Перевод суры Нух на суахили язык

  1. Сура mp3
  2. Другие суры
  3. суахили
Священный Коран | Перевод Корана | Язык суахили | Сура Нух | نوح - получите точный и надежный суахили текст сейчас - Количество аятов: 28 - Номер суры в мушафе: 71 - Значение названия суры на русском языке: Noah.

إِنَّا أَرْسَلْنَا نُوحًا إِلَىٰ قَوْمِهِ أَنْ أَنذِرْ قَوْمَكَ مِن قَبْلِ أَن يَأْتِيَهُمْ عَذَابٌ أَلِيمٌ(1)

 Hakika Sisi tulimtuma Nuh'u kwa watu wake: Uwaonye kaumu yako kabla ya kuwafikia adhabu chungu.

قَالَ يَا قَوْمِ إِنِّي لَكُمْ نَذِيرٌ مُّبِينٌ(2)

 Akasema: Enyi watu wangu! Kwa hakika mimi ni mwonyaji wa dhaahiri kwenu,

أَنِ اعْبُدُوا اللَّهَ وَاتَّقُوهُ وَأَطِيعُونِ(3)

 Ya kwamba mumuabudu Mwenyezi Mungu, na mumche Yeye, na mumt'ii.

يَغْفِرْ لَكُم مِّن ذُنُوبِكُمْ وَيُؤَخِّرْكُمْ إِلَىٰ أَجَلٍ مُّسَمًّى ۚ إِنَّ أَجَلَ اللَّهِ إِذَا جَاءَ لَا يُؤَخَّرُ ۖ لَوْ كُنتُمْ تَعْلَمُونَ(4)

 Atakughufirieni madhambi yenu, na atakuakhirisheni mpaka muda ulio wekwa. Hakika muda wa Mwenyezi Mungu utapo fika haucheleweshwi. Laiti mngejua!

قَالَ رَبِّ إِنِّي دَعَوْتُ قَوْمِي لَيْلًا وَنَهَارًا(5)

 Akasema: Ee Mola wangu Mlezi! Hakika mimi nimewaita watu wangu usiku na mchana,

فَلَمْ يَزِدْهُمْ دُعَائِي إِلَّا فِرَارًا(6)

 Lakini wito wangu haukuwazidisha ila kukimbia.

وَإِنِّي كُلَّمَا دَعَوْتُهُمْ لِتَغْفِرَ لَهُمْ جَعَلُوا أَصَابِعَهُمْ فِي آذَانِهِمْ وَاسْتَغْشَوْا ثِيَابَهُمْ وَأَصَرُّوا وَاسْتَكْبَرُوا اسْتِكْبَارًا(7)

 Na hakika mimi kila nilipo waita ili upate kuwaghufiria, walijiziba masikio yao kwa vidole vyao, na wakajigubika nguo zao, na wakakamia, na wakatakabari vikubwa mno!

ثُمَّ إِنِّي دَعَوْتُهُمْ جِهَارًا(8)

 Tena niliwaita kwa uwazi,

ثُمَّ إِنِّي أَعْلَنتُ لَهُمْ وَأَسْرَرْتُ لَهُمْ إِسْرَارًا(9)

 Kisha nikawatangazia kwa kelele, tena nikasema nao kwa siri.

فَقُلْتُ اسْتَغْفِرُوا رَبَّكُمْ إِنَّهُ كَانَ غَفَّارًا(10)

 Nikasema: Ombeni msamaha kwa Mola wenu Mlezi; hakika Yeye ni Mwingi wa kusamehe.

يُرْسِلِ السَّمَاءَ عَلَيْكُم مِّدْرَارًا(11)

 Atakuleteeni mvua inyeshe mfululizo.

وَيُمْدِدْكُم بِأَمْوَالٍ وَبَنِينَ وَيَجْعَل لَّكُمْ جَنَّاتٍ وَيَجْعَل لَّكُمْ أَنْهَارًا(12)

 Na atakupeni mali na wana, na atakupeni mabustani na atakufanyieni mito.

مَّا لَكُمْ لَا تَرْجُونَ لِلَّهِ وَقَارًا(13)

 Mna nini hamweki heshima ya Mwenyezi Mungu?

وَقَدْ خَلَقَكُمْ أَطْوَارًا(14)

 Na hali Yeye kakuumbeni daraja baada ya daraja?

أَلَمْ تَرَوْا كَيْفَ خَلَقَ اللَّهُ سَبْعَ سَمَاوَاتٍ طِبَاقًا(15)

 Kwani hamwoni jinsi Mwenyezi Mungu alivyo ziumba mbingu saba kwa matabaka?

وَجَعَلَ الْقَمَرَ فِيهِنَّ نُورًا وَجَعَلَ الشَّمْسَ سِرَاجًا(16)

 Na akaufanya mwezi ndani yake uwe nuru, na akalifanya jua kuwa taa?

وَاللَّهُ أَنبَتَكُم مِّنَ الْأَرْضِ نَبَاتًا(17)

 Na Mwenyezi Mungu amekuotesheni katika ardhi kama mimea.

ثُمَّ يُعِيدُكُمْ فِيهَا وَيُخْرِجُكُمْ إِخْرَاجًا(18)

 Kisha atakurudsheni humo na atakutoeni tena.

