Surah Al Imran aya 190 , Swahili translation of the meaning Ayah.

  1. Arabic
  2. tafsir
  3. mp3
  4. English
Quran in Swahili QUR,ANI TUKUFU na tafsiri ya maana yake kwenye lugha ya Kiswahili - Ali Muhsen Alberwany & English - Sahih International : Surah Al Imran aya 190 in arabic text(The Family of Imraan).
  
   
ayat 190 from Surah Al Imran

﴿إِنَّ فِي خَلْقِ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ وَاخْتِلَافِ اللَّيْلِ وَالنَّهَارِ لَآيَاتٍ لِّأُولِي الْأَلْبَابِ﴾
[ آل عمران: 190]

Hakika katika kuumbwa mbingu na ardhi na kukhitalifiana usiku na mchana ziko Ishara kwa wenye akili,

Surah Al Imran in Swahili

Swahili Translation - Al-Barwani

English - Sahih International


Indeed, in the creation of the heavens and the earth and the alternation of the night and the day are signs for those of understanding.


Tafsiri ya maana yake kwenye lugha ya Kiswahili


Hakika katika kuumbwa mbingu na ardhi na kukhitalifiana usiku na mchana ziko Ishara kwa wenye akili.


Hakika katika kuumbwa mbingu na ardhi na viliomo ndani yao kwa vile vilivyo umbwa tangu mwanzo na mipango yake, na kukhitalifiana usiku na mchana kwa mwangaza na giza, kwa urefu wake na ufupi, zipo dalili na ishara zilizo wazi kwa watu wenye akili na kutambua za kuthibitisha Umoja wa Mwenyezi Mungu na Uwezo wake. -Hakika katika kuumbwa mbingu na ardhi, na kukhitalifiana usiku na mchana ziko ishara kwa wenye akili- - Aya hii ina ukweli unao onyeshea taadhima ya Muumba. Mbingu ni moja katika Ishara za Mwenyezi Mungu inayo tubainikia kwetu kwa miale ya jua inayo piga juu ya anga linalo izunguka dunia. Miale hii inapo angukia chembe chembe na vumbi vumbi jembamba liliopo angani humulika mianga hiyo na kutawanyika kila upande. Huu mwanga mweupe kwa hakika ni mkusanyiko wa rangi zote zionekanazo. Hizi chembe chembe za angani huzimeza baadhi ya hizo rangi. Imedhihiri kuwa rangi yenye kuenea zaidi ni rangi ya kibuluu. Na hii inazidi kuzagaa linapo kuwa jua liko utosini, na ubuluu wake unapungua kidogo kidogo mpaka jua linapo kuwa upeo wa macho wakati wa magharibi au alfajiri. Wakati huo ile miale ya jua inakwenda masafa makubwa zaidi kabisa. Kwa hivyo zile chembe chembe za angani huzimeza rangi zote isipo kuwa rangi nyekundu. Usafi wa maneno ni: mwangaza wa mchana unahitaji miale ya jua na kuwepo vumbi la kutosha katika anga. Dalili ya hayo ni yale yaliyo tokea mwaka 1944 mbingu ilipo ingia kiza ghafla kati ya mchana. Jinsi ya kiza mchana ukawa kama usiku. Kwa wakati mfupi yakawa hayo, kisha mbingu ikawa nyekundu, kisha kidogo kidogo ikawa rangi ya machungwa, na kisha ya manjano mpaka mbingu ikarejea rangi yake ya tabia, baada ya saa au zaidi. Baadae ilibainika kuwa mambo hayo yalitokana na mripuko mbinguni likatokea jivu, likachukuliwa na upepo mbali mpaka Afrika ya kati na kaskazini, na kufika magharibi ya Asia. Huko ndiko ikaonekana hali hiyo katika pande za Syria. Maelezo yake ni kuwa vumbi lilioko hewani liliifunika nuru ya jua. Lilipo pungua jivu ulidhihiri mwangaza mwekundu na baadae wa manjano n.k. Mwanaadamu akipaa angani katika chombo atapitia matabaka yanayo khitalifiana sifa. Ataiona mbingu inazidi ubuluu mpaka akifika kwenye anga la nje lisio kuwa na hayo mavumbi n.k. ataona mbingu yote ni kiza kitupu kama kwamba ni usiku juu ya kuwa jua lipo juu. Kwa ufupi ni kuwa zipo mbingu nyingi si moja ziliyo pandana tabaka kwa tabaka kama maqubba, zinazo khitalifiana katika sifa zake na rangi zake. Haya ni katika Ishara za Mwenyezi Mungu Mtukufu Aliye takasika kuwa vyote viliomo mbinguni na ardhini vinamtukuza Yeye. Ama kukhitalifiana usiku na mchana, tumekwisha fahamu kuwa mwanga wa mchana unategemea miale ya jua kuanguka juu ya hili funiko la anga, lenye chembe chembe za vumbi kwa kiasi maalumu. Mwangaza huu ni mkali hata unaficha mwangaza unao toka kwenye nyota n.k. Ama wakati wa usiku mwangaza wa jua unapo fichika, inakuwa hapana katika anga isipo kuwa vumbi linalo tuzunguka na mianga dhaifu ya nyota. Kupishana usiku na mchana ni kwa sababu ya kuzunguka dunia kwa nafsi yake wenyewe, na tafauti ya misimu na kurefuka na kufupika usiku na mchana ni kwa mzunguko wa hii dunia kulizunguka jua. Na katika hikima yake Mwenyezi Mungu na uwezo wake ni kuwa kubadilika usiku na mchana, na kubadilika misimu ya joto na baridi, ni kutengeneza hali ya hewa iwe wastani, yaani kati na kati, kwa kusilihi maisha ya vilivyo hai.

