Surah Muminun aya 27 , Swahili translation of the meaning Ayah.

  1. Arabic
  2. tafsir
  3. mp3
  4. English
Quran in Swahili QUR,ANI TUKUFU na tafsiri ya maana yake kwenye lugha ya Kiswahili - Ali Muhsen Alberwany & English - Sahih International : Surah Muminun aya 27 in arabic text(The Believers).
  
   

﴿فَأَوْحَيْنَا إِلَيْهِ أَنِ اصْنَعِ الْفُلْكَ بِأَعْيُنِنَا وَوَحْيِنَا فَإِذَا جَاءَ أَمْرُنَا وَفَارَ التَّنُّورُ ۙ فَاسْلُكْ فِيهَا مِن كُلٍّ زَوْجَيْنِ اثْنَيْنِ وَأَهْلَكَ إِلَّا مَن سَبَقَ عَلَيْهِ الْقَوْلُ مِنْهُمْ ۖ وَلَا تُخَاطِبْنِي فِي الَّذِينَ ظَلَمُوا ۖ إِنَّهُم مُّغْرَقُونَ
[ المؤمنون: 27]

Tukampa wahyi: Unda jahazi mbele ya macho yetu na uwongozi wetu! Basi itapo fika amri yetu na ikafurika tanuri, hapo waingize ndani yake wa kila namna dume na jike, na ahali zako, isipo kuwa yule ambaye katika wao juu yake imekwisha tangulia kauli. Wala usinitajie hao walio dhulumu. Kwani hao bila ya shaka watazamishwa.

Surah Al-Muminun in Swahili

Swahili Translation - Al-Barwani

English - Sahih International


So We inspired to him, "Construct the ship under Our observation, and Our inspiration, and when Our command comes and the oven overflows, put into the ship from each [creature] two mates and your family, except those for whom the decree [of destruction] has proceeded. And do not address Me concerning those who have wronged; indeed, they are to be drowned.


Tafsiri ya maana yake kwenye lugha ya Kiswahili


Tukampa wahyi: Unda jahazi mbele ya macho yetu na uwongozi wetu! Basi itapo fika amri yetu na ikafurika tanuri, hapo waingize ndani yake wa kila namna dume na jike, na ahali zako, isipo kuwa yule ambaye katika wao juu yake imekwisha tangulia kauli. Wala usinitajie hao walio dhulumu. Kwani hao bila ya shaka watazamishwa.


Tukamwambia kwa njia ya ufunuo (wahyi): Unda jahazi, nawe utalindwa na uangalizi wetu. Shari yao haitokupata, nasi tutakuongoza katika kazi yako. Na ikifikilia miadi ya kuwaadhibu, na ukaona tanuri inafoka maji kwa amri yetu, basi waingize katika jahazi katika kila namna ya viumbe vilivyo hai dume na jike. Na waingize ahali zako, isipo kuwa walio kwisha thibitika adhabu yao kwa kukosa kwao Imani. Wala usiniombe kuwaokoa wale walio dhulumu nafsi zao na wakawadhulumu na wengineo kwa ukafiri na uasi. Kwani Mimi nimewahukumia kuwazamisha kwa sababu ya dhulma yao ya ushirikina na uasi. -Tukampa wahyi: Unda jahazi mbele ya macho yetu na uwongozi wetu! Basi itapo fika amri yetu na ikafurika tanuri, hapo waingize ndani yake wa kila namna dume na jike, na ahali zako, isipo kuwa yule ambaye katika wao juu yake imekwisha tangulia kauli. Wala usinitajie hao walio dhulumu. Kwani hao bila ya shaka watazamishwa.- Hakika haya maelezo ya Tofani lilio tokea ijapo kuwa ni kwa mukhtasari tu katika hizi Aya tukufu, kwa mwenye akili ya kuzingatia yana maana na mambo ya hakika mengi ya ki-ilimu ambayo yanawapitia watu wengi. Na -tanuri- kwa lugha ni jiko la kuchomea mikate, au pia ni uso wa ardhi na kila chenye kutimbuka maji, na kila penye mkusanyiko wa maji. Na si wepesi kusema kwa yakini taarikhi ya hiyo Tofani, kwani zilitokea tofani nyingi zama za kale, kama katika Babilonia, Bara Hindi na Amerika. Na zipo baadhi ya hadithi za kienyeji mbali mbali zinazo taja khabari ya Tofani. Lakini haielekei kuwa hadithi hizo ndio zimekhusu hii Tofani kubwa au Tofani ya Nuhu. Uchunguzi umethibitisha na pia zimeonekana tofani nyingi ulimwenguni. Na tofani ya mwisho ya ulimwengu mzima ilikuwa sababu yake ni kumalizika kipindi cha barafu cha mwisho, na kuyayuka barafu nyingi ya kaskazini kabisa na kusini kabisa kwa dunia. Na sisi hatujui kwa yakini lini mizani iligeuka na tanuri ikafurika - yaani uso wa ardhi - kwa kupanda kwa ghafla kwa hivyo kuyayuka barafu, hata yakapanda juu maji ya bahari na ya kamwagika maji. Yafaa kutaja kuwa kuyayuka barafu ya zama za barafu za mwisho kulileta hali ya hewa yenye mvua nyingi sana katika sehemu za dunia zilio mbali na huko kaskazini na kusini kabisa kwa ulimwengu, kama vile katika Bahari ya Kati (Mediterenian). Vyo vyote vile ilivyo inakubalika kuwa hatuna ushahidi wa kuweza kusema lini khasa zilikuwa hizo zama za Nuhu na kaumu yake. Yaliyo dhaahiri kuwa yote hayo ni muujiza wa Mwenyezi Mungu. Na katika miujiza ni kuwa Nuhu aliwanasihi watu wake na akawaonya na ghadhabu ya Mwenyezi Mungu. Na Mwenyezi Mungu akafunua kuwa atawazamisha ikiwa hawakutengenea. Na tena akamfunulia aunde marikebu. Kisha ikaja amri ya Mwenyezi Mungu, na mizani ikapinduka, na tanuri ikafurika, ikamiminika mvua kuthibitisha aliyo yasema Mwenyezi Mungu kumwambia Nuhu ya kwamba Mwenyezi Mungu anajua kuwa hatoamini mtu katika kaumu yake baada ya wale walio kwisha amini.

