Перевод суры Аль-Камар на суахили язык

  1. Сура mp3
  2. Другие суры
  3. суахили
Священный Коран | Перевод Корана | Язык суахили | Сура Аль-Камар | القمر - получите точный и надежный суахили текст сейчас - Количество аятов: 55 - Номер суры в мушафе: 54 - Значение названия суры на русском языке: The Moon.

اقْتَرَبَتِ السَّاعَةُ وَانشَقَّ الْقَمَرُ(1)

 Saa imekaribia, na mwezi umepasuka!

وَإِن يَرَوْا آيَةً يُعْرِضُوا وَيَقُولُوا سِحْرٌ مُّسْتَمِرٌّ(2)

 Na wakiona Ishara hugeuka upande na husema: Huu uchawi tu unazidi kuendelea.

وَكَذَّبُوا وَاتَّبَعُوا أَهْوَاءَهُمْ ۚ وَكُلُّ أَمْرٍ مُّسْتَقِرٌّ(3)

 Na wamekanusha na wamefuata matamanio yao. Na kila jambo ni lenye kuthibiti.

وَلَقَدْ جَاءَهُم مِّنَ الْأَنبَاءِ مَا فِيهِ مُزْدَجَرٌ(4)

 Na bila ya shaka zimewajia khabari zenye makaripio.

حِكْمَةٌ بَالِغَةٌ ۖ فَمَا تُغْنِ النُّذُرُ(5)

 Hikima kaamili; lakini maonyo hayafai kitu!

فَتَوَلَّ عَنْهُمْ ۘ يَوْمَ يَدْعُ الدَّاعِ إِلَىٰ شَيْءٍ نُّكُرٍ(6)

 Basi jiepushe nao. Siku atakapo ita mwitaji kuliendea jambo linalo chusha;

خُشَّعًا أَبْصَارُهُمْ يَخْرُجُونَ مِنَ الْأَجْدَاثِ كَأَنَّهُمْ جَرَادٌ مُّنتَشِرٌ(7)

 Macho yao yatainama; watatoka makaburini kama nzige walio tawanyika,

مُّهْطِعِينَ إِلَى الدَّاعِ ۖ يَقُولُ الْكَافِرُونَ هَٰذَا يَوْمٌ عَسِرٌ(8)

 Wanamkimbilia mwitaji, na makafiri wanasema: Hii ni siku ngumu.

۞ كَذَّبَتْ قَبْلَهُمْ قَوْمُ نُوحٍ فَكَذَّبُوا عَبْدَنَا وَقَالُوا مَجْنُونٌ وَازْدُجِرَ(9)

 Kabla yao kaumu ya Nuhu walikanusha; wakamkanusha mja wetu, na wakasema ni mwendawazimu, na akakaripiwa.

فَدَعَا رَبَّهُ أَنِّي مَغْلُوبٌ فَانتَصِرْ(10)

 Basi akamwomba Mola wake Mlezi akasema: Kwa hakika mimi nimeshindwa, basi ninusuru!

فَفَتَحْنَا أَبْوَابَ السَّمَاءِ بِمَاءٍ مُّنْهَمِرٍ(11)

 Basi tukaifungua milango ya mbingu kwa maji yanayo miminika.

وَفَجَّرْنَا الْأَرْضَ عُيُونًا فَالْتَقَى الْمَاءُ عَلَىٰ أَمْرٍ قَدْ قُدِرَ(12)

 Na tukazipasua ardhi kwa chemchem, yakakutana maji kwa jambo lilio kadiriwa.

وَحَمَلْنَاهُ عَلَىٰ ذَاتِ أَلْوَاحٍ وَدُسُرٍ(13)

 Na tukamchukua kwenye safina ya mbao na kamba.

تَجْرِي بِأَعْيُنِنَا جَزَاءً لِّمَن كَانَ كُفِرَ(14)

 Ikawa inakwenda kwa nadhari yetu, kuwa ni malipo kwa alivyo kuwa amekanushwa.

