Surah Hijr aya 22 , Swahili translation of the meaning Ayah.

  1. Arabic
  2. tafsir
  3. mp3
  4. English
Quran in Swahili QUR,ANI TUKUFU na tafsiri ya maana yake kwenye lugha ya Kiswahili - Ali Muhsen Alberwany & English - Sahih International : Surah Hijr aya 22 in arabic text(Al-Hijr City).
  
   

﴿وَأَرْسَلْنَا الرِّيَاحَ لَوَاقِحَ فَأَنزَلْنَا مِنَ السَّمَاءِ مَاءً فَأَسْقَيْنَاكُمُوهُ وَمَا أَنتُمْ لَهُ بِخَازِنِينَ﴾
[ الحجر: 22]

Na tunazipeleka pepo za kupandishia, na tunateremsha kutoka mbinguni maji, kisha tukakunywesheni maji hayo. Wala si nyinyi mnayo yaweka.

Surah Al-Hijr in Swahili

Swahili Translation - Al-Barwani

English - Sahih International


And We have sent the fertilizing winds and sent down water from the sky and given you drink from it. And you are not its retainers.


Tafsiri ya maana yake kwenye lugha ya Kiswahili


Na tunazipeleka pepo za kupandishia, na tunateremsha kutoka mbinguni maji, kisha tukakunywesheni maji hayo. Wala si nyinyi mnayo yaweka.


Na Sisi tulipeleka pepo zilizo beba mvua na zilizo beba mbegu za mimea, na tukateremsha maji ya kukunywesheni. Na hayo ni kwa kufuata vile tutakavyo. Na yeyote yule hawezi kuyatenda kama hayo ila awe nayo kwake kama mahodhi au mabirika. Aya hii imeitangulia sayansi kwa kusema kuwa upepo unafanya kazi kubwa katika kubeba pollen, chembe dume za kupandishia mimea, kupelekea sehemu za uke za mimea mingine, na kwa hivyo yakazalikana mazao. Na pia haikujuulikana ila mwanzo wa karne hii tuliyo nayo kwamba upepo unazalisha mawingu yanayo nyesha mvua. Kwani -Nucleons- ambazo juu yake hujumuika sehemu za mvuke wa maji na zikawa chembe chembe za maji ndani ya wingu, ndizo chanzo cha mvua inayo chukuliwa na pepo kupelekwa kwenye majimbo yanayo fikiwa na mawingu. Misingi ya hizo -Nucleons- ni chumvi ya bahari, na vinavyo chukuliwa na upepo juu ya uso wa ardhi, na -Oxides- na vumbi vumbi, n.k. Na vyote hivyo ni lazima kwa ajili ya mvua. -Wala si nyinyi mnayo yaweka-. Imethibiti kwa sayansi ya kisasa kuwa mvua inaanza kwa mvuke kutokana na uso wa ardhi na bahari, kisha inarejea hali ile ile tena kama ilivyo tajwa. Ikinya mvua hunywesha kila kilicho na uhai katika ardhi, na huinywesha ardhi yenyewe. Wala haiwezekani kuzuilika, kwa sababu ikichuruzika kutokana na vyote vyenye uhai na katika ardhi ikaingia baharini, tena kisha huanza kuzunguka mara ya pili kwa kupanda mvuke kutoka baharini. Basi hali ni hivyo mzunguko. Hapa ndio inabainika maana ya Aya -Wala si nyinyi mnayo yaweka.-

English Türkçe Indonesia
Русский Français فارسی
تفسير Bengali Urdu

listen to Verse 22 from Hijr


Ayats from Quran in Swahili

  1. Sema: Tembeeni katika ardhi na tazameni jinsi alivyo anzisha uumbaji; kisha Mwenyezi Mungu ndiye anaye
  2. Walipo tukasirisha tuliwapatiliza tukawazamisha wote!
  3. Na kwa yakini tulimpa Musa ishara tisa zilizo wazi. Waulize Wana wa Israili alipo wafikia,
  4. Nikasema: Ombeni msamaha kwa Mola wenu Mlezi; hakika Yeye ni Mwingi wa kusamehe.
  5. Hakika katika kuumbwa mbingu na ardhi na kukhitalifiana usiku na mchana ziko Ishara kwa wenye
  6. Na tutayaendea yale waliyo yatenda katika vitendo vyao, tuvifanye kama mavumbi yaliyo tawanyika.
  7. Yeye ndiye aliye lijaalia jua kuwa na mwangaza, na mwezi ukawa na nuru, na akaupimia
  8. Na tulipo chukua ahadi yenu na tukauinua mlima juu yenu (tukakwambieni): Kamateni kwa nguvu haya
  9. Na ikiwa kanzu yake imechanwa nyuma, basi mwanamke amesema uwongo, naye Yusuf ni katika wakweli.
  10. Basi Firauni akataka kuwafukuza katika nchi. Kwa hivyo tukamzamisha yeye na walio kuwa pamoja naye

Quran Surah in Swahili :

Al-Baqarah Al-'Imran An-Nisa'
Al-Ma'idah Yusuf Ibrahim
Al-Hijr Al-Kahf Maryam
Al-Hajj Al-Qasas Al-'Ankabut
As-Sajdah Ya Sin Ad-Dukhan
Al-Fath Al-Hujurat Qaf
An-Najm Ar-Rahman Al-Waqi'ah
Al-Hashr Al-Mulk Al-Haqqah
Al-Inshiqaq Al-A'la Al-Ghashiyah

Download Surah Hijr with the voice of the most famous Quran reciters :

Surah Hijr mp3 : choose the reciter to listen and download the chapter Hijr Complete with high quality
Surah Hijr Ahmed El Agamy
Ahmed Al Ajmy
Surah Hijr Bandar Balila
Bandar Balila
Surah Hijr Khalid Al Jalil
Khalid Al Jalil
Surah Hijr Saad Al Ghamdi
Saad Al Ghamdi
Surah Hijr Saud Al Shuraim
Saud Al Shuraim
Surah Hijr Abdul Basit Abdul Samad
Abdul Basit
Surah Hijr Abdul Rashid Sufi
Abdul Rashid Sufi
Surah Hijr Abdullah Basfar
Abdullah Basfar
Surah Hijr Abdullah Awwad Al Juhani
Abdullah Al Juhani
Surah Hijr Fares Abbad
Fares Abbad
Surah Hijr Maher Al Muaiqly
Maher Al Muaiqly
Surah Hijr Muhammad Siddiq Al Minshawi
Al Minshawi
Surah Hijr Al Hosary
Al Hosary
Surah Hijr Al-afasi
Mishari Al-afasi
Surah Hijr Yasser Al Dosari
Yasser Al Dosari


Tuesday, July 16, 2024

Please remember us in your sincere prayers