Surah Maidah aya 91 , Swahili translation of the meaning Ayah.

  1. Arabic
  2. tafsir
  3. mp3
  4. English
Quran in Swahili QUR,ANI TUKUFU na tafsiri ya maana yake kwenye lugha ya Kiswahili - Ali Muhsen Alberwany & English - Sahih International : Surah Maidah aya 91 in arabic text(The Table).
  
   

﴿إِنَّمَا يُرِيدُ الشَّيْطَانُ أَن يُوقِعَ بَيْنَكُمُ الْعَدَاوَةَ وَالْبَغْضَاءَ فِي الْخَمْرِ وَالْمَيْسِرِ وَيَصُدَّكُمْ عَن ذِكْرِ اللَّهِ وَعَنِ الصَّلَاةِ ۖ فَهَلْ أَنتُم مُّنتَهُونَ
[ المائدة: 91]

Hakika Shet'ani anataka kutia kati yenu uadui na chuki kwa ulevi na kamari, na akuzuieni kumkumbuka Mwenyezi Mungu na kusali. Basi je, mmeacha?

Surah Al-Maidah in Swahili

Swahili Translation - Al-Barwani

English - Sahih International


Satan only wants to cause between you animosity and hatred through intoxicants and gambling and to avert you from the remembrance of Allah and from prayer. So will you not desist?


Tafsiri ya maana yake kwenye lugha ya Kiswahili


Hakika Shetani anataka kutia kati yenu uadui na chuki kwa ulevi na kamari, na akuzuieni kumkumbuka Mwenyezi Mungu na kusali. Basi je, mmeacha?


Bila ya shaka Shetani hana atakalo kwa kukushawishini kunywa ulevi na kucheza kamari ila kuleta khitilafu na ugomvi na kuchukiana baina yenu ili mdhoofike kwa kuondoka masikizano, na uvunjike umoja wenu, kwa sababu anavyo kukupendeleeni mnywe ulevi na mcheze kamari. Na hayo ili mpate kuacha kumuabudu Mwenyezi Mungu, na muache Swala, ili Akhera yenu iwe ovu kama ilivyo dunia yenu. Basi jee! Baada ya nyinyi kujua maovu haya hamyatupilii mbali ninayo kukutazeni, mkamkosesha Iblisi makusudio yake? Mwenyezi Mungu Mtukufu Aliye takasika ametaja mambo mane yaliyo pelekea kuharimishwa ulevi na kamari: La Kwanza - Kuwa nafsi yake ni uchafu na uovu, kwani hayumkiniki kusifika kuwa ni mambo mazuri, kwa kuwa madhara yake yanaonekana wazi. Katika ulevi kuna uharibifu wa akili, na katika kamari ni kupoteza mali, na kwa yote mawili hayo upo uharibifu wa moyo. Na Shetani ndiye mwenye kuyapamba hayo. La pili - Hayo hueneza uadui na chuki. Kamari humalizikia ugomvi, na kama haifikii hayo basi huleta chuki na bughdha. Na ulevi ndio Mama wa Maasi. Utamwona mtu mwenye adabu zake mpole, akisha kunywa hugeuka nyama mwitu, akatenda mambo ya ukhalifu, kwani ulevi huidhoofisha sauti ya utu inayo mkataza mwanaadamu kutenda maovu. Utamwona mtu anajizuia kufanya kitendo kiovu, lakini akisha kunywa ulevi, au akavuta bangi, japo kidogo, huiendea shari bila ya kujali. Basi si kama ulevi unaharibu akili tu, bali unalaza dhamiri ya mtu. Anakuwa hana junaha. La tatu: Ni kuwa kamari na ulevi huuwa moyo. Mtu huwa hamkumbuki Mwenyezi Mungu, na kumkumbuka Mwenyezi Mungu ndiko kunako huisha nyoyo. Lane: Maasi hayo yanamzuilia mtu na Swala. Kamari na ulevi humsahaulisha Muumini na Swala zake, na akiwa anasali hatimizi nguzo zake kama zitakikanavyo. Basi inakuwa Swala zake ni kuinama na kuinuka bila ya kufuatana na moyo. Kwa hivyo basi imethibiti kuwa kuharimishwa mvinyo, pombe, tembo, bangi n.k. si kwa sababu ya kulevya kwake tu, bali ni kwa kumziba mtu fahamu zake, kumgubika asitambue atendalo. Na kwa hivyo ndio imepokewa kuwa kinacho levya kwa wingi wake, basi hata kidogo chake ni haramu, kwani hicho kidogo nacho kinapumbaza akili. Na juu ya haya pana madhara ya mwili kama madaktari walivyo thibitisha. Kwa hivyo ulevi hata kidogo ni haramu. Mwenyezi Mungu Subhanahu ametaja sababu mbili za kuharimisha ulevi, na udaktari umezidisha kuwa ulevi kidogo haupotezi akili, lakini huzidisha uchangamfu au husabibisha hali ya huzuni na kuona dhiki ya moyo. Na katika hali zote mbili anakuwa mtu amepungukiwa na ukamilifu wa akili yake kubeba jukumu, na kwa hivyo hutenda vitendo ambavyo kwa dhahiri ni sawa kumbe ni madhara. Ama kuuzoea ulevi hudhuru maini, matumbo, na mishipa ya akili na hisiya, na hurithisha madhara mpaka kwa vizazi.

English Türkçe Indonesia
Русский Français فارسی
تفسير Bengali Urdu

listen to Verse 91 from Maidah


Ayats from Quran in Swahili


    Quran Surah in Swahili :

    Al-Baqarah Al-'Imran An-Nisa'
    Al-Ma'idah Yusuf Ibrahim
    Al-Hijr Al-Kahf Maryam
    Al-Hajj Al-Qasas Al-'Ankabut
    As-Sajdah Ya Sin Ad-Dukhan
    Al-Fath Al-Hujurat Qaf
    An-Najm Ar-Rahman Al-Waqi'ah
    Al-Hashr Al-Mulk Al-Haqqah
    Al-Inshiqaq Al-A'la Al-Ghashiyah

    Download Surah Maidah with the voice of the most famous Quran reciters :

    Surah Maidah mp3 : choose the reciter to listen and download the chapter Maidah Complete with high quality
    Surah Maidah Ahmed El Agamy
    Ahmed Al Ajmy
    Surah Maidah Bandar Balila
    Bandar Balila
    Surah Maidah Khalid Al Jalil
    Khalid Al Jalil
    Surah Maidah Saad Al Ghamdi
    Saad Al Ghamdi
    Surah Maidah Saud Al Shuraim
    Saud Al Shuraim
    Surah Maidah Abdul Basit Abdul Samad
    Abdul Basit
    Surah Maidah Ammar Al-Mulla
    Ammar Al-Mulla
    Surah Maidah Abdullah Basfar
    Abdullah Basfar
    Surah Maidah Abdullah Awwad Al Juhani
    Abdullah Al Juhani
    Surah Maidah Fares Abbad
    Fares Abbad
    Surah Maidah Maher Al Muaiqly
    Maher Al Muaiqly
    Surah Maidah Muhammad Siddiq Al Minshawi
    Al Minshawi
    Surah Maidah Al Hosary
    Al Hosary
    Surah Maidah Al-afasi
    Mishari Al-afasi
    Surah Maidah Yasser Al Dosari
    Yasser Al Dosari


    Monday, June 23, 2025

    Please remember us in your sincere prayers