Surah Fatir aya 12 , Swahili translation of the meaning Ayah.

  1. Arabic
  2. tafsir
  3. mp3
  4. English
Quran in Swahili QUR,ANI TUKUFU na tafsiri ya maana yake kwenye lugha ya Kiswahili - Ali Muhsen Alberwany & English - Sahih International : Surah Fatir aya 12 in arabic text(The Originator).
  
   
ayat 12 from Surah Fatir

﴿وَمَا يَسْتَوِي الْبَحْرَانِ هَٰذَا عَذْبٌ فُرَاتٌ سَائِغٌ شَرَابُهُ وَهَٰذَا مِلْحٌ أُجَاجٌ ۖ وَمِن كُلٍّ تَأْكُلُونَ لَحْمًا طَرِيًّا وَتَسْتَخْرِجُونَ حِلْيَةً تَلْبَسُونَهَا ۖ وَتَرَى الْفُلْكَ فِيهِ مَوَاخِرَ لِتَبْتَغُوا مِن فَضْلِهِ وَلَعَلَّكُمْ تَشْكُرُونَ
[ فاطر: 12]

Na bahari mbili haziwi sawa; haya ni matamu yenye ladha, mazuri kunywa. Na haya ni ya chumvi, machungu. Na kutokana na bahari zote mnakula nyama mpya (isiyo chacha). Na mnatoa mapambo mnayo yavaa. Na unaona ndani yake marikebu zinakata maji ili mtafute fadhila zake, na ili mpate kushukuru.

Surah Fatir in Swahili

Swahili Translation - Al-Barwani

English - Sahih International


And not alike are the two bodies of water. One is fresh and sweet, palatable for drinking, and one is salty and bitter. And from each you eat tender meat and extract ornaments which you wear, and you see the ships plowing through [them] that you might seek of His bounty; and perhaps you will be grateful.


Tafsiri ya maana yake kwenye lugha ya Kiswahili


Na bahari mbili haziwi sawa; haya ni matamu yenye ladha, mazuri kunywa. Na haya ni ya chumvi, machungu. Na kutokana na bahari zote mnakula nyama mpya (isiyo chacha). Na mnatoa mapambo mnayo yavaa. Na unaona ndani yake marikebu zinakata maji ili mtafute fadhila zake, na ili mpate kushukuru.


Na haziwi sawa bahari mbili katika ujuzi wetu na makadirio yetu, ijapo kuwa zinashirikiana katika baadhi ya manufaa yao. Haya maji matamu yanakata kiu kwa uzuri wake, na utamu wake, na wepesi wake kuyanywa. Na haya mengine ni maji ya chumvi, uchumvi wake mkali. Na kutokana na namna zote mbili mnakula nyama mpya (fresh, haikuchacha) nayo ni samaki mnao wavua. Na mnatoa kutoka maji ya chumvi mapambo mnayo yavaa, kama lulu na marijani. Na wewe, mwenye kutazama, unaona vipi vyombo vya baharini vinavyo kwenda, vikipasua maji kwa mwendo wake, ili mkatafute baadhi ya fadhila za Mwenyezi Mungu kwa kufanya biashara, na ili asaa mpate kumshukuru Mola wenu Mlezi kwa neema hizi. Na katika Ishara za Mwenyezi Mungu ambazo anawaitia watu wazizingatie na ambazo amewaneemesha fadhila zake ni mwendo wa marikebu na kukata kwake maji baharini kwa mujibu wa kawaida zake alizo ziwekea katika tabia za maumbile, nazo ni hizo sharia za vitu kuelea, (The law of boayancy). Ni maarufu kuwa baadhi ya mapambo yanapatikana kutoka maji ya chumvi, na baadhi ya watu labda wanaona haiwi maji matamu kutoa mapambo vile vile. Lakini ilimu na mambo yalivyo yamethibitisha kinyume cha hivyo. Ama lulu kama zinavyo patikana katika maji ya chumvi, basi vile vile zinapatikana kwenye namna fulani nyengine za chaza wa mitoni. Hupatikana lulu katika maji matamu katika Uingereza, Scotland, Wales. Czechoslovakia na Japan.. n.k. mbali na lulu za baharini maarufu. Na pia vinaingia katika vinavyo patikana katika maji matamu maadini thamini ngumu kama almasi, zinazo patikana katika udongo unao tupwa na mito. Hupatikana pia Yaakuti, katika mito ya Mojok karibu na Andalas katika Burma ya juu. Ama katika Siam (Thailand) na Sri Lanka hupatikana Yaakuti katika mito. Na katika mawe ambayo yashabihiana na ya ghali na hutumiwa kwa pambo ni Topaz. Na hupatikana pia kwenye mito mwahali mwingi katika Brazil na Urusi (Ural na Siberia) Fluro-sylicate of aluminium. Aghlabu hiyo huwa ya manjano au rangi ya kahawia. Circom ni jiwe thamini linavutia. Sifa zake zinakaribia za Almasi. Namna zake nyingi hupatikana kwenye mito. (Kadhaalika dhahabu, ambayo inaitwa Alluvial gold yaani dhahabu ya mtoni, hupatikana nchi nyingi, mojawapo ni Zaire.)

