Surah Raad aya 4 , Swahili translation of the meaning Ayah.
﴿وَفِي الْأَرْضِ قِطَعٌ مُّتَجَاوِرَاتٌ وَجَنَّاتٌ مِّنْ أَعْنَابٍ وَزَرْعٌ وَنَخِيلٌ صِنْوَانٌ وَغَيْرُ صِنْوَانٍ يُسْقَىٰ بِمَاءٍ وَاحِدٍ وَنُفَضِّلُ بَعْضَهَا عَلَىٰ بَعْضٍ فِي الْأُكُلِ ۚ إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَآيَاتٍ لِّقَوْمٍ يَعْقِلُونَ﴾
[ الرعد: 4]
Na katika ardhi vimo vipande vilivyo karibiana, na zipo bustani za mizabibu, na mimea mingine, na mitende yenye kuchipua kwenye shina moja na isio chipua kwenye shina moja, nayo inatiliwa maji yale yale. Na tunaifanya baadhi yao bora kuliko mengine katika kula. Hakika katika hayo zimo ishara kwa watu wanao tia mambo akilini.
Surah Ar-Rad in SwahiliSwahili Translation - Al-Barwani
English - Sahih International
And within the land are neighboring plots and gardens of grapevines and crops and palm trees, [growing] several from a root or otherwise, watered with one water; but We make some of them exceed others in [quality of] fruit. Indeed in that are signs for a people who reason.
Tafsiri ya maana yake kwenye lugha ya Kiswahili
Na katika ardhi vimo vipande vilivyo karibiana, na zipo bustani za mizabibu, na mimea mingine, na mitende yenye kuchipua kwenye shina moja na isio chipua kwenye shina moja, nayo inatiliwa maji yale yale. Na tunaifanya baadhi yao bora kuliko mengine katika kula. Hakika katika hayo zimo ishara kwa watu wanao tia mambo akilini.
Na hakika hiyo ardhi nafsi yake ina maajabu. Ndani yake vipo vipande vilivyo karibiana, navyo juu ya hivyo vina udongo mbali mbali. Vingine ardhi yaabisi, na vingine vya rutba, ijapo kuwa ni udongo ule ule. Ndani yake yapo mabustani yaliyo jaa miti ya mizabibu, na ndani yake mazao mengine yanavunwa, na mitende yenye kuzaa, nayo ama iliyo kusanyika au iko mbali mbali. Na yote hayo ijapo kuwa inanyweshwa maji yale yale yanakhitalifiana kwa utamu wao. Na hakika katika ajabu hizi zipo dalili wazi za kuonyesha uwezo wa Mwenyezi Mungu kwa mwenye akili ya kufikiria. Aya hii tukufu inaonyesha ilimu ya ardhi (Geology) na ilimu ya mazingira (Ecology) na athari yao juu ya sifa za mimea. Inajuulikana katika ilimu kuwa rutuba ya ardhi inategemea juu ya chembe chembe za maadeni zinazo khitalifiana kwa namna na ukubwa, na maji yanayo toka kwenye mvua, na hewa, na vitu vyenye asili ya uhai, kama mimea na vyenginevyo, ambavyo hupatikana juu ya udongo au ndani yake. Huwapo hivyo kwa mamilioni vidogo vidogo hata havionekani kwa jicho tu. Kwa jumla ukizingatia haya utaona yanaonyesha uwezo wa Muumba na busara ya uumbaji, kwani ardhi kama wasemavyo wakulimu inakhitalifiana kila shubiri. Na inajuulikana kwa wanazuoni wa sayansi kuwa ukipatikana upungufu katika hivyo vitu vya msingi katika udongo basi hudhihirisha upungufu wake katika mimea, na kwa hivyo wakulima hujalizia upungufu huo kwa kutia mbolea mbali mbali na hutengeneza hali ya mazingira. Na hayo yana athari zake juu ya mazao ikiwa kwa mmea wa namna moja au namna mbali. Ametakasika Mwenyezi Mungu ambaye katika mikono yake upo ufalme wa kila kitu, naye ni Muweza wa kila kitu.
English | Türkçe | Indonesia |
Русский | Français | فارسی |
تفسير | Bengali | Urdu |
Ayats from Quran in Swahili
- Hao wanao fanya kuwa pamoja na Mwenyezi Mungu yupo mungu mwingine. Basi, watakuja jua!
- Na kwa yakini tumeziumba juu yenu njia saba. Nasi hatukuwa wenye kughafilika na viumbe.
- Badala ya Mwenyezi Mungu. Waongozeni njia ya Jahannamu!
- Enyi wanangu! Nendeni mkamtafute Yusuf na nduguye, wala msikate tamaa na faraji ya Mwenyezi Mungu.
- Sema: Ewe Mwenyezi Mungu! Muumba mbingu na ardhi! Mjuzi wa yasiyo onekana na yanayo onekana!
- Anaye kufuru basi ukafiri wake utakuwa juu yake mwenyewe, na anaye tenda mema, basi wanazitengezea
- Enyi mlio amini! Wanaume wasiwadharau wanaume wenzao, wala wanawake wasiwadharau wanawake wenzao. Huenda hao wakawa
- Isipo kuwa wale walio tubu baada ya hayo na wakatengenea; kwani bila ya shaka Mwenyezi
- Piganeni na wasio muamini Mwenyezi Mungu wala Siku ya Mwisho, wala hawaharimishi alivyo harimisha Mwenyezi
- Wala hawatakuwa na walinzi wa kuwanusuru mbele ya Mwenyezi Mungu. Na ambaye Mwenyezi Mungu amemwacha
Quran Surah in Swahili :
Download Surah Raad with the voice of the most famous Quran reciters :
Surah Raad mp3 : choose the reciter to listen and download the chapter Raad Complete with high quality
Ahmed Al Ajmy
Bandar Balila
Khalid Al Jalil
Saad Al Ghamdi
Saud Al Shuraim
Abdul Basit
Ammar Al-Mulla
Abdullah Basfar
Abdullah Al Juhani
Fares Abbad
Maher Al Muaiqly
Al Minshawi
Al Hosary
Mishari Al-afasi
Yasser Al Dosari
Please remember us in your sincere prayers