Surah Saba aya 28 , Swahili translation of the meaning Ayah.
﴿وَمَا أَرْسَلْنَاكَ إِلَّا كَافَّةً لِّلنَّاسِ بَشِيرًا وَنَذِيرًا وَلَٰكِنَّ أَكْثَرَ النَّاسِ لَا يَعْلَمُونَ﴾
[ سبأ: 28]
Na hatukukutuma ila kwa watu wote, uwe mbashiri, na mwonyaji. Lakini watu wengi hawajui.
Surah Saba in SwahiliSwahili Translation - Al-Barwani
English - Sahih International
And We have not sent you except comprehensively to mankind as a bringer of good tidings and a warner. But most of the people do not know.
Tafsiri ya maana yake kwenye lugha ya Kiswahili
Na hatukukutuma ila kwa watu wote, uwe mbashiri, na mwonyaji. Lakini watu wengi hawajui.
Na Sisi hatukukutuma ewe Muhammad, ila kwa watu wote. Uwe ni mwenye kuwabashiria Waumini kuwa watapata kheri, na mwenye kuwaonya makafiri kuwa watapata shari. Lakini aghlabu ya watu hawaujui ukweli wako, wala kuwa Utume wako ni wa kwa watu wote. (Haya ni kwa sababu hapana Mtume aliye kuja kwa watu wote ila huyu Nabii Muhammad s.a.w. Nabii Musa alikuja kwa Wana wa Israili kuwatoa Misri. Nabii Isa, Yesu Kristo, pia kaja kwa Wana wa Israili tu, kama isemavyo Qurani 3.49, na Injili ya Mathayo 10.5-6 Yesu alipo sema: -Afadhali shikeni njia kuwaendea kondoo waliopotea wa nyumba ya Israeli.- Na 15.24 alipo sema: -Sikutumwa ila kwa kondoo waliopotea wa nyumba ya Israeli.- Na Injili ya Yohana 17.9)
| English | Türkçe | Indonesia |
| Русский | Français | فارسی |
| تفسير | Bengali | Urdu |
Ayats from Quran in Swahili
- Na tutawafanya vijana,
- Hakika Yeye ndiye Mwenye kusikia Mwenye kujua.
- Akasema: Kweli amekudhulumu kwa kumtaka kondoo wako mmoja kuongezea kwenye kondoo wake. Na hakika washirika
- Basi hao huenda Mwenyezi Mungu akawasamehe. Na Mwenyezi Mungu ni Mwingi wa kusamehe, Mwingi wa
- Akasema: Hebu nini amri yenu, enyi wajumbe?
- Msiombe kufa mara moja tu, bali mfe mara nyingi!
- Na namna hivi tuliwa juulisha kwa watu wapate kujua ya kwamba ahadi ya Mwenyezi Mungu
- Na hakika Mola wako Mlezi atawatimilizia malipo ya vitendo vyao. Hakika Yeye anayo khabari ya
- Akasema Zakariya: Mola wangu Mlezi! Vipi nitapata mwana na hali ukongwe umenifikia, na mke wangu
- Au wewe unawaomba ujira, na kwa hivyo ndio wanaelemewa na uzito wa gharama?
Quran Surah in Swahili :
Download Surah Saba with the voice of the most famous Quran reciters :
Surah Saba mp3 : choose the reciter to listen and download the chapter Saba Complete with high quality
Ahmed Al Ajmy
Bandar Balila
Khalid Al Jalil
Saad Al Ghamdi
Saud Al Shuraim
Abdul Basit
Ammar Al-Mulla
Abdullah Basfar
Abdullah Al Juhani
Fares Abbad
Maher Al Muaiqly
Al Minshawi
Al Hosary
Mishari Al-afasi
Yasser Al Dosari
Please remember us in your sincere prayers