وَاللَّهُ جَعَلَ لَكُمُ الْأَرْضَ بِسَاطًا(19)

 Na Mwenyezi Mungu amekukunjulieni ardhi kama busati.

لِّتَسْلُكُوا مِنْهَا سُبُلًا فِجَاجًا(20)

 Ili mtembee humo katika njia zilizo pana.

قَالَ نُوحٌ رَّبِّ إِنَّهُمْ عَصَوْنِي وَاتَّبَعُوا مَن لَّمْ يَزِدْهُ مَالُهُ وَوَلَدُهُ إِلَّا خَسَارًا(21)

 Nuh'u akasema: Mola wangu Mlezi! Hakika hao wameniasi, na wamemfuata yule ambaye mali yake na wanawe hawakumzidishia ila khasara.

وَمَكَرُوا مَكْرًا كُبَّارًا(22)

 Na wakapanga vitimbi vikubwa.

وَقَالُوا لَا تَذَرُنَّ آلِهَتَكُمْ وَلَا تَذَرُنَّ وَدًّا وَلَا سُوَاعًا وَلَا يَغُوثَ وَيَعُوقَ وَنَسْرًا(23)

 Na wakasema: Msiwaache miungu yenu, wala msimwache Wadda wala Suwaa' wala Yaghutha, wala Yau'qa, wala Nasra.

وَقَدْ أَضَلُّوا كَثِيرًا ۖ وَلَا تَزِدِ الظَّالِمِينَ إِلَّا ضَلَالًا(24)

 Na hao walikwisha wapoteza wengi, wala usiwazidishie walio dhulumu ila kupotea.

مِّمَّا خَطِيئَاتِهِمْ أُغْرِقُوا فَأُدْخِلُوا نَارًا فَلَمْ يَجِدُوا لَهُم مِّن دُونِ اللَّهِ أَنصَارًا(25)

 Basi kwa ajili ya makosa yao waligharikishwa wakaingizwa Motoni, wala hawakuwapata wa kuwanusuru badala ya Mwenyezi Mungu.

وَقَالَ نُوحٌ رَّبِّ لَا تَذَرْ عَلَى الْأَرْضِ مِنَ الْكَافِرِينَ دَيَّارًا(26)

 Na Nuh'u akasema: Mola wangu Mlezi! Usimwache juu ya ardhi mkaazi wake yeyote katika makafiri!

إِنَّكَ إِن تَذَرْهُمْ يُضِلُّوا عِبَادَكَ وَلَا يَلِدُوا إِلَّا فَاجِرًا كَفَّارًا(27)

 Hakika ukiwaacha watawapoteza waja wako, wala wao hawatazaa ila waovu makafiri.

رَّبِّ اغْفِرْ لِي وَلِوَالِدَيَّ وَلِمَن دَخَلَ بَيْتِيَ مُؤْمِنًا وَلِلْمُؤْمِنِينَ وَالْمُؤْمِنَاتِ وَلَا تَزِدِ الظَّالِمِينَ إِلَّا تَبَارًا(28)

 Mola wangu Mlezi! Nighufirie mimi na wazazi wangu, na kila aliye ingia nyumbani mwangu kuwa ni mwenye kuamini, na Waumini wote wanaume, na Waumini wanawake. Na wala usiwazidishie walio dhulumu ila kupotea.


Больше сур в суахили:


Аль-Бакара Аль-'Имран Ан-Ниса'
Аль-Маида Юсуф Ибрахим
Аль-Хиджр Аль-Кахф Марьям
Аль-Хадж Аль-Касас Аль-'Анкабут
Ас-Саджда Я-Син Ад-Духан
Аль-Фатх Аль-Худжурат Каф
Ан-Наджм Ар-Рахман Аль-Ваки'а
Аль-Хашр Аль-Мульк Аль-Хакка
Аль-Иншикак Аль-А'ла Аль-Гашия

Скачать суру Nuh с голосом самых известных рекитаторов Корана:

Сура Nuh mp3: выберите рекитатора, чтобы прослушать и скачать главу Nuh полностью в высоком качестве
surah Nuh Ahmed El Agamy
Ahmed Al Ajmy
surah Nuh Bandar Balila
Bandar Balila
surah Nuh Khalid Al Jalil
Khalid Al Jalil
surah Nuh Saad Al Ghamdi
Saad Al Ghamdi
surah Nuh Saud Al Shuraim
Saud Al Shuraim
surah Nuh Abdul Basit Abdul Samad
Abdul Basit
surah Nuh Abdul Rashid Sufi
Abdul Rashid Sufi
surah Nuh Abdullah Basfar
Abdullah Basfar
surah Nuh Abdullah Awwad Al Juhani
Abdullah Al Juhani
surah Nuh Fares Abbad
Fares Abbad
surah Nuh Maher Al Muaiqly
Maher Al Muaiqly
surah Nuh Muhammad Siddiq Al Minshawi
Al Minshawi
surah Nuh Al Hosary
Al Hosary
surah Nuh Al-afasi
Mishari Al-afasi
surah Nuh Yasser Al Dosari
Yasser Al Dosari


Thursday, May 9, 2024

Помолитесь за нас хорошей молитвой