وَلَقَد تَّرَكْنَاهَا آيَةً فَهَلْ مِن مُّدَّكِرٍ(15)

 Na bila ya shaka tuliiacha iwe ni Ishara. Lakini je, yupo anaye kumbuka?

فَكَيْفَ كَانَ عَذَابِي وَنُذُرِ(16)

 Basi ilikuwaje adhabu yangu, na maonyo yangu.

وَلَقَدْ يَسَّرْنَا الْقُرْآنَ لِلذِّكْرِ فَهَلْ مِن مُّدَّكِرٍ(17)

 Na bila ya shaka Sisi tumeifanya Qur'ani iwe nyepesi kufahamika. Lakini yupo anaye kumbuka?

كَذَّبَتْ عَادٌ فَكَيْفَ كَانَ عَذَابِي وَنُذُرِ(18)

 Kina A'di walikanusha. Basi ilikuwaje adhabu yangu na maonyo yangu?

إِنَّا أَرْسَلْنَا عَلَيْهِمْ رِيحًا صَرْصَرًا فِي يَوْمِ نَحْسٍ مُّسْتَمِرٍّ(19)

 Hakika Sisi tuliwapelekea upepo wa kimbunga katika siku korofi mfululizo,

تَنزِعُ النَّاسَ كَأَنَّهُمْ أَعْجَازُ نَخْلٍ مُّنقَعِرٍ(20)

 Ukiwang'oa watu kama vigogo vya mitende vilio ng'olewa.

فَكَيْفَ كَانَ عَذَابِي وَنُذُرِ(21)

 Basi ilikuwaje adhabu yangu na maonyo yangu?

وَلَقَدْ يَسَّرْنَا الْقُرْآنَ لِلذِّكْرِ فَهَلْ مِن مُّدَّكِرٍ(22)

 Na bila ya shaka Sisi tumeifanya Qur'ani nyepesi kufahamika; lakini yupo anaye kumbuka?

كَذَّبَتْ ثَمُودُ بِالنُّذُرِ(23)

 Thamudi waliwakanusha Waonyaji.

فَقَالُوا أَبَشَرًا مِّنَّا وَاحِدًا نَّتَّبِعُهُ إِنَّا إِذًا لَّفِي ضَلَالٍ وَسُعُرٍ(24)

 Wakasema: Ati tumfuate binaadamu mmoja katika sisi? Basi hivyo sisi tutakuwa katika upotofu na kichaa!

أَأُلْقِيَ الذِّكْرُ عَلَيْهِ مِن بَيْنِنَا بَلْ هُوَ كَذَّابٌ أَشِرٌ(25)

 Ni yeye tu aliye teremshiwa huo ukumbusho kati yetu sote? Bali huyu ni mwongo mwenye kiburi!

سَيَعْلَمُونَ غَدًا مَّنِ الْكَذَّابُ الْأَشِرُ(26)

 Kesho watajua ni nani huyo mwongo mwenye kiburi.

إِنَّا مُرْسِلُو النَّاقَةِ فِتْنَةً لَّهُمْ فَارْتَقِبْهُمْ وَاصْطَبِرْ(27)

 Hakika Sisi tutawapelekea ngamia jike ili kuwajaribu, basi watazame tu na ustahamili.

وَنَبِّئْهُمْ أَنَّ الْمَاءَ قِسْمَةٌ بَيْنَهُمْ ۖ كُلُّ شِرْبٍ مُّحْتَضَرٌ(28)

 Na waambie kwamba maji yatagawanywa baina yao; kila sehemu ya maji itahudhuriwa na aliye khusika.

فَنَادَوْا صَاحِبَهُمْ فَتَعَاطَىٰ فَعَقَرَ(29)

 Basi wakamwita mtu wao akaja akamchinja.

فَكَيْفَ كَانَ عَذَابِي وَنُذُرِ(30)

 Basi ilikuwaje adhabu yangu na maonyo yangu!