English Türkçe Indonesia
Русский Français فارسی
تفسير Bengali Urdu

listen to Verse 190 from Al Imran


Ayats from Quran in Swahili

  1. Nasi tutaweka mizani za uadilifu kwa Siku ya Kiyama. Basi nafsi haitadhulumiwa kitu chochote. Hata
  2. Na ama A'di waliangamizwa kwa upepo mkali usio zuilika.
  3. Anaye tenda mema basi anajitendea mwenyewe nafsi yake, na mwenye kutenda uovu basi ni juu
  4. Au hao wana miungu ya kishirikina walio watungia dini asiyo itolea idhini Mwenyezi Mungu? Na
  5. Kisha tukawafanya kuwa watangulizi na mfano kwa wa baadaye.
  6. Je! Mnaiona mbegu ya uzazi mnayo idondokeza?
  7. Wameridhia kuwa pamoja na wabakiao nyuma, na nyoyo zao zikapigwa muhuri; kwa hivyo hawafahamu.
  8. Basi tukamwokoa yeye na ahali zake, isipo kuwa mkewe; tukamkadiria katika walio baki nyuma.
  9. Mzinifu mwanamke na mzinifu mwanamume, mtandikeni kila mmoja katika wao bakora mia. Wala isikushikeni huruma
  10. Watu wamepambiwa kupenda matamanio ya wanawake, na wana, na mirundi ya dhahabu na fedha, na

Quran Surah in Swahili :

Al-Baqarah Al-'Imran An-Nisa'
Al-Ma'idah Yusuf Ibrahim
Al-Hijr Al-Kahf Maryam
Al-Hajj Al-Qasas Al-'Ankabut
As-Sajdah Ya Sin Ad-Dukhan
Al-Fath Al-Hujurat Qaf
An-Najm Ar-Rahman Al-Waqi'ah
Al-Hashr Al-Mulk Al-Haqqah
Al-Inshiqaq Al-A'la Al-Ghashiyah

Download Surah Al Imran with the voice of the most famous Quran reciters :

Surah Al Imran mp3 : choose the reciter to listen and download the chapter Al Imran Complete with high quality
Surah Al Imran Ahmed El Agamy
Ahmed Al Ajmy
Surah Al Imran Bandar Balila
Bandar Balila
Surah Al Imran Khalid Al Jalil
Khalid Al Jalil
Surah Al Imran Saad Al Ghamdi
Saad Al Ghamdi
Surah Al Imran Saud Al Shuraim
Saud Al Shuraim
Surah Al Imran Abdul Basit Abdul Samad
Abdul Basit
Surah Al Imran Abdul Rashid Sufi
Abdul Rashid Sufi
Surah Al Imran Abdullah Basfar
Abdullah Basfar
Surah Al Imran Abdullah Awwad Al Juhani
Abdullah Al Juhani
Surah Al Imran Fares Abbad
Fares Abbad
Surah Al Imran Maher Al Muaiqly
Maher Al Muaiqly
Surah Al Imran Muhammad Siddiq Al Minshawi
Al Minshawi
Surah Al Imran Al Hosary
Al Hosary
Surah Al Imran Al-afasi
Mishari Al-afasi
Surah Al Imran Yasser Al Dosari
Yasser Al Dosari


Monday, May 13, 2024

لا تنسنا من دعوة صالحة بظهر الغيب