Surah Fatir aya 12 , Swahili translation of the meaning Ayah.

  1. Arabic
  2. tafsir
  3. mp3
  4. English
Quran in Swahili QUR,ANI TUKUFU na tafsiri ya maana yake kwenye lugha ya Kiswahili - Ali Muhsen Alberwany & English - Sahih International : Surah Fatir aya 12 in arabic text(The Originator).
  
   
ayat 12 from Surah Fatir

﴿وَمَا يَسْتَوِي الْبَحْرَانِ هَٰذَا عَذْبٌ فُرَاتٌ سَائِغٌ شَرَابُهُ وَهَٰذَا مِلْحٌ أُجَاجٌ ۖ وَمِن كُلٍّ تَأْكُلُونَ لَحْمًا طَرِيًّا وَتَسْتَخْرِجُونَ حِلْيَةً تَلْبَسُونَهَا ۖ وَتَرَى الْفُلْكَ فِيهِ مَوَاخِرَ لِتَبْتَغُوا مِن فَضْلِهِ وَلَعَلَّكُمْ تَشْكُرُونَ
[ فاطر: 12]

Na bahari mbili haziwi sawa; haya ni matamu yenye ladha, mazuri kunywa. Na haya ni ya chumvi, machungu. Na kutokana na bahari zote mnakula nyama mpya (isiyo chacha). Na mnatoa mapambo mnayo yavaa. Na unaona ndani yake marikebu zinakata maji ili mtafute fadhila zake, na ili mpate kushukuru.

Surah Fatir in Swahili

Swahili Translation - Al-Barwani

English - Sahih International


And not alike are the two bodies of water. One is fresh and sweet, palatable for drinking, and one is salty and bitter. And from each you eat tender meat and extract ornaments which you wear, and you see the ships plowing through [them] that you might seek of His bounty; and perhaps you will be grateful.


Tafsiri ya maana yake kwenye lugha ya Kiswahili


Na bahari mbili haziwi sawa; haya ni matamu yenye ladha, mazuri kunywa. Na haya ni ya chumvi, machungu. Na kutokana na bahari zote mnakula nyama mpya (isiyo chacha). Na mnatoa mapambo mnayo yavaa. Na unaona ndani yake marikebu zinakata maji ili mtafute fadhila zake, na ili mpate kushukuru.


Na haziwi sawa bahari mbili katika ujuzi wetu na makadirio yetu, ijapo kuwa zinashirikiana katika baadhi ya manufaa yao. Haya maji matamu yanakata kiu kwa uzuri wake, na utamu wake, na wepesi wake kuyanywa. Na haya mengine ni maji ya chumvi, uchumvi wake mkali. Na kutokana na namna zote mbili mnakula nyama mpya (fresh, haikuchacha) nayo ni samaki mnao wavua. Na mnatoa kutoka maji ya chumvi mapambo mnayo yavaa, kama lulu na marijani. Na wewe, mwenye kutazama, unaona vipi vyombo vya baharini vinavyo kwenda, vikipasua maji kwa mwendo wake, ili mkatafute baadhi ya fadhila za Mwenyezi Mungu kwa kufanya biashara, na ili asaa mpate kumshukuru Mola wenu Mlezi kwa neema hizi. Na katika Ishara za Mwenyezi Mungu ambazo anawaitia watu wazizingatie na ambazo amewaneemesha fadhila zake ni mwendo wa marikebu na kukata kwake maji baharini kwa mujibu wa kawaida zake alizo ziwekea katika tabia za maumbile, nazo ni hizo sharia za vitu kuelea, (The law of boayancy). Ni maarufu kuwa baadhi ya mapambo yanapatikana kutoka maji ya chumvi, na baadhi ya watu labda wanaona haiwi maji matamu kutoa mapambo vile vile. Lakini ilimu na mambo yalivyo yamethibitisha kinyume cha hivyo. Ama lulu kama zinavyo patikana katika maji ya chumvi, basi vile vile zinapatikana kwenye namna fulani nyengine za chaza wa mitoni. Hupatikana lulu katika maji matamu katika Uingereza, Scotland, Wales. Czechoslovakia na Japan.. n.k. mbali na lulu za baharini maarufu. Na pia vinaingia katika vinavyo patikana katika maji matamu maadini thamini ngumu kama almasi, zinazo patikana katika udongo unao tupwa na mito. Hupatikana pia Yaakuti, katika mito ya Mojok karibu na Andalas katika Burma ya juu. Ama katika Siam (Thailand) na Sri Lanka hupatikana Yaakuti katika mito. Na katika mawe ambayo yashabihiana na ya ghali na hutumiwa kwa pambo ni Topaz. Na hupatikana pia kwenye mito mwahali mwingi katika Brazil na Urusi (Ural na Siberia) Fluro-sylicate of aluminium. Aghlabu hiyo huwa ya manjano au rangi ya kahawia. Circom ni jiwe thamini linavutia. Sifa zake zinakaribia za Almasi. Namna zake nyingi hupatikana kwenye mito. (Kadhaalika dhahabu, ambayo inaitwa Alluvial gold yaani dhahabu ya mtoni, hupatikana nchi nyingi, mojawapo ni Zaire.)

English Türkçe Indonesia
Русский Français فارسی
تفسير Bengali Urdu

listen to Verse 12 from Fatir


Ayats from Quran in Swahili


    Quran Surah in Swahili :

    Al-Baqarah Al-'Imran An-Nisa'
    Al-Ma'idah Yusuf Ibrahim
    Al-Hijr Al-Kahf Maryam
    Al-Hajj Al-Qasas Al-'Ankabut
    As-Sajdah Ya Sin Ad-Dukhan
    Al-Fath Al-Hujurat Qaf
    An-Najm Ar-Rahman Al-Waqi'ah
    Al-Hashr Al-Mulk Al-Haqqah
    Al-Inshiqaq Al-A'la Al-Ghashiyah

    Download Surah Fatir with the voice of the most famous Quran reciters :

    Surah Fatir mp3 : choose the reciter to listen and download the chapter Fatir Complete with high quality
    Surah Fatir Ahmed El Agamy
    Ahmed Al Ajmy
    Surah Fatir Bandar Balila
    Bandar Balila
    Surah Fatir Khalid Al Jalil
    Khalid Al Jalil
    Surah Fatir Saad Al Ghamdi
    Saad Al Ghamdi
    Surah Fatir Saud Al Shuraim
    Saud Al Shuraim
    Surah Fatir Abdul Basit Abdul Samad
    Abdul Basit
    Surah Fatir Ammar Al-Mulla
    Ammar Al-Mulla
    Surah Fatir Abdullah Basfar
    Abdullah Basfar
    Surah Fatir Abdullah Awwad Al Juhani
    Abdullah Al Juhani
    Surah Fatir Fares Abbad
    Fares Abbad
    Surah Fatir Maher Al Muaiqly
    Maher Al Muaiqly
    Surah Fatir Muhammad Siddiq Al Minshawi
    Al Minshawi
    Surah Fatir Al Hosary
    Al Hosary
    Surah Fatir Al-afasi
    Mishari Al-afasi
    Surah Fatir Yasser Al Dosari
    Yasser Al Dosari


    Monday, June 23, 2025

    Please remember us in your sincere prayers