Surah Nisa aya 102 , Swahili translation of the meaning Ayah.

  1. Arabic
  2. tafsir
  3. mp3
  4. English
Quran in Swahili QUR,ANI TUKUFU na tafsiri ya maana yake kwenye lugha ya Kiswahili - Ali Muhsen Alberwany & English - Sahih International : Surah Nisa aya 102 in arabic text(The Women).
  
   
ayat 102 from Surah An-Nisa

﴿وَإِذَا كُنتَ فِيهِمْ فَأَقَمْتَ لَهُمُ الصَّلَاةَ فَلْتَقُمْ طَائِفَةٌ مِّنْهُم مَّعَكَ وَلْيَأْخُذُوا أَسْلِحَتَهُمْ فَإِذَا سَجَدُوا فَلْيَكُونُوا مِن وَرَائِكُمْ وَلْتَأْتِ طَائِفَةٌ أُخْرَىٰ لَمْ يُصَلُّوا فَلْيُصَلُّوا مَعَكَ وَلْيَأْخُذُوا حِذْرَهُمْ وَأَسْلِحَتَهُمْ ۗ وَدَّ الَّذِينَ كَفَرُوا لَوْ تَغْفُلُونَ عَنْ أَسْلِحَتِكُمْ وَأَمْتِعَتِكُمْ فَيَمِيلُونَ عَلَيْكُم مَّيْلَةً وَاحِدَةً ۚ وَلَا جُنَاحَ عَلَيْكُمْ إِن كَانَ بِكُمْ أَذًى مِّن مَّطَرٍ أَوْ كُنتُم مَّرْضَىٰ أَن تَضَعُوا أَسْلِحَتَكُمْ ۖ وَخُذُوا حِذْرَكُمْ ۗ إِنَّ اللَّهَ أَعَدَّ لِلْكَافِرِينَ عَذَابًا مُّهِينًا
[ النساء: 102]

Na unapo kuwa pamoja nao, ukawasalisha, basi kundi moja miongoni mwao wasimame pamoja nawe na wachukue silaha zao. Na watakapo maliza sijida zao, basi nawende nyuma yenu, na lije kundi jingine ambalo halijasali, lisali pamoja nawe. Nao wachukue hadhari yao na silaha zao. Walio kufuru wanapenda mghafilike na silaha zenu na vifaa vyenu ili wakuvamieni mvamio wa mara moja. Wala si vibaya kwenu ikiwa mnaona udhia kwa sababu ya mvua au mkawa wagonjwa, mkaziweka silaha zenu. Na chukueni hadhari yenu. Hakika Mwenyezi Mungu amewaandalia makafiri adhabu ya kudhalilisha.

Surah An-Nisa in Swahili

Swahili Translation - Al-Barwani

English - Sahih International


And when you are among them and lead them in prayer, let a group of them stand [in prayer] with you and let them carry their arms. And when they have prostrated, let them be [in position] behind you and have the other group come forward which has not [yet] prayed and let them pray with you, taking precaution and carrying their arms. Those who disbelieve wish that you would neglect your weapons and your baggage so they could come down upon you in one [single] attack. But there is no blame upon you, if you are troubled by rain or are ill, for putting down your arms, but take precaution. Indeed, Allah has prepared for the disbelievers a humiliating punishment.


Tafsiri ya maana yake kwenye lugha ya Kiswahili


Na unapo kuwa pamoja nao, ukawasalisha, basi kundi moja miongoni mwao wasimame pamoja nawe na wachukue silaha zao. Na watakapo maliza sijida zao, basi nawende nyuma yenu, na lije kundi jingine ambalo halijasali, lisali pamoja nawe. Nao wachukue hadhari yao na silaha zao. Walio kufuru wanapenda mghafilike na silaha zenu na vifaa vyenu ili wakuvamieni mvamio wa mara moja. Wala si vibaya kwenu ikiwa mnaona udhia kwa sababu ya mvua au mkawa wagonjwa, mkaziweka silaha zenu. Na chukueni hadhari yenu. Hakika Mwenyezi Mungu amewaandalia makafiri adhabu ya kudhalilisha.


