Surah Maidah aya 110 , Swahili translation of the meaning Ayah.

  1. Arabic
  2. tafsir
  3. mp3
  4. English
Quran in Swahili QUR,ANI TUKUFU na tafsiri ya maana yake kwenye lugha ya Kiswahili - Ali Muhsen Alberwany & English - Sahih International : Surah Maidah aya 110 in arabic text(The Table).
  
   

﴿إِذْ قَالَ اللَّهُ يَا عِيسَى ابْنَ مَرْيَمَ اذْكُرْ نِعْمَتِي عَلَيْكَ وَعَلَىٰ وَالِدَتِكَ إِذْ أَيَّدتُّكَ بِرُوحِ الْقُدُسِ تُكَلِّمُ النَّاسَ فِي الْمَهْدِ وَكَهْلًا ۖ وَإِذْ عَلَّمْتُكَ الْكِتَابَ وَالْحِكْمَةَ وَالتَّوْرَاةَ وَالْإِنجِيلَ ۖ وَإِذْ تَخْلُقُ مِنَ الطِّينِ كَهَيْئَةِ الطَّيْرِ بِإِذْنِي فَتَنفُخُ فِيهَا فَتَكُونُ طَيْرًا بِإِذْنِي ۖ وَتُبْرِئُ الْأَكْمَهَ وَالْأَبْرَصَ بِإِذْنِي ۖ وَإِذْ تُخْرِجُ الْمَوْتَىٰ بِإِذْنِي ۖ وَإِذْ كَفَفْتُ بَنِي إِسْرَائِيلَ عَنكَ إِذْ جِئْتَهُم بِالْبَيِّنَاتِ فَقَالَ الَّذِينَ كَفَرُوا مِنْهُمْ إِنْ هَٰذَا إِلَّا سِحْرٌ مُّبِينٌ
[ المائدة: 110]

Na pale Mwenyezi Mungu atapo sema: Ewe Isa bin Maryamu! Kumbuka neema yangu juu yako, na juu ya mama yako, nilipo kutia nguvu kwa Roho Takatifu, ukazungumza na watu katika utoto na utuuzimani. Na nilivyo kufunza kuandika na hikima na Taurati na Injili. Na ulipo tengeneza udongo sura ya ndege, kwa idhini yangu, kisha ukapuliza ikawa ndege kwa idhini yangu; na ulipo waponesha vipofu na wakoma kwa idhini yangu; na ulipo wafufua wafu kwa idhini yangu; na nilipo kukinga na Wana wa Israili ulipo wajia na hoja zilizo wazi, na wakasema walio kufuru miongoni mwao: Haya si lolote ila ni uchawi mtupu!

Surah Al-Maidah in Swahili

Swahili Translation - Al-Barwani

English - Sahih International


[The Day] when Allah will say, "O Jesus, Son of Mary, remember My favor upon you and upon your mother when I supported you with the Pure Spirit and you spoke to the people in the cradle and in maturity; and [remember] when I taught you writing and wisdom and the Torah and the Gospel; and when you designed from clay [what was] like the form of a bird with My permission, then you breathed into it, and it became a bird with My permission; and you healed the blind and the leper with My permission; and when you brought forth the dead with My permission; and when I restrained the Children of Israel from [killing] you when you came to them with clear proofs and those who disbelieved among them said, "This is not but obvious magic."


Tafsiri ya maana yake kwenye lugha ya Kiswahili


Na pale Mwenyezi Mungu atapo sema: Ewe Isa bin Maryamu! Kumbuka neema yangu juu yako, na juu ya mama yako, nilipo kutia nguvu kwa Roho Takatifu, ukazungumza na watu katika utoto na utuuzimani. Na nilivyo kufunza kuandika na hikima na Taurati na Injili. Na ulipo tengeneza udongo sura ya ndege, kwa idhini yangu, kisha ukapuliza ikawa ndege kwa idhini yangu; na ulipo waponesha vipofu na wakoma kwa idhini yangu; na ulipo wafufua wafu kwa idhini yangu; na nilipo kukinga na Wana wa Israili ulipo wajia na hoja zilizo wazi, na wakasema walio kufuru miongoni mwao: Haya si lolote ila ni uchawi mtupu!.


