Surah Yusuf aya 31 , Swahili translation of the meaning Ayah.
﴿فَلَمَّا سَمِعَتْ بِمَكْرِهِنَّ أَرْسَلَتْ إِلَيْهِنَّ وَأَعْتَدَتْ لَهُنَّ مُتَّكَأً وَآتَتْ كُلَّ وَاحِدَةٍ مِّنْهُنَّ سِكِّينًا وَقَالَتِ اخْرُجْ عَلَيْهِنَّ ۖ فَلَمَّا رَأَيْنَهُ أَكْبَرْنَهُ وَقَطَّعْنَ أَيْدِيَهُنَّ وَقُلْنَ حَاشَ لِلَّهِ مَا هَٰذَا بَشَرًا إِنْ هَٰذَا إِلَّا مَلَكٌ كَرِيمٌ﴾
[ يوسف: 31]
Alipo sikia yule bibi masengenyo yao aliwaita, na akawawekea matakia ya kuegemea, na akampa kila mmoja wao kisu. Akamwambia Yusuf: Tokeza mbele yao. Basi walipo mwona waliona ni kitu kikubwa kabisa, na wakajikata mikono yao. Wakasema: Hasha Lillahi! Huyu si mwanaadamu. Hakuwa huyu ila ni Malaika mtukufu.
Surah Yusuf in SwahiliSwahili Translation - Al-Barwani
English - Sahih International
So when she heard of their scheming, she sent for them and prepared for them a banquet and gave each one of them a knife and said [to Joseph], "Come out before them." And when they saw him, they greatly admired him and cut their hands and said, "Perfect is Allah! This is not a man; this is none but a noble angel."
Tafsiri ya maana yake kwenye lugha ya Kiswahili
Alipo sikia yule bibi masengenyo yao aliwaita, na akawawekea matakia ya kuegemea, na akampa kila mmoja wao kisu. Akamwambia Yusuf: Tokeza mbele yao. Basi walipo mwona waliona ni kitu kikubwa kabisa, na wakajikata mikono yao. Wakasema: Hasha Lillahi! Huyu si mwanaadamu. Hakuwa huyu ila ni Malaika mtukufu.
Yule bibi alipo yasikia masengenyo yao wale wanawake na kuwa wanamsema kwa vibaya, aliwaalika nyumbani kwake na akawapangia matakia na mito ya kuegemea, na akampa kila mmoja wao kisu, baada ya kwisha hudhuria na wakakaa wakiegemea. Akawaletea chakula na visu vya kulia. Akamwambia Yusuf: Hebu watokee! Alipotokeza wakamwona walistaajabu. Uzuri wake ulio pita mpaka uliwatwaa wasijitambue, wakawa wanajikata mikono yao jinsi ya kushtuka kwao, na huku wanadhani wanakata chakula! Wakasema kwa mastaajabu na kushituka: Hasha Lillahi! Mungu apishe mbali! Huyu tunaye mwona si binaadamu! Hapana binaadamu mwenye uzuri namna hii, na mwenye jamali kama hivi, na usafi kama huu, na kunyooka kama huku! Huyu ni Malaika tu, mwenye uzuri huu, na sifa hizi zilio timia!
| English | Türkçe | Indonesia |
| Русский | Français | فارسی |
| تفسير | Bengali | Urdu |
Ayats from Quran in Swahili
- Sema: Lau kuwa bahari ndio wino kwa maneno ya Mola wangu Mlezi, basi bahari ingeli
- Na Lut'i alipo waambia watu wake: Je! Mnafanya uchafu nanyi mnaona?
- Kwani? Hakika Mola wake Mlezi alikuwa akimwona!
- Mola wangu Mlezi! Niokoe mimi na ahali zangu na haya wayatendayo.
- Hawatakuwa na chakula isipo kuwa kichungu chenye miba.
- Na walio amini na wakatenda mema, kwa yakini tutawafutia makosa yao, na tutawalipa bora ya
- Kwani hakujaalia vitimbi vyao kuharibika?
- Kisha tukakufunulia ya kwamba ufuate mila ya Ibrahim, mwongofu, wala hakuwa miongoni mwa washirikina.
- Na kwa hakika hii ndiyo Njia yangu Iliyo Nyooka. Basi ifuateni, wala msifuate njia nyingine,
- Je! Huoni kwamba Mwenyezi Mungu huteremsha maji kutoka mbinguni, na mara ardhi inakuwa chanikiwiti? Hakika
Quran Surah in Swahili :
Download Surah Yusuf with the voice of the most famous Quran reciters :
Surah Yusuf mp3 : choose the reciter to listen and download the chapter Yusuf Complete with high quality
Ahmed Al Ajmy
Bandar Balila
Khalid Al Jalil
Saad Al Ghamdi
Saud Al Shuraim
Abdul Basit
Ammar Al-Mulla
Abdullah Basfar
Abdullah Al Juhani
Fares Abbad
Maher Al Muaiqly
Al Minshawi
Al Hosary
Mishari Al-afasi
Yasser Al Dosari
Please remember us in your sincere prayers



