Surah Al-Maarij with Swahili

  1. Surah mp3
  2. More
  3. Swahili
The Holy Quran | Quran translation | Language Swahili | Surah Maarij | المعارج - Ayat Count 44 - The number of the surah in moshaf: 70 - The meaning of the surah in English: The Ways of Ascent.

سَأَلَ سَائِلٌ بِعَذَابٍ وَاقِعٍ(1)

 Muulizaji aliuliza juu ya adhabu itakayo tokea,

لِّلْكَافِرِينَ لَيْسَ لَهُ دَافِعٌ(2)

 Kwa makafiri - ambayo hapana awezaye kuizuia -

مِّنَ اللَّهِ ذِي الْمَعَارِجِ(3)

 Kutoka kwa Mwenyezi Mungu Mwenye mbingu za daraja.

تَعْرُجُ الْمَلَائِكَةُ وَالرُّوحُ إِلَيْهِ فِي يَوْمٍ كَانَ مِقْدَارُهُ خَمْسِينَ أَلْفَ سَنَةٍ(4)

 Malaika na Roho hupanda kwendea kwake katika siku ambayo kadiri yake ni miaka khamsini elfu!

فَاصْبِرْ صَبْرًا جَمِيلًا(5)

 Basi subiri kwa subira njema.

إِنَّهُمْ يَرَوْنَهُ بَعِيدًا(6)

 Hakika wao wanaiona iko mbali,

وَنَرَاهُ قَرِيبًا(7)

 Na Sisi tunaiona iko karibu.

يَوْمَ تَكُونُ السَّمَاءُ كَالْمُهْلِ(8)

 Siku ambayo mbingu zitakapo kuwa kama maadeni iliyo yayushwa.

وَتَكُونُ الْجِبَالُ كَالْعِهْنِ(9)

 Na milima itakuwa kama sufi.

وَلَا يَسْأَلُ حَمِيمٌ حَمِيمًا(10)

 Wala jamaa hatamuuliza jamaa yake.

يُبَصَّرُونَهُمْ ۚ يَوَدُّ الْمُجْرِمُ لَوْ يَفْتَدِي مِنْ عَذَابِ يَوْمِئِذٍ بِبَنِيهِ(11)

 Ijapo kuwa wataonyeshwa waonane. Atatamani mkosefu lau ajikomboe na adhabu ya siku hiyo kwa kuwatoa fidia wanawe,

وَصَاحِبَتِهِ وَأَخِيهِ(12)

 Na mkewe, na nduguye,

وَفَصِيلَتِهِ الَّتِي تُؤْوِيهِ(13)

 Na jamaa zake walio kuwa wakimkimu,

وَمَن فِي الْأَرْضِ جَمِيعًا ثُمَّ يُنجِيهِ(14)

 Na wote waliomo duniani, kisha aokoke yeye.

كَلَّا ۖ إِنَّهَا لَظَىٰ(15)

 La, hasha! Kwa hakika huo ni Moto mkali kabisa,

نَزَّاعَةً لِّلشَّوَىٰ(16)

 Unao babua ngozi ya kichwa!

تَدْعُو مَنْ أَدْبَرَ وَتَوَلَّىٰ(17)

 Utamwita kila aliye geuza mgongo na akageuka.

وَجَمَعَ فَأَوْعَىٰ(18)

 Na akakusanya mali, kisha akayahifadhi.

۞ إِنَّ الْإِنسَانَ خُلِقَ هَلُوعًا(19)

 Hakika mtu ameumbwa na papara.

إِذَا مَسَّهُ الشَّرُّ جَزُوعًا(20)

 Inapo mgusa shari hupapatika.

وَإِذَا مَسَّهُ الْخَيْرُ مَنُوعًا(21)

 Na inapo mgusa kheri huizuilia.

إِلَّا الْمُصَلِّينَ(22)

 Isipo kuwa wanao sali,

الَّذِينَ هُمْ عَلَىٰ صَلَاتِهِمْ دَائِمُونَ(23)

 Ambao wanadumisha Sala zao,

وَالَّذِينَ فِي أَمْوَالِهِمْ حَقٌّ مَّعْلُومٌ(24)

 Na ambao katika mali yao iko haki maalumu

لِّلسَّائِلِ وَالْمَحْرُومِ(25)

 Kwa mwenye kuomba na anaye jizuilia kuomba;

وَالَّذِينَ يُصَدِّقُونَ بِيَوْمِ الدِّينِ(26)

 Na ambao wanaisadiki Siku ya Malipo,

وَالَّذِينَ هُم مِّنْ عَذَابِ رَبِّهِم مُّشْفِقُونَ(27)

 Na ambao wanaiogopa adhabu itokayo kwa Mola wao Mlezi.

إِنَّ عَذَابَ رَبِّهِمْ غَيْرُ مَأْمُونٍ(28)

 Hakika adhabu ya Mola wao Mlezi si ya kuaminika nayo.

وَالَّذِينَ هُمْ لِفُرُوجِهِمْ حَافِظُونَ(29)

 Na ambao wanahifadhi tupu zao.