English Türkçe Indonesia
Русский Français فارسی
تفسير Bengali Urdu

listen to Verse 27 from Muminun


Ayats from Quran in Swahili

  1. Na baada yake walimfanya ndama kutokana na mapambo yao (kumuabudu), kiwiliwili tu kilicho kuwa na
  2. Wanamshukia kila mzushi mkubwa mwingi wa dhambi.
  3. Na Mola wako Mlezi ni Msamehevu Mwenye rehema. Lau angeli wachukulia kwa mujibu waliyo yachuma,
  4. Wala si kauli ya mtunga mashairi. Ni machache sana mnayo yaamini.
  5. Na alipo watengenezea tayari haja yao alisema: Nileteeni ndugu yenu kwa baba. Je! Hamwoni ya
  6. Na rejeeni kwa Mola wenu Mlezi, na silimuni kwake, kabla ya kukujieni adhabu. Kisha hapo
  7. Hakika Mwenyezi Mungu yu pamoja na wenye kumcha, na watendao mema.
  8. Je! Mola wenu Mlezi amekuteulieni wavulana, na Yeye akawafanya Malaika ni banati zake? Kwa hakika
  9. Na kwa yakini tulimtuma Musa pamoja na Ishara zetu na uthibitisho ulio wazi,
  10. Isipo kuwa njia ya Jahannamu. Humo watadumu milele. Na hayo kwa Mwenyezi Mungu ni mepesi.

Quran Surah in Swahili :

Al-Baqarah Al-'Imran An-Nisa'
Al-Ma'idah Yusuf Ibrahim
Al-Hijr Al-Kahf Maryam
Al-Hajj Al-Qasas Al-'Ankabut
As-Sajdah Ya Sin Ad-Dukhan
Al-Fath Al-Hujurat Qaf
An-Najm Ar-Rahman Al-Waqi'ah
Al-Hashr Al-Mulk Al-Haqqah
Al-Inshiqaq Al-A'la Al-Ghashiyah

Download Surah Muminun with the voice of the most famous Quran reciters :

Surah Muminun mp3 : choose the reciter to listen and download the chapter Muminun Complete with high quality
Surah Muminun Ahmed El Agamy
Ahmed Al Ajmy
Surah Muminun Bandar Balila
Bandar Balila
Surah Muminun Khalid Al Jalil
Khalid Al Jalil
Surah Muminun Saad Al Ghamdi
Saad Al Ghamdi
Surah Muminun Saud Al Shuraim
Saud Al Shuraim
Surah Muminun Abdul Basit Abdul Samad
Abdul Basit
Surah Muminun Abdul Rashid Sufi
Abdul Rashid Sufi
Surah Muminun Abdullah Basfar
Abdullah Basfar
Surah Muminun Abdullah Awwad Al Juhani
Abdullah Al Juhani
Surah Muminun Fares Abbad
Fares Abbad
Surah Muminun Maher Al Muaiqly
Maher Al Muaiqly
Surah Muminun Muhammad Siddiq Al Minshawi
Al Minshawi
Surah Muminun Al Hosary
Al Hosary
Surah Muminun Al-afasi
Mishari Al-afasi
Surah Muminun Yasser Al Dosari
Yasser Al Dosari


Friday, May 10, 2024

لا تنسنا من دعوة صالحة بظهر الغيب