Surah Anbiya aya 32 , Swahili translation of the meaning Ayah.
﴿وَجَعَلْنَا السَّمَاءَ سَقْفًا مَّحْفُوظًا ۖ وَهُمْ عَنْ آيَاتِهَا مُعْرِضُونَ﴾
[ الأنبياء: 32]
Na tukaifanya mbingu kuwa dari iliyo hifadhiwa, lakini wanazipuuza Ishara zake.
Surah Al-Anbiya in SwahiliSwahili Translation - Al-Barwani
English - Sahih International
And We made the sky a protected ceiling, but they, from its signs, are turning away.
Tafsiri ya maana yake kwenye lugha ya Kiswahili
Na tukaifanya mbingu kuwa dari iliyo hifadhiwa, lakini wanazipuuza Ishara zake.
Na tumeifanya mbingu kama dari iliyo nyanyuliwa, na tukailinda isianguke, au visianguke viliomo humo. Na juu ya hayo, wao hawazioni wala hawaziingatii Ishara zetu zenye kuonyesha uweza wetu na hikima yetu na rehema yetu. Maoni ya wataalamu juu ya Aya 32: -Na tukaifanya mbingu kuwa dari iliyo hifadhiwa lakini wanazipuuza Ishara zake. -: Aya hii tukufu imethibitisha kuwa mbingu na vyote viliomo ndani yake vimehifadhiwa visiwe na ila yoyote, na vimehifadhiwa visidondoke juu ya ardhi. Na mbingu ni kila kilicho juu yetu, kuanzia kifuniko hichi cha hewa inayo walinda walioko juu ya ardhi na khatari nyingi za angani ambazo zinazuia maisha, mfano wa vimondo vya nyota za mkia, na miyale. Na juu ya ardhi pana kifuniko cha hewa kinacho linda ardhi kwa nguvu za mvutano, na haifai kukosekana hivyo bila ya maangamizo kabisa. Na juu ya kifuniko cha hewa ndio kuna hizo sayari za mbinguni, na zipo kwa umbali mbali mbali kufuatana na nyendo zao tangu mwanzo. -Na tukaifanya mbingu kuwa dari iliyo hifadhiwa- yaani hizo sayari na vyote vilio mbinguni vyaonekana kwa nadhari yetu kama kwamba ni dari, na tunaona vilio juu ya vichwa vyetu kama ni vidogo kuliko vilioko upeo wa macho. Na hayo ni kiini macho tu, kama tunapo liona jua kubwa wakati wa kuchomoza na kuchwa kuliko adhuhuri. Na hili qubba la mbingu lina sifa zake, zinazo khitalifiana kila ukizidi mnyanyuko wa ardhi, kama hizo sayari za mbinguni kwa mujibu wa jicho linavyo ona katika qubba la mbingu.
English | Türkçe | Indonesia |
Русский | Français | فارسی |
تفسير | Bengali | Urdu |
Ayats from Quran in Swahili
- Na watasema: Je, tutapewa muhula?
- Wewe huna lako jambo katika haya - ama atawahurumia au atawaadhibu, kwani wao ni madhaalimu.
- Mnamdhania nini Mola Mlezi wa walimwengu wote?
- Na wakati tulipo waleta kundi la majini kuja kwako kusikiliza Qur'ani. Basi walipo ihudhuria walisema:
- Na kwa nini msile katika walio somewa jina la Mwenyezi Mungu, naye amekwisha kubainishieni alivyo
- Na kwa wengine ambao bado hawajaungana nao. Na Yeye ndiye Mwenye nguvu, Mwenye hikima.
- Na tulimuinua daraja ya juu.
- Siku kitapo tetemeka cha kutetemeka,
- Ameangamia mwanaadamu! Nini kinacho mkufurisha?
- Na lau ungeli ona watavyo simamishwa mbele ya Mola wao Mlezi, akawaambia: Je, si kweli
Quran Surah in Swahili :
Download Surah Anbiya with the voice of the most famous Quran reciters :
Surah Anbiya mp3 : choose the reciter to listen and download the chapter Anbiya Complete with high quality
Ahmed Al Ajmy
Bandar Balila
Khalid Al Jalil
Saad Al Ghamdi
Saud Al Shuraim
Abdul Basit
Ammar Al-Mulla
Abdullah Basfar
Abdullah Al Juhani
Fares Abbad
Maher Al Muaiqly
Al Minshawi
Al Hosary
Mishari Al-afasi
Yasser Al Dosari
Please remember us in your sincere prayers