سورة القمر بالسواحلية

  1. استمع للسورة
  2. سور أخرى
  3. ترجمة السورة
القرآن الكريم | ترجمة معاني القرآن | اللغة السواحلية | سورة القمر | Al Qamar - عدد آياتها 55 - رقم السورة في المصحف: 54 - معنى السورة بالإنجليزية: The Moon.

اقْتَرَبَتِ السَّاعَةُ وَانشَقَّ الْقَمَرُ(1)

Saa imekaribia, na mwezi umepasuka!

وَإِن يَرَوْا آيَةً يُعْرِضُوا وَيَقُولُوا سِحْرٌ مُّسْتَمِرٌّ(2)

Na wakiona Ishara hugeuka upande na husema: Huu uchawi tu unazidi kuendelea.

وَكَذَّبُوا وَاتَّبَعُوا أَهْوَاءَهُمْ ۚ وَكُلُّ أَمْرٍ مُّسْتَقِرٌّ(3)

Na wamekanusha na wamefuata matamanio yao. Na kila jambo ni lenye kuthibiti.

وَلَقَدْ جَاءَهُم مِّنَ الْأَنبَاءِ مَا فِيهِ مُزْدَجَرٌ(4)

Na bila ya shaka zimewajia khabari zenye makaripio.

حِكْمَةٌ بَالِغَةٌ ۖ فَمَا تُغْنِ النُّذُرُ(5)

Hikima kaamili; lakini maonyo hayafai kitu!

فَتَوَلَّ عَنْهُمْ ۘ يَوْمَ يَدْعُ الدَّاعِ إِلَىٰ شَيْءٍ نُّكُرٍ(6)

Basi jiepushe nao. Siku atakapo ita mwitaji kuliendea jambo linalo chusha;

خُشَّعًا أَبْصَارُهُمْ يَخْرُجُونَ مِنَ الْأَجْدَاثِ كَأَنَّهُمْ جَرَادٌ مُّنتَشِرٌ(7)

Macho yao yatainama; watatoka makaburini kama nzige walio tawanyika,

مُّهْطِعِينَ إِلَى الدَّاعِ ۖ يَقُولُ الْكَافِرُونَ هَٰذَا يَوْمٌ عَسِرٌ(8)

Wanamkimbilia mwitaji, na makafiri wanasema: Hii ni siku ngumu.

۞ كَذَّبَتْ قَبْلَهُمْ قَوْمُ نُوحٍ فَكَذَّبُوا عَبْدَنَا وَقَالُوا مَجْنُونٌ وَازْدُجِرَ(9)

Kabla yao kaumu ya Nuhu walikanusha; wakamkanusha mja wetu, na wakasema ni mwendawazimu, na akakaripiwa.

فَدَعَا رَبَّهُ أَنِّي مَغْلُوبٌ فَانتَصِرْ(10)

Basi akamwomba Mola wake Mlezi akasema: Kwa hakika mimi nimeshindwa, basi ninusuru!

فَفَتَحْنَا أَبْوَابَ السَّمَاءِ بِمَاءٍ مُّنْهَمِرٍ(11)

Basi tukaifungua milango ya mbingu kwa maji yanayo miminika.

وَفَجَّرْنَا الْأَرْضَ عُيُونًا فَالْتَقَى الْمَاءُ عَلَىٰ أَمْرٍ قَدْ قُدِرَ(12)

Na tukazipasua ardhi kwa chemchem, yakakutana maji kwa jambo lilio kadiriwa.

وَحَمَلْنَاهُ عَلَىٰ ذَاتِ أَلْوَاحٍ وَدُسُرٍ(13)

Na tukamchukua kwenye safina ya mbao na kamba.

تَجْرِي بِأَعْيُنِنَا جَزَاءً لِّمَن كَانَ كُفِرَ(14)

Ikawa inakwenda kwa nadhari yetu, kuwa ni malipo kwa alivyo kuwa amekanushwa.

وَلَقَد تَّرَكْنَاهَا آيَةً فَهَلْ مِن مُّدَّكِرٍ(15)

Na bila ya shaka tuliiacha iwe ni Ishara. Lakini je, yupo anaye kumbuka?

فَكَيْفَ كَانَ عَذَابِي وَنُذُرِ(16)

Basi ilikuwaje adhabu yangu, na maonyo yangu.

وَلَقَدْ يَسَّرْنَا الْقُرْآنَ لِلذِّكْرِ فَهَلْ مِن مُّدَّكِرٍ(17)

Na bila ya shaka Sisi tumeifanya Qur'ani iwe nyepesi kufahamika. Lakini yupo anaye kumbuka?

كَذَّبَتْ عَادٌ فَكَيْفَ كَانَ عَذَابِي وَنُذُرِ(18)

Kina A'di walikanusha. Basi ilikuwaje adhabu yangu na maonyo yangu?

