Surah Maidah aya 103 , Swahili translation of the meaning Ayah.
﴿مَا جَعَلَ اللَّهُ مِن بَحِيرَةٍ وَلَا سَائِبَةٍ وَلَا وَصِيلَةٍ وَلَا حَامٍ ۙ وَلَٰكِنَّ الَّذِينَ كَفَرُوا يَفْتَرُونَ عَلَى اللَّهِ الْكَذِبَ ۖ وَأَكْثَرُهُمْ لَا يَعْقِلُونَ﴾
[ المائدة: 103]
Mwenyezi Mungu hakujaalia uharamu wowote juu ya "Bahira" wala "Saiba" wala "Wasila" wala "Hami". Lakini walio kufuru humzulia uwongo Mwenyezi Mungu, na wengi wao hawatumii akili.
Surah Al-Maidah in SwahiliSwahili Translation - Al-Barwani
English - Sahih International
Allah has not appointed [such innovations as] bahirah or sa'ibah or wasilah or ham. But those who disbelieve invent falsehood about Allah, and most of them do not reason.
Tafsiri ya maana yake kwenye lugha ya Kiswahili
Mwenyezi Mungu hakujaalia uharamu wowote juu ya -Bahira- wala -Saiba- wala -Wasila- wala -Hami-. Lakini walio kufuru humzulia uwongo Mwenyezi Mungu, na wengi wao hawatumii akili.
Mwenyezi Mungu hakukupeni ruhusa kuharimisha kitu alicho kuhalalishieni, na kwa hivyo mkenda mkawapasua ngamia masikio yao, na mkajizuia kuwatumia mkawaita -Bahira- mkawawacha kwa kuwekea nadhiri, na mkawaita -Saiba-; na mkaharimisha kula kondoo dume, na mkawatoa kuwa tunza kwa masanamu; na hata kondoo akizaa dume na jike mkamwita -Wasila-, na mkakataa kumchinja dume lake. Wala Mwenyezi Mungu hakukufanyieni sharia ya kukuharimishieni msimtumie ngamia dume baada wakisha zalikana kutokana naye matumbo kumi, naye mkamwita -Hami-! Mwenyezi Mungu hakukutungieni sharia yoyote ya namna hiyo. Lakini walio kufuru wanazua uwongo na wanamsingizia Mwenyezi Mungu. Na wengi wao hawatumii akili. Wakati wa Jahiliya, kabla ya Uislamu, Waarabu wakijiharimshia wenyewe asiyo yaharimisha Mwenyezi Mungu. Katika hizo ni kuwa:- 1. Ngamia akizaa mara tano na mtoto wa mwisho akawa dume, basi wakimpasua sikio lake na wakaharimisha kumpanda, na akawa haijuzu kumfukuza kwenye kunywa maji au kula machunga. Na wakimwita: -Bahira-, yaani aliyepasuliwa sikio. 2. Ilikuwa mtu husema: Nikirejea safarini, au nikipona maradhi yangu, basi ngamia wangu ni -Saiba-, yaani aliye achwa, na anakuwa kama -Bahira-. 3. Na walikuwa kondoo akizaa jike humfanya huyo mtoto ni wao, na akizaa dume humfanya ni wa miungu yao; na akizaa dume na jike basi hawamtoi mhanga huyo dume tena kwa miungu yao, na humwita huyo kondoo jike: -WAsila-, yaani amemuwasilia nduguye dume. 4. Na pia walikuwa akitokana na fahali mizao kumi basi husema mgongo wake umehamika,yaani umehifadhika, na wakamwita -Hami-. Huwa basi hapandwi, wala hatwikiwi mizigo.
English | Türkçe | Indonesia |
Русский | Français | فارسی |
تفسير | Bengali | Urdu |
Ayats from Quran in Swahili
- Wanapo pokea wapokeaji wawili, wanao kaa kuliani na kushotoni.
- Basi naapa kwa Mola Mlezi wa mbingu na ardhi, hakika haya ni kweli kama ilivyo
- Enyi mlio pewa Kitabu! Aminini tuliyo yateremsha yenye kusadikisha yale mliyo nayo, kabla hatujazigeuza nyuso
- Ndani yake zimo chemchem mbili zinazo pita.
- Na soma uliyo funuliwa katika Kitabu cha Mola wako Mlezi. Hapana wa kubadilisha maneno yake.
- Bila ya shaka watakusanywa kwa wakati wa siku maalumu.
- Hakika Mwenyezi Mungu amenunua kwa Waumini nafsi zao na mali zao kwa kuwa wao watapata
- Ewe Nabii! Tumekuhalalishia wake zako ulio wapa mahari yao, na ulio wamiliki kwa mkono wako
- Qaaf. Naapa kwa Qur'ani tukufu!
- Na hakika katika nyama hoa nyinyi mna mazingatio. Tunakunywesheni katika vile viliomo matumboni mwao, vikatoka
Quran Surah in Swahili :
Download Surah Maidah with the voice of the most famous Quran reciters :
Surah Maidah mp3 : choose the reciter to listen and download the chapter Maidah Complete with high quality
Ahmed Al Ajmy
Bandar Balila
Khalid Al Jalil
Saad Al Ghamdi
Saud Al Shuraim
Abdul Basit
Ammar Al-Mulla
Abdullah Basfar
Abdullah Al Juhani
Fares Abbad
Maher Al Muaiqly
Al Minshawi
Al Hosary
Mishari Al-afasi
Yasser Al Dosari
Please remember us in your sincere prayers