إِنَّا أَرْسَلْنَا عَلَيْهِمْ صَيْحَةً وَاحِدَةً فَكَانُوا كَهَشِيمِ الْمُحْتَظِرِ(31)

 Hakika Sisi tuliwapelekea ukelele mmoja tu, wakawa kama mabuwa ya kujengea uwa.

وَلَقَدْ يَسَّرْنَا الْقُرْآنَ لِلذِّكْرِ فَهَلْ مِن مُّدَّكِرٍ(32)

 Na bila ya shaka Sisi tumeifanya Qur'ani iwe nyepesi kwa kukumbuka, lakini yupo akumbukaye?

كَذَّبَتْ قَوْمُ لُوطٍ بِالنُّذُرِ(33)

 Kaumu Lut'i nao waliwakadhibisha Waonyaji.

إِنَّا أَرْسَلْنَا عَلَيْهِمْ حَاصِبًا إِلَّا آلَ لُوطٍ ۖ نَّجَّيْنَاهُم بِسَحَرٍ(34)

 Hakika Sisi tukawapelekea kimbunga cha vijiwe, isipo kuwa wafuasi wa Lut'i. Hao tuliwaokoa karibu na alfajiri.

نِّعْمَةً مِّنْ عِندِنَا ۚ كَذَٰلِكَ نَجْزِي مَن شَكَرَ(35)

 Kwa neema inayo toka kwetu. Hivyo ndivyo tumlipavyo anaye shukuru.

وَلَقَدْ أَنذَرَهُم بَطْشَتَنَا فَتَمَارَوْا بِالنُّذُرِ(36)

 Na hakika yeye aliwaonya adhabu yetu; lakini wao waliyatilia shaka hayo maonyo.

وَلَقَدْ رَاوَدُوهُ عَن ضَيْفِهِ فَطَمَسْنَا أَعْيُنَهُمْ فَذُوقُوا عَذَابِي وَنُذُرِ(37)

 Na walimtaka awape wageni wake. Tukayapofua macho yao, na tukawaambia: Onjeni basi adhabu na maonyo yangu!

وَلَقَدْ صَبَّحَهُم بُكْرَةً عَذَابٌ مُّسْتَقِرٌّ(38)

 Na iliwafikia wakati wa asubuhi adhabu yangu ya kuendelea.

فَذُوقُوا عَذَابِي وَنُذُرِ(39)

 Basi onjeni adhabu na maonyo yangu!

وَلَقَدْ يَسَّرْنَا الْقُرْآنَ لِلذِّكْرِ فَهَلْ مِن مُّدَّكِرٍ(40)

 Na hakika tumeisahilisha Qur'ani kuikumbuka. Lakini yupo anaye kumbuka?

وَلَقَدْ جَاءَ آلَ فِرْعَوْنَ النُّذُرُ(41)

 Na Waonyaji waliwafikia watu wa Firauni.

كَذَّبُوا بِآيَاتِنَا كُلِّهَا فَأَخَذْنَاهُمْ أَخْذَ عَزِيزٍ مُّقْتَدِرٍ(42)

 Walizikadhibisha Ishara zetu zote, nasi tukawashika kama anavyo shika Mwenye nguvu Mwenye uweza.

أَكُفَّارُكُمْ خَيْرٌ مِّنْ أُولَٰئِكُمْ أَمْ لَكُم بَرَاءَةٌ فِي الزُّبُرِ(43)

 Je! Makafiri wenu ni bora kuliko hao, au yameandikwa vitabuni kuwa nyinyi hamtiwi makosani?

أَمْ يَقُولُونَ نَحْنُ جَمِيعٌ مُّنتَصِرٌ(44)

 Au ndio wanasema: Sisi ni wengi tutashinda tu.

سَيُهْزَمُ الْجَمْعُ وَيُوَلُّونَ الدُّبُرَ(45)

 Wingi wao huu utashindwa, na wao watasukumwa nyuma.

بَلِ السَّاعَةُ مَوْعِدُهُمْ وَالسَّاعَةُ أَدْهَىٰ وَأَمَرُّ(46)

 Bali Saa ya Kiyama ndio miadi yao, na Saa hiyo ni nzito zaidi na chungu zaidi.

