Surah Maidah aya 38 , Swahili translation of the meaning Ayah.
﴿وَالسَّارِقُ وَالسَّارِقَةُ فَاقْطَعُوا أَيْدِيَهُمَا جَزَاءً بِمَا كَسَبَا نَكَالًا مِّنَ اللَّهِ ۗ وَاللَّهُ عَزِيزٌ حَكِيمٌ﴾
[ المائدة: 38]
Na mwizi mwanamume na mwizi mwanamke, ikateni mikono yao, hayo ni malipo ya waliyo yachuma, ndiyo adhabu ya mfano itokayo kwa Mwenyezi Mungu. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye nguvu na Mwenye hikima.
Surah Al-Maidah in SwahiliSwahili Translation - Al-Barwani
English - Sahih International
[As for] the thief, the male and the female, amputate their hands in recompense for what they committed as a deterrent [punishment] from Allah. And Allah is Exalted in Might and Wise.
Tafsiri ya maana yake kwenye lugha ya Kiswahili
Na mwizi mwanamume na mwizi mwanamke, ikateni mikono yao, hayo ni malipo ya waliyo yachuma, ndiyo adhabu ya mfano itokayo kwa Mwenyezi Mungu. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye nguvu na Mwenye hikima.
Na mwanamume aliye iba, na mwanamke aliye iba, ikateni mikono yao kuwa ni malipo ya madhambi waliyo yatenda, na njia ya kuwaonya wenginewe wasitende jambo hilo. Hiyo ni hukumu ya Mwenyezi Mungu, na amri ya Mwenyezi Mungu ndiyo yenye kushinda, naye ndiye Mwenye hikima katika kutunga Sharia. Kila ukhalifu ameuwekea malipo yake, yenye kumzuia mtu asitende tena na wengine watahadhari wasifanye kama hayo. (Ajabu iliopo ni kuwepo wajinga wakashtushwa na amri hii ya Mwenyezi Mungu aliye tuumba, na wasiseme lolote kuwa katika China wakati wa vita na Taiwan ilikuwapo sharia ya kuwa mwizi auwawe, na katika baadhi ya wilaya za Amerika mpaka hii leo ipo sharia ya kuwa mwizi wa farasi auwawe, na katika Kenya adabu ya wizi wa kutumia nguvu ni kunyongwa, na katika sharia za Kiingereza na nchi zote za magharibi mtu ana haki ya kuuwa kwa ajili ya kulinda mali na roho. Ikiwa ni haki ya mtu kumuuwa atakaye kuja kwiba, jee ni kuu hilo kwa serikali kumkata mkono aliye kwisha iba?) Kwa kuwepo sharia kama hii ndiyo ikawa wizi umetoweka katika nchi kama Saudi Arabia, na ukawa vururu kwengineko.
English | Türkçe | Indonesia |
Русский | Français | فارسی |
تفسير | Bengali | Urdu |
Ayats from Quran in Swahili
- Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
- Au akaangushiwa khazina juu yake, au akawa na bustani ale katika hiyo? Wakasema madhaalimu: Nyinyi
- Na tuna nini hata tusimtegemee Mwenyezi Mungu, na hali Yeye ametuongoa kwenye Njia zetu. Na
- Na Zakariya alipo mwita Mola wake Mlezi: Mola wangu Mlezi! Usiniache peke yangu, na Wewe
- Sema: Mwenyezi Mungu tu namuabudu kwa kumsafishia Yeye tu Dini yangu.
- Na kama wakigeuka basi jueni kwamba Mwenyezi Mungu ndiye Mola wenu, ni Mola Mwema na
- Je! Wao hawaoni jinsi Mwenyezi Mungu anavyo anzisha uumbaji, na kisha akarudisha tena. Hakika hayo
- Na Nuhu alipo ita zamani, nasi tukamuitikia, na tukamwokoa yeye na watu wake kutokana na
- Na wanasema: Lini ahadi hii, ikiwa mnasema kweli?
- Wakasema: Ametakasika Mola wetu Mlezi! Hakika sisi tulikuwa wenye kudhulumu.
Quran Surah in Swahili :
Download Surah Maidah with the voice of the most famous Quran reciters :
Surah Maidah mp3 : choose the reciter to listen and download the chapter Maidah Complete with high quality
Ahmed Al Ajmy
Bandar Balila
Khalid Al Jalil
Saad Al Ghamdi
Saud Al Shuraim
Abdul Basit
Abdul Rashid Sufi
Abdullah Basfar
Abdullah Al Juhani
Fares Abbad
Maher Al Muaiqly
Al Minshawi
Al Hosary
Mishari Al-afasi
Yasser Al Dosari
Please remember us in your sincere prayers