Surah Al Imran aya 200 , Swahili translation of the meaning Ayah.
﴿يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا اصْبِرُوا وَصَابِرُوا وَرَابِطُوا وَاتَّقُوا اللَّهَ لَعَلَّكُمْ تُفْلِحُونَ﴾
[ آل عمران: 200]
Enyi mlio amini! Subirini, na shindaneni kusubiri, na kuweni macho, na mcheni Mwenyezi Mungu, ili mpate kufanikiwa.
Surah Al Imran in SwahiliSwahili Translation - Al-Barwani
English - Sahih International
O you who have believed, persevere and endure and remain stationed and fear Allah that you may be successful.
Tafsiri ya maana yake kwenye lugha ya Kiswahili
Enyi mlio amini! Subirini, na shindaneni kusubiri, na kuweni macho, na mcheni Mwenyezi Mungu, ili mpate kufanikiwa.
Enyi mlio amini! Shikamaneni na subira, na mwashinde maadui zenu katika kusubiri. Na kaeni macho kuilinda mipaka, na mkhofini Mola Mlezi wenu. Katika haya yote ndio mtaraji kufanikiwa. (Jee! Baada ya kuijua Qurani yamfalia Muislamu kusema kuwa dini ni kitu mbali na siyasa? Vipi uamrishe mema, ukataze maovu, uhukumu, ukatibiane mikataba na dola nyengine, ukusanye zaka na kuzigawa, upigane Jihadi, ulinde mipaka n.k., n.k. na uiepuke siyasa? Amesema Prof. Khurshid Ahmad: -Uislamu si dini kwa maana ya ovyo ovyo kama lilivyo potoshwa neno hilo, yaani kuwa umemkhusu mtu maisha yake ya binafsi tu. Ni mwendo kaamili wa maisha, unao angalia kila midani ya uhai wa binaadamu. Uislamu ni uwongozi katika kila nyendo za maisha - za binafsi na za jamii, za kimwili na kiroho, za uchumi na siyasa, za sharia na mila, za taifa na za mataifa.---Uislamu, Maana na Ujumbe wake uk. 37)
| English | Türkçe | Indonesia |
| Русский | Français | فارسی |
| تفسير | Bengali | Urdu |
Ayats from Quran in Swahili
- Na kwa siku iliyo ahidiwa!
- Akasema: Enyi watu wangu! Mimi simo katika upotofu, lakini mimi ni Mtume nitokaye kwa Mola
- Na ama ukuta, huo ulikuwa ni wa vijana wawili mayatima kule mjini. Na chini yake
- Na tukampa ahali zake na wengine kama wao pamoja nao, kuwa ni rehema itokayo kwetu,
- Basi tulipo waondolea adhabu hiyo, mara wakaingia kuvunja ahadi.
- Basi walitaka kumfanyia vitimbi, lakini tukawafanya wao ndio wa chini.
- Kilipo ufunika huo Mkunazi hicho kilicho ufunuika.
- Na haya ni makumbusho yaliyo barikiwa, tuliyo yateremsha. Basi je! Mnayakataa?
- Akasema: Itupe, ewe Musa!
- Na wapeni wanawake mahari yao hali ya kuwa ni kipawa. Lakini wakikutunukieni kitu katika mahari,
Quran Surah in Swahili :
Download Surah Al Imran with the voice of the most famous Quran reciters :
Surah Al Imran mp3 : choose the reciter to listen and download the chapter Al Imran Complete with high quality
Ahmed Al Ajmy
Bandar Balila
Khalid Al Jalil
Saad Al Ghamdi
Saud Al Shuraim
Abdul Basit
Ammar Al-Mulla
Abdullah Basfar
Abdullah Al Juhani
Fares Abbad
Maher Al Muaiqly
Al Minshawi
Al Hosary
Mishari Al-afasi
Yasser Al Dosari
Please remember us in your sincere prayers