إِنَّا أَرْسَلْنَا عَلَيْهِمْ رِيحًا صَرْصَرًا فِي يَوْمِ نَحْسٍ مُّسْتَمِرٍّ(19)

Hakika Sisi tuliwapelekea upepo wa kimbunga katika siku korofi mfululizo,

تَنزِعُ النَّاسَ كَأَنَّهُمْ أَعْجَازُ نَخْلٍ مُّنقَعِرٍ(20)

Ukiwang'oa watu kama vigogo vya mitende vilio ng'olewa.

فَكَيْفَ كَانَ عَذَابِي وَنُذُرِ(21)

Basi ilikuwaje adhabu yangu na maonyo yangu?

وَلَقَدْ يَسَّرْنَا الْقُرْآنَ لِلذِّكْرِ فَهَلْ مِن مُّدَّكِرٍ(22)

Na bila ya shaka Sisi tumeifanya Qur'ani nyepesi kufahamika; lakini yupo anaye kumbuka?

كَذَّبَتْ ثَمُودُ بِالنُّذُرِ(23)

Thamudi waliwakanusha Waonyaji.

فَقَالُوا أَبَشَرًا مِّنَّا وَاحِدًا نَّتَّبِعُهُ إِنَّا إِذًا لَّفِي ضَلَالٍ وَسُعُرٍ(24)

Wakasema: Ati tumfuate binaadamu mmoja katika sisi? Basi hivyo sisi tutakuwa katika upotofu na kichaa!

أَأُلْقِيَ الذِّكْرُ عَلَيْهِ مِن بَيْنِنَا بَلْ هُوَ كَذَّابٌ أَشِرٌ(25)

Ni yeye tu aliye teremshiwa huo ukumbusho kati yetu sote? Bali huyu ni mwongo mwenye kiburi!

سَيَعْلَمُونَ غَدًا مَّنِ الْكَذَّابُ الْأَشِرُ(26)

Kesho watajua ni nani huyo mwongo mwenye kiburi.

إِنَّا مُرْسِلُو النَّاقَةِ فِتْنَةً لَّهُمْ فَارْتَقِبْهُمْ وَاصْطَبِرْ(27)

Hakika Sisi tutawapelekea ngamia jike ili kuwajaribu, basi watazame tu na ustahamili.

وَنَبِّئْهُمْ أَنَّ الْمَاءَ قِسْمَةٌ بَيْنَهُمْ ۖ كُلُّ شِرْبٍ مُّحْتَضَرٌ(28)

Na waambie kwamba maji yatagawanywa baina yao; kila sehemu ya maji itahudhuriwa na aliye khusika.

فَنَادَوْا صَاحِبَهُمْ فَتَعَاطَىٰ فَعَقَرَ(29)

Basi wakamwita mtu wao akaja akamchinja.

فَكَيْفَ كَانَ عَذَابِي وَنُذُرِ(30)

Basi ilikuwaje adhabu yangu na maonyo yangu!

إِنَّا أَرْسَلْنَا عَلَيْهِمْ صَيْحَةً وَاحِدَةً فَكَانُوا كَهَشِيمِ الْمُحْتَظِرِ(31)

Hakika Sisi tuliwapelekea ukelele mmoja tu, wakawa kama mabuwa ya kujengea uwa.

وَلَقَدْ يَسَّرْنَا الْقُرْآنَ لِلذِّكْرِ فَهَلْ مِن مُّدَّكِرٍ(32)

Na bila ya shaka Sisi tumeifanya Qur'ani iwe nyepesi kwa kukumbuka, lakini yupo akumbukaye?

كَذَّبَتْ قَوْمُ لُوطٍ بِالنُّذُرِ(33)

Kaumu Lut'i nao waliwakadhibisha Waonyaji.

إِنَّا أَرْسَلْنَا عَلَيْهِمْ حَاصِبًا إِلَّا آلَ لُوطٍ ۖ نَّجَّيْنَاهُم بِسَحَرٍ(34)

Hakika Sisi tukawapelekea kimbunga cha vijiwe, isipo kuwa wafuasi wa Lut'i. Hao tuliwaokoa karibu na alfajiri.

نِّعْمَةً مِّنْ عِندِنَا ۚ كَذَٰلِكَ نَجْزِي مَن شَكَرَ(35)

Kwa neema inayo toka kwetu. Hivyo ndivyo tumlipavyo anaye shukuru.

وَلَقَدْ أَنذَرَهُم بَطْشَتَنَا فَتَمَارَوْا بِالنُّذُرِ(36)

Na hakika yeye aliwaonya adhabu yetu; lakini wao waliyatilia shaka hayo maonyo.

وَلَقَدْ رَاوَدُوهُ عَن ضَيْفِهِ فَطَمَسْنَا أَعْيُنَهُمْ فَذُوقُوا عَذَابِي وَنُذُرِ(37)

Na walimtaka awape wageni wake. Tukayapofua macho yao, na tukawaambia: Onjeni basi adhabu na maonyo yangu!

وَلَقَدْ صَبَّحَهُم بُكْرَةً عَذَابٌ مُّسْتَقِرٌّ(38)

Na iliwafikia wakati wa asubuhi adhabu yangu ya kuendelea.

فَذُوقُوا عَذَابِي وَنُذُرِ(39)

Basi onjeni adhabu na maonyo yangu!

