Surah Nisa aya 135 , Swahili translation of the meaning Ayah.
﴿۞ يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا كُونُوا قَوَّامِينَ بِالْقِسْطِ شُهَدَاءَ لِلَّهِ وَلَوْ عَلَىٰ أَنفُسِكُمْ أَوِ الْوَالِدَيْنِ وَالْأَقْرَبِينَ ۚ إِن يَكُنْ غَنِيًّا أَوْ فَقِيرًا فَاللَّهُ أَوْلَىٰ بِهِمَا ۖ فَلَا تَتَّبِعُوا الْهَوَىٰ أَن تَعْدِلُوا ۚ وَإِن تَلْوُوا أَوْ تُعْرِضُوا فَإِنَّ اللَّهَ كَانَ بِمَا تَعْمَلُونَ خَبِيرًا﴾
[ النساء: 135]
Enyi mlio amini! Kuweni wenye kusimamisha uadilifu, mtowao ushahidi kwa ajili ya Mwenyezi Mungu, ijapo kuwa ni juu ya nafsi zenu, au wazazi wawili na jamaa zenu. Akiwa tajiri au masikini Mwenyezi Mungu anawastahikia zaidi. Basi msifuate matamanio, mkaacha kufanya uadilifu. Na mkiupotoa au mkajitenga nao basi Mwenyezi Mungu anajua vyema mnayo yatenda.
Surah An-Nisa in SwahiliSwahili Translation - Al-Barwani
English - Sahih International
O you who have believed, be persistently standing firm in justice, witnesses for Allah, even if it be against yourselves or parents and relatives. Whether one is rich or poor, Allah is more worthy of both. So follow not [personal] inclination, lest you not be just. And if you distort [your testimony] or refuse [to give it], then indeed Allah is ever, with what you do, Acquainted.
Tafsiri ya maana yake kwenye lugha ya Kiswahili
Enyi mlio amini! Kuweni wenye kusimamisha uadilifu, mtowao ushahidi kwa ajili ya Mwenyezi Mungu, ijapo kuwa ni juu ya nafsi zenu, au wazazi wawili na jamaa zenu. Akiwa tajiri au masikini Mwenyezi Mungu anawastahikia zaidi. Basi msifuate matamanio, mkaacha kufanya uadilifu. Na mkiupotoa au mkajitenga nao basi Mwenyezi Mungu anajua vyema mnayo yatenda.
Uadilifu ndio nidhamu ya maumbile. Na hiyo ndiyo sharia ambayo haiwezi kuwapo ndani yake maoni ya kukhitalifiana. Basi enyi mlio mtii Mwenyezi Mungu wa Haki, na wito wa Mitume wake, kuweni macho nafsi zenu katika kuutii uadilifu, na kuweni macho kwa ajili ya watu. Mfanyieni insafu aliye dhulumiwa, na msimame imara, si kwa ajili ya kumpendelea tajiri, au kumwonea huruma masikini. Kwani Mwenyezi Mungu aliye waumba matajiri na masikini anastahiki zaidi kuangalia hali ya tajiri au fakiri. Matamanio ndiyo yanayo mpelekea mtu kumili nafsi yake, basi msiyafuate matamanio mkaacha uadilifu. Na mkikengeuka mkaacha uadilifu, au mkapuuza kusimamisha uadilifu, basi mjue Mwenyezi Mungu anayajua myatendayo, tena anayajua kwa ujuzi wa ndani. Naye atakulipeni kwa mujibu wa amali yenu; ikiwa njema mtalipwa wema, ikiwa ovu mtalipwa shari.
English | Türkçe | Indonesia |
Русский | Français | فارسی |
تفسير | Bengali | Urdu |
Ayats from Quran in Swahili
- Naapa kwa pepo zinazo tawanya,
- Na hakika watu wa Kichakani walikuwa wenye kudhulumu.
- Na hakika yeye mwenyewe bila ya shaka ni shahidi wa hayo!
- Hakika wale walio nunua ukafiri kwa Imani hawatamdhuru kitu Mwenyezi Mungu, na yao wao ni
- Yatawafaa nini yale waliyo stareheshewa?
- Ili Yeye awalipe ujira wao kwa ukamilifu, na awazidishie kutokana na fadhila zake. Hakika Yeye
- Na wengine wafungwao kwa minyororo.
- Na ama atakaye pewa kitabu chake katika mkono wake wa kushoto, basi yeye atasema: Laiti
- Hivyo nyinyi mmewatetea hawa katika uhai huu wa duniani. Basi nani atakaye watetea kwa Mwenyezi
- Sema: Ni nani anaye kuruzukuni kutoka mbinguni na kwenye ardhi? Sema: Mwenyezi Mungu! Na hakika
Quran Surah in Swahili :
Download Surah Nisa with the voice of the most famous Quran reciters :
Surah Nisa mp3 : choose the reciter to listen and download the chapter Nisa Complete with high quality
Ahmed Al Ajmy
Bandar Balila
Khalid Al Jalil
Saad Al Ghamdi
Saud Al Shuraim
Abdul Basit
Abdul Rashid Sufi
Abdullah Basfar
Abdullah Al Juhani
Fares Abbad
Maher Al Muaiqly
Al Minshawi
Al Hosary
Mishari Al-afasi
Yasser Al Dosari
Please remember us in your sincere prayers