Surah Maidah aya 95 , Swahili translation of the meaning Ayah.

  1. Arabic
  2. tafsir
  3. mp3
  4. English
Quran in Swahili QUR,ANI TUKUFU na tafsiri ya maana yake kwenye lugha ya Kiswahili - Ali Muhsen Alberwany & English - Sahih International : Surah Maidah aya 95 in arabic text(The Table).
  
   

﴿يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا لَا تَقْتُلُوا الصَّيْدَ وَأَنتُمْ حُرُمٌ ۚ وَمَن قَتَلَهُ مِنكُم مُّتَعَمِّدًا فَجَزَاءٌ مِّثْلُ مَا قَتَلَ مِنَ النَّعَمِ يَحْكُمُ بِهِ ذَوَا عَدْلٍ مِّنكُمْ هَدْيًا بَالِغَ الْكَعْبَةِ أَوْ كَفَّارَةٌ طَعَامُ مَسَاكِينَ أَوْ عَدْلُ ذَٰلِكَ صِيَامًا لِّيَذُوقَ وَبَالَ أَمْرِهِ ۗ عَفَا اللَّهُ عَمَّا سَلَفَ ۚ وَمَنْ عَادَ فَيَنتَقِمُ اللَّهُ مِنْهُ ۗ وَاللَّهُ عَزِيزٌ ذُو انتِقَامٍ
[ المائدة: 95]

Enyi mlio amini! Msiue wanyama wa kuwinda nanyi mmeharimia katika Hija. Na miongoni mwenu atakaye muuwa makusudi, basi malipo yake yatakuwa kwa kuchinja kilicho sawa na alicho kiuwa, katika mifugo, kama wanavyo hukumu waadilifu wawili miongoni mwenu. Mnyama huyo apelekwe kwenye Al Kaaba, au kutoa kafara kwa kuwalisha masikini; au badala ya hayo ni kufunga, ili aonje ubaya wa jambo lake hili. Mwenyezi Mungu amekwisha yafuta yaliyo pita; lakini atakaye fanya tena Mwenyezi Mungu atampa adhabu. Na Mwenyezi Mungu ndiye Mwenye nguvu na Mwenye kuadhibu.

Surah Al-Maidah in Swahili

Swahili Translation - Al-Barwani

English - Sahih International


O you who have believed, do not kill game while you are in the state of ihram. And whoever of you kills it intentionally - the penalty is an equivalent from sacrificial animals to what he killed, as judged by two just men among you as an offering [to Allah] delivered to the Ka'bah, or an expiation: the feeding of needy people or the equivalent of that in fasting, that he may taste the consequence of his deed. Allah has pardoned what is past; but whoever returns [to violation], then Allah will take retribution from him. And Allah is Exalted in Might and Owner of Retribution.


Tafsiri ya maana yake kwenye lugha ya Kiswahili


Enyi mlio amini! Msiue wanyama wa kuwinda nanyi mmeharimia katika Hija. Na miongoni mwenu atakaye muuwa makusudi, basi malipo yake yatakuwa kwa kuchinja kilicho sawa na alicho kiuwa, katika mifugo, kama wanavyo hukumu waadilifu wawili miongoni mwenu. Mnyama huyo apelekwe kwenye Al Kaaba, au kutoa kafara kwa kuwalisha masikini; au badala ya hayo ni kufunga, ili aonje ubaya wa jambo lake hili. Mwenyezi Mungu amekwisha yafuta yaliyo pita; lakini atakaye fanya tena Mwenyezi Mungu atampa adhabu. Na Mwenyezi Mungu ndiye Mwenye nguvu na Mwenye kuadhibu.


