Surah Ahqaf aya 21 , Swahili translation of the meaning Ayah.
﴿۞ وَاذْكُرْ أَخَا عَادٍ إِذْ أَنذَرَ قَوْمَهُ بِالْأَحْقَافِ وَقَدْ خَلَتِ النُّذُرُ مِن بَيْنِ يَدَيْهِ وَمِنْ خَلْفِهِ أَلَّا تَعْبُدُوا إِلَّا اللَّهَ إِنِّي أَخَافُ عَلَيْكُمْ عَذَابَ يَوْمٍ عَظِيمٍ﴾
[ الأحقاف: 21]
Na mtaje ndugu wa kina A'di, alipo waonya watu wake kwenye vilima vya mchanga. Na kwa yakini waonyaji wengi walitokea kabla yake na baada yake kuwaambia: Msimuabudu isipo kuwa Mwenyezi Mungu. Hakika mimi nakukhofieni isikupateni adhabu ya siku iliyo kuu.
Surah Al-Ahqaaf in SwahiliSwahili Translation - Al-Barwani
English - Sahih International
And mention, [O Muhammad], the brother of 'Aad, when he warned his people in the [region of] al-Ahqaf - and warners had already passed on before him and after him - [saying], "Do not worship except Allah. Indeed, I fear for you the punishment of a terrible day."
Tafsiri ya maana yake kwenye lugha ya Kiswahili
Na mtaje ndugu wa kina Adi, alipo waonya watu wake kwenye vilima vya mchanga. Na kwa yakini waonyaji wengi walitokea kabla yake na baada yake kuwaambia: Msimuabudu isipo kuwa Mwenyezi Mungu. Hakika mimi nakukhofieni isikupateni adhabu ya siku iliyo kuu.
Mtaje Hud, mwenzao kabila ya Adi, alipo wahadharisha watu wake wanao kaa Ahqaaf, kwenye vilima vya mchanga. Na Mitume kadhaa walikuja kabla yake na baada yake kwa maonyo kama yake ya kusema: Msimuabudu ila Mwenyezi Mungu. Mimi nakukhofieni isikupateni adhabu yenye vitisho vikuu. Maskani ya kabila hii ilikuwa huko Ahqaaf, kwenye vilima vya mchanga. Na wapi hapo Ahqaaf? Zipo khitilafu. Baadhi ya wanazuoni wa taarikh (historia) wanasema kuwa hapo ni baina ya Yaman na Oman mpaka Hadhramaut na Shihr, yaani mashariki ya kusini ya Bara Arabu. Na baadhi ya wachunguzi wa zama za karibu wanaona ni mashariki ya aqaba, wakitegemea maandishi ya Nabatia waliyo yakuta katika magofu ya hekalu walilo livumbua katika mlima wa Arim. Walikuta pembezoni mwa mlima huo mabaki ya siku za Jahiliya za zamani. Wakasahihisha kuwa hapo ndipo ilipo Arim iliyo tajwa katika Qurani tukufu. Kisha kabila hiyo ikatoka hapo kabla ya Uislamu, na hapana kilicho baki chao isipo kuwa chemchem ya maji ambayo wafanyi biashara na watu wa misafara wakishukia hapo katika njia yao kwendea Shamu.
English | Türkçe | Indonesia |
Русский | Français | فارسی |
تفسير | Bengali | Urdu |
Ayats from Quran in Swahili
- Na Mola wako Mlezi mtukuze!
- Ila wale walio subiri wakatenda mema. Hao watapata msamaha na ujira mkubwa.
- Na hatukuziumba mbingu na ardhi na vilivyomo ndani yake ila kwa ajili ya Haki. Na
- Sema: Enyi waja wangu walio jidhulumu nafsi zao! Msikate tamaa na rehema ya Mwenyezi Mungu.
- Zimeghafilika nyoyo zao. Na wale walio dhulumu hunong'onezana kwa siri: Ni nani ati huyu isipo
- Na inapo teremshwa Sura wapo miongoni mwao wasemao: Ni nani miongoni mwenu Sura hii imemzidishia
- Ama wale ambao mizani zao zitakuwa nzito, hao ndio wenye kufanikiwa.
- Basi nyinyi mkikufuru, mtawezaje kujikinga na Siku ambayo itawafanya watoto wadogo waote mvi?
- Basi hapana shaka tutawaonjesha hao walio kufuru adhabu kali, na hapana shaka tutawalipa malipo mabaya
- Hao watapata nyumba ya salama kwa Mola Mlezi wao. Naye ndiye Rafiki Mlinzi wao kwa
Quran Surah in Swahili :
Download Surah Ahqaf with the voice of the most famous Quran reciters :
Surah Ahqaf mp3 : choose the reciter to listen and download the chapter Ahqaf Complete with high quality
Ahmed Al Ajmy
Bandar Balila
Khalid Al Jalil
Saad Al Ghamdi
Saud Al Shuraim
Abdul Basit
Ammar Al-Mulla
Abdullah Basfar
Abdullah Al Juhani
Fares Abbad
Maher Al Muaiqly
Al Minshawi
Al Hosary
Mishari Al-afasi
Yasser Al Dosari
Please remember us in your sincere prayers