Surah Anfal aya 60 , Swahili translation of the meaning Ayah.

  1. Arabic
  2. tafsir
  3. mp3
  4. English
Quran in Swahili QUR,ANI TUKUFU na tafsiri ya maana yake kwenye lugha ya Kiswahili - Ali Muhsen Alberwany & English - Sahih International : Surah Anfal aya 60 in arabic text(The Spoils of War).
  
   

﴿وَأَعِدُّوا لَهُم مَّا اسْتَطَعْتُم مِّن قُوَّةٍ وَمِن رِّبَاطِ الْخَيْلِ تُرْهِبُونَ بِهِ عَدُوَّ اللَّهِ وَعَدُوَّكُمْ وَآخَرِينَ مِن دُونِهِمْ لَا تَعْلَمُونَهُمُ اللَّهُ يَعْلَمُهُمْ ۚ وَمَا تُنفِقُوا مِن شَيْءٍ فِي سَبِيلِ اللَّهِ يُوَفَّ إِلَيْكُمْ وَأَنتُمْ لَا تُظْلَمُونَ
[ الأنفال: 60]

Basi waandalieni nguvu kama muwezavyo, na kwa farasi walio fungwa tayari-tayari, ili kuwatishia maadui wa Mwenyezi Mungu na maadui zenu, na wengineo ambao hamwajui, lakini Mwenyezi Mungu anawajua. Na mkitoa chochote katika Njia ya Mwenyezi Mungu mtarudishiwa, na wala nyinyi hamtadhulumiwa.

Surah Al-Anfal in Swahili

Swahili Translation - Al-Barwani

English - Sahih International


And prepare against them whatever you are able of power and of steeds of war by which you may terrify the enemy of Allah and your enemy and others besides them whom you do not know [but] whom Allah knows. And whatever you spend in the cause of Allah will be fully repaid to you, and you will not be wronged.


Tafsiri ya maana yake kwenye lugha ya Kiswahili


Basi waandalieni nguvu kama muwezavyo, na kwa farasi walio fungwa tayari-tayari, ili kuwatishia maadui wa Mwenyezi Mungu na maadui zenu, na wengineo ambao hamwajui, lakini Mwenyezi Mungu anawajua. Na mkitoa chochote katika Njia ya Mwenyezi Mungu mtarudishiwa, na wala nyinyi hamtadhulumiwa.


Enyi Umma wa Kiislamu! Tayarisheni kila muwezavyo nguvu za vita za namna zote kwa ajili ya kujizatiti kwa ajili ya kupigana, na wekeni askari walinzi na farasi wao mipakani na kando kando ya nchi, ili kwa hivi mjitayarishe na ulinzi mwatie kiwewe adui za Mwenyezi Mungu na adui zenu miongoni mwa hao makafiri ambao wamo kungojea likupateni jambo. Na pia mpate kuwatishia wenginewe ambao nyinyi hamwajui hivi sasa, lakini Mwenyezi Mungu anawajua, kwani hapana jambo linalo jificha kwake. Na kila mnacho kitoa kwa kuzitayarisha nguvu zenu kwa ajili ya Mwenyezi Mungu, basi Yeye atakulipeni malipo ya kutosha, bila ya kupunguka hata chembe katika mnayo stahiki katika fadhila ya Mola wenu Mlezi Katika Aya hii tukufu pana kuhimizwa na kuamrishwa kujitayarisha kwa ajili ya kupambana na adui. Kwani vita, zamani na sasa, ni jambo la khatari na muhimu kabisa. Juu yake inategemea kheri na shari, kufa kupona kwa umati na umati. Basi yapasa kujitayarisha, kujizatiti, na kujitengeneza kwa jiha mbali mbali za vifaa na silaha na zana. Kuingia vitani bila ya kujipatia zana zote na kujitayarisha ni kutafuta kushindwa. Na tunaona hivi sasa madola yanavyo jiandaa wakati wa amani na vita, na yanavyo jenga siasa zao na mipango yao na wanavyo kusanya uwezekano wao wote ili wapate ushindi katika vita. Na vita sasa havimsazi mtu. Wanashiriki katika vita wanajeshi na raia. Kwa hivyo ndio inapasa zaidi kujitengeneza kila mmoja wao kwa matengenezo ya kuwakusanya na kuwaweka tayari wote ili upatikane ushindi.

