُونَ(66)

 Mkisema: Hakika sisi tumegharimika;

بَلْ نَحْنُ مَحْرُومُونَ(67)

 Bali sisi tumenyimwa.

أَفَرَأَيْتُمُ الْمَاءَ الَّذِي تَشْرَبُونَ(68)

 Je! Mnayaona maji mnayo yanywa?

أَأَنتُمْ أَنزَلْتُمُوهُ مِنَ الْمُزْنِ أَمْ نَحْنُ الْمُنزِلُونَ(69)

 Je! Ni nyinyi mnayo yateremsha kutoka mawinguni au ni Sisi ndio wenye kuyateremsha?

لَوْ نَشَاءُ جَعَلْنَاهُ أُجَاجًا فَلَوْلَا تَشْكُرُونَ(70)

 Tungeli penda tungeli yafanya ya chumvi. Basi mbona hamshukuru?

أَفَرَأَيْتُمُ النَّارَ الَّتِي تُورُونَ(71)

 Je! Mnauona moto mnao uwasha?

أَأَنتُمْ أَنشَأْتُمْ شَجَرَتَهَا أَمْ نَحْنُ الْمُنشِئُونَ(72)

 Ni nyinyi mlio uumba mti wake au Sisi ndio Waumbaji?

نَحْنُ جَعَلْنَاهَا تَذْكِرَةً وَمَتَاعًا لِّلْمُقْوِينَ(73)

 Sisi tumeufanya uwe ni ukumbusho na manufaa kwa walioko nyikani.

فَسَبِّحْ بِاسْمِ رَبِّكَ الْعَظِيمِ(74)

 Basi litakase jina la Mola wako Mlezi aliye Mkuu.

۞ فَلَا أُقْسِمُ بِمَوَاقِعِ النُّجُومِ(75)

 Basi naapa kwa maanguko ya nyota,

وَإِنَّهُ لَقَسَمٌ لَّوْ تَعْلَمُونَ عَظِيمٌ(76)

 Na hakika bila ya shaka hichi ni kiapo kikubwa, laiti mngeli jua!

إِنَّهُ لَقُرْآنٌ كَرِيمٌ(77)

 Hakika hii bila ya shaka ni Qur'ani Tukufu,

فِي كِتَابٍ مَّكْنُونٍ(78)

 Katika Kitabu kilicho hifadhiwa.

لَّا يَمَسُّهُ إِلَّا الْمُطَهَّرُونَ(79)

 Hapana akigusaye ila walio takaswa.

تَنزِيلٌ مِّن رَّبِّ الْعَالَمِينَ(80)

 Ni uteremsho unao toka kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.

أَفَبِهَٰذَا الْحَدِيثِ أَنتُم مُّدْهِنُونَ(81)

 Ni maneno haya ndiyo nyinyi mnayapuuza?

وَتَجْعَلُونَ رِزْقَكُمْ أَنَّكُمْ تُكَذِّبُونَ(82)

 Na badala ya kushukuru kwa riziki yenu mnafanya kuwa mnakadhibisha?

فَلَوْلَا إِذَا بَلَغَتِ الْحُلْقُومَ(83)

 Yawaje basi itakapo fika roho kwenye koo,

وَأَنتُمْ حِينَئِذٍ تَنظُرُونَ(84)

 Na nyinyi wakati huo mnatazama!

وَنَحْنُ أَقْرَبُ إِلَيْهِ مِنكُمْ وَلَٰكِن لَّا تُبْصِرُونَ(85)

 Na Sisi tuko karibu zaidi naye kuliko nyinyi.

فَلَوْلَا إِن كُنتُمْ غَيْرَ مَدِينِينَ(86)

 Na lau kuwa nyinyi hamumo katika mamlaka yangu,

تَرْجِعُونَهَا إِن كُنتُمْ صَادِقِينَ(87)

 Kwanini hamuirudishi hiyo roho, ikiwa nyinyi mnasema kweli?

فَأَمَّا إِن كَانَ مِنَ الْمُقَرَّبِينَ(88)

 Basi akiwa miongoni mwa walio karibishwa,

فَرَوْحٌ وَرَيْحَانٌ وَجَنَّتُ نَعِيمٍ(89)

 Basi ni raha, na manukato, na Bustani zenye neema.

وَأَمَّا إِن كَانَ مِنْ أَصْحَابِ الْيَمِينِ(90)

 Na akiwa katika watu wa upande wa kulia,

فَسَلَامٌ لَّكَ مِنْ أَصْحَابِ الْيَمِينِ(91)

 Basi ni Salamu kwako uliye miongoni mwa watu wa upande wa kulia.

وَأَمَّا إِن كَانَ مِنَ الْمُكَذِّبِينَ الضَّالِّينَ(92)

 Na ama akiwa katika walio kadhibisha wapotovu,

فَنُزُلٌ مِّنْ حَمِيمٍ(93)

 Basi karamu yake ni maji yanayo chemka,

وَتَصْلِيَةُ جَحِيمٍ(94)

 Na kutiwa Motoni.

إِنَّ هَٰذَا لَهُوَ حَقُّ الْيَقِينِ(95)

 Hakika hii ndiyo haki yenye yakini.

فَسَبِّحْ بِاسْمِ رَبِّكَ الْعَظِيمِ(96)

 Basi litakase jina la Mola wako Mlezi aliye Mkubwa.


More surahs in Swahili:


Al-Baqarah Al-'Imran An-Nisa'
Al-Ma'idah Yusuf Ibrahim
Al-Hijr Al-Kahf Maryam
Al-Hajj Al-Qasas Al-'Ankabut
As-Sajdah Ya Sin Ad-Dukhan
Al-Fath Al-Hujurat Qaf
An-Najm Ar-Rahman Al-Waqi'ah
Al-Hashr Al-Mulk Al-Haqqah
Al-Inshiqaq Al-A'la Al-Ghashiyah

Download surah Al-Waqiah with the voice of the most famous Quran reciters :

surah Al-Waqiah mp3 : choose the reciter to listen and download the chapter Al-Waqiah Complete with high quality
surah Al-Waqiah Ahmed El Agamy
Ahmed Al Ajmy
surah Al-Waqiah Bandar Balila
Bandar Balila
surah Al-Waqiah Khalid Al Jalil
Khalid Al Jalil
surah Al-Waqiah Saad Al Ghamdi
Saad Al Ghamdi
surah Al-Waqiah Saud Al Shuraim
Saud Al Shuraim
surah Al-Waqiah Abdul Basit Abdul Samad
Abdul Basit
surah Al-Waqiah Abdul Rashid Sufi
Abdul Rashid Sufi
surah Al-Waqiah Abdullah Basfar
Abdullah Basfar
surah Al-Waqiah Abdullah Awwad Al Juhani
Abdullah Al Juhani
surah Al-Waqiah Fares Abbad
Fares Abbad
surah Al-Waqiah Maher Al Muaiqly
Maher Al Muaiqly
surah Al-Waqiah Muhammad Siddiq Al Minshawi
Al Minshawi
surah Al-Waqiah Al Hosary
Al Hosary
surah Al-Waqiah Al-afasi
Mishari Al-afasi
surah Al-Waqiah Yasser Al Dosari
Yasser Al Dosari


Monday, May 6, 2024

لا تنسنا من دعوة صالحة بظهر الغيب