Enyi ambao mmeamini! Msiuwe nyama wa kuwinda nanyi mmenuia Hija na Umra na mmo kuzitimiliza. Na mwenye kumuuwa mnyama kama huyo kwa kukusudia basi itampasa atoe fidiya mfano wa mnyama aliye muuwa, ikiwa katika ngamia, ngombe au kondoo. Na hujuulikana huyo mfano wake kwa kukadiriwa na watu wawili waadilifu kati yenu, wahukumu na wawape mafakiri kwenye Al Kaaba, au atoe badala yake awape, au atoe chakula kadiri ya yule mnyama kuwapa mafakiri. Kila fakiri apewe chakula cha kumtosha kutwa yake. Hayo ndio kuondoa dhambi za kuwinda kuliko katazwa. Au badala ya hayo yote, afunge idadi ya siku za kadri ya wale masikini iliyo mbidi kuwalisha lau angewalisha. Na Mwenyezi Mungu amelazimisha hayo ili huyo mwenye kufanya lile kosa apate kuhisi matokeo ya kosa lake na uwovu wa malipo yake. Mwenyezi Mungu, lakini, amesamehe ukhalifu ulio tendekea kabla ya jambo hilo halijaharimishwa. Na mwenye kurejea tena kufanya uovu baada ya kujua kuwa ni haramu, basi hakika Mwenyezi Mungu atampa adabu kwa kitendo chake, naye Mwenyezi Mungu ni Mwenye kushinda hashindiki, Mkali wa kumuadhibu anaye kakamia kutenda dhambi. (Tunaona kuwa Uislamu ulianzisha kulinda mazingara, na utajiri wa asili tangu hapo kale. Kutokana na kuhifadhiwa wanyama na ndege wa porini huko Makka, ndio hii leo tunaona zipo nyanda na mapori yanayo hifadhiwa wanyama wake, kwa mujibu wa utaalamu wa kisasa.)

English Türkçe Indonesia
Русский Français فارسی
تفسير Bengali Urdu

listen to Verse 95 from Maidah


Ayats from Quran in Swahili

  1. Wamesema: Mwenyezi Mungu ana mwana. Subhanahu, Aliye takasika! Yeye ni Mkwasi, Mwenye Kujitosheleza. Vyote viliomo
  2. Hakika hii bila ya shaka ni Qur'ani Tukufu,
  3. Hakika tumekuhadharisheni adhabu iliyo karibu kufika; Siku ambayo mtu atakapo ona yaliyo tangulizwa na mikono
  4. Hakika vinyama vilio viovu kabisa mbele ya Mwenyezi Mungu ni wale wanao kufuru, basi hao
  5. Na Shet'ani atasema itapo katwa hukumu: Hakika Mwenyezi Mungu alikuahidini ahadi ya kweli. Nami nalikuahidini;
  6. Kwani hawaoni yaliyo mbele yao na yaliyo nyuma yao ya mbingu na ardhi? Tungeli penda
  7. Lakini makundi yakakhitalifiana wao kwa wao. Basi ole wao hao walio kufuru kwa kuhudhuria Siku
  8. Wala si mzaha.
  9. Mpeleke kesho pamoja nasi, ale kwa furaha na acheze; na bila ya shaka sisi tutamhifadhi.
  10. Au tumewaumba Malaika kuwa ni wanawake, na wao wakashuhudia?

Quran Surah in Swahili :

Al-Baqarah Al-'Imran An-Nisa'
Al-Ma'idah Yusuf Ibrahim
Al-Hijr Al-Kahf Maryam
Al-Hajj Al-Qasas Al-'Ankabut
As-Sajdah Ya Sin Ad-Dukhan
Al-Fath Al-Hujurat Qaf
An-Najm Ar-Rahman Al-Waqi'ah
Al-Hashr Al-Mulk Al-Haqqah
Al-Inshiqaq Al-A'la Al-Ghashiyah

Download Surah Maidah with the voice of the most famous Quran reciters :

Surah Maidah mp3 : choose the reciter to listen and download the chapter Maidah Complete with high quality
Surah Maidah Ahmed El Agamy
Ahmed Al Ajmy
Surah Maidah Bandar Balila
Bandar Balila
Surah Maidah Khalid Al Jalil
Khalid Al Jalil
Surah Maidah Saad Al Ghamdi
Saad Al Ghamdi
Surah Maidah Saud Al Shuraim
Saud Al Shuraim
Surah Maidah Abdul Basit Abdul Samad
Abdul Basit
Surah Maidah Abdul Rashid Sufi
Abdul Rashid Sufi
Surah Maidah Abdullah Basfar
Abdullah Basfar
Surah Maidah Abdullah Awwad Al Juhani
Abdullah Al Juhani
Surah Maidah Fares Abbad
Fares Abbad
Surah Maidah Maher Al Muaiqly
Maher Al Muaiqly
Surah Maidah Muhammad Siddiq Al Minshawi
Al Minshawi
Surah Maidah Al Hosary
Al Hosary
Surah Maidah Al-afasi
Mishari Al-afasi
Surah Maidah Yasser Al Dosari
Yasser Al Dosari


Monday, May 13, 2024

لا تنسنا من دعوة صالحة بظهر الغيب