Surah Baqarah aya 229 , Swahili translation of the meaning Ayah.

  1. Arabic
  2. tafsir
  3. mp3
  4. English
Quran in Swahili QUR,ANI TUKUFU na tafsiri ya maana yake kwenye lugha ya Kiswahili - Ali Muhsen Alberwany & English - Sahih International : Surah Baqarah aya 229 in arabic text(The Cow).
  
   

﴿الطَّلَاقُ مَرَّتَانِ ۖ فَإِمْسَاكٌ بِمَعْرُوفٍ أَوْ تَسْرِيحٌ بِإِحْسَانٍ ۗ وَلَا يَحِلُّ لَكُمْ أَن تَأْخُذُوا مِمَّا آتَيْتُمُوهُنَّ شَيْئًا إِلَّا أَن يَخَافَا أَلَّا يُقِيمَا حُدُودَ اللَّهِ ۖ فَإِنْ خِفْتُمْ أَلَّا يُقِيمَا حُدُودَ اللَّهِ فَلَا جُنَاحَ عَلَيْهِمَا فِيمَا افْتَدَتْ بِهِ ۗ تِلْكَ حُدُودُ اللَّهِ فَلَا تَعْتَدُوهَا ۚ وَمَن يَتَعَدَّ حُدُودَ اللَّهِ فَأُولَٰئِكَ هُمُ الظَّالِمُونَ
[ البقرة: 229]

T'alaka ni mara mbili. Kisha ni kukaa kwa wema au kuachana kwa vizuri. Wala si halali kwenu kuchukua chochote mlicho wapa wake zenu, ila ikiwa wote wawili wakiogopa ya kwamba hawataweza kushikamana na mipaka ya Mwenyezi Mungu. Basi mkiogopa kuwa hawataweza kushikamana na mipaka ya Mwenyezi Mungu hapo itakuwa hapana lawama ikiwa mwanamke atajikomboa. Hii ndiyo mipaka ya Mwenyezi Mungu; basi msiikiuke. Na watakao ikiuka mipaka ya Mwenyezi Mungu, hao ndio madhaalimu.

Surah Al-Baqarah in Swahili

Swahili Translation - Al-Barwani

English - Sahih International


Divorce is twice. Then, either keep [her] in an acceptable manner or release [her] with good treatment. And it is not lawful for you to take anything of what you have given them unless both fear that they will not be able to keep [within] the limits of Allah. But if you fear that they will not keep [within] the limits of Allah, then there is no blame upon either of them concerning that by which she ransoms herself. These are the limits of Allah, so do not transgress them. And whoever transgresses the limits of Allah - it is those who are the wrongdoers.


Tafsiri ya maana yake kwenye lugha ya Kiswahili


talaka ni mara mbili. Kisha ni kukaa kwa wema au kuachana kwa vizuri. Wala si halali kwenu kuchukua chochote mlicho wapa wake zenu, ila ikiwa wote wawili wakiogopa ya kwamba hawataweza kushikamana na mipaka ya Mwenyezi Mungu. Basi mkiogopa kuwa hawataweza kushikamana na mipaka ya Mwenyezi Mungu hapo itakuwa hapana lawama ikiwa mwanamke atajikomboa. Hii ndiyo mipaka ya Mwenyezi Mungu; basi msiikiuke. Na watakao ikiuka mipaka ya Mwenyezi Mungu, hao ndio madhaalimu.


talaka ni mara mbili. Baada ya kila talaka ana haki mume kukaa naye kwa kumrejea kabla ya kwisha siku za eda, au kumrejesha katika dhamana yake kwa kumwoa upya. Na katika hali hiyo inapasa makusudio yake ni kukaa naye kwa uadilifu na kumtendea wema, au kuachana kwa ihsani na heshima bila ya kukhasimiana. Wala si halali kwenu, enyi waume, kuchukua chochote mlicho wapa wanawake ila mkikhofu kuwa hamtoweza kufuata haki za uke na ume alizo kubainishieni Mwenyezi Mungu Subhanahu wa Taala, na akaku lazimisheni mzifuate. Mkikhofu, enyi Waislamu, kutofuata haki za mume na mke vilivyo kama alivyo eleza Mwenyezi Mungu basi ameamrisha mke atoe mali kwa ajili ya kutokana na mumewe. Na hizi ni hukumu zilizo pitishwa, msiende kinyume nazo, mkazipindukia. Mwenye kufanya hivyo amejidhulumu nafsi yake na amedhulumu jamii anayo ishi kati yake. Mwenyezi Mungu Subhanahu wa Taala ameifanyia sharia talaka, na akampa mwanamume kwanza uwezo wa kuacha. Baadhi ya watu wanadhani kuwa haya huleta madhara katika maisha na kusahilisha kuvunjika nyumba za watu. (a) Ama kupewa haki ya kuacha mwanamume kwa hakika hakupewa haki hiyo bila ya masharti yoyote. Katika masharti hayo aliyo wekewa ni: KWANZA hana ruhusa kuacha ila talaka moja ya kuweza kurejea, yaani anakuwa na haki ya kumrejea mke kabla ya kwisha eda. Ama amrejee naye yu ndani ya eda au amwache, na hivyo tena ni dalili ya hadi ya kuchukiana, na hapana maisha ya mume na mke tena kuchukiana kumefika hadi hiyo. PILI asimwache wakati wa hedhi, kwani wakati huo mwanamke huwa na hamaki, kwa hivyo huwa hapana utulivu. Na huenda hiyo hedhi ndiyo sababu ya hizo chuki zilizo zidi. Basi asiache mpaka mambo yawe yametua. TATU asimwache naye yumo katika tahara aliyo kwisha muingilia, kwani hiyo yaweza kuonekana huko kuchukiana kunatokana na kutokuwa na raghba na mkewe. Basi mambo yakiwa hivi talaka inakuwa katika hali ya chuki iliyo na nguvu, na kukatika mapenzi ya daima.