إِلَّا عَلَىٰ أَزْوَاجِهِمْ أَوْ مَا مَلَكَتْ أَيْمَانُهُمْ فَإِنَّهُمْ غَيْرُ مَلُومِينَ(30)

 Isipo kuwa kwa wake zao, au iliyo wamiliki mikono yao ya kuume, basi hao hawalaumiwi -

فَمَنِ ابْتَغَىٰ وَرَاءَ ذَٰلِكَ فَأُولَٰئِكَ هُمُ الْعَادُونَ(31)

 Lakini wanao taka kinyume ya haya, basi hao ndio wanao ruka mipaka.

وَالَّذِينَ هُمْ لِأَمَانَاتِهِمْ وَعَهْدِهِمْ رَاعُونَ(32)

 Na ambao wanazichunga amana zao na ahadi zao,

وَالَّذِينَ هُم بِشَهَادَاتِهِمْ قَائِمُونَ(33)

 Na ambao wanasimama imara katika ushahidi wao,

وَالَّذِينَ هُمْ عَلَىٰ صَلَاتِهِمْ يُحَافِظُونَ(34)

 Na ambao wanazihifadhi Sala zao.

أُولَٰئِكَ فِي جَنَّاتٍ مُّكْرَمُونَ(35)

 Hao ndio watakao hishimiwa Peponi.

فَمَالِ الَّذِينَ كَفَرُوا قِبَلَكَ مُهْطِعِينَ(36)

 Wana nini wale walio kufuru wanakutumbulia macho tu?

عَنِ الْيَمِينِ وَعَنِ الشِّمَالِ عِزِينَ(37)

 Makundi kwa makundi upande wa kulia na upande wa kushoto!

أَيَطْمَعُ كُلُّ امْرِئٍ مِّنْهُمْ أَن يُدْخَلَ جَنَّةَ نَعِيمٍ(38)

 Kwani kila mmoja wao anatumai kuingizwa katika Pepo ya neema?

كَلَّا ۖ إِنَّا خَلَقْنَاهُم مِّمَّا يَعْلَمُونَ(39)

 La, hasha! Hakika Sisi tumewaumba kutokana na wanacho kijua.

فَلَا أُقْسِمُ بِرَبِّ الْمَشَارِقِ وَالْمَغَارِبِ إِنَّا لَقَادِرُونَ(40)

 Basi naapa kwa Mola Mlezi wa mashariki zote na magharibi zote kwamba Sisi tunaweza

عَلَىٰ أَن نُّبَدِّلَ خَيْرًا مِّنْهُمْ وَمَا نَحْنُ بِمَسْبُوقِينَ(41)

 Kuwabadili kwa walio bora kuliko wao; na Sisi hatushindwi.

فَذَرْهُمْ يَخُوضُوا وَيَلْعَبُوا حَتَّىٰ يُلَاقُوا يَوْمَهُمُ الَّذِي يُوعَدُونَ(42)

 Basi waache wapige porojo na wacheze, mpaka wakutane na siku yao wanayo ahidiwa,

يَوْمَ يَخْرُجُونَ مِنَ الْأَجْدَاثِ سِرَاعًا كَأَنَّهُمْ إِلَىٰ نُصُبٍ يُوفِضُونَ(43)

 Siku watakapotoka makaburini kwa upesi kama kwamba wanakimbilia mfundo,

خَاشِعَةً أَبْصَارُهُمْ تَرْهَقُهُمْ ذِلَّةٌ ۚ ذَٰلِكَ الْيَوْمُ الَّذِي كَانُوا يُوعَدُونَ(44)

 Macho yao yatainama, fedheha itawafunika. Hiyo ndiyo Siku waliyo kuwa wakiahidiwa.


More surahs in Swahili:


Al-Baqarah Al-'Imran An-Nisa'
Al-Ma'idah Yusuf Ibrahim
Al-Hijr Al-Kahf Maryam
Al-Hajj Al-Qasas Al-'Ankabut
As-Sajdah Ya Sin Ad-Dukhan
Al-Fath Al-Hujurat Qaf
An-Najm Ar-Rahman Al-Waqi'ah
Al-Hashr Al-Mulk Al-Haqqah
Al-Inshiqaq Al-A'la Al-Ghashiyah

Download surah Al-Maarij with the voice of the most famous Quran reciters :

surah Al-Maarij mp3 : choose the reciter to listen and download the chapter Al-Maarij Complete with high quality
surah Al-Maarij Ahmed El Agamy
Ahmed Al Ajmy
surah Al-Maarij Bandar Balila
Bandar Balila
surah Al-Maarij Khalid Al Jalil
Khalid Al Jalil
surah Al-Maarij Saad Al Ghamdi
Saad Al Ghamdi
surah Al-Maarij Saud Al Shuraim
Saud Al Shuraim
surah Al-Maarij Abdul Basit Abdul Samad
Abdul Basit
surah Al-Maarij Abdul Rashid Sufi
Abdul Rashid Sufi
surah Al-Maarij Abdullah Basfar
Abdullah Basfar
surah Al-Maarij Abdullah Awwad Al Juhani
Abdullah Al Juhani
surah Al-Maarij Fares Abbad
Fares Abbad
surah Al-Maarij Maher Al Muaiqly
Maher Al Muaiqly
surah Al-Maarij Muhammad Siddiq Al Minshawi
Al Minshawi
surah Al-Maarij Al Hosary
Al Hosary
surah Al-Maarij Al-afasi
Mishari Al-afasi
surah Al-Maarij Yasser Al Dosari
Yasser Al Dosari


Monday, May 6, 2024

لا تنسنا من دعوة صالحة بظهر الغيب