Ewe Nabii Muaminifu, ukiwa nao na Swala ya Jamaa inasaliwa, msisahau kutahadhari na maadui. Na hayo ni kuwagawa Waislamu makundi mawili. Moja lianze kuswali kwa kukufuata wewe, na wakati huo la pili lisimame kwa hadhari na silaha likilinda vifaa. Ukisha nusu ya Swala, kundi lilio sali nawe lende nyuma yako, na lije jengine lisali nawe Swala iliyo bakia. Kisha litimize sehemu waliyo ikosa. Na lile la kwanza lisali baki ya Swala. Na hii huitwa -Laahiqah-, yaani iliyo kutwa na nyengine inaitwa -Masbuuqah-, yaani iliyo tanguliwa ,kwa kuwa inasaliwa mwanzo wa Swala ya Jamaa; na -Laahiqah- inasaliwa mwisho wa Swala ya Jamaa. Mpango huu ni kwa sababu isikosekane Swala, na kutahadhari na makafiri ambao wanapenda mghafilike na silaha zenu na vifaa vyenu wapate kukuvamieni kwa ghafla, na wakumalizeni nanyi mmo katika Swala. Vita na washirikina ni waajibu, na havina ukomo. Lakini hapana dhambi juu yenu kusita kwa ajili ya udhuru kama mvua au maradhi, juu ya kuwa lazima muwe na hadhari ya kudumu. Na hii ni adhabu ya Mwenyezi Mungu kwa makafiri hapa duniani, na Akhera amewaandalia adhabu ya fedheha na udhalili. -Laahiq- ni anaye swali na Imam mwanzo wa Swala na akalazimika kusali iliyo baki peke yake, na -Masbuuq- anaye iwahi sehemu ya mwisho ya Swala ya Jamaa, kisha akatimiza sehemu aliyo ikosa peke yake.

English Türkçe Indonesia
Русский Français فارسی
تفسير Bengali Urdu

listen to Verse 102 from Nisa


Ayats from Quran in Swahili

  1. Basi litapo pulizwa baragumu hapo hautakuwapo ujamaa baina yao siku hiyo, wala hawataulizana.
  2. Na kwa usiku na unavyo vikusanya,
  3. Na ambaye amewafyonya wazazi wake na akawaambia: Ati ndio mnanitisha kuwa nitafufuliwa, na hali vizazi
  4. Na tutatoa shahidi katika kila umma, na tutasema: Leteni hoja zenu! Hapo watajua kwamba hakika
  5. Wakasema: Ndivyo vivyo hivyo alivyo sema Mola wako Mlezi. Hakika Yeye ni Mwenye hikima na
  6. Na hakuna siri katika mbingu na ardhi ila imo katika Kitabu kinacho bainisha.
  7. Hayo ni kwa kuwa Mwenyezi Mungu ndiye Wa Kweli, na kwamba wale wanao waomba badala
  8. Masihi hataona uvunjifu kuwa mtumwa wa Mwenyezi Mungu, wala Malaika walio karibishwa. Na watakao ona
  9. Hakika haya yamo katika Vitabu vya mwanzo,
  10. Na hakuna chochote ila asili yake inatokana na Sisi; wala hatukiteremshi ila kwa kipimo maalumu.

Quran Surah in Swahili :

Al-Baqarah Al-'Imran An-Nisa'
Al-Ma'idah Yusuf Ibrahim
Al-Hijr Al-Kahf Maryam
Al-Hajj Al-Qasas Al-'Ankabut
As-Sajdah Ya Sin Ad-Dukhan
Al-Fath Al-Hujurat Qaf
An-Najm Ar-Rahman Al-Waqi'ah
Al-Hashr Al-Mulk Al-Haqqah
Al-Inshiqaq Al-A'la Al-Ghashiyah

Download Surah Nisa with the voice of the most famous Quran reciters :

Surah Nisa mp3 : choose the reciter to listen and download the chapter Nisa Complete with high quality
Surah Nisa Ahmed El Agamy
Ahmed Al Ajmy
Surah Nisa Bandar Balila
Bandar Balila
Surah Nisa Khalid Al Jalil
Khalid Al Jalil
Surah Nisa Saad Al Ghamdi
Saad Al Ghamdi
Surah Nisa Saud Al Shuraim
Saud Al Shuraim
Surah Nisa Abdul Basit Abdul Samad
Abdul Basit
Surah Nisa Abdul Rashid Sufi
Abdul Rashid Sufi
Surah Nisa Abdullah Basfar
Abdullah Basfar
Surah Nisa Abdullah Awwad Al Juhani
Abdullah Al Juhani
Surah Nisa Fares Abbad
Fares Abbad
Surah Nisa Maher Al Muaiqly
Maher Al Muaiqly
Surah Nisa Muhammad Siddiq Al Minshawi
Al Minshawi
Surah Nisa Al Hosary
Al Hosary
Surah Nisa Al-afasi
Mishari Al-afasi
Surah Nisa Yasser Al Dosari
Yasser Al Dosari


Sunday, May 12, 2024

لا تنسنا من دعوة صالحة بظهر الغيب