Fecr suresi çevirisi Svahili

  1. Suresi mp3
  2. Başka bir sure
  3. Svahili
Kuranı Kerim türkçe meali | Kur'an çevirileri | Svahili dili | Fecr Suresi | الفجر - Ayet sayısı 30 - Moshaf'taki surenin numarası: 89 - surenin ingilizce anlamı: The Break of Day.

وَالْفَجْرِ(1)

 Naapa kwa alfajiri,

وَلَيَالٍ عَشْرٍ(2)

 Na kwa masiku kumi,

وَالشَّفْعِ وَالْوَتْرِ(3)

 Na kwa viwili viwili na kimoja kimoja,

وَاللَّيْلِ إِذَا يَسْرِ(4)

 Na kwa usiku unapo pita,

هَلْ فِي ذَٰلِكَ قَسَمٌ لِّذِي حِجْرٍ(5)

 Je! Hapana katika haya kiapo kwa mwenye akili?

أَلَمْ تَرَ كَيْفَ فَعَلَ رَبُّكَ بِعَادٍ(6)

 Kwani hukuona jinsi Mola wako Mlezi alivyo wafanya kina A'di?

إِرَمَ ذَاتِ الْعِمَادِ(7)

 Wa Iram, wenye majumba marefu?

الَّتِي لَمْ يُخْلَقْ مِثْلُهَا فِي الْبِلَادِ(8)

 Ambao haukuumbwa mfano wake katika nchi?

وَثَمُودَ الَّذِينَ جَابُوا الصَّخْرَ بِالْوَادِ(9)

 Na Thamudi walio chonga majabali huko bondeni?

وَفِرْعَوْنَ ذِي الْأَوْتَادِ(10)

 Na Firauni mwenye vigingi?

الَّذِينَ طَغَوْا فِي الْبِلَادِ(11)

 Ambao walifanya jeuri katika nchi?

فَأَكْثَرُوا فِيهَا الْفَسَادَ(12)

 Wakakithirisha humo ufisadi?

فَصَبَّ عَلَيْهِمْ رَبُّكَ سَوْطَ عَذَابٍ(13)

 Basi Mola wako Mlezi aliwapiga mjeledi wa adhabu.

إِنَّ رَبَّكَ لَبِالْمِرْصَادِ(14)

 Hakika Mola wako Mlezi yupo kwenye mavizio anawavizia.

فَأَمَّا الْإِنسَانُ إِذَا مَا ابْتَلَاهُ رَبُّهُ فَأَكْرَمَهُ وَنَعَّمَهُ فَيَقُولُ رَبِّي أَكْرَمَنِ(15)

 Ama mtu anapo jaribiwa na Mola wake Mlezi, akamkirimu na akamneemesha, husema: Mola wangu Mlezi amenikirimu!

وَأَمَّا إِذَا مَا ابْتَلَاهُ فَقَدَرَ عَلَيْهِ رِزْقَهُ فَيَقُولُ رَبِّي أَهَانَنِ(16)

 Na ama anapo mjaribu akampunguzia riziki yake, husema: Mola wangu Mlezi amenitia unyonge!

كَلَّا ۖ بَل لَّا تُكْرِمُونَ الْيَتِيمَ(17)

 Sivyo hivyo! Bali nyinyi hamuwakirimu mayatima,

وَلَا تَحَاضُّونَ عَلَىٰ طَعَامِ الْمِسْكِينِ(18)

 Wala hamhimizani kulisha masikini;

وَتَأْكُلُونَ التُّرَاثَ أَكْلًا لَّمًّا(19)

 Na mnakula urithi kwa ulaji wa pupa,

وَتُحِبُّونَ الْمَالَ حُبًّا جَمًّا(20)

 Na mnapenda mali pendo la kupita kiasi.

كَلَّا إِذَا دُكَّتِ الْأَرْضُ دَكًّا دَكًّا(21)

 Sivyo hivyo! Itakapo vunjwa ardhi vipande vipande,

وَجَاءَ رَبُّكَ وَالْمَلَكُ صَفًّا صَفًّا(22)

 Na akaja Mola wako Mlezi na Malaika safu safu,

وَجِيءَ يَوْمَئِذٍ بِجَهَنَّمَ ۚ يَوْمَئِذٍ يَتَذَكَّرُ الْإِنسَانُ وَأَنَّىٰ لَهُ الذِّكْرَىٰ(23)

 Na ikaletwa Jahannamu siku hiyo, siku hiyo mtu atakumbuka! Lakini kukumbuka huko kutamfaa nini?

يَقُولُ يَا لَيْتَنِي قَدَّمْتُ لِحَيَاتِي(24)

 Atasema: Laiti ningeli jitangulizia kwa uhai wangu!

فَيَوْمَئِذٍ لَّا يُعَذِّبُ عَذَابَهُ أَحَدٌ(25)

 Basi siku hiyo hataadhibu yeyote namna ya kuadhibu kwake.

وَلَا يُوثِقُ وَثَاقَهُ أَحَدٌ(26)

 Wala hatafunga yeyote kama kufunga kwake.

يَا أَيَّتُهَا النَّفْسُ الْمُطْمَئِنَّةُ(27)

 Ewe nafsi iliyo tua!

ارْجِعِي إِلَىٰ رَبِّكِ رَاضِيَةً مَّرْضِيَّةً(28)

 Rejea kwa Mola wako Mlezi umeridhika, na umemridhisha.

فَادْخُلِي فِي عِبَادِي(29)

 Basi ingia miongoni mwa waja wangu,

وَادْخُلِي جَنَّتِي(30)

 Na ingia katika Pepo yangu.


Svahili diğer sureler:

Bakara suresi Âl-i İmrân Nisâ suresi
Mâide suresi Yûsuf suresi İbrâhîm suresi
Hicr suresi Kehf suresi Meryem suresi
Hac suresi Kasas suresi Ankebût suresi
As-Sajdah Yâsîn suresi Duhân suresi
fetih suresi Hucurât suresi Kâf suresi
Necm suresi Rahmân suresi vakıa suresi
Haşr suresi Mülk suresi Hâkka suresi
İnşikâk suresi Alâ suresi Gâşiye suresi

En ünlü okuyucuların sesiyle Fecr Suresi indirin:

Surah Al-Fajr mp3: yüksek kalitede dinlemek ve indirmek için okuyucuyu seçerek
Fecr Suresi Ahmed El Agamy
Ahmed El Agamy
Fecr Suresi Saad Al Ghamdi
Saad Al Ghamdi
Fecr Suresi Saud Al Shuraim
Saud Al Shuraim
Fecr Suresi Abdul Basit Abdul Samad
Abdul Basit
Fecr Suresi Abdullah Basfar
Abdullah Basfar
Fecr Suresi Abdullah Awwad Al Juhani
Abdullah Al Juhani
Fecr Suresi Ali Al Hudhaifi
Ali Al Hudhaifi
Fecr Suresi Fares Abbad
Fares Abbad
Fecr Suresi Maher Al Muaiqly
Maher Al Muaiqly
Fecr Suresi Muhammad Jibril
Muhammad Jibril
Fecr Suresi Muhammad Siddiq Al Minshawi
Al Minshawi
Fecr Suresi Al Hosary
Al Hosary
Fecr Suresi Al-afasi
Mishari Al-afasi
Fecr Suresi Nasser Al Qatami
Nasser Al Qatami
Fecr Suresi Yasser Al Dosari
Yasser Al Dosari


Friday, May 10, 2024

Bizim için dua et, teşekkürler