English Türkçe Indonesia
Русский Français فارسی
تفسير Bengali Urdu

listen to Verse 229 from Baqarah


Ayats from Quran in Swahili

  1. Je! Wakati haujafika bado kwa walio amini zikanyenyekea nyoyo zao kwa kumkumbuka Mwenyezi Mungu na
  2. Yeye ndiye aliye kujaalieni usiku mpate kutulia humo, na mchana wa kuonea. Hakika katika haya
  3. Basi walipo yasahau waliyo kumbushwa, tuliwaokoa walio kuwa wakikataza maovu, na tukawatesa walio dhulumu kwa
  4. Nyoyoni mwao mna maradhi, na Mwenyezi Mungu amewazidishia maradhi. Basi watakuwa na adhabu chungu kwa
  5. Basi wakipuuza wewe sema: Nakuhadharisheni adhabu mfano wa adhabu ya A'di na Thamudi,
  6. Ili Mwenyezi Mungu akusamehe makosa yako yaliyo tangulia na yajayo, na akutimizie neema zake, na
  7. Basi alipo taka kumshika kwa nguvu yule aliye adui wao wote wawili, akasema: Ewe Musa!
  8. Basi atachungulia amwone katikati ya Jahannamu.
  9. Basi aliwachezea watu wake, na wakamt'ii. Kwa hakika hao walikuwa watu wapotovu.
  10. Hapo Mwenyezi Mungu akamleta kunguru anaye fukua katika ardhi ili amwonyeshe vipi kumsitiri nduguye. Akasema:

Quran Surah in Swahili :

Al-Baqarah Al-'Imran An-Nisa'
Al-Ma'idah Yusuf Ibrahim
Al-Hijr Al-Kahf Maryam
Al-Hajj Al-Qasas Al-'Ankabut
As-Sajdah Ya Sin Ad-Dukhan
Al-Fath Al-Hujurat Qaf
An-Najm Ar-Rahman Al-Waqi'ah
Al-Hashr Al-Mulk Al-Haqqah
Al-Inshiqaq Al-A'la Al-Ghashiyah

Download Surah Baqarah with the voice of the most famous Quran reciters :

Surah Baqarah mp3 : choose the reciter to listen and download the chapter Baqarah Complete with high quality
Surah Baqarah Ahmed El Agamy
Ahmed Al Ajmy
Surah Baqarah Bandar Balila
Bandar Balila
Surah Baqarah Khalid Al Jalil
Khalid Al Jalil
Surah Baqarah Saad Al Ghamdi
Saad Al Ghamdi
Surah Baqarah Saud Al Shuraim
Saud Al Shuraim
Surah Baqarah Abdul Basit Abdul Samad
Abdul Basit
Surah Baqarah Abdul Rashid Sufi
Abdul Rashid Sufi
Surah Baqarah Abdullah Basfar
Abdullah Basfar
Surah Baqarah Abdullah Awwad Al Juhani
Abdullah Al Juhani
Surah Baqarah Fares Abbad
Fares Abbad
Surah Baqarah Maher Al Muaiqly
Maher Al Muaiqly
Surah Baqarah Muhammad Siddiq Al Minshawi
Al Minshawi
Surah Baqarah Al Hosary
Al Hosary
Surah Baqarah Al-afasi
Mishari Al-afasi
Surah Baqarah Yasser Al Dosari
Yasser Al Dosari


Sunday, May 19, 2024

لا تنسنا من دعوة صالحة بظهر الغيب