Surah Muminun aya 4 , Swahili translation of the meaning Ayah.

  1. Arabic
  2. tafsir
  3. mp3
  4. English
Quran in Swahili QUR,ANI TUKUFU na tafsiri ya maana yake kwenye lugha ya Kiswahili - Ali Muhsen Alberwany & English - Sahih International : Surah Muminun aya 4 in arabic text(The Believers).
  
   

﴿وَالَّذِينَ هُمْ لِلزَّكَاةِ فَاعِلُونَ﴾
[ المؤمنون: 4]

Na ambao wanatoa Zaka,

Surah Al-Muminun in Swahili

Swahili Translation - Al-Barwani

English - Sahih International


And they who are observant of zakah


Tafsiri ya maana yake kwenye lugha ya Kiswahili


Na ambao wanatoa Zaka!


Nao wanashikilia kutoa Zaka kuwapa wanao stahiki. Kwa hivyo wanakusanya ibada ya mwili na ibada ya mali, na baina ya kujisafisha nafsi na kuyasafisha mali. -Na ambao wanatoa Zaka,-: Huu waajibu wa kutoa Zaka unapelekea kujenga mashikamano ya umoja baina ya Waislamu, na kutia katika moyo wa kila mtu kuwa ana jukumu kwa nduguye, anahisi kama anavyo hisi yeye, na anaungulika kama anavyo ungulika yeye. Kwa hivyo ni waajibu wake kufanya awezavyo kumkinga na balaa za kilimwengu, na machungu ya ukosefu. Kwa hivyo fakiri au masikini hatomchukia tajiri, bali wote watahisi kama ni ukoo mmoja unao saidiana na wenye kushikamana na Kamba ya Mwenyezi Mungu. Wala mwenye deni hakati tamaa kuweza kulipa deni lake lilio bakia ikiwa hana cha kumalizia hilo deni. Wala haianguki chini azma ya mujaahidi anaye pigana katika Njia ya Mwenyezi Mungu kuinusuru Dini yake na kukomboa nchi yake kwa sababu ya kukosa mali ya kutimizia makusudio yake. Wala msafiri au mgeni mhitaji aliye mbali na mali yake hakosi wa kumkidhia haja zake kwa kumsaidia mpaka afike kwake. Na juu ya haya Zaka ilikuwa ni njia moja katika njia kubwa ulio chukua Uislamu kukombolea mateka na wafungwa na kuondoa utumwa. Na Uislamu umeongeza kutimiza malengo yake ya kijamii kwa ulimwengu mzima ikatupilia mbali chuki zinazo chusha za kidini, na ikatoa ruhusa Zaka wapewe makafiri ikihitajia haja kuwakopesha. Hali kadhaalika hupewa wale wanao itumikia Zaka, kama kuikusanya na kuigawa. Pia waandishi, na wasafiri, na wanao khasiri kwa ajili ya kupatanisha wenye kugombana, na wanao wasaidia Waislamu katika vita. Ama makusudio ya kiuchumi ya Zaka ni kuondoa ufakiri popote ulipo, na kumsaidia kila mwenye haja kama ilivyo kwisha tangulia.

English Türkçe Indonesia
Русский Français فارسی
تفسير Bengali Urdu

listen to Verse 4 from Muminun


Ayats from Quran in Swahili


Quran Surah in Swahili :

Al-Baqarah Al-'Imran An-Nisa'
Al-Ma'idah Yusuf Ibrahim
Al-Hijr Al-Kahf Maryam
Al-Hajj Al-Qasas Al-'Ankabut
As-Sajdah Ya Sin Ad-Dukhan
Al-Fath Al-Hujurat Qaf
An-Najm Ar-Rahman Al-Waqi'ah
Al-Hashr Al-Mulk Al-Haqqah
Al-Inshiqaq Al-A'la Al-Ghashiyah

Download Surah Muminun with the voice of the most famous Quran reciters :

Surah Muminun mp3 : choose the reciter to listen and download the chapter Muminun Complete with high quality
Surah Muminun Ahmed El Agamy
Ahmed Al Ajmy
Surah Muminun Bandar Balila
Bandar Balila
Surah Muminun Khalid Al Jalil
Khalid Al Jalil
Surah Muminun Saad Al Ghamdi
Saad Al Ghamdi
Surah Muminun Saud Al Shuraim
Saud Al Shuraim
Surah Muminun Abdul Basit Abdul Samad
Abdul Basit
Surah Muminun Abdul Rashid Sufi
Abdul Rashid Sufi
Surah Muminun Abdullah Basfar
Abdullah Basfar
Surah Muminun Abdullah Awwad Al Juhani
Abdullah Al Juhani
Surah Muminun Fares Abbad
Fares Abbad
Surah Muminun Maher Al Muaiqly
Maher Al Muaiqly
Surah Muminun Muhammad Siddiq Al Minshawi
Al Minshawi
Surah Muminun Al Hosary
Al Hosary
Surah Muminun Al-afasi
Mishari Al-afasi
Surah Muminun Yasser Al Dosari
Yasser Al Dosari


Friday, May 10, 2024

لا تنسنا من دعوة صالحة بظهر الغيب