Surah Yunus aya 5 , Swahili translation of the meaning Ayah.
﴿هُوَ الَّذِي جَعَلَ الشَّمْسَ ضِيَاءً وَالْقَمَرَ نُورًا وَقَدَّرَهُ مَنَازِلَ لِتَعْلَمُوا عَدَدَ السِّنِينَ وَالْحِسَابَ ۚ مَا خَلَقَ اللَّهُ ذَٰلِكَ إِلَّا بِالْحَقِّ ۚ يُفَصِّلُ الْآيَاتِ لِقَوْمٍ يَعْلَمُونَ﴾
[ يونس: 5]
Yeye ndiye aliye lijaalia jua kuwa na mwangaza, na mwezi ukawa na nuru, na akaupimia vituo ili mjue idadi ya miaka na hisabu. Mwenyezi Mungu hakuviumba hivyo ila kwa Haki. Anazipambanua Ishara kwa watu wanao jua.
Surah Yunus in SwahiliSwahili Translation - Al-Barwani
English - Sahih International
It is He who made the sun a shining light and the moon a derived light and determined for it phases - that you may know the number of years and account [of time]. Allah has not created this except in truth. He details the signs for a people who know
Tafsiri ya maana yake kwenye lugha ya Kiswahili
Yeye ndiye aliye lijaalia jua kuwa na mwangaza, na mwezi ukawa na nuru, na akaupimia vituo ili mjue idadi ya miaka na hisabu. Mwenyezi Mungu hakuviumba hivyo ila kwa Haki. Anazipambanua Ishara kwa watu wanao jua.
Na Mola wenu Mlezi ndiye aliye ziumba mbingu na ardhi, na akalifanya jua litoe mwanga, na mwezi utoe nuru. Na akajaalia mwezi uwe na vituo ili vikusaidieni kuweza kupima nyakati zenu, na mjue idadi ya miaka na hisabu. Na wala Mwenyezi Mungu hakuumba hayo ila kwa hikima. Na Yeye Subhanahu katika Kitabu chake anazikunjua Ishara zenye kuonyesha Ungu wake na ukamilifu wa uwezo wake, ili mpate kuzingatia kwa akili zenu, na mkubali kwa yanayo hitajia ujuzi. Aya hii ya 5 inahakikisha ukweli wa kisayansi ambao haukujuulikana na hiyo sayansi ila hivi mwishoni. Hapo kwanza haukujuulikana, nao ni kuwa jua ni umbo lenye kuwaka moto, na ndio chanzo cha nguvu za kufanyia kazi zote, kwa Kiarabu huitwa taaqa, na kwa Kiingereza Energy, na kwa Kiswahili cha sasa Nishati. Katika nguvu hizo ni huo Mwangaza na Joto. Ama mwezi hauwaki moto, bali unarudisha mwangaza wa jua, kama kioo, kwa hivyo huonekana una nuru. Kwa hivyo Subhanahu ameeleza kuwa jua lina mwangaza wa asli, na mwezi unatoa nuru tu. Na Aya hii imeashiria hakika ya nyendo za falaki, nayo ni kuwa mwezi unaizunguka ardhi, na kila siku unakuwa katika mahala fulani kwa mintarafu ya dunia. Ukimaliza mzunguko wake ndio unatimia mwezi, huu wa siku 30 au 29. Kwa hivyo tunaweza kujua kiasi cha mwaka, na kwa hivyo twaweza kujua hisabu za miaka, miezi na siku.
| English | Türkçe | Indonesia |
| Русский | Français | فارسی |
| تفسير | Bengali | Urdu |
Ayats from Quran in Swahili
- Na akautoa mkono wake, na mara ukawa mweupe kwa watazamao.
- Hakika wale walio amini na wakatenda mema mashukio yao yatakuwa kwenye Pepo za Firdausi.
- Akasema: Yale Mola wangu aliyo niwezesha ni bora zaidi. Lakini nyinyi nisaidieni kwa nguvu zenu.
- Basi akawalipa unaafiki kuutia nyoyoni mwao mpaka Siku watapo kutana naye, kwa sababu ya kuwa
- Na hakika hii bila ya shaka ni haki ya yakini.
- Kama wanaafiki na wale wenye maradhi nyoyoni mwao, na waenezao fitna katika Madina hawatoacha, basi
- Msitoe udhuru; mmekwisha kufuru baada ya kuamini kwenu! Tukilisamehe kundi moja kati yenu, tutaliadhibu kundi
- Na sema: Alhamdulillah, Himdi zote ni za Mwenyezi Mungu ambaye hana mwana, wala hana mshirika
- Haliwi jua kuufikia mwezi, wala usiku kuupita mchana. Na vyote vinaogelea katika njia zao.
- Je! Anaye isimamia kila nafsi kwa yale iliyo yachuma...? Na wamemfanyia Mwenyezi Mungu kuwa na
Quran Surah in Swahili :
Download Surah Yunus with the voice of the most famous Quran reciters :
Surah Yunus mp3 : choose the reciter to listen and download the chapter Yunus Complete with high quality
Ahmed Al Ajmy
Bandar Balila
Khalid Al Jalil
Saad Al Ghamdi
Saud Al Shuraim
Abdul Basit
Ammar Al-Mulla
Abdullah Basfar
Abdullah Al Juhani
Fares Abbad
Maher Al Muaiqly
Al Minshawi
Al Hosary
Mishari Al-afasi
Yasser Al Dosari
Please remember us in your sincere prayers



