Surah Najm aya 49 , Swahili translation of the meaning Ayah.
﴿وَأَنَّهُ هُوَ رَبُّ الشِّعْرَىٰ﴾
[ النجم: 49]
Na kwamba hakika Yeye ndiye Mola Mlezi wa nyota ya Shii'ra.
Surah An-Najm in SwahiliSwahili Translation - Al-Barwani
English - Sahih International
And that it is He who is the Lord of Sirius
Tafsiri ya maana yake kwenye lugha ya Kiswahili
Na kwamba hakika Yeye ndiye Mola Mlezi wa nyota ya Shiira.
Na hakika Yeye ndiye Mola Mlezi wa hii nyota kubwa inayo itwa Shiira (Sirius, Dog Star). Makusudio hapa ni Nyota hiyo inayo itwa Ash-shira Alyamaaniya, au wanavyo ita Wazungu Sirius au Dog Star. Nyota hii inangara kwa nguvu zaidi kuliko nyota zote ziliomo katika kikundi cha nyota kinacho itwa Alkalbu l-akbar, kwa Kizungu Canis Major au Greater Dog. Nyota hiyo ndiyo inayo zagaa sana mbinguni, na huonekana kusini ya mstari wa kati wa mbinguni kiasi ya daraja 18. Na kwa jina hilo la Nyota ya Mbwa ikijuulikana hata miaka elfu tatu ilio pita. Katika mabaki ya michoro ya Mafirauni wa Misri imeashiriwa pia. Mwenyezi Mungu ameitaja khasa kwa kuwa Waarabu walikuwa wakiiabudu hapo kale, na pia Wamisri wa zamani, kwani kutokea kwake upande wa mashariki katikati ya mwezi wa Julai kabla ya kuchomoza jua kulikuwa kunawafikiana na wakati wa mafuriko ya Misri ya kati, yaani katika tukio muhimu kabisa katika ulimwengu huo wa kale. Na tukio hili huenda ndilo lilio fanya kuanzisha kuwekea kiwango urefu wa mwaka katika dunia nzima. Kwani kudhihiri Nyota ya Shiira kabla ya kuchomoza jua hakutokei ila mara moja tu katika mwaka. Basi huu ndio mwanzo wa mwaka mpya.
| English | Türkçe | Indonesia |
| Русский | Français | فارسی |
| تفسير | Bengali | Urdu |
Ayats from Quran in Swahili
- Hapana shaka ya kwamba hao ndio wenye kukhasiri Akhera.
- Na mfalme akasema: Mleteni kwangu! Basi mjumbe alipo mjia Yusuf alisema: Rejea kwa bwana wako
- Mwenyezi Mungu ndiye aliye umba mbingu na ardhi na viliomo baina yao kwa siku sita,
- Hakika wewe ni miongoni mwa walio tumwa,
- Siku hiyo uombezi haufai kitu, ila wa aliye mruhusu Arrahmani Mwingi wa Rehema na akamridhia
- Tena mtakunywa kama wanavyo kunywa ngamia wenye kiu.
- Enyi mlio amini! Mnapo nong'ona msinong'one kwa sababu ya mambo ya madhambi, na uadui, na
- Na pale ulipo toka asubuhi, ukaacha ahali zako uwapange Waumini kwenye vituo kwa ajili ya
- Je! Tuwafanye walio amini na wakatenda mema kama wafanyao uharibifu katika nchi? Au tuwafanye wachamngu
- Hakika Mwenyezi Mungu ndiye mpasuaji mbegu na kokwa, zikachipua. Humtoa aliye hai kutoka maiti, naye
Quran Surah in Swahili :
Download Surah Najm with the voice of the most famous Quran reciters :
Surah Najm mp3 : choose the reciter to listen and download the chapter Najm Complete with high quality
Ahmed Al Ajmy
Bandar Balila
Khalid Al Jalil
Saad Al Ghamdi
Saud Al Shuraim
Abdul Basit
Ammar Al-Mulla
Abdullah Basfar
Abdullah Al Juhani
Fares Abbad
Maher Al Muaiqly
Al Minshawi
Al Hosary
Mishari Al-afasi
Yasser Al Dosari
Please remember us in your sincere prayers