إِنَّ الْمُجْرِمِينَ فِي ضَلَالٍ وَسُعُرٍ(47)

 Hakika wakosefu wamo katika upotofu na wazimu.

يَوْمَ يُسْحَبُونَ فِي النَّارِ عَلَىٰ وُجُوهِهِمْ ذُوقُوا مَسَّ سَقَرَ(48)

 Siku watakapo kokotwa Motoni kifudifudi waambiwe: Onjeni mguso wa Jahannamu!

إِنَّا كُلَّ شَيْءٍ خَلَقْنَاهُ بِقَدَرٍ(49)

 Kwa hakika Sisi tumekiumba kila kitu kwa kipimo.

وَمَا أَمْرُنَا إِلَّا وَاحِدَةٌ كَلَمْحٍ بِالْبَصَرِ(50)

 Na amri yetu haikuwa ila ni moja tu, kama kupepesa jicho.

وَلَقَدْ أَهْلَكْنَا أَشْيَاعَكُمْ فَهَلْ مِن مُّدَّكِرٍ(51)

 Na bila ya shaka tumekwisha waangamiza wenzenu. Lakini yupo anaye kumbuka?

وَكُلُّ شَيْءٍ فَعَلُوهُ فِي الزُّبُرِ(52)

 Na kila jambo walilo lifanya limo vitabuni.

وَكُلُّ صَغِيرٍ وَكَبِيرٍ مُّسْتَطَرٌ(53)

 Na kila kidogo na kikubwa kimeandikwa.

إِنَّ الْمُتَّقِينَ فِي جَنَّاتٍ وَنَهَرٍ(54)

 Hakika wachamngu watakuwa katika Mabustani na mito.

فِي مَقْعَدِ صِدْقٍ عِندَ مَلِيكٍ مُّقْتَدِرٍ(55)

 Katika makalio ya haki kwa Mfalme Mwenye uweza.


Больше сур в суахили:


Аль-Бакара Аль-'Имран Ан-Ниса'
Аль-Маида Юсуф Ибрахим
Аль-Хиджр Аль-Кахф Марьям
Аль-Хадж Аль-Касас Аль-'Анкабут
Ас-Саджда Я-Син Ад-Духан
Аль-Фатх Аль-Худжурат Каф
Ан-Наджм Ар-Рахман Аль-Ваки'а
Аль-Хашр Аль-Мульк Аль-Хакка
Аль-Иншикак Аль-А'ла Аль-Гашия

Скачать суру Al-Qamar с голосом самых известных рекитаторов Корана:

Сура Al-Qamar mp3: выберите рекитатора, чтобы прослушать и скачать главу Al-Qamar полностью в высоком качестве
surah Al-Qamar Ahmed El Agamy
Ahmed Al Ajmy
surah Al-Qamar Bandar Balila
Bandar Balila
surah Al-Qamar Khalid Al Jalil
Khalid Al Jalil
surah Al-Qamar Saad Al Ghamdi
Saad Al Ghamdi
surah Al-Qamar Saud Al Shuraim
Saud Al Shuraim
surah Al-Qamar Abdul Basit Abdul Samad
Abdul Basit
surah Al-Qamar Abdul Rashid Sufi
Abdul Rashid Sufi
surah Al-Qamar Abdullah Basfar
Abdullah Basfar
surah Al-Qamar Abdullah Awwad Al Juhani
Abdullah Al Juhani
surah Al-Qamar Fares Abbad
Fares Abbad
surah Al-Qamar Maher Al Muaiqly
Maher Al Muaiqly
surah Al-Qamar Muhammad Siddiq Al Minshawi
Al Minshawi
surah Al-Qamar Al Hosary
Al Hosary
surah Al-Qamar Al-afasi
Mishari Al-afasi
surah Al-Qamar Yasser Al Dosari
Yasser Al Dosari


Thursday, May 9, 2024

Помолитесь за нас хорошей молитвой