Surah Qasas aya 73 , Swahili translation of the meaning Ayah.

  1. Arabic
  2. tafsir
  3. mp3
  4. English
Quran in Swahili QUR,ANI TUKUFU na tafsiri ya maana yake kwenye lugha ya Kiswahili - Ali Muhsen Alberwany & English - Sahih International : Surah Qasas aya 73 in arabic text(The Stories).
  
   

﴿وَمِن رَّحْمَتِهِ جَعَلَ لَكُمُ اللَّيْلَ وَالنَّهَارَ لِتَسْكُنُوا فِيهِ وَلِتَبْتَغُوا مِن فَضْلِهِ وَلَعَلَّكُمْ تَشْكُرُونَ﴾
[ القصص: 73]

Na ni katika rehema zake amekufanyieni usiku na mchana mpate kupumzika humo na mtafute fadhila zake, na ili mpate kushukuru.

Surah Al-Qasas in Swahili

Swahili Translation - Al-Barwani

English - Sahih International


And out of His mercy He made for you the night and the day that you may rest therein and [by day] seek from His bounty and [that] perhaps you will be grateful.


Tafsiri ya maana yake kwenye lugha ya Kiswahili


Na ni katika rehema zake amekufanyieni usiku na mchana mpate kupumzika humo na mtafute fadhila zake, na ili mpate kushukuru.


Na miongoni mwa rehema za Mwenyezi Mungu kwa viumbe vyake ni kuwa kawaumbia usiku na mchana, inayo fuatana, ili wapate kupumzika usiku, na washughulikie kutafuta riziki zao na manufaa yao mengine wakati wa mchana, na watambue fadhila za Mwenyezi Mungu juu yao wapate kumshukuru. -Sema: Mwaonaje, Mwenyezi Mungu angeli ufanya usiku umekukalieni moja kwa moja, mungu gani asiye kuwa Mwenyezi Mungu atakaye kuleteeni mwangaza? Basi je, hamsikii? Sema: Mwaonaje, Mwenyezi Mungu angeli ufanya mchana umekukalieni moja kwa moja mpaka Siku ya Kiyama, mungu gani asiye kuwa Mwenyezi Mungu ataye kuleteeni usiku mkapumzika humo? Basi je, hamwoni? Na ni katika rehema zake amekufanyieni usiku na mchana mpate kupumzika humo na mtafute fadhila zake, na ili mpate kushukuru.- Hapana shaka kuwa kuumbwa kwa dunia kwa namna yake ilivyo sasa na ilivyo wekwa kwa mnasaba wa jua, na kuzunguka kwake wenyewe kwa wenyewe kila siku, na kulizunguka jua kila mwaka, hapana shaka kwamba haya yanaonyesha dhaahiri uwezo wa Mwenyezi Mungu na upweke wake. Na Aya tukufu inawazindua watu watambue ukweli ambao yawapasa wauelewe, nao ni kwamba Yeye Mtukufu lau kuwa aliumba dunia iwe na usiku wa milele, au iwe na mchana wa milele, basi hapanapo mungu mwengine anaye weza kuwaneemesha watu kwa mchana na usiku wa kufuatana kama hivi. Na hivyo ni kuwa lau kuwa dunia inazunguka juu ya msumari-kati wake na pia kulizunguka jua kwa kiwango kimoja kiasi ya siku 365 takriban, yangeli tokea mabadiliko makubwa mno. Miongoni mwao ni kudumu giza katika nusu ya dunia, na kudumu mwangaza katika nusu ya pili takriban. Na kwa hivi joto lingeli panda katika nusu yenye mwangaza kwa kiasi kisicho weza kuchukulika. Na nusu yenye giza ingeganda kwa barafu. Na pande zote mbili zisingeweza kuchukua kitu chochote chenye uhai. Ama huu mpango ulivyo sasa unapelekea kupishana usiku na mchana, na kwa hivyo kunapatikana mapumziko na utulivu wakati wa usiku, na kushughulika wakati wa mchana. Na hali ya hewa inasilihi uhai wa binaadamu, na wanyama, na mimea. Na haya ni katika fadhila za Mwenyezi Mungu juu ya waja wake, ambazo zinapelekea tukubali uwezo wake, na tudumu kumshukuru.

English Türkçe Indonesia
Русский Français فارسی
تفسير Bengali Urdu

listen to Verse 73 from Qasas


Ayats from Quran in Swahili


    Quran Surah in Swahili :

    Al-Baqarah Al-'Imran An-Nisa'
    Al-Ma'idah Yusuf Ibrahim
    Al-Hijr Al-Kahf Maryam
    Al-Hajj Al-Qasas Al-'Ankabut
    As-Sajdah Ya Sin Ad-Dukhan
    Al-Fath Al-Hujurat Qaf
    An-Najm Ar-Rahman Al-Waqi'ah
    Al-Hashr Al-Mulk Al-Haqqah
    Al-Inshiqaq Al-A'la Al-Ghashiyah

    Download Surah Qasas with the voice of the most famous Quran reciters :

    Surah Qasas mp3 : choose the reciter to listen and download the chapter Qasas Complete with high quality
    Surah Qasas Ahmed El Agamy
    Ahmed Al Ajmy
    Surah Qasas Bandar Balila
    Bandar Balila
    Surah Qasas Khalid Al Jalil
    Khalid Al Jalil
    Surah Qasas Saad Al Ghamdi
    Saad Al Ghamdi
    Surah Qasas Saud Al Shuraim
    Saud Al Shuraim
    Surah Qasas Abdul Basit Abdul Samad
    Abdul Basit
    Surah Qasas Ammar Al-Mulla
    Ammar Al-Mulla
    Surah Qasas Abdullah Basfar
    Abdullah Basfar
    Surah Qasas Abdullah Awwad Al Juhani
    Abdullah Al Juhani
    Surah Qasas Fares Abbad
    Fares Abbad
    Surah Qasas Maher Al Muaiqly
    Maher Al Muaiqly
    Surah Qasas Muhammad Siddiq Al Minshawi
    Al Minshawi
    Surah Qasas Al Hosary
    Al Hosary
    Surah Qasas Al-afasi
    Mishari Al-afasi
    Surah Qasas Yasser Al Dosari
    Yasser Al Dosari


    Friday, May 2, 2025

    Please remember us in your sincere prayers