وَلَقَدْ يَسَّرْنَا الْقُرْآنَ لِلذِّكْرِ فَهَلْ مِن مُّدَّكِرٍ(40)

Na hakika tumeisahilisha Qur'ani kuikumbuka. Lakini yupo anaye kumbuka?

وَلَقَدْ جَاءَ آلَ فِرْعَوْنَ النُّذُرُ(41)

Na Waonyaji waliwafikia watu wa Firauni.

كَذَّبُوا بِآيَاتِنَا كُلِّهَا فَأَخَذْنَاهُمْ أَخْذَ عَزِيزٍ مُّقْتَدِرٍ(42)

Walizikadhibisha Ishara zetu zote, nasi tukawashika kama anavyo shika Mwenye nguvu Mwenye uweza.

أَكُفَّارُكُمْ خَيْرٌ مِّنْ أُولَٰئِكُمْ أَمْ لَكُم بَرَاءَةٌ فِي الزُّبُرِ(43)

Je! Makafiri wenu ni bora kuliko hao, au yameandikwa vitabuni kuwa nyinyi hamtiwi makosani?

أَمْ يَقُولُونَ نَحْنُ جَمِيعٌ مُّنتَصِرٌ(44)

Au ndio wanasema: Sisi ni wengi tutashinda tu.

سَيُهْزَمُ الْجَمْعُ وَيُوَلُّونَ الدُّبُرَ(45)

Wingi wao huu utashindwa, na wao watasukumwa nyuma.

بَلِ السَّاعَةُ مَوْعِدُهُمْ وَالسَّاعَةُ أَدْهَىٰ وَأَمَرُّ(46)

Bali Saa ya Kiyama ndio miadi yao, na Saa hiyo ni nzito zaidi na chungu zaidi.

إِنَّ الْمُجْرِمِينَ فِي ضَلَالٍ وَسُعُرٍ(47)

Hakika wakosefu wamo katika upotofu na wazimu.

يَوْمَ يُسْحَبُونَ فِي النَّارِ عَلَىٰ وُجُوهِهِمْ ذُوقُوا مَسَّ سَقَرَ(48)

Siku watakapo kokotwa Motoni kifudifudi waambiwe: Onjeni mguso wa Jahannamu!

إِنَّا كُلَّ شَيْءٍ خَلَقْنَاهُ بِقَدَرٍ(49)

Kwa hakika Sisi tumekiumba kila kitu kwa kipimo.

وَمَا أَمْرُنَا إِلَّا وَاحِدَةٌ كَلَمْحٍ بِالْبَصَرِ(50)

Na amri yetu haikuwa ila ni moja tu, kama kupepesa jicho.

وَلَقَدْ أَهْلَكْنَا أَشْيَاعَكُمْ فَهَلْ مِن مُّدَّكِرٍ(51)

Na bila ya shaka tumekwisha waangamiza wenzenu. Lakini yupo anaye kumbuka?

وَكُلُّ شَيْءٍ فَعَلُوهُ فِي الزُّبُرِ(52)

Na kila jambo walilo lifanya limo vitabuni.

وَكُلُّ صَغِيرٍ وَكَبِيرٍ مُّسْتَطَرٌ(53)

Na kila kidogo na kikubwa kimeandikwa.

إِنَّ الْمُتَّقِينَ فِي جَنَّاتٍ وَنَهَرٍ(54)

Hakika wachamngu watakuwa katika Mabustani na mito.

فِي مَقْعَدِ صِدْقٍ عِندَ مَلِيكٍ مُّقْتَدِرٍ(55)

Katika makalio ya haki kwa Mfalme Mwenye uweza.


المزيد من السور باللغة السواحلية:

سورة البقرة آل عمران سورة النساء
سورة المائدة سورة يوسف سورة ابراهيم
سورة الحجر سورة الكهف سورة مريم
سورة السجدة سورة يس سورة الدخان
سورة النجم سورة الرحمن سورة الواقعة
سورة الحشر سورة الملك سورة الحاقة

تحميل سورة القمر بصوت أشهر القراء :

قم باختيار القارئ للاستماع و تحميل سورة القمر كاملة بجودة عالية
سورة القمر أحمد العجمي
أحمد العجمي
سورة القمر خالد الجليل
خالد الجليل
سورة القمر سعد الغامدي
سعد الغامدي
سورة القمر سعود الشريم
سعود الشريم
سورة القمر عبد الباسط عبد الصمد
عبد الباسط
سورة القمر عبد الله عواد الجهني
عبد الله الجهني
سورة القمر علي الحذيفي
علي الحذيفي
سورة القمر فارس عباد
فارس عباد
سورة القمر ماهر المعيقلي
ماهر المعيقلي
سورة القمر محمد جبريل
محمد جبريل
سورة القمر محمد صديق المنشاوي
المنشاوي
سورة القمر الحصري
الحصري
سورة القمر العفاسي
مشاري العفاسي
سورة القمر ناصر القطامي
ناصر القطامي
سورة القمر ياسر الدوسري
ياسر الدوسري



Sunday, April 28, 2024

لا تنسنا من دعوة صالحة بظهر الغيب