Surah Furqan aya 53 , Swahili translation of the meaning Ayah.

  1. Arabic
  2. tafsir
  3. mp3
  4. English
Quran in Swahili QUR,ANI TUKUFU na tafsiri ya maana yake kwenye lugha ya Kiswahili - Ali Muhsen Alberwany & English - Sahih International : Surah Furqan aya 53 in arabic text(The Criterion).
  
   

﴿۞ وَهُوَ الَّذِي مَرَجَ الْبَحْرَيْنِ هَٰذَا عَذْبٌ فُرَاتٌ وَهَٰذَا مِلْحٌ أُجَاجٌ وَجَعَلَ بَيْنَهُمَا بَرْزَخًا وَحِجْرًا مَّحْجُورًا﴾
[ الفرقان: 53]

Naye ndiye aliye zipeleka bahari mbili, hii tamu mno, na hii ya chumvi chungu. Na akaweka baina yao kinga na kizuizi kizuiacho.

Surah Al-Furqan in Swahili

Swahili Translation - Al-Barwani

English - Sahih International


And it is He who has released [simultaneously] the two seas, one fresh and sweet and one salty and bitter, and He placed between them a barrier and prohibiting partition.


Tafsiri ya maana yake kwenye lugha ya Kiswahili


Naye ndiye aliye zipeleka bahari mbili, hii tamu mno, na hii ya chumvi chungu. Na akaweka baina yao kinga na kizuizi kizuiacho.


Na Mwenyezi Mungu ndiye aliye ziendesha bahari mbili, bahari ya maji matamu na bahari ya maji ya chumvi. Na akafanya njia ya kila moja inakaribiana na nyengine. Na juu ya hivyo maji yao hayachanganyikani. Hiyo ni neema na rehema kwa watu. -Naye ndiye aliye zipeleka bahari mbili, hii tamu mno, na hii ya chumvi chungu. Na akaweka baina yao kinga na kizuizi kizuiacho.- Yamkini Aya hii inaashiria neema ya Mwenyezi Mungu kwa waja wake kwa kuto changanyika maji ya chumvi yanayo penya kutoka baharini kwenye miamba ya karibu na mwambao, na maji matamu yanayo penya kutoka bara, yasichanganyike kwa ukamilifu na hali nayo yanakutana. Matamu yanakuwa yako juu ya maji chumvi kama kwamba baina yao pana kinga kinacho zuia haya yasiingiane na haya, na kizuizi kizuiacho, yaani kizuizi chembamba tusicho weza kukiona. Na haya si tu, bali ipo kanuni madhubuti inayo hukumu makhusiano haya, na inayo yahukumu kwa maslaha ya wanaadamu wanao kaa katika maeneo hayo, na maisha yao yanategemea kuwepo hayo maji matamu. Kwani imethibiti kuwa tabaka ya maji matamu yalioko juu huzidi unene wake kwa mujibu wa kuzidi usawa (level) wa bahari kwa mpango maalumu. Hata inakuwa yawezekana kuhisabu kina cha mwisho cha maji matamu ambayo yamkinika kuyapata. Kwani hiyo ni sawa sawa na kadri ya khitilafu baina ya usawa (level) wa ardhi na usawa wa bahari mara arubaini.

English Türkçe Indonesia
Русский Français فارسی
تفسير Bengali Urdu

listen to Verse 53 from Furqan


Ayats from Quran in Swahili

  1. Hukumwona yule aliye hojiana na Ibrahim juu ya Mola wake Mlezi kwa sababu Mwenyezi Mungu
  2. Na watasema wale walio fuata: Laiti tungeweza kurudi tukawakataa wao kama wanavyo tukataa sisi! Hivi
  3. Huyo ndiye anaye msukuma yatima,
  4. Na hakuna siri katika mbingu na ardhi ila imo katika Kitabu kinacho bainisha.
  5. Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
  6. Na nani dhaalimu zaidi kuliko anaye mzulia uwongo Mwenyezi Mungu, na akazikanusha Ishara zake? Hakika
  7. Na Mwenyezi Mungu alikutimilizieni miadi yake, vile mlivyo kuwa mnawauwa kwa idhini yake, mpaka mlipo
  8. Wakasema: Ewe Shua'ibu! Mengi katika hayo unayo yasema hatuyafahamu. Na sisi tunakuona huna nguvu kwetu.
  9. Na mti utokao katika mlima wa Sinai, unatoa mafuta na kuwa kitoweo kwa walao.
  10. Wala usimwombe pamoja na Mwenyezi Mungu mungu mwenginewe. Hapana mungu ila Yeye. Kila kitu kitaangamia

Quran Surah in Swahili :

Al-Baqarah Al-'Imran An-Nisa'
Al-Ma'idah Yusuf Ibrahim
Al-Hijr Al-Kahf Maryam
Al-Hajj Al-Qasas Al-'Ankabut
As-Sajdah Ya Sin Ad-Dukhan
Al-Fath Al-Hujurat Qaf
An-Najm Ar-Rahman Al-Waqi'ah
Al-Hashr Al-Mulk Al-Haqqah
Al-Inshiqaq Al-A'la Al-Ghashiyah

Download Surah Furqan with the voice of the most famous Quran reciters :

Surah Furqan mp3 : choose the reciter to listen and download the chapter Furqan Complete with high quality
Surah Furqan Ahmed El Agamy
Ahmed Al Ajmy
Surah Furqan Bandar Balila
Bandar Balila
Surah Furqan Khalid Al Jalil
Khalid Al Jalil
Surah Furqan Saad Al Ghamdi
Saad Al Ghamdi
Surah Furqan Saud Al Shuraim
Saud Al Shuraim
Surah Furqan Abdul Basit Abdul Samad
Abdul Basit
Surah Furqan Abdul Rashid Sufi
Abdul Rashid Sufi
Surah Furqan Abdullah Basfar
Abdullah Basfar
Surah Furqan Abdullah Awwad Al Juhani
Abdullah Al Juhani
Surah Furqan Fares Abbad
Fares Abbad
Surah Furqan Maher Al Muaiqly
Maher Al Muaiqly
Surah Furqan Muhammad Siddiq Al Minshawi
Al Minshawi
Surah Furqan Al Hosary
Al Hosary
Surah Furqan Al-afasi
Mishari Al-afasi
Surah Furqan Yasser Al Dosari
Yasser Al Dosari


Sunday, May 19, 2024

لا تنسنا من دعوة صالحة بظهر الغيب