English Türkçe Indonesia
Русский Français فارسی
تفسير Bengali Urdu

listen to Verse 60 from Anfal


Ayats from Quran in Swahili

  1. Na Musa alisema: Ewe Firauni! Hakika mimi ni Mtume nitokaye kwa Mola Mlezi wa viumbe
  2. Sema: Mwenyezi Mungu anatosha kuwa Shahidi baina yangu na nyinyi. Hakika Yeye anawajua vyema waja
  3. Kauli yetu kwa kitu tunacho kitaka kiwe, ni kukiambia: Kuwa! Basi kinakuwa.
  4. Mitume wao wakasema: Ati pana shaka na Mwenyezi Mungu, Muumba mbingu na ardhi? Yeye anakuiteni
  5. Wala wasikuhuzunishe wale wanao kimbilia ukafirini. Hakika hao hawamdhuru kitu Mwenyezi Mungu. Mwenyezi Mungu anataka
  6. Mwenye kutaka utukufu basi utukufu wote uko kwa Mwenyezi Mungu. Kwake Yeye hupanda neno zuri,
  7. Basi usimwombe mungu mwingine pamoja na Mwenyezi Mungu ukawa miongoni mwa watakao adhibiwa.
  8. Na atakaye mjia naye ni Muumini aliye tenda mema, basi hao ndio wenye vyeo vya
  9. Hakika yeye ni katika waja wetu walio amini.
  10. Mnadhani mko salama kwa alioko juu kuwa hatakudidimizeni kwenye ardhi, na tahamaki hiyo inatikisika!

Quran Surah in Swahili :

Al-Baqarah Al-'Imran An-Nisa'
Al-Ma'idah Yusuf Ibrahim
Al-Hijr Al-Kahf Maryam
Al-Hajj Al-Qasas Al-'Ankabut
As-Sajdah Ya Sin Ad-Dukhan
Al-Fath Al-Hujurat Qaf
An-Najm Ar-Rahman Al-Waqi'ah
Al-Hashr Al-Mulk Al-Haqqah
Al-Inshiqaq Al-A'la Al-Ghashiyah

Download Surah Anfal with the voice of the most famous Quran reciters :

Surah Anfal mp3 : choose the reciter to listen and download the chapter Anfal Complete with high quality
Surah Anfal Ahmed El Agamy
Ahmed Al Ajmy
Surah Anfal Bandar Balila
Bandar Balila
Surah Anfal Khalid Al Jalil
Khalid Al Jalil
Surah Anfal Saad Al Ghamdi
Saad Al Ghamdi
Surah Anfal Saud Al Shuraim
Saud Al Shuraim
Surah Anfal Abdul Basit Abdul Samad
Abdul Basit
Surah Anfal Abdul Rashid Sufi
Abdul Rashid Sufi
Surah Anfal Abdullah Basfar
Abdullah Basfar
Surah Anfal Abdullah Awwad Al Juhani
Abdullah Al Juhani
Surah Anfal Fares Abbad
Fares Abbad
Surah Anfal Maher Al Muaiqly
Maher Al Muaiqly
Surah Anfal Muhammad Siddiq Al Minshawi
Al Minshawi
Surah Anfal Al Hosary
Al Hosary
Surah Anfal Al-afasi
Mishari Al-afasi
Surah Anfal Yasser Al Dosari
Yasser Al Dosari


Friday, May 10, 2024

لا تنسنا من دعوة صالحة بظهر الغيب