Na wakati huo, Mwenyezi Mungu atamwambia Isa mwana wa Maryamu miongoni mwa Mitume: Kumbuka neema niliyo kuneemesha wewe na mama yako katika dunia, nilipo kutia nguvu kwa Wahyi,(Ufunuo), na nikakutamkisha nawe ni mtoto mchanga ili kumuondolea tuhuma aliyo tuhumiwa mama yako, kama nilivyo kutamkisha nawe ni mtu mzima kwa ufunuo niliyo kufunulia; na nilipo kuneemesha kwa kukufunza kuandika, na nikakuwezesha kusema na kutenda yaliyo sawa, na nikakufunza Kitabu cha Musa na Injili niliyo kuteremshia wewe, na nikakuwezesha kutenda miujiza asiyo weza mtu mwingine kuitenda, ulipo tengeneza ndege kwa udongo kwa idhini ya Mwenyezi Mungu, ukapuliza akawa ndege aliye hai kwa uweza wa Mwenyezi Mungu, si kwa uweza wako, na ukamponesha mtoto kipofu, na ukamponesha mkoma kwa idhini na uweza wa Mwenyezi Mungu, na yakawa kwa kupitia mikononi mwako makadara ya kufufuka maiti kwa idhini ya Mwenyezi Mungu na kudra yake, na pale nilipo wazuia Mayahudi wasikuuwe na kukusalibu nilipo waletea miujiza wapate kuamini, nao baadhi yao walikanya na wakadai kuwa hiyo miujiza si lolote ila ni dhaahiri uchawi tu. (Katika Injili ya Luka inasemwa -Malaika kutoka mbinguni akamtokea akamtia nguvu.- Luka 22.43. Na katika Injili ya Yohana 5.30 Yesu anakiri: -Mimi siwezi kufanya neno mwenyewe.-)

English Türkçe Indonesia
Русский Français فارسی
تفسير Bengali Urdu

listen to Verse 110 from Maidah


Ayats from Quran in Swahili

  1. Wanakuuliza watoe nini? Sema: Kheri mnayo itoa ni kwa ajili ya wazazi na jamaa na
  2. Mwenye kutaka mavuno ya Akhera tutamzidishia katika mavuno yake, na mwenye kutaka mavuno ya duniani
  3. Usiutikisie huu wahyi ulimi wako kwa kuufanyia haraka.
  4. Hayo ni kwa sababu ya kuwa Mola wako Mlezi hakuwa wa kuiangamiza miji kwa dhulma,
  5. Enyi mlio amini! Msiwe kama wale walio kufuru na wakawasema ndugu zao walipo safiri katika
  6. Alipo kuwa kasimama chumbani akisali, Malaika kamnadia: Hakika Mwenyezi Mungu anakubashiria Yahya, ataye kuwa mwenye
  7. Isipo kuwa walio mfuata Luut'i. Bila ya shaka sisi tutawaokoa hao wote.
  8. Yasikufurahishe mali yao wala wana wao. Hakika Mwenyezi Mungu anataka kuwaadhibu kwayo hapa duniani, na
  9. Akasema: Kwa kuwa umenihukumia upotofu, basi nitawavizia katika Njia yako Iliyo Nyooka.
  10. Wanatimiza ahadi, na wanaiogopa siku ambayo shari yake inaenea sana,

Quran Surah in Swahili :

Al-Baqarah Al-'Imran An-Nisa'
Al-Ma'idah Yusuf Ibrahim
Al-Hijr Al-Kahf Maryam
Al-Hajj Al-Qasas Al-'Ankabut
As-Sajdah Ya Sin Ad-Dukhan
Al-Fath Al-Hujurat Qaf
An-Najm Ar-Rahman Al-Waqi'ah
Al-Hashr Al-Mulk Al-Haqqah
Al-Inshiqaq Al-A'la Al-Ghashiyah

Download Surah Maidah with the voice of the most famous Quran reciters :

Surah Maidah mp3 : choose the reciter to listen and download the chapter Maidah Complete with high quality
Surah Maidah Ahmed El Agamy
Ahmed Al Ajmy
Surah Maidah Bandar Balila
Bandar Balila
Surah Maidah Khalid Al Jalil
Khalid Al Jalil
Surah Maidah Saad Al Ghamdi
Saad Al Ghamdi
Surah Maidah Saud Al Shuraim
Saud Al Shuraim
Surah Maidah Abdul Basit Abdul Samad
Abdul Basit
Surah Maidah Abdul Rashid Sufi
Abdul Rashid Sufi
Surah Maidah Abdullah Basfar
Abdullah Basfar
Surah Maidah Abdullah Awwad Al Juhani
Abdullah Al Juhani
Surah Maidah Fares Abbad
Fares Abbad
Surah Maidah Maher Al Muaiqly
Maher Al Muaiqly
Surah Maidah Muhammad Siddiq Al Minshawi
Al Minshawi
Surah Maidah Al Hosary
Al Hosary
Surah Maidah Al-afasi
Mishari Al-afasi
Surah Maidah Yasser Al Dosari
Yasser Al Dosari


Monday, May 13, 2024

لا تنسنا من دعوة صالحة بظهر الغيب