English Türkçe Indonesia
Русский Français فارسی
تفسير Bengali Urdu

listen to Verse 12 from Fatir


Ayats from Quran in Swahili

  1. Lakini Shet'ani alimtia wasiwasi, akamwambia: Ewe Adam! Nikujuulishe mti wa kuishi milele na ufalme usio
  2. Lakini mlidhani kwamba Mtume na Waumini hawatarudi kabisa kwa ahali zao, na mkapambiwa hayo katika
  3. Na mt'iini Mwenyezi Mungu na Mtume wake, wala msizozane mkaingiwa woga, na zikapotea nguvu zenu.
  4. Na mpe aliye jamaa yako haki yake, na masikini, na msafiri; wala usitumie ovyo kwa
  5. Na mtakapo wapa wanawake t'alaka, nao wakafikia kumaliza eda yao, basi warejeeni kwa wema au
  6. Ewe mwanangu! Kikiwapo kitu cha uzito wa chembe ya khardali kikawa ndani ya jabali au
  7. Kwa hivyo tutawatoa katika hao wale walio amini.
  8. Ni nini kilicho kupelekeni Motoni?
  9. Sisi tumewaumba, na tukavitia nguvu viungo vyao. Na tukitaka tutawabadilisha mfano wao wawe badala yao.
  10. Na walisema: Hautatugusa Moto ila kwa siku chache tu. Sema: Mmechukua ahadi kwa Mwenyezi Mungu?

Quran Surah in Swahili :

Al-Baqarah Al-'Imran An-Nisa'
Al-Ma'idah Yusuf Ibrahim
Al-Hijr Al-Kahf Maryam
Al-Hajj Al-Qasas Al-'Ankabut
As-Sajdah Ya Sin Ad-Dukhan
Al-Fath Al-Hujurat Qaf
An-Najm Ar-Rahman Al-Waqi'ah
Al-Hashr Al-Mulk Al-Haqqah
Al-Inshiqaq Al-A'la Al-Ghashiyah

Download Surah Fatir with the voice of the most famous Quran reciters :

Surah Fatir mp3 : choose the reciter to listen and download the chapter Fatir Complete with high quality
Surah Fatir Ahmed El Agamy
Ahmed Al Ajmy
Surah Fatir Bandar Balila
Bandar Balila
Surah Fatir Khalid Al Jalil
Khalid Al Jalil
Surah Fatir Saad Al Ghamdi
Saad Al Ghamdi
Surah Fatir Saud Al Shuraim
Saud Al Shuraim
Surah Fatir Abdul Basit Abdul Samad
Abdul Basit
Surah Fatir Abdul Rashid Sufi
Abdul Rashid Sufi
Surah Fatir Abdullah Basfar
Abdullah Basfar
Surah Fatir Abdullah Awwad Al Juhani
Abdullah Al Juhani
Surah Fatir Fares Abbad
Fares Abbad
Surah Fatir Maher Al Muaiqly
Maher Al Muaiqly
Surah Fatir Muhammad Siddiq Al Minshawi
Al Minshawi
Surah Fatir Al Hosary
Al Hosary
Surah Fatir Al-afasi
Mishari Al-afasi
Surah Fatir Yasser Al Dosari
Yasser Al Dosari


Wednesday, May 15, 2024

لا تنسنا من دعوة صالحة بظهر الغيب