Surah An Nur aya 43 , Swahili translation of the meaning Ayah.

  1. Arabic
  2. tafsir
  3. mp3
  4. English
Quran in Swahili QUR,ANI TUKUFU na tafsiri ya maana yake kwenye lugha ya Kiswahili - Ali Muhsen Alberwany & English - Sahih International : Surah An Nur aya 43 in arabic text(The Light).
  
   
ayat 43 from Surah An-Nur

﴿أَلَمْ تَرَ أَنَّ اللَّهَ يُزْجِي سَحَابًا ثُمَّ يُؤَلِّفُ بَيْنَهُ ثُمَّ يَجْعَلُهُ رُكَامًا فَتَرَى الْوَدْقَ يَخْرُجُ مِنْ خِلَالِهِ وَيُنَزِّلُ مِنَ السَّمَاءِ مِن جِبَالٍ فِيهَا مِن بَرَدٍ فَيُصِيبُ بِهِ مَن يَشَاءُ وَيَصْرِفُهُ عَن مَّن يَشَاءُ ۖ يَكَادُ سَنَا بَرْقِهِ يَذْهَبُ بِالْأَبْصَارِ
[ النور: 43]

Je! Huoni ya kwamba Mwenyezi Mungu huyasukuma mawingu, kisha huyaambatisha, kisha huyafanya mirundi? Basi utaona mvua ikitoka kati yake. Na huteremsha kutoka juu kwenye milima ya mawingu mvua ya mawe, akamsibu nayo amtakaye na akamuepusha nayo amtakaye. Hukurubia mmetuko wa umeme wake kupofua macho.

Surah An-Nur in Swahili

Swahili Translation - Al-Barwani

English - Sahih International


Do you not see that Allah drives clouds? Then He brings them together, then He makes them into a mass, and you see the rain emerge from within it. And He sends down from the sky, mountains [of clouds] within which is hail, and He strikes with it whom He wills and averts it from whom He wills. The flash of its lightening almost takes away the eyesight.


Tafsiri ya maana yake kwenye lugha ya Kiswahili


Je! Huoni ya kwamba Mwenyezi Mungu huyasukuma mawingu, kisha huyaambatisha, kisha huyafanya mirundi? Basi utaona mvua ikitoka kati yake. Na huteremsha kutoka juu kwenye milima ya mawingu mvua ya mawe, akamsibu nayo amtakaye na akamuepusha nayo amtakaye. Hukurubia mmetuko wa umeme wake kupofua macho.


Ewe Nabii! Huoni kwamba Mwenyezi Mungu huyavuta mawingu, kisha huyakusanya na kuyarindika moja juu ya moja. Utaona mvua inatoka kwenye mawingu. Na Mwenyezi Mungu huteremsha kutokana na mawingu yaliyo rindikana yanayo shabihi milima kwa ukubwa wake, vipande vya barafu kama changarawe, vikawaangukia watu vikawaletea manufaa au madhara, kufuatana na kanuni zake na matakwa yake, wala asiwateremshie wenginewe kwa mujibu apendavyo Yeye Subhanahu, Mtendaji, Mwenye kukhitari. Mwangaza wa umeme unao tokea kwa kugongana mawingu hukaribia kutia upofu kwa ukali wake. Na mambo kama haya ya kuonekana ni dalili za kuonyesha uwezo wa Mwenyezi Mungu ambao unao wajibisha kuleta Imani ya kumuamini Yeye. Hajui kushabihiana baina ya mawingu na milima ila mwenye kupanda ndege (eropleni) inayo ruka juu ya mawingu, akayaona kutoka huko juu kama ni milima na vilima. Ilivyo kuwa ndege hizo hazijawa bado zama za Mtume s.a.w. basi hii inakuwa ni dalili kuwa maneno haya yanatokana na Mwenyezi Mungu anaye jua ya juu na chini. -Je! Huoni ya kwamba Mwenyezi Mungu huyasukuma mawingu, kisha huyaambatisha, kisha huyafanya mirundi? Basi utaona mvua ikitoka kati yake. Na huteremsha kutoka juu kwenye milima ya mawingu mvua ya mawe, akamsibu nayo amtakaye na akamuepusha nayo amtakaye. Hukurubia mmetuko wa umeme wake kupofua macho.- Aya hii tukufu imeutangulia msafara wa sayansi. Kwani hii yaeleza daraja za kuundika mawingu yanayo rindikana, na sifa zake, na yaliyo juulikana hivi karibuni ki-sayansi ya kwamba mawingu ya mvua huanzia kwa sura ya moja moja kisha yakajumuika yakawa kikundi, ndiyo hayo mawingu yaliyo rindikana, yaani mawingu yanayo endelea kukua kwa kuelekea utosini. Hayo hukua kimo chake hata kufikia urefu wa kilomita 15 au 20, na hapo huonekana kama ni milima mikubwa iliyo nyanyuka. Na yajuulikanayo ki-sayansi ni kuwa mawingu yaliyo rindika yanapitia daraja tatu, nazo: Daraja ya kukusanyika na kukua. Daraja ya kunyesha. Na mwisho daraja ya kumalizikia. Kama ilivyo kuwa mawingu hayo - nayo ni peke yao - yenye mvua ya mawe na inabeba nguvu za umeme (electricity, Kahrabaa) , huweza kuwa yakashika mfululizo wa umeme na radi, hata huweza ikawa ni miripuko karibu 40 kwa dakika moja, hata mtu anaye tazama akawa hawezi tena kuona kwa ukali wa mwanga wake. Na haya ndiyo khasa yanayo wapata marubani wa meli na ndege wakati wa midharuba ya radi.

English Türkçe Indonesia
Русский Français فارسی
تفسير Bengali Urdu

listen to Verse 43 from An Nur


Ayats from Quran in Swahili


Quran Surah in Swahili :

Al-Baqarah Al-'Imran An-Nisa'
Al-Ma'idah Yusuf Ibrahim
Al-Hijr Al-Kahf Maryam
Al-Hajj Al-Qasas Al-'Ankabut
As-Sajdah Ya Sin Ad-Dukhan
Al-Fath Al-Hujurat Qaf
An-Najm Ar-Rahman Al-Waqi'ah
Al-Hashr Al-Mulk Al-Haqqah
Al-Inshiqaq Al-A'la Al-Ghashiyah

Download Surah An Nur with the voice of the most famous Quran reciters :

Surah An Nur mp3 : choose the reciter to listen and download the chapter An Nur Complete with high quality
Surah An Nur Ahmed El Agamy
Ahmed Al Ajmy
Surah An Nur Bandar Balila
Bandar Balila
Surah An Nur Khalid Al Jalil
Khalid Al Jalil
Surah An Nur Saad Al Ghamdi
Saad Al Ghamdi
Surah An Nur Saud Al Shuraim
Saud Al Shuraim
Surah An Nur Abdul Basit Abdul Samad
Abdul Basit
Surah An Nur Abdul Rashid Sufi
Abdul Rashid Sufi
Surah An Nur Abdullah Basfar
Abdullah Basfar
Surah An Nur Abdullah Awwad Al Juhani
Abdullah Al Juhani
Surah An Nur Fares Abbad
Fares Abbad
Surah An Nur Maher Al Muaiqly
Maher Al Muaiqly
Surah An Nur Muhammad Siddiq Al Minshawi
Al Minshawi
Surah An Nur Al Hosary
Al Hosary
Surah An Nur Al-afasi
Mishari Al-afasi
Surah An Nur Yasser Al Dosari
Yasser Al Dosari


Saturday, May 11, 2024

لا تنسنا من دعوة صالحة بظهر الغيب