Surah Muminun aya 18 , Swahili translation of the meaning Ayah.

  1. Arabic
  2. tafsir
  3. mp3
  4. English
Quran in Swahili QUR,ANI TUKUFU na tafsiri ya maana yake kwenye lugha ya Kiswahili - Ali Muhsen Alberwany & English - Sahih International : Surah Muminun aya 18 in arabic text(The Believers).
  
   

﴿وَأَنزَلْنَا مِنَ السَّمَاءِ مَاءً بِقَدَرٍ فَأَسْكَنَّاهُ فِي الْأَرْضِ ۖ وَإِنَّا عَلَىٰ ذَهَابٍ بِهِ لَقَادِرُونَ
[ المؤمنون: 18]

Na tumeteremsha kutoka mbinguni maji kwa kiasi na tukayatuliza katika ardhi. Na hakika Sisi tunaweza kuyaondoa.

Surah Al-Muminun in Swahili

Swahili Translation - Al-Barwani

English - Sahih International


And We have sent down rain from the sky in a measured amount and settled it in the earth. And indeed, We are Able to take it away.


Tafsiri ya maana yake kwenye lugha ya Kiswahili


Na tumeteremsha kutoka mbinguni maji kwa kiasi na tukayatuliza katika ardhi. Na hakika Sisi tunaweza kuyaondoa.


Na Sisi tumeteremsha kutoka mbinguni mvua kwa hikima na kipimo katika umbo lake na kuteremka kwake. Na kusahilisha kwa ajili ya manufaa tumeijaalia ikae juu ya uso wa ardhi na ndani yake chini. Na Sisi hakika ni wenye kuweza kuiondoa wasipate kunafiika nayo. Lakini hatukufanya hayo kwa kukuoneeni huruma. Basi muaminini Mwenye kuiumba na mumshukuru. -Na tumeteremsha kutoka mbinguni maji kwa kiasi na tukayatuliza katika ardhi. Na hakika Sisi tunaweza kuyaondoa.- Aya hii tukufu inaashiria maana ya kisayansi yenye kukhusu mzunguko wa maji katika ardhi. Yajuulikana kuwa mvuke unao paa kutoka baharini hupelekea kufanyika mawingu ambayo ndiyo huteremsha mvua. Na hivyo ndio chanzo cha maji matamu juu ya uso wa ardhi, na ndio chombo cha msingi cha uhai wa ardhini. Kutokana na mvua ndio huzuka mito inayo zua uhai katika sehemu kamwe zisio pitikiwa na mvua. Kisha hiyo mito inamiminika baharini, na khulka inarejea tena kutoka baharini kwenda angani na kwendea nchi kavu, na kisha kuingia baharini mara ya pili. Isipo kuwa baadhi ya hayo maji ya mvua yanatulia na yanazama kuhifadhika katika mahodhi ya chini ya ardhi, yakawekeka kwa muda mrefu. Mfano wa hayo ni hayo maji yanayo patikana chini ya Jangwa la Magharibi katika Libya, ambayo yamegunduliwa na watafiti hivi karibuni kutokana na asli yake ya kale. Na huenda maji kama haya yalio hifadhika chini yakapatwa na mabadiliko ya joto wanayo yaita wataalamu wa ilimu ya tabaka za ardhi (Geology) kuwa ni Mikondo ya Jiolojia, ikenda hiyo na maji mpaka pahala pengine pakavu, ikaleta uhai baada ya kuwa ni maiti. Na Aya hii inaonyesha hikima kubwa ya uenezaji wa maji kwa kipimo, yaani kipimo cha haki na hikima, kwa ajili ya kuleta manufaa na kupinga madhara. Na tena maana nyengine ya Aya tukufu ni kufahamisha apendavyo Mwenye Kuumba, Aliye tukuka, navyo ni kujaalia yawepo maji ya kiasi maalumu katika bahari za ulimwengu kutosha kuwepo mizani ya joto la kufaa katika sayari hii, na ili isiwepo khitilafu kubwa mno baina ya joto la siku za joto, na baridi ya siku za baridi, hata ikawa ni muhali kubakia uhai, kama ilivyo katika sayari nyengine na katika mwezi. Kadhaalika maji ya ardhi yanateremka kwa kiasi maalumu, hayazidi yakafunika ardhi yote, wala hayatindikii sana hata yasipatikane hata kidogo kunyweshea baadhi ya nchi kavu.

English Türkçe Indonesia
Русский Français فارسی
تفسير Bengali Urdu

listen to Verse 18 from Muminun


Ayats from Quran in Swahili

  1. Bila ya shaka mnaye niitia kumuabudu hastahiki wito duniani wala Akhera. Na hakika marejeo yetu
  2. Atawaongoza na awatengezee hali yao.
  3. Na kutokana na matunda ya mitende na mizabibu mnatengeneza ulevi na riziki nzuri. Hakika katika
  4. Lakini walio bobea katika ilimu miongoni mwao, na Waumini, wanayaamini uliyo teremshiwa wewe, na yaliyo
  5. Na ikiwa unajikurupusha nao, nawe unatafuta rehema ya Mola wako Mlezi unayo itaraji, basi sema
  6. Na Mola wako Mlezi amemfunulia nyuki: Jitengenezee majumba yako katika milima, na katika miti, na
  7. Basi nawacheke kidogo; watalia sana. Hayo ni malipo ya yale waliyo kuwa wakiyachuma.
  8. Nyinyi - ulipo kusibuni msiba ambao nyinyi mmekwisha watia mara mbili mfano wa huo -
  9. Basi hizo nyumba zao ni tupu kwa sababu ya walivyo dhulumu. Hakika bila ya shaka
  10. Hiki ni Kitabu kisichokuwa na shaka ndani yake; ni uwongofu kwa wachamungu,

Quran Surah in Swahili :

Al-Baqarah Al-'Imran An-Nisa'
Al-Ma'idah Yusuf Ibrahim
Al-Hijr Al-Kahf Maryam
Al-Hajj Al-Qasas Al-'Ankabut
As-Sajdah Ya Sin Ad-Dukhan
Al-Fath Al-Hujurat Qaf
An-Najm Ar-Rahman Al-Waqi'ah
Al-Hashr Al-Mulk Al-Haqqah
Al-Inshiqaq Al-A'la Al-Ghashiyah

Download Surah Muminun with the voice of the most famous Quran reciters :

Surah Muminun mp3 : choose the reciter to listen and download the chapter Muminun Complete with high quality
Surah Muminun Ahmed El Agamy
Ahmed Al Ajmy
Surah Muminun Bandar Balila
Bandar Balila
Surah Muminun Khalid Al Jalil
Khalid Al Jalil
Surah Muminun Saad Al Ghamdi
Saad Al Ghamdi
Surah Muminun Saud Al Shuraim
Saud Al Shuraim
Surah Muminun Abdul Basit Abdul Samad
Abdul Basit
Surah Muminun Abdul Rashid Sufi
Abdul Rashid Sufi
Surah Muminun Abdullah Basfar
Abdullah Basfar
Surah Muminun Abdullah Awwad Al Juhani
Abdullah Al Juhani
Surah Muminun Fares Abbad
Fares Abbad
Surah Muminun Maher Al Muaiqly
Maher Al Muaiqly
Surah Muminun Muhammad Siddiq Al Minshawi
Al Minshawi
Surah Muminun Al Hosary
Al Hosary
Surah Muminun Al-afasi
Mishari Al-afasi
Surah Muminun Yasser Al Dosari
Yasser Al Dosari


Friday, May 10, 2024

لا تنسنا من دعوة صالحة بظهر الغيب