La sourate Al-Balad en Swahili
لَا أُقْسِمُ بِهَٰذَا الْبَلَدِ(1) Naapa kwa Mji huu! |
وَأَنتَ حِلٌّ بِهَٰذَا الْبَلَدِ(2) Nawe unaukaa Mji huu. |
وَوَالِدٍ وَمَا وَلَدَ(3) Na naapa kwa mzazi na alicho kizaa. |
لَقَدْ خَلَقْنَا الْإِنسَانَ فِي كَبَدٍ(4) Hakika tumemuumba mtu katika taabu. |
أَيَحْسَبُ أَن لَّن يَقْدِرَ عَلَيْهِ أَحَدٌ(5) Ati anadhani hapana yeyote ataye muweza? |
يَقُولُ أَهْلَكْتُ مَالًا لُّبَدًا(6) Anasema: Nimeteketeza chungu ya mali. |
أَيَحْسَبُ أَن لَّمْ يَرَهُ أَحَدٌ(7) Ati anadhani ya kuwa hapana yeyote anaye mwona? |
أَلَمْ نَجْعَل لَّهُ عَيْنَيْنِ(8) Kwani hatukumpa macho mawili? |
وَلِسَانًا وَشَفَتَيْنِ(9) Na ulimi, na midomo miwili? |
وَهَدَيْنَاهُ النَّجْدَيْنِ(10) Na tukambainishia zote njia mbili? |
فَلَا اقْتَحَمَ الْعَقَبَةَ(11) Lakini hakujitoma kwenye njia ya vikwazo vya milimani. |
وَمَا أَدْرَاكَ مَا الْعَقَبَةُ(12) Na nini kitakujuvya ni nini njia ya vikwazo vya milimani? |
فَكُّ رَقَبَةٍ(13) Kumkomboa mtumwa; |
أَوْ إِطْعَامٌ فِي يَوْمٍ ذِي مَسْغَبَةٍ(14) Au kumlisha siku ya njaa |
يَتِيمًا ذَا مَقْرَبَةٍ(15) Yatima aliye jamaa, |
أَوْ مِسْكِينًا ذَا مَتْرَبَةٍ(16) Au masikini aliye vumbini. |
ثُمَّ كَانَ مِنَ الَّذِينَ آمَنُوا وَتَوَاصَوْا بِالصَّبْرِ وَتَوَاصَوْا بِالْمَرْحَمَةِ(17) Tena awe miongoni mwa walio amini na wakausiana kusubiri na wakausiana kuhurumiana. |
أُولَٰئِكَ أَصْحَابُ الْمَيْمَنَةِ(18) Hao ndio watu wa kheri wa kuliani. |
وَالَّذِينَ كَفَرُوا بِآيَاتِنَا هُمْ أَصْحَابُ الْمَشْأَمَةِ(19) Lakini walio zikataa Ishara zetu, hao ndio watu wa shari wa kushotoni. |
عَلَيْهِمْ نَارٌ مُّؤْصَدَةٌ(20) Juu yao utakuwa Moto ulio fungiwa kila upande. |
Plus de sourates en Swahili :
Téléchargez la sourate avec la voix des récitants du Coran les plus célèbres :
Téléchargez le fichier mp3 de la sourate Al-Balad : choisissez le récitateur pour écouter et télécharger la sourate Al-Balad complète en haute qualité.
Ahmed Al Ajmy
Bandar Balila
Khalid Al Jalil
Saad Al Ghamdi
Saud Al Shuraim
Abdul Basit
Abdul Rashid Sufi
Abdullah Basfar
Abdullah Al Juhani
Fares Abbad
Maher Al Muaiqly
Al Minshawi
Al Hosary
Mishari Al-afasi
Yasser Al Dosari
Donnez-nous une invitation valide




