Surah Muminun aya 5 , Swahili translation of the meaning Ayah.
﴿وَالَّذِينَ هُمْ لِفُرُوجِهِمْ حَافِظُونَ﴾
[ المؤمنون: 5]
Na ambao wanazilinda tupu zao,
Surah Al-Muminun in SwahiliSwahili Translation - Al-Barwani
English - Sahih International
And they who guard their private parts
Tafsiri ya maana yake kwenye lugha ya Kiswahili
Na ambao wanazilinda tupu zao!
Nao wanajihifadhi nafsi zao wasiingiane na wanawake. -Na ambao wanazilinda tupu zao, isipo kuwa kwa wake zao au kwa iliyo wamiliki mikono yao ya kulia. Kwani hao si wenye kulaumiwa. Lakini anaye taka kinyume cha haya, basi hao ndio warukao mipaka.- Aya hizi zinaambatana na Aya nyengine ziliomo katika Suratun Nur zilio anzia: -Mzinifu mwanamke na mzinifu mwanamume, mpigeni kila mmoja wao bakora mia.- Hakika Aya hizi tukufu zilizo tajwa zinaashiria maovu ya katika umma yanayo tokea kwa uzinzi. Ama katika umma ni kuvurugika nasaba ya watoto isijuulikane, ama katika siha ni sehemu mbili. KWANZA ni katika mwili, mfano wa kisonono, tego, AIDS n.k. Kisonono huweza kuzalisha maradhi ya urithi kwa watoto hata huweza kuleta upofu. Ama tego (Syphilis) huenea katika mishipa ya damu na ya hisiya na huweza kuishia wazimu, na pia huenea mpaka kwa vizazi, na huenda mtoto akafa tumboni au akatoka na kilema. Ama maradhi ya AIDS (Ukimwi) hayo ni maafa yasiyo semeka, Mwenyezi Mungu atulinde nayo. PILI ni kuathirika mishipa ya hisiya na akili, kwani uzinzi huweza kuathiri dhamiri ya mtu, na kuadhibika nayo, na hata mwishoe huweza kuingia wazimu.
English | Türkçe | Indonesia |
Русский | Français | فارسی |
تفسير | Bengali | Urdu |
Ayats from Quran in Swahili
- Sema: Sioni katika yale niliyo funuliwa mimi kitu kilicho harimishwa kwa mlaji kukila isipo kuwa
- Hapana umma uwezao kutanguliza ajali yake wala kuikawiza.
- Tukio la haki.
- Wakasema: Sisi ni wenye nguvu na wakali kwa vita; na amri iko kwako, basi tazama
- Nitakuja mtia kwenye Moto wa Saqar.
- Na miongoni mwao wapo wanao iamini, na miongoni mwao wapo wasio iamini. Na Mola wako
- Na vipi mkufuru hali nyinyi mnasomewa Aya za Mwenyezi Mungu na Mtume yuko kati yenu?
- Na pia ndege walio kusanywa makundi kwa makundi; wote walikuwa wanyenyekevu kwake.
- Hakika Sisi tuliwapelekea ukelele mmoja tu, wakawa kama mabuwa ya kujengea uwa.
- Na laiti ungeli ona Malaika wanapo wafisha wale walio kufuru wakiwapiga nyuso zao na migongo
Quran Surah in Swahili :
Download Surah Muminun with the voice of the most famous Quran reciters :
Surah Muminun mp3 : choose the reciter to listen and download the chapter Muminun Complete with high quality
Ahmed Al Ajmy
Bandar Balila
Khalid Al Jalil
Saad Al Ghamdi
Saud Al Shuraim
Abdul Basit
Ammar Al-Mulla
Abdullah Basfar
Abdullah Al Juhani
Fares Abbad
Maher Al Muaiqly
Al Minshawi
Al Hosary
Mishari Al-afasi
Yasser Al Dosari
Please remember us in your sincere prayers