Surah shura aya 45 , Swahili translation of the meaning Ayah.
﴿وَتَرَاهُمْ يُعْرَضُونَ عَلَيْهَا خَاشِعِينَ مِنَ الذُّلِّ يَنظُرُونَ مِن طَرْفٍ خَفِيٍّ ۗ وَقَالَ الَّذِينَ آمَنُوا إِنَّ الْخَاسِرِينَ الَّذِينَ خَسِرُوا أَنفُسَهُمْ وَأَهْلِيهِمْ يَوْمَ الْقِيَامَةِ ۗ أَلَا إِنَّ الظَّالِمِينَ فِي عَذَابٍ مُّقِيمٍ﴾
[ الشورى: 45]
Na utawaona wanapelekwa kwenye Moto, nao wamenyenyekea kwa unyonge, wanatazama kwa mtazamo wa kificho. Na walio amini watasema: Hakika wapatao khasara ni hao walio khasiri nafsi zao na ahali zao Siku ya Kiyama. Ama hakika wenye kudhulumu watakuwa katika adhabu ya daima.
Surah Ash_shuraa in SwahiliSwahili Translation - Al-Barwani
English - Sahih International
And you will see them being exposed to the Fire, humbled from humiliation, looking from [behind] a covert glance. And those who had believed will say, "Indeed, the [true] losers are the ones who lost themselves and their families on the Day of Resurrection. Unquestionably, the wrongdoers are in an enduring punishment."
Tafsiri ya maana yake kwenye lugha ya Kiswahili
Na utawaona wanapelekwa kwenye Moto, nao wamenyenyekea kwa unyonge, wanatazama kwa mtazamo wa kificho. Na walio amini watasema: Hakika wapatao khasara ni hao walio khasiri nafsi zao na ahali zao Siku ya Kiyama. Ama hakika wenye kudhulumu watakuwa katika adhabu ya daima.
Na kadhaalika, utawaona walio dhulumu, wakipelekwa Motoni, wamenywea kwa sababu ya unyonge ulio tokana na hivyo vitisho walivyo vikuta, wakitupia jicho kwa kificho kwenye huo Moto kwa kuukhofu vituko vyake. Na hapo Waumini watasema: Hakika walio khasiri kweli ni hao walio dhulumu nafsi zao kwa ukafiri wao, na wakawakhasiri wake zao na watoto wao na jamaa zao kwa mfarakano walio usabibisha baina yao. Na Mwenyezi Mungu ananabihisha kwamba wenye kudhulumu watakuwa katika adhabu ya milele.
English | Türkçe | Indonesia |
Русский | Français | فارسی |
تفسير | Bengali | Urdu |
Ayats from Quran in Swahili
- Zitacheka, zitachangamka;
- Wakasema: Je! Umetujia kwa maneno ya kweli au wewe ni katika wachezao tu?
- Basi wape muhula makafiri - wape muhula pole pole.
- Na fanyeni juhudi kwa ajili ya Mwenyezi Mungu kama inavyo stahiki jihadi yake. Yeye amekuteueni.
- Na akaufanya mwezi ndani yake uwe nuru, na akalifanya jua kuwa taa?
- Wakasema: Je! Umetujia ili utuachishe tuliyo wakuta nayo baba zetu, na mpate nyinyi wawili ukubwa
- Na hao walikwisha wapoteza wengi, wala usiwazidishie walio dhulumu ila kupotea.
- Kwa hakika tuliwatuma Mitume wetu kwa dalili waziwazi, na tukateremsha Kitabu pamoja nao na Mizani,
- Je! Mwenye kuwa na bayana kutoka kwa Mola wake Mlezi ni kama aliye pambiwa uovu
- Na alipo sema Ibrahim: Mola wangu Mlezi! Nionyeshe vipi unavyo fufua wafu. Mwenyezi Mungu akasema:
Quran Surah in Swahili :
Download Surah shura with the voice of the most famous Quran reciters :
Surah shura mp3 : choose the reciter to listen and download the chapter shura Complete with high quality
Ahmed Al Ajmy
Bandar Balila
Khalid Al Jalil
Saad Al Ghamdi
Saud Al Shuraim
Abdul Basit
Abdul Rashid Sufi
Abdullah Basfar
Abdullah Al Juhani
Fares Abbad
Maher Al Muaiqly
Al Minshawi
Al Hosary
Mishari Al-afasi
Yasser Al Dosari
لا تنسنا من دعوة صالحة بظهر الغيب