Surah Nahl aya 15 , Swahili translation of the meaning Ayah.
﴿وَأَلْقَىٰ فِي الْأَرْضِ رَوَاسِيَ أَن تَمِيدَ بِكُمْ وَأَنْهَارًا وَسُبُلًا لَّعَلَّكُمْ تَهْتَدُونَ﴾
[ النحل: 15]
Na kaweka katika ardhi milima ili ardhi isiyumbe yumbe nanyi. Na mito, na njia ili mpate kuongoka.
Surah An-Nahl in SwahiliSwahili Translation - Al-Barwani
English - Sahih International
And He has cast into the earth firmly set mountains, lest it shift with you, and [made] rivers and roads, that you may be guided,
Tafsiri ya maana yake kwenye lugha ya Kiswahili
Na kaweka katika ardhi milima ili ardhi isiyumbe yumbe nanyi.Na mito, na njia ili mpate kuongoka.
Na Mwenyezi Mungu amefanya katika ardhi milima iliyo simama imara, ili kuizuia isiyumbe yumbe.(Mwaka 1956 wataalamu wa geology, ilimu ya tabaka za ardhi, wamegundua kuwa kweli milima inasaidia kuizuia ardhi isitaharaki na kuachana. Wamevumbua kuwa mabara, continents, yamo katika kutaharaki. Kwa mfano kusini ya Amerika iliambatana na Afrika ya Magharibi, na ilisota mpaka ikafanyikana milima ya Andes. Hali kadhaalika Milima ya Himalaya ikazuia kusota kwa Bara Hindi. Pia wamegundua kuwa maki ya gamba la ardhi kwa kawaida halizidi kilomita 6, lakini chini ya milima hufika hata kilomita 35. Basi ni kweli kuwa milima ni kama vigingi vya kuzuia ardhi isiyumbe, kama ilivyo sema Qurani miaka 1400 iliyo pita.) Na Mwenyezi Mungu amefanya katika ardhi mito inayo pita na maji yanayo faa kunywa na kunyweshea makulima, na njia zilizo tengenezwa ili mpate kuzipitia kwendea mtakako.
| English | Türkçe | Indonesia |
| Русский | Français | فارسی |
| تفسير | Bengali | Urdu |
Ayats from Quran in Swahili
- (Musa) akasema: Nilitenda hayo hapo nilipo kuwa miongoni mwa wale walio potea.
- Kwa hakika Mwenyezi Mungu anawajua hao wanao zuilia, na wanao waambia ndugu zao: Njooni kwetu!
- Na mlipo kutana akakuonyesheni machoni mwenu kuwa wao ni wachache, na akakufanyeni nyinyi ni wachache
- Hakika wanaafiki wanamkhadaa Mwenyezi Mungu, na hali ni Yeye ndiye mwenye kuwakhadaa wao. Na wanapo
- Na nini kitakujuulisha pengine yeye atatakasika?
- Basi waache mpaka wakutane na siku yao watakapo hilikishwa.
- Na ikamsikiliza Mola wake Mlezi, na ikapasiwa kumsikiliza,
- Na bila ya shaka hii ni Uteremsho wa Mola Mlezi wa walimwengu wote.
- Na kila jambo walilo lifanya limo vitabuni.
- Walio kufuru na wakazuilia njia ya Mwenyezi Mungu, Yeye atavipotoa vitendo vyao.
Quran Surah in Swahili :
Download Surah Nahl with the voice of the most famous Quran reciters :
Surah Nahl mp3 : choose the reciter to listen and download the chapter Nahl Complete with high quality
Ahmed Al Ajmy
Bandar Balila
Khalid Al Jalil
Saad Al Ghamdi
Saud Al Shuraim
Abdul Basit
Ammar Al-Mulla
Abdullah Basfar
Abdullah Al Juhani
Fares Abbad
Maher Al Muaiqly
Al Minshawi
Al Hosary
Mishari Al-afasi
Yasser Al Dosari
Please remember us in your sincere prayers



