Surah Yasin aya 68 , Swahili translation of the meaning Ayah.

  1. Arabic
  2. tafsir
  3. mp3
  4. English
Quran in Swahili QUR,ANI TUKUFU na tafsiri ya maana yake kwenye lugha ya Kiswahili - Ali Muhsen Alberwany & English - Sahih International : Surah Yasin aya 68 in arabic text(yaseen).
  
   
ayat 68 from Surah Ya-Sin

﴿وَمَن نُّعَمِّرْهُ نُنَكِّسْهُ فِي الْخَلْقِ ۖ أَفَلَا يَعْقِلُونَ
[ يس: 68]

Na tunaye mzeesha tunamrudisha nyuma katika umbo. Basi je! hawazingatii?

Surah Ya-Sin in Swahili

Swahili Translation - Al-Barwani

English - Sahih International


And he to whom We grant long life We reverse in creation; so will they not understand?


Tafsiri ya maana yake kwenye lugha ya Kiswahili


Na tunaye mzeesha tunamrudisha nyuma katika umbo. Basi je! hawazingatii?


Na tunaye mfanyia umri wake ukawa mrefu, tunamrudisha, kutoka nguvu akawa dhaifu. Basi je hawayazingatii haya wakayatia akilini ya uweza wetu kuyafanya haya, na wao wakajua kuwa dunia ni nyumba ya kupita ina mwisho wake, na kuwa Akhera ndiyo nyumba ya kubaki na kudumu? Na tunaye mfanyia umri wake uwe mrefu tunamrejesha awe kinyume na alivyo kuwa. Yaani baada ya kuwa na nguvu anakuwa dhaifu. Hayo ni kwa kuwa maisha ya mwanaadamu yanapitia vipindi vitatu, kukua, kutimia kukua; na ukongwe unaanza kwa kunywea kwa mafigo, ini, Ghudda Ddarqiya au Thyroid gland, na Pancreas, yaani Dongoronya. Na haya huleta athari katika kudhoofika mwili wote. Mishipa ya damu nayo huanza kukacha na kunywea, na kwa hivyo hupunguka damu inayo kwenda katika viungo vyote vya mwili, basi ndio huzidi udhaifu juu ya udhaifu. Na katika sababu za kukonga ni kuzidi nguvu za kubomoka kuliko kujengeka katika mwili, yaani Metabolism. Na hayo ni kwa kuwa Khalaya au Cells, za mwili zote zimo katika hali ya kugeuka, na pia Khalaya za damu, isipo kuwa Khalaya za ubongo wa kichwani na wa katika mifupa. Hizo hazigeuki muda wote wa uhai. Ikiwa kiasi ya kuundika upya ni sawa ya kiasi cha kuharibika, basi hapana madhara yanayo tokea. Lakini ikiwa kuharibika ni kukubwa kuliko kujengeka katika kiungo chochote basi hapo hudhihiri madhara kwenye kiungo hicho. Na kwa hivyo kila umri ukiwa mkubwa kiasi cha kujengeka kinapungua na kinazidi kiasi cha kubomoka kwa Khalaya, na kunadhihiri kunywea, na kupungua nguvu kote. Na hukhitalifiana kiasi cha kujengeka kwa mnasaba wa kubomoka kwa kukhitalifiana namna ya mfumo (Nasiij, Texture). Katika hayo yanayo dhihiri kama ngozi iliyo funika mwili, na zilio funika paipu za kusaga chakula, na paipu za Ghudad, Glands, zinachakaa kwa upesi zaidi kila miaka ya binaadamu ikipita. Na hii ni sababu ya kuonekana upesi alama za kuzeeka.

English Türkçe Indonesia
Русский Français فارسی
تفسير Bengali Urdu

listen to Verse 68 from Yasin


Ayats from Quran in Swahili


Quran Surah in Swahili :

Al-Baqarah Al-'Imran An-Nisa'
Al-Ma'idah Yusuf Ibrahim
Al-Hijr Al-Kahf Maryam
Al-Hajj Al-Qasas Al-'Ankabut
As-Sajdah Ya Sin Ad-Dukhan
Al-Fath Al-Hujurat Qaf
An-Najm Ar-Rahman Al-Waqi'ah
Al-Hashr Al-Mulk Al-Haqqah
Al-Inshiqaq Al-A'la Al-Ghashiyah

Download Surah Yasin with the voice of the most famous Quran reciters :

Surah Yasin mp3 : choose the reciter to listen and download the chapter Yasin Complete with high quality
Surah Yasin Ahmed El Agamy
Ahmed Al Ajmy
Surah Yasin Bandar Balila
Bandar Balila
Surah Yasin Khalid Al Jalil
Khalid Al Jalil
Surah Yasin Saad Al Ghamdi
Saad Al Ghamdi
Surah Yasin Saud Al Shuraim
Saud Al Shuraim
Surah Yasin Abdul Basit Abdul Samad
Abdul Basit
Surah Yasin Abdul Rashid Sufi
Abdul Rashid Sufi
Surah Yasin Abdullah Basfar
Abdullah Basfar
Surah Yasin Abdullah Awwad Al Juhani
Abdullah Al Juhani
Surah Yasin Fares Abbad
Fares Abbad
Surah Yasin Maher Al Muaiqly
Maher Al Muaiqly
Surah Yasin Muhammad Siddiq Al Minshawi
Al Minshawi
Surah Yasin Al Hosary
Al Hosary
Surah Yasin Al-afasi
Mishari Al-afasi
Surah Yasin Yasser Al Dosari
Yasser Al Dosari


Sunday, May 19, 2024

لا تنسنا من دعوة صالحة بظهر الغيب